Kwanini wanafunzi wasianze kidato cha kwanza na michepuo ya sayansi (Physics, Chemistry) au arts kwa kuzingatia matokeo ya Darasa la Saba?

Kwanini wanafunzi wasianze kidato cha kwanza na michepuo ya sayansi (Physics, Chemistry) au arts kwa kuzingatia matokeo ya Darasa la Saba?

Unaruhusiwa kumuamisha mwanao Mkuu..

Ila hakuna elimu bora duniani kama inayopatikana shule za ufundi.
Blogger sio kweli ila ngoja nikupe tofauti za waliosoma shule za ufundi na shule za kawaida ila mizania yangu itajikita kwenye aliye na FTC au Diploma na mwenye degree.Tuchukulie kwenye somo la ujenzi au CIVIL
Waliosoma ufundi FTC au Diploma wako very well kwenye know HOW
Waliosoma shule za kawaida wakasoma hadi degree wako vizuri kweye know WHY
Mtu wa FTC ukampa mchoro umefanya design kila kitu ukampa materials ya kazi atakufanyia kazi nzuri mno mambo ya WHY hayajui wala sio issue zake wala levels zake.
Aliyesoma civil engineering yeye kabla jengo halijanyanyuka atakaa mezani ataweka mambo sawa na kujua kitatumika nini na nini ila kiukweli kiutendaji hayuko vizuri kuliko mtu wa FTC unaweza kuta hata kushika kijiko hajui ila anajua theory ya kushika kijiko.
Ila hili halimfanyi aliyesoma Civil engineering kuwa ni mweupe la hasha.Mambo yote makubwa sana yanaanzishwa na watu waliobobea kwa elimu kubwa kisha wa level za chini wanakabidhiwa kiutendani na kazi inakwenda huo ndo mgawanyiko wa kazi.
Hili limefanya sehemu nyingi FTC waonekane wako vizuri hata migodini kuliko wenye shahada ila kiukweli kabla mgodi kuanza waliofanya setting design na kila kitu hadi kufikia hatua ya kuchimba ni watu wenye elimu zilizotukuka.
Ness anayempiga sindano mgonjwa au kumfunga kidonda mgonjwa kwa ufasaha hakumfanyi Nesi anaonekane kuwa ni bora kuliko daktari.
 
... lengo la mitihani ya F2 sio tu kuchuja wale wenye uwezo hafifu bali pia kuwawezesha wanafunzi kufanya maamuzi sahihi ya masomo gani ya kuendelea nayo kwani ndani ya miaka miwili waliyojifunza wanakuwa wameshaelewa hatma ya kusoma au kutosoma kitu fulani; ni kipindi muhimu cha kufanya maamuzi ya maisha yao ya baadaye. STD7 bado ni underage kufanya maamuzi ya aina hiyo.
Kama mwanafunzi bado yupo chini ya miaka 18 bado ni underage tu bila kujali yupo darasa la saba ama kidato cha pili. Hii hoja yako haina mashiko mkuu.
 
Kama mwanafunzi bado yupo chini ya miaka 18 bado ni underage tu bila kujali yupo darasa la saba ama kidato cha pili. Hii hoja yako haina mashiko mkuu.
... Mkuu tukienda hivyo utaniambia uelewa wa under 5 hauna tofauti na wa 15yrs kwa sababu wote ni underage! Hujanishawishi graduate wa F2 ni sawa na wa STD7; kwa mabadiliko ya watoto, miaka miwili ni mingi sana.

Na kwa mfumo wetu wa elimu huo mchepuo wa sayansi unaoshauri uanze kufundishwa since STD7 watafundishwa kwa Kiswahili au Kiingereza? Kwa sababu medium of instruction kuanzia F1 ndio Kiingereza huanzia. Confusion!
 
... lengo la mitihani ya F2 sio tu kuchuja wale wenye uwezo hafifu bali pia kuwawezesha wanafunzi kufanya maamuzi sahihi ya masomo gani ya kuendelea nayo kwani ndani ya miaka miwili waliyojifunza wanakuwa wameshaelewa hatma ya kusoma au kutosoma kitu fulani; ni kipindi muhimu cha kufanya maamuzi ya maisha yao ya baadaye. STD7 bado ni underage kufanya maamuzi ya aina hiyo.
Sahihi mkuu.
 
... Mkuu tukienda hivyo utaniambia uelewa wa under 5 hauna tofauti na wa 15yrs kwa sababu wote ni underage! Hujanishawishi graduate wa F2 ni sawa na wa STD7; kwa mabadiliko ya watoto, miaka miwili ni mingi sana.
Mwanafunzi wa darasa la saba na kidato cha pili hawa ni watoto wa rika moja kwa kuwa wamepishana madaraja mawili tu ya elimu hivyo wapo-equivalent katika kufanya maamuzi mkuu...
 
kusoma michepuo hapo si itakuwa tatizo zaidi.
Tunahitaji Scientific Breakthroughs mkuu, and nothing comes with ease. Somo moja lile lile la Sayansi linavunjwa mara tatu na tunapata Fizikia, Kemia pamoja na Baiolojia
 
Lengo la mwanafunzi wa O'level kusoma masomo yote nikupata foundation knowledge ya somo husika ebu fikiria mtoto atakapoanza kidato cha kwanza asisome biolojia, mwisho wa siku utakuta huyo mwanafunzi hawezi ata kujua makundi ya chakula na kazi zake mwilini, mfumo wa kusoma masomo yote kwa vidato vya chini nikumpa mtoto ile general views ya somo husika ambayo itakuwa faida yake mwenyewe katika maisha ya kila siku,
Foundation anaisoma primary.

Kwani wewe shule ya msingi hujajifunza makundi ya vyakula?
 
Kuna hii nimeiona katika baadhi ya mataifa ya west africa, ukianza form one unaanza na mchepuo/kozi ulioomba wakati wa kumaliza elimu ya msingi. Kwa hio unapomaliza kidato cha sita unakua na cheti kinacholingana advanced diploma ya Tanzania.
 
Na kwa mfumo wetu wa elimu huo mchepuo wa sayansi unaoshauri uanze kufundishwa since STD7 watafundishwa kwa Kiswahili au Kiingereza? Kwa sababu medium of instruction kuanzia F1 ndio Kiingereza huanzia. Confusion!
Kwenye bandiko langu kuu nimeandika hivi;

NB: Suala la lugha ya kufundishia kati ya Kiingereza na Kiswahili kwa shule za msingi na secondary sio lengo la mada hii ninaomba tusilizungumzie kwa sasa.
 
Masomo tena 7 yanaulizima gani,mfano mtoto anayeanza masomo ya sayansi physics,chemistry na mathematics ana ulazima gani wa kusoma kiswahili au history tena???
 
All in all, mfumo wetu wa elimu inabid urekebishwe. Tunatumia muda mwingi mno darasani.
 
Apo sidhan kama itakuwa sawa, maana kuna watu primary wanakuwaga vipanga wa mahesebu wakifika secondary wanachemka vibaya sana, na ushahid wa washikaji zangu wengi tu
Ndio nilitaka kukisema hiki ila umenisemea tayari.
Kwa mfano mimi shule ya msingi masomo ya sayansi nilikuwa siyapendi na nilikuwa mdhaifu lakini nilivyofika sekondari nikawa mtabe kwenye masomo ya sayansi na ndio yanayonipa msosi hii leo.
Kwa hyo kufaulu shule ya msingi sio kigezo kabisa na kingine tena cha kufahamu kuwa shule ya msingi ni maandalizi tu hakuna uchambuzi wa kina wa masomo.
 
Back
Top Bottom