Kwanini Watanzania lazima tuweke magrill kwenye madirisha?

Kwanini Watanzania lazima tuweke magrill kwenye madirisha?

Wengi wanaweka grill lakini awaachi escaping zone ikitokea dharura ya moto thus ukitokea unaua familia nzima.Mimi nimeweka escaping zone na members wote wa familia nimewapa shule unabetua tu dirisha linakuwa ngazi wanajump nje
 
Grill sio njia ya kumzuia kibaka endapo nyumba haina uzio.

Nilipanga geto mitaa ya Mecco South(Mwanza) nyumba ilikuwa haina uzio ila ina grills.

Siku nikawa nachati na kinokia changu double line huku nachaji. Kosa kubwa nlilofanya ni kuacha taa inawaka, maana usingizi ulinipitia, nilikuja kushtuka saa tisa usiku chaja inaning'inia simu haipo. chungulia uvunguni hola, cheki kitandani hola, Vibaka wakawa "wamelowa".

Asubuhi nikazunguka dirishani nikakuta wameniwekea line zangu.

Ikapita muda akaja ndugu wa mwenye nyumba akiwa na mkewe walikuwa wana safari, sababu walikuwa na mtoto mdogo anaumwa wakaacha taa inawaka, suruali ya jamaa ilivutwa na vibaka kwa waya toka alipotundika wakachukua hela ambazo walikuwa wazitumie wakati wa safari yao.
 
Mimi kinachoniudhi ni yale maukuta (fence) yanazunguka nyumba marefu kuliko nyumba yenyewe, sijui hata hewa wanapataje huko ndani na yanaharibu sura ya mtaa kabisa
Wengine hawapendi unoko wa Wana mtaa kujua Mambo yao wanaamua kufunga ukuta
 
Back
Top Bottom