Kwanini utajiri wa watu wa Nyanda za juu Kusini, huwa hauchechemui watu?


Northern Highland ni Punje ,South Highland ni NGENDE......
 

Huyo jamaa alitikisa miaka ya 90 huyo Tajiri nasikia alikuwa na "DRUM" akawa anajipigia mademu wa zanaki ,kisutu na jangwani.
 
Unatunza pesa miaka 15 ili uzipeleke wapi? Mbona wakifa hatuoni hata vizazi vyao vikiendelea na utajiri huo?
Hiyo ni changamoto sana na inapelekea hata imani kuwa watu waanatumia nguvu za giza zipate mashiko. Majuzi RC wa Njombe akiongea na wafanyabiashara aliwashangaa kuwa mtu anakufa wanakuta benki ana 500M hadi 600M, lakini maisha yake yalikuwa duni sana na ya kujinyima, hata nyumba tu ni yakuunga unga. Hawa wa hivi wapo ila inawezekana ni exposure ndogo tu ya maisha, wanachojua na kinacho wamotivate ni kutafuta pesa tu bila ya kuweka misingi imara ya hiyo pesa kuendelezwa.
 
Vizazi vinavyofuata hujua matumizi na si kutafuta pesa.Wanakuwa hawana morali na mbinu za kuendeleza walichoachiwa.
Hata mali yenyewe hawaikuti. Nitakupa mfano wa Rodrick Mahenge..Kwenye miaka ya 1990s alikuwa ana miliki mabasi ya SAFINA zaidi ya 20 yakisafiri kati ya Dar- Mbeya, Iringa na Songea. Alikuwa ndiye mshindani mkubwa wa Scandinavia. Alikufa mwaka 2000 na watoto wake sikuwaona na chochote
 
Watu wanaishi dingii acha stori za vijiweni
Nitajie Mkinga mmoja anayeishi maisha kama binadamu sawa na hela alizonzo? Yule mwenye Paradise Hotel pale Soweto anaitwa Kasisi, alikuwa anaishi nyumba ya tope kule Ilemi hata haikuwa na umeme. Ulishamuona Shaban Chawe (Fresh ya Shamba) siku hizi? Zile mali ziko wapi? Shaban Chawe anapanda bodaboda, mtu ambaye miaka ya 1990 alikuwa anaendesha Mercedes Benz na akimiliki ma Scania na mabasi siyo chini ya 10
 
Halafu haohao imani yao ipo kwenye ushirikina kwamba upo ila waambie kuna nguvu za MUNGU uone watakavyokupinga.
 
Huko kaskazini huwa hawafilisiki?
 
Niwakumbushe tu Wakinga siku hizi wanapeleka watoto wao shule nzuri. Na mfumo huu ulianza mwishoni mwa miaka ya tisini na mwanzoni mwa miaka ya 2000. Wakati huu baadhi ya wazazi waliwekeza kwenye kupanda miti kwenye maeneo yoye yasiyo na rutuba kwa mazao wakiendelea kuwasomesha watoto wao kupitia biashara wanazofanya. Miaka hiyo ya nyuma ilikuwa ngumu kuwakuta wakinga kwenye taasisi za serikali au binafsi kwa wingi kama ilivyo kwa Wanyakyusa, Wachaga, Wahaya na makabila mengine ukiachana na yule mzee wa degree kumi na mbili Tuntemeke Sanga. Huyu mzee ndiye aliyesisitiza umuhimu wa Elimu kwa famiĺia za kikinga.

Watoto hawa wa Kikinga wamesoma mpaka vyuo vikuu nchini na ughaibuni. Walipomaliza masomo yao ndio tumepata jamii ya vijana kama Mbunge Festo Sanga, Fred Vunjabei kutia ndani kaka zao waliowatangulia pamoja na wadogo zao ambao wametapakaa kwenye taasisi mbalimbali za elimu. Kizazi hiki kinafanya biashara tofauti na wazazi wao. Hawa ni wa kidigitali. Kwa sababu ya elimu wanafuata mzigo China na Dubai na kuja kutulangua nchini. They are making big money kutokana na mtaji waliochiwa na wazazi wao. Jaribu kufikiria deal la vunjabei na Simba bila figisu angekuwa anatengeneza pesa kiasi gani.

Uchawi na pesa ni ujinga mtupu. Kama ni mvivu na huna self controls ya matumizi ya pesa hata upewe pesa kiasi gani utakuwa maskini wa kutupwa tu. Wakinga wanainvest on both formal and informal education kwa watoto wao.
 
Kwenye shule hakika wanawasomesha sana watoto wao siku hizi, tena shule nzuri kabisa O-levle na A-level
 
Fredy vunja bei
 
Watanganyika wengi bado wajinga sana. Mtu dunia ya leo anaamini kuna utajiri wa kishirikina? How stupid can one be?

Wakinga wanachofanya ni kubana matumizi tu ambayo ni universal principle ya biashara yeyote ile duniani iwe kubwa au ndogo. Anakuja mtu mjinga anayewaza bata Monday to Mondaya anasema eti uchawi. So stupid.

Kufananisha utajiriwa wa Bakhresaa au Dewji na mkinga mwenye kagorofa kamoja alikojengwa in 20yrs nao ni ujinga wa kiwango cha PhD. Mkinga gani mwenye hata robo ya utajiri Bakhressa by eye test?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…