Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Tulisha wahi muuliza mkuu wa nchi swali hili na akasema na wala katu hajui ni kwanini hasa tanzania na watanzania ni maskini,.....hata kiranja wake mkuu naye hajui na wala hwajishughulishi kujua kamwe.
 
Hapa kwetu ukionana na mtu kwa mara ya kwanza anakuuliza km umeoa au la!..............
 
TANZANIA NI MOJA YA NCHI MASIKINI DUNIANI.KWANINI SISI NI MASIKINI
1.HISTORIA YA TANZANIA
Tulipata uhuru wetu mnamo mwaka 1961 kutoka kwa uingerenza ndio mwalimu nyerere akawa waziri mkuu wa kwanza mwaka ulifuta ndipo mwalimu nyerere akawa raisi wa kwanza wa taifa hili.kwa maono yangu tanganyika wakati tunapata uhuru hatukuwa tayari kujitawala kama taifa changa ambalo lilikuwa na wasomi ambao hawafiki hata 100 kujitalawa ingekuwa ngumu sana.Tumpongeze nyerere na sera yake ya ujamaa pia nyerere alijitahidi kufungua viwanda vingi lakini vyote vilikufa kutokana na elimu ndogo na kutukujua jinsi ya uongozi naweza kusema taifa lilikimbilia sana kupata uhuru hatukuwa tayari.baada ya hapo sera yetu kubwa ikiwa kusaidia mataifa mengi ya africa yapate uhuru tulitumia mali zetu nyingi kusaaidia hayo mataifa tujiulize ni mangapi yamerudisha fadhila haya ni machavhe ya mataifa tuliyoyasaidia KENYA,UGANDA,ZANZIBAR,SOUTHAFRICA,ZAMBIA na mengineyo.baada ya hapo tukaja kukumbana na vita vya uganda ambayo madhara yake hadi leo yanaonekana vita hivi tulipoteza pesa nyingi sana na unajua taifa linapoingia kwenye vita shughuli nyingine zote za maendeleo husimama na pesa zote hupelekwa kwenye vita.akaja mwinyi kila kitu ruksa akja mkapa na sera za uwazi na ukweli hapo akajaa kikwete na ari mpya kasi mpya nguvu mpya.lakini kusema ukweli ufisadi ulikuwepo toka awamu ya kwanza sema ulikomaa awamu ya pili mpaka sasa umeota mzizi.
2.VIONGOZI WABOVU NA VIPAUMBELE VISIVYOTEKELEZEKA
tanzania ni taifa lenye viongozi wabovu.VIONGOZI WAPENDA ANASA viongozi wanaweka maslai yao mbele kuliko ya wananchi waliowaweka madarakani baada ya kupata uhuru taifa kama taifa halikujenga viongozi wenye maslai ya taifa mbele tulijisahau sana ile cream yote ya nyerere yote baada ya kuisha hatukuwa na watu mbadala wa kuwaweka kwenye uongozi hebu nenda katafuta wale viongozi walikuwa pamoja nyerere maisha yao yalivyo ya kawaida tu.sasa tunajuta unataka kuniambia viongozi ambao hawajasoma hata tanzania watakuja kujua matatizo yetu sis watanzania hapana hakuna.viongozi wenga hawana uchungu na nchi yetu.tufanyaje ili tupate viongozi bora hatuna budi kuanzia chini tuvunje shule zote za kata wanafunzi wote wawe wanachanganywa mfano msukuma akasome moshi mchaga akasome mbeya hapo tutaweza kutengeza viongozi bora somo la siasa na urai lianzie toka shule za msingi.tuwajenge vijana wetu uzalendo toka wakiwa wadogo.taifa limekuwa na sera zisizo tekelezeka mfano sera ujamaa iko wapi,kilimo kwanza,elimu iko wapi.
3.UFISADI
tanzania sasa kuna ufisadi ukubwa wa mali za umma mifano ya ufisadi richmond,epa,rada,meremeta,migodi,samaki na menginenyo
4.watanzania ni wavivu sana wa kusoma hata vitabu tunataka vitu kwa mteremko sana
jinsi kutoka kwenye umasikini
1.taifa lianze kuandaa viongozi kwa njia lizoorodhesha hapo juu sio kila mtu ni kiongozi tunaona kwa ndugu yetu jakaya kikwete tutafanyaje kashakuwa baba yetu kama baba ana kasora na ushajizua kasoro zake unaenda nae taratibu
2.tuwekeze kwenye sayansi na teknolojia
taifa liwekeze kwenye sayansi hatuna watalamu wengi wa sayansi kabisa tuwekeze kwenye research tunaweza kutoka.
tufungue vyuo kam vitatu vikubwa vya sayansi vitatusaidia sana kufika tunakotaka kwenda
3.umeme
tuweke sera nzuri zitakazo hakikisgha umeme unapatikana wa uhakika tuache ujinga tuwekeze kwenye umeme wa upepo,uranium kwa kuwa itaanza kuchimbwa soon,umeme wa baharini,umeme wa gesi serikali iwekeze kwenye umeme nadhani kame tirlioni 3 zinatoshe kabisha kuondoa tatizo la umeme
4.TRA
bado haijanifurahisha ukushanyji wake wa kodi tuwabane makampuni makubwa,wafanyabiashara wakubwa,viongozi,mitandao ya simu,kwanini ziwa viktoria lina mapato makubwa kuliko bahari ya hindi
5.tupanue bandari yetu
bandari yetu ni ndogo ndio sababu watu wanapitisha mizigo nchi nyingine pia msongamano,
6.tuboreshe miundombinu
tujenge barabara nzuru hadi kwa majirani nzetu ili waoitishe mizigi yao kwetu
7.kilimo
tafuta posti yangu tz bila njaa inawezekana
8.bunge na serikali
swali kwanini zanzibar inatoa wabunge ambao wanakaribi 100.wakati ni sawa na jimbo la ubungo idadi ya watu wa zanzibar na ubungo wabunge wa zanzibar wapunguzwe hadi 5 na wasizidi 10.viti maalamu vifutwe havina tija kuna wabunge zaidi ya 100 wa viti maalumu wanamaliza kodi zetu kama ni haki sawa tutenge kwenye kila mkoa ambapo wanawake wenyewe watasimama kama dar tutenge majimbo matatu kwa ajili ya wanawake tu.hakuna haja ya mawaziri 50,wakuu wa mikoa,wakuu wa wilaya.
9.katiba mpya sina mengi maana yameshaongelewa
10.tume huru ya uchaguzi
11.madaraka ya raisi yapunguzwe
12.elimu na huduma za jamii ziboreshwe
ni hayo mengine mtajiza nawatakia weekend njema
wenu katika ujenzi wa taifa fk
 
Hata mimi sijui kwanini Tanzania ni masikini labda nikupe namba ya Kikwete anaweza kuwa anajua.
 
Hata mimi sijui kwanini Tanzania ni masikini labda nikupe namba ya Kikwete anaweza kuwa anajua.

Quinine lakini hata yeye alisema hajui kwa nini tu masikini sasa hata mkimpigia simu jibu atakua hajui !
 
Nilishawahi kuandika gazeti swali hili kwa watanzania wenzangu, nimefurahishwa na mada hii tena isipokuwa wkt huu nikiwa na mtazamo wangu binafsi, kutokana na swali hili....!

Umaskini wa mtanzania unatengenezwa, na master plan au processor wa poverty maker ni serikali, uhsusani katika nchi maskini, kwanza sera ya utawala rahisi ni ule ambao unazingatia umbumbu wa jamii husika, the less education the simpler way to lead, people accepts words of impossibilities, no wonder in a society like tz some one can stand up and say tomorrow i will take all of you tanzanian to amerca, and still this person will be trusted and honored, this is tz, as we have been heard every single day, if you believe this.....! Look at electricity issues...! Dip down it is an issue to be resolved with a month for serious gov't only if they would have priotised regarding an issue has swallowed alot of opportunies, coal mine has been discoverd since 1964, hydroelectrict power has never been stable and it is very known, but believe me... There is moere secret agenda that a resources itself......! Electricity was not supposed to be a problem rather a small challnge for a kin gov't
 
Embu tujiulize, ni vipi kama serikali yetu inge priotise katika mambo machache kwanza, tumekuwa tunajisifia ujenzi wa barabara, sisemi kuwa ni mbaya, hakika na upongeza napongeza pia wizara husika,lkn kama ipo haja ya kushirikishana ktk kutatua matatizo yetu tungekuwa wapi leo? wizara zinachangiana utaalamu kufaniskisha mambo, na kuhusisha wataalamu hata wasio ndani ya serikali, wapo watu ambao kwa hakika wana nia na moyo wa kulifanyia taifa lao kitu ni vile tu hawaja pata nafasi, alafu ifike wakati viongozi wakiri kama kuna kushindwa kwani haita waondolea heshima zao kwani ni dhahiri kuna mambo ambayo yapo nje ya uwezo wao na yanaonekana dhahiri kuwashinda, manung'uniko ya watanzania wengi yanakosesha nchi baraka.
 
Kutokana na wimbi la ufisadi kupamba moto tangu awamu ya pili, watu wengi wanadhania umaskini unaletwa na ufisadi pekee na wanakinai kutofikiria zaidi. Hii si kweli. Ufisadi ni moja tu ya sababu, na pengine inachangia asilimia 10 tu ya tatizo.

Wakati wa Mwalimu ufisadi haukuwa umetapakaa, lakini hivyo hivyo Watanzania waliendelea kuwa maskini. Nadhani wangekuwa maskini zaidi kama Mwalimu angeendelea hadi leo na mfumo ule ule.

Nakaribisha mawazo tufikirie kwa pamoja kiini cha hali yetu. Tukishajua, itakuwa rahisi kujua namna ya kujikwamua. Sisemi kuwa tutarekebisha hali zetu, kwani kujua na kutumia uliyoyajua ni vitu viwili tofauti. Pamoja na hivyo umuhimu wa kujua ni mkubwa. Naanza kwa kueleza sababu nizionazo mimi:

1- (na kubwa) Ni ukosefu wa elimu- kwa maana elimu inayomwezesha binadamu kujua njia za kubadili hali yake. Hii ni tofauti na kwenda shule. Kwenda shule tu si elimu. Shule ipo kwa kumsaidia mtu kufikiri namna ya kubadili mazingira yake, siyo kutoa jawabu lililo tayari. Mfumo wa elimu Tanzania haumpelekei mtu kuwa na uwezo wa kufikiri na kujikomboa na umaskini kwa njia za kisasa. Hivyo basi, ili hali ya WaTZ ibadilike, kwanza ni kutokomeza mtaala wote wa elimu uliopo sasa. Zaidi ya hayo, watoto wote wabakie shule angalau hadi kumaliza Sekondari ya juu.

2-Uongozi mbaya na siasa za kipumbavu (sina la kuongeza)

3- Utamaduni mbeleko: Watanzania wengi wanaishi kwa kutegemea wengine, au wana uhakika kwamba hawawezi kupata shida kiasi cha maafa kwa vile ndugu wapo. Utamaduni mbeleko ndio unaowafanya wengi kutofikiria namna ya kujikwamua

4- Kuuawa kwa kazi za mikono na kazi ndogo ndogo: Wakati nainukia katika miaka ya sabini kulikuwa na kazi nyingi (na michezo) mtu alijifanyia mwenyewe, kama vile ufundi cherahani, ushona viatu, usonara, ufundi saa, unoaji visu n.k. kazi hizi nyingi sasa zimepotea lakini kibaya zaidi ubunifu wa kazi nyingine pia umepotea. Ni kana kwamba watu wamekinai kuwa kwa kila tatizo Mchina ataleta ufumbuzi. Hii imechangia umaskini$

5- Utamaduni wa upweke: Na hii nadhani ni kwa Waafrika wote. Waafrika hawapendi kushirikiana, si kwa kiwango cha nchi au kiwango cha jamii. Jamii nyingi zilizoendelea zimefanya hivyo kwa kushirikiana. Hapa ni lazima kuwepo na mabadiliko ya dhati.

Nitaishia hapo kwanza. Kitu muhimu utakachokiona hapa ni kuwa sababu nyingi za umaskini kwa kweli hazihusiki sana na uongozi au siasa za serikali bali ni discipline (nidhamu) ya mtu. Sikatai kuwa serikali inachangia. Katika mifano mingi ya umaskini Tanzania ni watu wenyewe ndio wasio na mazoea na tabia za kutaka hali bora.

Na wewe jee, una sababu zipi?
 
Nimependa saana na post yako… Ila napingana na assumption yako kua ufisadi unachukua tu asilimia kumi (10) Ni zaidi ya hizo asilimia... katika suala zima la kueleza kua nini kiini cha Umasikini Tanzania… Labda kama kuna ukanganyiko umepata ya nini ufisadi na ni wapi hasa unaathiri…. Kikubwa cha Kigezo cha kukwama kwa maendeleo na sector nyingi hapa Tanzania kwetu ni utumiaji mbaya na ovyo kabisa wa pesa … pesa ambayo inapelekea sula zima la Ufisadi… Nafikiri umeona response ya vyombo mbali mbali na Wananchi wenyewe wa Tanzania walivyomaka na kupinga kwa jazba kuhusu suala zima la pesa za BAE…Why?? Sababu ziko wazi kwa kila mtu….

Katika elimu umezungumzia kana kwamba wanaoenda shule wanafundishwa isivyo… Kana kwamba ufindishwaji uboreshwe... IMO Sioni sababu ya kusema uboreshwe, yaani stage iliyopo ni ya kujenga from scratch... Naomaba ujue kua asilimia zaidi ya 50 za shule hawasomi kabisa!! Ndio JK kakazana mno kujenga mashule, data kibao za kusifia idadi za shule… Shule zenyewe bado hazina viwango vya kuitwa hivyo…. Shule gani haina Walimu, haina Maktaba, haina labaratory (in this world of science and technology of today... what a disgrace!) In short hazina Vifaa…. Sector ya Elimu wamesahau kabisa walimu… wao ndio inatakiwa kuwaangalia na kuwaridhisha… then unakuja jengo/shule... You can force the donkey to go to the River but never to drink the water from the river….

Nimegusia elimu sitaki niende zaidi.... kwanza tuwekane sawa hapa.... then we can talk....
 
Nimependa saana na post yako… Ila napingana na assumption yako kua ufisadi unachukua tu asilimia kumi (10) Ni zaidi ya hizo asilimia... katika suala zima la kueleza kua nini kiini cha Umasikini Tanzania… Labda kama kuna ukanganyiko umepata ya nini ufisadi na ni wapi hasa unaathiri…. Kikubwa cha Kigezo cha kukwama kwa maendeleo na sector nyingi hapa Tanzania kwetu ni utumiaji mbaya na ovyo kabisa wa pesa … pesa ambayo inapelekea sula zima la Ufisadi… Nafikiri umeona response ya vyombo mbali mbali na Wananchi wenyewe wa Tanzania walivyomaka na kupinga kwa jazba kuhusu suala zima la pesa za BAE…Why?? Sababu ziko wazi kwa kila mtu….

Katika elimu umezungumzia kana kwamba wanaoenda shule wanafundishwa isivyo… Kana kwamba ufindishwaji uboreshwe... IMO Sioni sababu ya kusema uboreshwe, yaani stage iliyopo ni ya kujenga from scratch... Naomaba ujue kua asilimia zaidi ya 50 za shule hawasomi kabisa!! Ndio JK kakazana mno kujenga mashule, data kibao za kusifia idadi za shule… Shule zenyewe bado hazina viwango vya kuitwa hivyo…. Shule gani haina Walimu, haina Maktaba, haina labaratory (in this world of science and technology of today... what a disgrace!) In short hazina Vifaa…. Sector ya Elimu wamesahau kabisa walimu… wao ndio inatakiwa kuwaangalia na kuwaridhisha… then unakuja jengo/shule... You can force the donkey to go to the River but never to drink the water from the river….

Nimegusia elimu sitaki niende zaidi.... kwanza tuwekane sawa hapa.... then we can talk....

Elimu yetu ina mapungufu mengi sana. Na wasiobahatika kuipata hata hii elimu yenye mapungufu matokeo yao ndio hao hao mafisadi wanaowaibia wakijiuzulu wenzetu wanalia na kusaga meno na kuzirai........kazi ipo
 
Ndugu wanabodi,
Leo nawarudisha nyuma ambako siku zote za mijadala hapa JF tumejaribu sana kuepuka swali hili. Pengine zipo mada zinazofanana na swali hili lakini bado kabisa tumekuwa tukiepa sana kutoa majibu kwa sababu linatugusa moja kwa moja na wakosa ni sisi wenyewe japokuwa kwa mila na desturi za Mtanzania tunaamini kwamba matokeo mabaya ya matarajio yetu lazima kuna mkono wa mtu sii bure.

Hivi kweli tumewahi jiuliza kwa nini sisi maskini? na kama sisi maskini tumewahi tafakari kwa undani zaidi tumefika fikaje hapa tulipo ili tupate ufumbuzi wa matatizo yetu maana tumeimba sana nyimbo, hadithi na ngonjela zinazohusiana na maadui zetu wakubwa Ujnga , Umaskini na Maradhi lakini ukweli ni kwamba jitihada ndogo sana zimetumika kuelekeza mapambano yetu ktk maadui hao. Tunatumia mabillioni ya fedha ktk miradi ambayo hailengi kutuondoa hapo tulipokwama bali tunatarajia kuongeza kasi ya mwendo wakati tumekwama na gari letu la maendeleo haliendi popote..

Baada ya kuwa mwanajanvi wa JF kwa muda mrefu sana, kusoma mabandiko mbalimbali na kusoma makala za magazeti, mawazo ya wasomi wetu na kadhalika nimegundua kitu kimoja ya kwamba sisi Watanzania - We are into denial..Ni maskini lakini hatudhani kama sisi ni maskini kweli na tumejenga fikra za kwamba MTU akifanya kazi kwa bidiii kubwa bila shaka ataweza kufanikiwa kutokana na umaskini. Lakini tunasahau kwamba Umaskini ni stage ya mtu kukwama ktk hali na mali na mbinu zinazotumika hapa ni tofauti kabisa na zile za kuendelea mbele. Sasa unapoweka nguvu kubwa ktk uzalishaji kweli unaweza kujiondoa ktk umaskini hali umaskini unatokana na sababu zake kama vile gari lililokwama tunatakiwa kutazama limekwamba wapi Je, ktk tope, mchanga au shimo na ndipo tutafahamu jinsi ya kujikwamua na sii kukanyaga mafuta kuongeza kasi. Magurudumu yatazunguka tu hatutatoka hapo tulipokwama.

MTU, hili neno pekee linajenga Ubinafsi na kubomoa nguvu ya jumla, inavunja Utaifa na kuelekeza mapambano haya kwa fikra za kila mmoja wetu atachunga mzigo wake kama abiria walikosa matumaini ya usafiri baada ya gari lao kukwama na hivyo kila mmoja wao atafute usafiri wake..Fikra hizi za kila mmoja atafute usafiri wake, ndicho kinachofanyika nchini na ndio sababu tumeshindwa kutoka ktk umaskini maana sote tumeliacha gari la Taifa lilipokwama na kila mmoja wetu anatazama usafiri wake hali tuko katikati ya msitu na pasipo dira..na maskini ya Mungu hatufahamu tunaelekea wapi. Ni kweli kabisa kwamba uongozi mbaya ndio ulotupeleka ktk korongo hili la umaskini na tumekwama lakini sio uongozi mbaya unaotufanya tuchukue maamuzi ya kila mtu abebe msalaba wake..

Je, tunafikiri fikra za kwamba tukipata kiongozi au uongozi mzuri tutaweza kujinasua ktk umaskini tulipokwama? na huyu kiongozi au viongozi wanatakiwa wawe na moyo gani, wananchi wenyewe wanaweka matumaini yapio ikiwa leo kila mmoja wetu anadai maisha magumu aongezewe mshahara na posho ili hali wanajua fika kwamba tumekwama sote. Hivi kweli ikiwa wabunge kujiongezea posho ni makosa basi yatulazimu sisi wote tuombe raha hizo sawa na wao japokuwa tunajua fika kwamba wanayodai viongozi wetu ni makosa makubwa na ndizo sababu zinazotuweka ktk umaskini?..Ndizo sababu zinazotufanya tuwatake waondoke ktk madaraka na mageuzi ya kweli lazima yazingatie kwanza kwamba tumekwama na uzalendo unatakiwa kwanza.

Watanzania wenzangu ifike mahala tufikirie tumetoka wapi na tumekwama wapi, badala ya kuendelea kufikiria tunakwenda wapi.. Tanzania tumekwama ktk umaskini na tumeshindwa kutoka ktk umaskini. Na kibaya zaidi ni kwamba - WE CAN"T HANDLE THE TRUTH!.. bado tupo ktk kuamini kutoamini kwamba tuna watu wachache sana WAZURI (A few good men) ktk ngazi zote za uongozi na uwajibikaji kuweka Uzalendo mbele ya kila kitu. Hivi kweli Utawala wa leo toka Azimio la Zanzibar wamekosa aibu kabisa ya kufikiria Ufisadi mkubwa wanaoufanya kwa wananchi wao huku wakiendesha siasa za chuki baina ya watanzania kwa kutumia mapungufu ya Mtanzania huyo (ujinga, umaskini na maradhi) kama nyenzo ya kumuumiza zaidi.

Tuna msemo wa kwamba TAIFA MBELE? hivi tunaposema Taifa kwanza huwa tuna maana gani? Ni vitu gani vinatangulia ktk kulinda maslahi ya Taifa hadi tuseme TAIFA kwanza hali nafsi zetu zimegawanyika ktk makundi ya Ukabila, dini, rangi wanawake na wanaume, vyama na kadhalika. Hivi tunaposema Utaifa kwanza huwa tunatazama sifa zipi za uzalendo ikiwa kila mmoja wetu anatafuta riziki yake, anapanga malengo yake kwa manufaa ya maslahi yake ikiwa ni haki yake ya kuzaliwa na kama mtu huru?. Nini maana na kipimo cha UTU wa kila mmoja wetu ktk Utaifa wetu na huu utaifa unatokana na mipaka gani?.

Wanabodi lazima tukubali ukweli uliosimama ya kwamba tumeshindwa!...TUMESHINDWA!... na hakuna njia bora zaidi ya kufikiria - Ikiwa kweli tumeshindwa, je tulikosea wapi?... Mada nyingi sana hapa JF zinazungumzia sana matumizi mabaya ya mamlaka kwa viongozi wetu lakini katu tumeshindwa kujitazama sisi wenyewe sote kama ni MASIKINI na tumekwama ktk umaskini kama Taifa na sii mtu au kundi la watu pekee.. Vita ya kujikomboa kutokana na umaskini, ujinga na maradhi imekuwa sii vita ya kitaifa japokuwa tunasema na kulalama siku zote kwamba sisi ni Maskini.

Ebu tufikirie mfano mmoja mdogo sana ktk kutazama mbinu za kidunia ktk ubunifu. Leo hii Somalia wako ktk matatizo makubwa ya Ukame (drought and famine) na wamekwama... Hivi kweli itakuwa busara kwao leo kufikiria kupambana na matatizo haya ya ukame inatakiwa regime change?.. au kila mmoja wao atie nguvu ktk uzalishaji. Kama ndivyo tumewahi jiuliza kwa nini Somalia imeshindwa kuondokana na vita kwa zaidi ya miaka 20 sasa hivi hadi wamefikia hapo walipo!...
- Je, kumpata kiongozi bora inaweza kuwaondolea njaa na ukame ili hali regime change na nguvu ya kumtafuta kiongozi bora zaidi ndio chanzo cha mtafaruku baina yao toka aondolewe Siad Barre na leo wamefikia hapo walipo?..
- Je, sii kweli kwamba ukame ni matokeo ya vita ambayo imetokana na kupoteza UZALENDO unaomfanya kila mmoja wao kuto heshimu na kuwajibika kwa taifa lake kwanza. Somalia wamekwama na hawataweza kujikwamua hata siku moja kama hawatarudi nyuma na kutazama jinsi gani walipoteza Utaifa wao.

Kwa hiyo, wanabodi tuumize vichwa vyetu kutazama tumekwama wapi na sababu zipi zilizotukwamisha na sii wapi tunakwenda ama tunataka kwenda. Ni imani yangu kwamba siku tuloomba Uhuru tulijua fika tunataka kwenda wapi na nadhani hakuna shida ya leo kujua tunataka kwenda wap bvali kuondoka ktk shimo hili la umaskini tulipokwama. Ni lazima tukubali vichwani mwetu kwamba tumekwama ili tupate kufikiria na kutunga mbinu zote za ujasiri, mhanga na uzalendo zilenge ktk kujinasua ktk shimo hili.

Hao Somalia leo hawawezi kufikiria kutafuta chakula kilichopikwa na chef toka hotel za nyota tano kama suluhisho la ukame. Itakuwa ujinga na ulimbukeni mkubwa sana lna bahati mbaya sisi Watanzania tunajaribu sana kutafuta suluhisho la umaskini wetu kwa kutafuta vitu kutoka nyota tano, kutafuta ushauri wa ki nyota tano bila kujali kwamba tumekwama. Huu ni ulimbukenii wa kuficha uchafu wetu wenyewe, ni ulimbukeni wa kujisitir aibu na kamwe hatuwezi kupambana na imaskini kwa majigambo na usanii wa kuweka viraka ktk nguo iliyochakaa. Watanzania wenzangu hatuwezi ondokana na Ujinga umaskini na maradhi ikiwa vita hii ni ya mtu mmoja mmoja kwa fikra kwamba umaskini wetu ni wakujitakia, kila mmoja wetu atabeba msalaba wake wa matatizo.

Sio Ufisadi wala uongozi mbaya ndizo sababu kubwa, bali haya yote ni matokeo ya upungufu ktk imani inayomjenga mtu mmoja mmoja kujinasua ktk lindi la Umaskini, hivyo ktk jitihada za kujikomboa tunajikuta tunakanyagana hovyo kila mmoja wetu akitaka atoke yeye kwanza utafikiri kaa wa bahari waliowekwa ktk kapu wakisubiri kutiwa ktk sufuria la maji ya moto.

Hivi kweli watumishi wa umma hasa wataalam na mabingwa wetu wanaolipwa mshahara chini ya mil 2 lakini hupewa nyumba, wasilipe maji na umeme, wamepewa fursa ya kufanya biashara nje ya ajira walizoajiriwa wakijenga conflict of interest kiutawala kwa taaluma zao ili kujineemesha bado wana haki ya ki UTU kudai wao malipo zaidi kutokana na ugumu wa maisha japokuwa wanajua fika kwamba Tanzania ni nchi maskini na tumekwama kt umaskini. Viongozi wetu ngazi zote za kijamii tafadhali lihurumieni Taifa letu, wahurumieni waja wenu walipa kodi maana mnawaweka ktk nafasi ngumu sana ya kufikia maamuzi ya kinyama maana tofauti baina ya binadamu na mnyama kifikra ni ndogo sana..
 
Ni swali GUMU sana hili mkuu; hebu jaribu kulifikisha pale Magogoni huenda safari hii wakawa na jibu maridhawa.
 
Mkuu Mkandara,
Nakubaliana na wewe kimsingi kwenye maeneo mengi. Mimi naomba tu niuchokoze tu huu mjadala kidogo. Mtazamo kuhusu umaskini wetu umegawanyika katika maeneo mawili:Mtazamo wa ndani na Mtazamo wa Nje. Kwa upande moja, mtazamo wa ndani una jenga hoja kwamba umaskini wetu ni matokeo ya vitu kama uongozi mbovu (especially lack of political will), sera za ovyo, ufisadi na attitude ya watanzania kuhusu ‘kazi' (attitude towards work). Wajenga hoja hii wanadai kwamba haya ni matatizo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu. Kwa upande mwingine, mtazamo wa nje unajenga hoja kwamba umaskini wetu ni matokeo ya ukoloni mamboleo ambao umetufunga nchi maskini kwenye mfumo wa kibepari wa kimataifa usiotendea haki mataifa madogo kama Tanzania. Wajenga hoja hii wanadai kwamba haya ni matatizo yaliyo nje ya uwezo wetu.

Nadhani mjadala ungekuwa na afya zaidi iwapo tungejaribu kutenganisha mitazamo hii kabla ya kuichanganya pamoja ili kubaini majibu sahihi.
 
sababu haiwezi kuwa moja tu zipo kadhaa lakini mojawapo ni uvivu wa sisi watanzania kukabiliana na changamoto za maisha
 
watanzania wengi tunapenda kujiuliza serikali imetufanyia nini wananchi lakini tumepuuza kabisa kujiuliza sisi wananchi tumeifanyia nini nchi yetu.
 
sisi watanzania ni wavivu wa kusoma jambo ambalo linarudisha nyuma weredi wetu na kupunguza kufikiri kwa kina na hatimaye maendeleo yetu.
 
Back
Top Bottom