Kwanini Wakili Mwabukusi na wenzake wanastahili kuungwa mkono

Kwanini Wakili Mwabukusi na wenzake wanastahili kuungwa mkono

Mbona anafanya harakati zake kwa kushambulia wenzake wanaofanya zao kupitia vyama vyao?
Anapanga , anaamua anaweka ratiba na kupelekea wengine ili wafuate alichoamua.
Yeye na kichwa chake ndiye Halmashauri kuu, ndiye Kamati ndogo ya Halmashauri Kuu, Yaye ndiye Kamati Kuu. Wenzake wana uzoefu, yeye bado ni toddler.
Anayoyataka sasa wenzake walishayafanya mara nyingi tu back then.
Anapaswa kujifunza kujadiliana na kusikilizana pia awe tayari kupoteza.
Ili jambo lako lifanikiwe haupaswi kuwa mbinafsi.
Unaweza ukawa na vision, mission na objectives zako nzuri tu, ukishakaribisha watu ili mshirikiane, wataanza kuzipangua ibjectives moja mpaka nyingine, wataingia kwenye mission kote watasambaratisha, muda wote unatakiwa uwe mvumilivu, as long as Vision is still intact.
Sasa watu ukigusa tu objective ya kwanza, vita inaanzia hapo, maana kwenye objectives mdipo kwenye ulaji (pesa), ndipo kwenye ujiko (visibility) , ndipo penye connections, kwa kifupi pana vitu vingi vya kuweza kumpa mtu vingi na kubadili kabisa maisha yake binafsi huku vision , wakati mwingine vision vikibaki vipovipo tu.
Umeeleza vema sana...unfortunately not many will read and comprehend this!
 
Ni sawa, ila lazima tuone kwa vitendo na sio maneno matupu. Binafsi sijaliona hilo ila bado nangojea. Nilishauri nini cha kufanya. Huenda wahusika bado wanatafakari.

Ninaamini unajua tumedhamiria kweli kweli. Hii si ngoma ya vyama. Ushauri wote unakaribishwa.

"Maneno matupu hayavunji mfupa.

Kina Mwabukusi wanastahili kuungwa mkono, siyo kubagazwa."

Walipo tupo!
 
Mwabukusi ndio kaharibu hii ajenda alipoanza kuishambulia vyama vya upinzani akijiona yeye ndio mpinzani halisi. Akasahau kuwa wakati wenzake wanalimwa risasi na kuharibiwa Mali zao alikuwa kimya.
 
82.3% ya Wafuasi wa Chadema wanamuunga mkono Dr Slaa akiwemo Tundu Lisu na Mnyika

Sasa Mbowe na Mrema kila wakifikiria hilo wanamuona Mwabukusi ni hatarishi kwa Maslahi yao

Wewe ni ibilisi mchonganishi. Na hiki ndicho unachokitaka.
 
Mwabukusi ndio kaharibu hii ajenda alipoanza kuishambulia vyama vya upinzani akijiona yeye ndio mpinzani halisi. Akasahau kuwa wakati wenzake wanalimwa risasi na kuharibiwa Mali zao alikuwa kimya.
Kwenye siasa kupishana mawazo huwa kupo tu hayo tuyaweke nyuma yetu tugange yajayo sasa hivi sote tunaelekea Kanda ya Nyassa.

Mbeya moja
 
We jamaa una kichwa kizito sana. Slaa ameondoka Chadema kabla Magufuli hajawa Rais.Huko kuongwa ni kupi?Kati ya Mbowe na Slaa nani msaliti wa mapambano ya ukombozi?Mbowe ndiye aliyemleta Lowasa kubwa la mafisadi Chadema. Ulitaka Slaa naye azunguke nchi nzima kumnadi Lowasa na kusema sio fisadi?Shida Mbowe kawashika ufahamu hadi hamjui nani jinamizi huko kwenye chama chenu.

Wewe ndio mnafiki. Huyo Lowassa yupo CCM alipokuwepo Dr Slaa, mbona hakuama kipindi hicho mpaka ubalozi ulipotolewa kwake?. Slaa haaminiki hata afanyeje.
 
Chadema na wafuasi wao mkubwa saizi ni Akina Mwabukusi na Sukuma gang na sio CCM.Nikisema niki sio Chama bali genge la wahuni tuwe tunaelewana.

Wewe ndio muhuni, punguza dharau. Kauli ya Mwabukusi kwa vyama upinzani unadhani Ina Afya. Tatizo kila kukicha mnatafuta visababu vya kijinga ili kuishusha CHADEMA. Slaa alipomdhihaki Mbowe haukuona shida, ila leo unataka CHADEMA iwafuate watu waliokuwa CCM.
 
Wapi Mwabukusi kamtaja mtu. Una maana hawa wanaong'aka hIvi ndiyo wataka ubunge na ruzuku?

Hiyo kauli haikuwa na Afya, na ndio imeleta shida zote. Slaa alitaka kuiua CHADEMA kwa mikono yake sema akashindwa, Leo anataka aanze kuipangia CHADEMA Cha kufanya. Au mmesahau press conference zake 2015 na alipomaliza ubalozi kuhusu CHADEMA, Mbowe na katiba mpya?.
 
SIASA anazofanya Mbowe na genge lake zimepitwa na wakati na hazina impact yyt kwa Taifa hili chawa wa Mbowe mlijue. Hatutaki Siasa za kiwabembeleza watawala utadhani kufanya siasa ni hisani ya chama tawala. Tunataka SIASA za kuwawajibisha watawala pale wanapojiona wako juu ya katiba na sio SIASA za kuwabembeleza eti tupo kwenye maridhiano. Mnaridhiana nini na CCM?Wanauza bandari nyie mnaleta porojo za maridhiano, serious?Mnaacha kuungana na wanaopambana jino kwa jino na wezi nyie mnakuja na porojo za tuna ratiba zetu,mko serious?Toka mmeanza hizo operation mmeona CCM wakiangaika kujibu au kuwazuia?Lakini vipi hili valangati la akina Mdude?Hamuoni CCM wanakereka sana na SIASA za akina mdude kuliko zenu?

Acha zako, kwa hivyo wewe na wana CCM wenzako mjaze wabunge bungeni halafu uwajibikaji afanye CHADEMA?. Yani wenye mamlaka muwaweke kwa wingi kutoka CCM halafu lawama za uwajibikaji muwape CHADEMA, huku wabunge wa CCM waliojaa bungeni na halmashauri zote za CCM nchi nzima , na wenyeviti wa CCM wamejaa nchi nzima, mnawalamba miguu. Punguza unafiki.
 
Mwabukusi ndio kaharibu hii ajenda alipoanza kuishambulia vyama vya upinzani akijiona yeye ndio mpinzani halisi. Akasahau kuwa wakati wenzake wanalimwa risasi na kuharibiwa Mali zao alikuwa kimya.

Mwabukusi hakumtaja mtu. Labda tusaidiane kupeana taarifa zaidi. Kulikoni kuweka maneno yoyote ambayo hayakutamkwa naye?

Pia, hata kama angemtaja yeyote, nini hicho cha kuhalalisha kuacha kuunga mkono jitihada za wazi hizi:

Jitihada za kina Mwabukusi ni zenye mlengo wa kuwakabili maadui zetu kwa vitendo.

Kina Mwabukusi hawaongelei agenda za vyama. Kina Mwabukusi wanaongelea agenda za wananchi.


Kwamba Mwabukusi kakigusa nini hicho au nani huyo kuleta awaye yote kughairi agenda za wananchi?
 
Mwabukusi hakumtaja mtu. Labda tusaidiane kupeana taarifa zaidi. Kulikoni kuweka maneno yoyote ambayo hayakutamkwa naye?

Pia, hata kama angemtaja yeyote, nini hicho cha kuhalalisha kuacha kuunga mkono jitihada za wazi hizi:

Jitihada za kina Mwabukusi ni zenye mlengo wa kuwakabili maadui zetu kwa vitendo.

Kina Mwabukusi hawaongelei agenda za vyama. Kina Mwabukusi wanaongelea agenda za wananchi.


Kwamba Mwabukusi kakigusa nini hicho au nani huyo kuleta awaye yote kughairi agenda za wananchi?

Nani hamuungi mkono mwabukusi?. Kauli yake ndio inaukakasi. Na akiendelea watu watapungua.
 
Hiyo kauli haikuwa na Afya, na ndio imeleta shida zote. Slaa alitaka kuiua CHADEMA kwa mikono yake sema akashindwa, Leo anataka aanze kuipangia CHADEMA Cha kufanya. Au mmesahau press conference zake 2015 na alipomaliza ubalozi kuhusu CHADEMA, Mbowe na katiba mpya?.

Mkuu, movement ya kina Mwabukusi inao Chadema wengi tu mle.

Kwanini kuendeleza mawazo ya ramli ramli haya yanaendekezwa? Humu ndimo ma CCM yanakopitia.

Kulikoni kuwahukumu watu kwa hisia?

Tuwahukumu watu kwa wanachosema siyo kwa tunavyodhani. Huo ndiyo ustaarabu.

Wachawi wetu ni wapiga ramli hawa.
 
Mwambukusi kajichanganya tu hatakiwi kabisa kuambatana na slaa huyo ni yuda, uzuri wa Chadema wanachonga kinyago wenyewe na kikiwazinguwa wanakibomoa wenyewe

Maana yake Chadema ni mafundi wa kujenga na kubomoa pia wanajua anayebisha akamuulize shemasi wa kipindi kileee kule Twitter kwa wakati huo
 
Nani hamuungi mkono mwabukusi?. Kauli yake ndio inaukakasi. Na akiendelea watu watapungua.

Sentence yako ya mwanzo kama swali ni njema sana.

Kwa hakika ni mwenda wazimu tu ndiye atambagaza Mwabukusi na wenziwe kwenye agenda zao hizi.

Adui yetu ni mmoja.

Kauli ipi moja yenye ukakasi hiyo na labda hata kwa nani? Tushughulikie kauli hiyo au kama kweli zipo.

"Hatuwezi kutupa maji ya kuoga pamoja na mwana!"

Agenda za wananchi haziwezi kufanyiwa ajizi.

Mwabukusi na wenziwe ni mwendelezo mzuri wa ukombozi usioweza kuharamishwa ki reja reja.
 
Mkuu, movement ya kina Mwabukusi inao Chadema wengi tu mle.

Kwanini kuendeleza mawazo ya ramli ramli haya yanaendekezwa? Humu ndimo ma CCM yanakopitia.

Kulikoni kuwahukumu watu kwa hisia?

Tuwahukumu watu kwa wanachosema siyo kwa tunavyodhani. Huo ndiyo ustaarabu.

Wachawi wetu ni wapiga ramli hawa.

Mimi pia naunga mkono hizo harakati. Ila aipendezi kukebehi wengine wenye harakati zao.
 
Back
Top Bottom