Uchaguzi 2020 Kwanini Tundu Lissu anatumia muda mwingi kutafsiri Katiba na Sheria badala ya kutangaza sera?

Uchaguzi 2020 Kwanini Tundu Lissu anatumia muda mwingi kutafsiri Katiba na Sheria badala ya kutangaza sera?

Nijuavyo mikutano ya kampeni ni kwa ajili ya kutangaza sera na ilani za vyama lakini nashangazwa na Tundu Lissu ambaye hutumia muda mwingi kutafsiri sheria na katiba ya nchi.

Mfano katika mkutano wa leo ametumia muda mwingi kuelezea utaratibu wa kumshtaki mtu na jinsi ya kumuita shaurini.
Akatolea mfano wa yeye kuitwa na NEC kienyeji.

Tundu Lissu elewa kwamba watanzania hawahitaji darasa la sheria bali uwaeleze utawafanyia nini wakikuchagua.

Maendeleo hayana vyama!

Naona inakuuma sana kuona watanzania wanafunguliwa kutoka utumwani. Kutokujua sheria watanzania wengi ndo mtaji wa CCM kunyanyasa watu
 
Katiba ya nchi ndio dira kuu ya kuendesha nchi iwe kisiasa na mambo mengine yoote, ni vigumu kuikwepa katiba ya nchi hasa hasa kama una ndoto za kuongoza nchi pia maswali mengi anayokutana nayo kuulizwa ni ya kikatiba ivi kwani huoni watu wamemuelewa haraka kila siku makundi ya watu yanaongezeka
 
Anaelezea jinsi sheria zilivyokua zinavunjwa hapo nyuma na pia yapaswa mtu ajue kosa lake na utaratibu wa kuitwa kuhojiwa sio kienyeji kama walivyofanya hiyo tume so ni muhimu watu wawekwe wazi anapokosea na hatua anayochukua kwa uwazi! Tatizo wengine hamtaki watu wafahamu haki zao!
 
Yaani Leo katoa Pasi ya ovyo kabisa katika harakati zake za kujijenga kimaslahi. Sijui kama mnaona ninachokiona kwa Lissu. Au ndiyo mmeamua kuvaa miwani ya 'mabao'? Ebu vueni miwani hiyo!
Na Yule anayewadhalilisha wanawake ndo mwenye pasi kali?!!
 
Awe anatangaza Sera, au asitangaze nitamchagua hivyo hivyo. Nimeumizwa sana na utawala wa huyu mzee, Mimi namtumia mama yangu ela ya matumizi yeye analipia kitambusho.
 
Kwa sababu wewe ni kilaza huwezi kumuelewa Lissu!!! Umekaririshwa juu ya ukoloni kwa iyo ukisikia ukoloni unawaza ulivyokaririshwa!!

Lissu anaongelea kuweka mamlaka ya matumizi ya pesa na mgawanyo wake kwa wananchi kwamba, wananchi wasiwe ombaomba kwa kiongozi mkuu ila wao ndo waweke vipaumbele kwa miradi wanayotaka iwe miradi ya maji, elimu au miundombinu.

Hivi ndo ilivyokuwa kipindi cha mkoloni Ndo mana vyama vya ushirika vya wananchi enzi za mkoloni vilijenga shule na miradi mbalimbali kwa sababu sio gavana aliyekuwa anawaamulia matumizi ya pesa zao.

Baada ya Uhuru Nyerere alibadilisha sheria ya fedha kuweka hela zote chini ya Raisi, Ndo mana leo miradi yote hela lazima ziishinishwe na Raisi.

Ndo mana hadi leo watanzania wamekuwa ombaomba kwa serikali na Raisi , kila sehemu wanalia, Raisi tujengee shule, tuletee Maji, sijui tujengee barabara. Shida ni mfumo uliowekwa baada ya Uhuru kuweka fedha zote za nchi chini ya mtu mmoja.
Belezee baba
 
Leo akiwa Mkoa wa Kilimanjaro, Lissu kaahidi kuhakikisha anairejesha Tanzania enzi za ukoloni. Nimemsikia na kumona akiongea hayo mwenyewe kupitia televisheni ya ITV, muda mchache uliopita. Hivi maisha ya ukoloni yalikuwa bora kuliko yale baada ya uhuru?

Yaani Lissu kwa uongo hajambo, anaongeza kuwa Wakati wa ukoloni mamlaka yalikuwa kwa wananchi! Mambo ya ajabu sana haya...! Na mwenyekiti wake wa Chama anaogopa 'kumfunga' Lissu kengele.
Jitahidi Sana kuwa mkweli ! MUNGU anampenda mtu mkweli . Tusipende kuupotosha Umma !!!
 
Jitahidi Sana kuwa mkweli ! MUNGU anampenda mtu mkweli . Tusipende kuupotosha Umma !!!
Umetazama ITV leo usiku? Uongo kwangu mwiko.

Nakuwekea ushahidi. Tazama channel ya ITV kupitia youtube kwenye link hapa chini. Kuanzia dakika ya 8:33 mpaka 11:44.




Karibu usione aibu.
 
Nijuavyo mikutano ya kampeni ni kwa ajili ya kutangaza sera na ilani za vyama lakini nashangazwa na Tundu Lissu ambaye hutumia muda mwingi kutafsiri sheria na katiba ya nchi.

Mfano katika mkutano wa leo ametumia muda mwingi kuelezea utaratibu wa kumshtaki mtu na jinsi ya kumuita shaurini.
Akatolea mfano wa yeye kuitwa na NEC kienyeji.

Tundu Lissu elewa kwamba watanzania hawahitaji darasa la sheria bali uwaeleze utawafanyia nini wakikuchagua.

Maendeleo hayana vyama!
Haki, Uhuru na Maendeleo ya Watu...somo la Uraia ni muhimu maana Magufuli na Tume wamekuwa wakikanyaga Katiba na Sheria waziwazi
 
Nijuavyo mikutano ya kampeni ni kwa ajili ya kutangaza sera na ilani za vyama lakini nashangazwa na Tundu Lissu ambaye hutumia muda mwingi kutafsiri sheria na katiba ya nchi.

Mfano katika mkutano wa leo ametumia muda mwingi kuelezea utaratibu wa kumshtaki mtu na jinsi ya kumuita shaurini.
Akatolea mfano wa yeye kuitwa na NEC kienyeji.

Tundu Lissu elewa kwamba watanzania hawahitaji darasa la sheria bali uwaeleze utawafanyia nini wakikuchagua.

Maendeleo hayana vyama!
Ni mbinu nzuri sana ya kuwaelimisha wananchi kabla ya kumwaga sera na wengi tumefunguliwa macho tupo tayari kumpa kura zetu sasa.
 
Nijuavyo mikutano ya kampeni ni kwa ajili ya kutangaza sera na ilani za vyama lakini nashangazwa na Tundu Lissu ambaye hutumia muda mwingi kutafsiri sheria na katiba ya nchi.

Mfano katika mkutano wa leo ametumia muda mwingi kuelezea utaratibu wa kumshtaki mtu na jinsi ya kumuita shaurini.
Akatolea mfano wa yeye kuitwa na NEC kienyeji.

Tundu Lissu elewa kwamba watanzania hawahitaji darasa la sheria bali uwaeleze utawafanyia nini wakikuchagua.

Maendeleo hayana vyama!
Sheria na katiba ndio msingi wa uongozi ktk nchi.


Kwann John anatumia muda mwingi kutembea na wasanii ?
 
anatueleza mambo ya sheria ili tujue haki zetu na kuzipigania hata ikibidi kuingia barabarani.
 
Back
Top Bottom