Uchaguzi 2020 Kwanini Tundu Lissu anaweza kuwa kiongozi mzuri wa Taifa?

Uchaguzi 2020 Kwanini Tundu Lissu anaweza kuwa kiongozi mzuri wa Taifa?

Binafsi Nakipongeza Chama Changu kwa kumteua huyu Nguli wa Sheria Tundu Lissu kukiwakilisha Chama katika Ngazi ya Rais kwa sababu ni mtu Sahihi na anaijua Sheria Vizuri.
 
Ndoto zingine hadi unatamani iwe kweli, niliota Lissu anaongoza matokeo ya awali kwa 47%.

Mungu Baba bariki hii
 
Hata jaji Joseph Sinde Warioba aliwahi sema Lissu anaweza kurejesha furaha za watanzania.

Tumeona unaweza kumpa mke kila kitu lakini usipo mpa uhuru atakuacha na kwenda kukaa na hata muuza mkaa ili awe na uhuru.

Hoja za kujenga reli .....ipo ya mjerumani nani alijenga.


Hoja ya ndege baba wa taifa alinunua madege mengi na mwisho hakujenga kwao uwanja wa ndege hata nyumba ya kuishi kajengewa tu.

Hoja ya Bwawa la maji ......Baba wa taifa kajenga
Kidatu
Kihanzi
Nyumba ya Mungu
Hare
Na kikwete kaleta gesi mbona hakuna ikulu msoga

Leo vyombo vya habari mfukoni
Viongozi wa dini mfukoni
Wafanyakazi maandano wakati wa kikwete kwishney mfukoni

Kubomolewa kawaida tu yaani utake usitake hakuna fidia.
 
Lissu hafai hata kuwa Mkuu wa Wilaya. Sababu ni nyingi ila kwa uchache yeye si Mzalendo na licha ya ufahamu wake wa umajumui, lakini anajitoa fahamu kwa maksudi ama kimkakati, na kuamini kuwa maendeleo yetu bado yanategemea utegemezi wa kiakili na kifedha kutoka kwa mabeberu.

Ndio maana yupo radhi kutetea mirija ya mabeberu ( kwenye mikataba hovyo ya madini), kutoa siri za nchi kwa mabeberu, bila kujali athari zake kwa mustakabali wa nchi.

Kwa ukibaraka kama huo, iwapo kwa bahati au kwa ulevi tu wa kifikra, akapata fursa ya kuingia Ikulu ni hapana shaka tutarudishwa utumwani kwa mlango wa mbele kabisa, na hivyo kuchambia mafanikio ya Uhuru wetu yaliyopatikana kwa jasho la damu, tangu enzi zile za vita vya Majimaji, akina Mangi Meri, Mkwawa, Milambo nk.

Ubinafsi na uroho wa madaraka km wa Lissu et al, unawafanya wajiaminishe na kutaka kuwaaminisha wengine kuwa demokrasia ya kimagharibi ndio muarobaini wa matatizo ya nchi yetu, na kwa kudhani kuwa na uhuru tu kubwabwaja bila ya mipaka ndiko kunakoweza kutuleta shibe, maendeleo na kutuja mapeni mifukoni ni kujipumbaza kiakili.

Nchi inahitaji kufunga mkanda na kuachana na ukoloni mamboleo na kutengeneza mustakabali huru na wa dhati utakaotuwezesha SISI wenyewe kupanga njia na mbinu za kutuletea maendeleo yetu kwa kutumia vizuri fikra, utashi na raslimali zetu. Dr John Pombe Magufuli ameshaonyesha njia...Tumfuate.
 
Atumie mawakili wa ndani muwafutie uwakili kama Fatma Karume??? Mpige mabomu ofisi zao kama mlivyofanya kwa kampuni ya Imma advocates???!

Lissu kawashika pabaya sana Mataga na Lumumba!!! Poleni sana, jiandaeni tu kumkabidhi nchi hapo October kwa amani, maana hakuna namna!!

Kabisa una hakika ana shinda? Au unajipa moyo?

Dhambi hizi mkuu

Kama unaweza danganya nafsi yako, ...wewe katili
 
1. Anaijua sheria ataongoza taifa kwa misingi ya haki

2. Hana tamaa ya mali, hatokimbilia kujenga mahekalu kwa na kiwanja cha ndege cha kimataifa kijijini kwao Mahambe, hawezi, hawezi hubadili msitu wa Mahambe kua hifadhi ya wanyama.

3. Ni muelewa mzuri wa masuala ya kimataifa, atasaidia kuimarisha diplomasia ya kimataifa

4. Hatorusu kuingia mikataba ya kinyonyaji kwa sababu ni mjuzi wa sheria

5. Hana rekodi ya ufisadi wala tuhuma zozote rushwa. Ni mwadilifu

6. Haturuhusu DPP kuchelewesha kesi mahakamani kusababisha mrundikano wa wafungwa

7. Hatoruhusu ubambikiaji wa kesi na uonevu unaofanywa na baadhi ya polisi

Sasa tunachagua Rais au tunachagua judge mkuu?
 
Lissu hafai hata kuwa Mkuu wa Wilaya. Sababu ni nyingi ila kwa uchache yeye si Mzalendo na licha ya ufahamu wake wa umajumui, lakini anajitoa fahamu kwa maksudi ama kimkakati, na kuamini kuwa maendeleo yetu bado yanategemea utegemezi wa kiakili na kifedha kutoka kwa mabeberu.

Ndio maana yupo radhi kutetea mirija ya mabeberu ( kwenye mikataba hovyo ya madini), kutoa siri za nchi kwa mabeberu, bila kujali athari zake kwa mustakabali wa nchi.

Kwa ukibaraka kama huo, iwapo kwa bahati au kwa ulevi tu wa kifikra, akapata fursa ya kuingia Ikulu ni hapana shaka tutarudishwa utumwani kwa mlango wa mbele kabisa, na hivyo kuchambia mafanikio ya Uhuru wetu yaliyopatikana kwa jasho la damu, tangu enzi zile za vita vya Majimaji, akina Mangi Meri, Mkwawa, Milambo nk.

Ubinafsi na uroho wa madaraka km wa Lissu et al, unawafanya wajiaminishe na kutaka kuwaaminisha wengine kuwa demokrasia ya kimagharibi ndio muarobaini wa matatizo ya nchi yetu, na kwa kudhani kuwa na uhuru tu kubwabwaja bila ya mipaka ndiko kunakoweza kutuleta shibe, maendeleo na kutuja mapeni mifukoni ni kujipumbaza kiakili.

Nchi inahitaji kufunga mkanda na kuachana na ukoloni mamboleo na kutengeneza mustakabali huru na wa dhati utakaotuwezesha SISI wenyewe kupanga njia na mbinu za kutuletea maendeleo yetu kwa kutumia vizuri fikra, utashi na raslimali zetu. Dr John Pombe Magufuli ameshaonyesha njia...Tumfuate.
Kapongo, uzalendo upi unauongelea ?!
1. Nani waliogawa madini hayo kwa hao mabeberu kwa mikataba mibovu ya miaka 100 ?!
2. Ni nani anayevunja mikataba hiyo bila utaratibu , na kupelekea nchi kushtakiwa ? . Hao ndiyo wazalendo kweli ??!!
3. Aliyepiga kelele toka Mkapa anawapa hao jamaa migodi ni nani kama si Lissu ?!
 
ila watanzania tungekua na akili kwakweli mahakama kwa mara ya kwnza zingeenda kua hurua na haki ingetendeka ndugu zetu wanasota rumande tuwaonee huruma...lakin Sioni CCM wakibadilika na kutuheshim wapiga kura
 
Kusema kweli tunajisumbua tu.. Tundu Lissu hawezi kuwa Rais sio kwasababu kura hazitatoshaa bali ni kwasababu ya corwadice ya Watanzania.
Bonge moja la point. Ndiyo maan wakati mwingine namuonea huruma Anko Tundu Lisu. Kutetea maskini ni kazi sana. Maskini wengi ni wapumbavu sana.
 
Hawezi kuwa raisi. Kamwe hatokuwa, maana wenye uelewa na utambuzi (wasomi, wafanyabiashara, wakulima wakubwa,na raia wa kawaida) wa kiongozi bora ni wachache sana. Waliowengi ni wajinga wanaosikia sauti ya wengi na kufwata upepo. Pia Tundu lisu hafahamiki maeneo mengi ya vijijini na wakati wa kampeni pekee hautoshi kumtambulisha.
 
Mkuu hii ni level nyingine ya uhalisia sio ile ya mange ya kusadikika.
Siku Lissu anaingia nchini Jana yake tamko LA Polisi lingesababisha kila MTU kuingia mvunguni but what happened?

Issue ya Bomang'ombe kwa Sabaya ilikuwa mtego wa kuharibu zoezi zima la Lissu kutafuta wadhamini. Damu ingemwagika pale nyumbani kwa Mbowe picha ingesoma vibaya lakini Chadema waligundua hill na wakaruka kihunzi hicho.
Mungu atupe uzima, October sio mbali tutarudi hapa..
 
Ndio hatujawahi tangu Taifa hili liwe huru.

Tatizo siyo kuwekewa damu Tatizo Ni huyo yeye kuongea mbele za vyombo vya habari kuwa; "Mimi Ni mkenya mwenzenu kwasabab Nina damu nyingi ya wakenya" TL.

Je huyu ndo rais anaetufaa kuongoza nchi ya kizalendo Kama Tanzania?
Sisi ni waafrika na Afrika ni moja. Ile ni kauli ya kujenga umoja tuu, mbona kama tungekuwa tunaendekeza uadui hivyo huyu Mrundi angepata cheo chochote cha juu? Maana TL ile ni kauli huyu ni uhalisia!
 
Bonge moja la point. Ndiyo maan wakati mwingine namuonea huruma Anko Tundu Lisu. Kutetea maskini ni kazi sana. Maskini wengi ni wapumbavu sana.
Watu wanajipa matumaini ambayo hayapo kabisa..

Bila tume huru na Mahakama huru ni kazi bure tu.. Hakuna Mtanzania ataingia barabarani kama wanavyojidanganya, Watanzania ni wanafki na waoga mno.

Wajifunze kwenye maandamano yao kuanzia UKUTA na mengineyo kuna waliyofaulu??
 
1. Anaijua sheria ataongoza taifa kwa misingi ya haki

2. Hana tamaa ya mali, hatokimbilia kujenga mahekalu kwa na kiwanja cha ndege cha kimataifa kijijini kwao Mahambe, hawezi, hawezi hubadili msitu wa Mahambe kua hifadhi ya wanyama.

3. Ni muelewa mzuri wa masuala ya kimataifa, atasaidia kuimarisha diplomasia ya kimataifa

4. Hatorusu kuingia mikataba ya kinyonyaji kwa sababu ni mjuzi wa sheria

5. Hana rekodi ya ufisadi wala tuhuma zozote rushwa. Ni mwadilifu

6. Haturuhusu DPP kuchelewesha kesi mahakamani kusababisha mrundikano wa wafungwa

7. Hatoruhusu ubambikiaji wa kesi na uonevu unaofanywa na baadhi ya polisi
1. Lisu hana uadilifu - lilidhihirika katika sakata la kina kitila kinyume kabisa na anavyombagaza mh jpm
2. LISU hana misimamo-lilidhihirika kipindi cha Lowasa
3.Lisu hana maono-limedhihirika ndani ya Taasisi ya CDM Ndio maana hakuna hats proposal moja kutoka kwa Lisu akielekeza chama kunako maendeleo
4.Lisu Ana misimamo mikali-hili limedhihirika wazi kuhusu misimamo wake juu ya muungano na kuwatusi waasisi wa taifa mfano baba wa Taifa
 
Serikali ya awamu ya awamu ya 6 licha ya kuzidi kujikita ktk kuyaendeleza mambo mazuri yaliyokwisha kuanza kutekelezwa kupitia kodi za wananchi, kwa namna ya pekee itunge sera rafiki zenye uwezo wa kuwakwamua kiuchumi wakulima maskini na hasa wengi wao waishio vijijini.

Awamu hii isije kutuletea tena miradi mingine mikubwa yenye kugharimu fedha nyingi kwa gharama ya kuwanyima haki makundi mengine ya watu mathalani wafanyakazi. Serikali iwe tayari kutoa majibu ya uhakika hata kama yatabeba ukweli mchungu, kuliko kutafuta visingizio vingi na porojo tupo zenye kubeba ahadi za uongo.View attachment 1540781

Miradi mikubwa kihivyo haikuwepo vipindi vya awamu za nyuma na bado wanafunzi walisomea chini ya miti na madarasani kulikuwa hamna madawati, watoto walikaa chini sembuse hawa waliokaa juu ya tofali na darasani. Hamna ushahidi hata hivyo hii picha ni yalini.

Baadhi ya watu wanaakili za kusahau kama kuku, mara tu mmeshesahau ule wimbo uliokuwa unaimbwa na wapinzani kutwa kucha kuhusu tatizo la madawati? Baada ya JPM kuingia madarakani 2015 hata mwaka haukuisha kelele za madawati zikafutika.

Hili la madawati ni moja ya mambo makubwa na mafanikio ya kupigiwa mfano wa serikali ya awamu ya tano. Ni kigezo kimoja wapo cha umahiri wa utendaji wa serikali hii. Serikali hii imefanya mengi sana mpaka mengine yanasahaulika likiwemo la madawati.
 
wewe unajikuta heti huishi kwa Amani.
Kwa maisha gani uliyonayo yani wewe hata ukienda kulala polini ukiondoa kudhuliwa na wanyama wakali utabaki salama kabisa.

Mtu hujawahi hata kusikia mlio wa bunduki tangu uwepo hapa Tanzania ndo unakuwa wa kwanza kuleta unafiki wako hapa.

Siasa Ni Mbaya Sana .
kweli siasa ni mbaya maana hata unayoyaandika yanaonyesha una hisia za kinjaa tu.
 
Mtatatizo makubwa mara ngapi mbona tuna mtatizo makubwa tayari? Ccm must go!

Ona wewe nanga wa Lissu, ukisema hivi Iraq, Ufughanistan, Somalia ,Yemen kwa mfano watasema nini? Hawa nao huko nyuma waliwachekea waabudu ushoga wa kwao waliokimbilia huko Ulaya na USA kama huyu Lissu wa kwetu hapa. Wakimbizi hawa wakarudi kutoka huko USA na Ulaya wamenyweshwa sumu ya mbinu za kufarakanisha raia wa nchi zao, ambacho ndicho Lissu anafanya sasa ,raia wanzao wakawa shadadia na kuwa chekea kama wewe na baadhi ya watanzania sasa wanavyo fanya kwa Lissu sasa. Matokeo yake nchi hizo zimegeuka jehanamu na raia wake wamebakia na kilio na kusaga meno.

Sisi Tanzania tuna bahati ya kujifunza kitu kutokana na mataifa haya na kwa sababu hiyo Lissu hatachekewa na kuachwa atuingize jehanamu ya duniani.
 
Kwa Komredi Lissu haya yanawezekana;
Demokrasia ya kweli
Utawala wa sheria na kufuata katiba
Hotoba zenye weledi
hakuna ukanda wala ukabila
haki sawa kwa wote
Ukweli na uwazi.
hakuna cha 'watu wasiojulikana'
 
Back
Top Bottom