Kwanini waajiriwa wengi hawana utamaduni wa kufanya savings nchini?

Kwanini waajiriwa wengi hawana utamaduni wa kufanya savings nchini?

ubarinolutu

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2012
Posts
2,424
Reaction score
4,954
Nimejaribu kufanya tathmini na nimegundua watanzania hasa hawa waajiriwa wa Serikalini hawana tamaduni za kutunza pesa, Wazungu wanaita savings.

Ni vema watanzania wengi tukaanza kupiga mfumo wa Wazungu kuwa unapopata kamshahara kako basi angalau asilimia 20 itunze, halafu ndo uanze matumizi kwa hiyo 80 iliyobaki. Hali hii ya kutotunza pesa imekuwa mbaya kiasi kwamba mtu amefanya kazi miaka 10 lakini akisimamishwa kazi Mwezi mmoja anageuka kuwa omba omba, na anashindwa kuendesha familia hata kwa miezi miwili Bali ni mizinga tu.

Hali hii pia inachangiwa na ugonjwa unaoitwa spending/shopping addiction yaani ukipata pesa unakuja na kimuhemuhe Cha kuzitumia. Pia kutunza pesa kwa waajiriwa ni changamoto wengi wakisema extended family zinawanyonya sana kiasi kwamba huwezi kutunza shilingi kumi.

Wafanyabiashara Tanzania kwenye hili wanajitahidi sana, na wengi ni watunza pesa wazuri kuliko waajiriwa.
Na Hali ya uhakika wa kupata pesa kila mwisho wa Mwezi unafanya watu kubweteka.

Ukitunza pesa itakusaidia wakati wa emergency na kukuondolea aibu ya kuomba omba pindi unapopata na shida.

Mnaonaje wadau, je ni muhimu kutunza angalau asilimia 20 ya mshahara wako wa Mwezi au ni kuzitandika zote?
 
Kipato Tsh 500,000. Mahitaji Tsh 700,000.
Hapo savings inatoka wapi?
Savings inaweza kupatikana iwapo baba na mama wanaoamka asubuhi kwenda kazini wanagawana majukumu... Baba akilipia umeme, mama alipie maji!
Tatizo wanawake wengi siku hizi ni goi goi. Kazi za nyumbani anatakiwa azifanye yeye. Basi kama yeye kaamua kwenda kazini kutafuta basi mama ndio alitakiwa amlipe house girl mshahara kwa kumsaidia majukumu yake lakini kinyume chake unakuta baba ndio anamlipa house girl mshahara. Huu ni unyonyaji.
Kwenye familia za kiafrika, baba ni mtu anayenyonywa sana kwa kuwa yeye ndie anayebebeshwa mzigo mkubwa wa kuendesha familia hata kama mama ana kipato kizuri unakuta contribution yake ni ndogo sana...
Ndio maana nawafurahia waarabu walioamua kuwa 'mama awe ni mtu wa kukaa nyumbani'! It saves cost.
Piga picha mtu anakaa Tegeta, ana mke anafanya kazi Posta, unakuta badala ya mke aweke mafuta kwenye gari yake kwa mshahara anaopata kazini, baba wa watu anajipiga hapo unakuta kiwese kinamgharimu laki tatu. Pia house girl anamgharimu laki.
Unaona! Kama huyu mama angekaa tu nyumbani huyu baba wa watu angeokoa Tsh laki nne! Ya mafuta na ya kumlipa house girl... Hivyo kumfanya awe na savings...
 
Nimejaribu kufanya tathmini na nimegundua watanzania hasa hawa waajiriwa wa Serikalini hawana tamaduni za kutunza pesa, Wazungu wanaita savings.

Ni vema watanzania wengi tukaanza kupiga mfumo wa Wazungu kuwa unapopata kamshahara kako basi angalau asilimia 20 itunze, halafu ndo uanze matumizi kwa hiyo 80 iliyobaki. Hali hii ya kutotunza pesa imekuwa mbaya kiasi kwamba mtu amefanya kazi miaka 10 lakini akisimamishwa kazi Mwezi mmoja anageuka kuwa omba omba, na anashindwa kuendesha familia hata kwa miezi miwili Bali ni mizinga tu.

Hali hii pia inachangiwa na ugonjwa unaoitwa spending/shopping addiction yaani ukipata pesa unakuja na kimuhemuhe Cha kuzitumia. Pia kutunza pesa kwa waajiriwa ni changamoto wengi wakisema extended family zinawanyonya sana kiasi kwamba huwezi kutunza shilingi kumi.

Wafanyabiashara Tanzania kwenye hili wanajitahidi sana, na wengi ni watunza pesa wazuri kuliko waajiriwa.
Na Hali ya uhakika wa kupata pesa kila mwisho wa Mwezi unafanya watu kubweteka.

Ukitunza pesa itakusaidia wakati wa emergency na kukuondolea aibu ya kuomba omba pindi unapopata na shida.

Mnaonaje wadau, je ni muhimu kutunza angalau asilimia 20 ya mshahara wako wa Mwezi au ni kuzitandika zote?
Hili limesemwa sana na watu tofauti several times. Wanajua ila wengi wao ujuaji ni mwingi na non-budget planning.

Kwa hiyo bwasheee usione umeleta new topic/thread humu, hii ni old slogan. Tuwape elimu/uelewa ili wawe vizuri kiuchumi.
 
Hili limesemwa sana na watu tofauti several times. Wanajua ila wengi wao ujuaji ni mwingi na non-budget planning.

Kwa hiyo bwasheee usione umeleta new topic/thread humu, hii ni old slogan. Tuwape elimu/uelewa ili wawe vizuri kiuchumi.
Ni kweli, Ila ni muhimu watu wakaelimika Mara kwa Mara juu ya jambo hili
 
Mshahara wenyewe mdogo mkuu hautoshi hyo savings itafanyika vipi.
Wengi Wana usemi huo huo, anaepokea 500k, anaepokea 1M, anaepokea 2M. Wote wanakuambia mshahara kidogo hatuwezi kusave, Ila Kuna mtu alikuwa anaepokea laki 6, alikuwa anajibana anasave, baadae umesaidia sana na maisha yamebadilika, kwani alisevu akainvest
 
Back
Top Bottom