Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Vijana waliomaliza shule, vyuo na hawajaajiriwa(tambua kwamba mfumo wa elimu yetu, haumwandai kijana kujiajiri bali kuajiriwa)ni tatizo na bomu likilipuka hakuna ambaye atakuwa salama. Kutokana na hali hii kwa sasa vijana wamekuwa na mawazo ambayo yanasubiri kichokoo na ndipo kila mtu ataweza kuyatambua nini wanafikiri.

Siasa za maneno bila mipango madhubuti ambazo zinatawala sasa hapa kwetu zinakotupeka siko
 
Ahsante Mengi kwa kulisema hili. Ngonjera za CCM kwamba Tanzania ni nchi maskini hazikubaliki tena. Tunaona viongozi uchwara wakifanya ufisadi wa hali ya juu na kuwa mabilionea. Tunaona makampuni makubwa toka nchi za magharibi "yakiwekeza" au kutaka kufanya hivyo katika sekta mbali mbali ili wajipatie faida. Hivyo hili la Tanzania ni maskini halikubaliki tena na hatutaki kulisikia. Tunataka kuona utajiri wa Tanzania unawanufaisha Watanzania walio wengi.

Mengi:Tanzania ni tajiri lakini wananchi ni maskini

2008-03-18
Na Joseph Mwendapole

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Bw. Reginald Mengi, amesema Tanzania sio maskini ila wananchi wake ndio wanakabiliwa na changamoto ya umaskini.

Aliyasema hayo jana ofisini kwake wakati akizungumza na wanafunzi wa Shahada ya Pili kutoka Chuo Kikuu cha PACE kilichoko katika mji wa New York, Marekani.

Wanafunzi hao 15, wanaosomea masuala ya biashara, walimtembelea Bw. Mengi ofisini kwake kupata uzoefu na mbinu mbalimbali za kufanya biashara.

``Tutofautishe umaskini wa watu na wa nchi, watu wakiwa maskini huwezi kusema nchi ni maskini na kwa imani yangu, Tanzania ni nchi tajiri ila wananchi wake ni maskini,`` alisema.

Bw. Mengi aliwataka wanafunzi hao kuyaona matatizo wanayokabiliana nayo kama changamoto na kufikiri namna ya kujikwamua.

Alisema mtu akiyachukulia matatizo kama changamoto, anatafuta mbinu za kukabiliana nayo na hatimaye kuondokana nayo kabisa.

``Ukiona changamoto ukasema ni tatizo litakaa begani kwako siku zote lakini ukilichukulia kama changamoto, utafanikiwa na wengi waliojaribu hivyo wamefanikiwa,`` alisema na kuongeza kuwa yeye binafsi hakuona umaskini kama tatizo bali changamoto aliyojitahidi kukabiliana nayo.

Bw. Mengi pia alielezea siri ya mafanikio yake kuwa ni kumwamini Mungu na aliwashauri kumweka mbele katika kila jambo wanalofanya.

Alisema licha ya kumweka Mungu mbele, wanapaswa pia kujiamini kuwa wanaweza kufanya mambo makubwa kama wengine waliofanikiwa.

``Kila ukiamka, muombe Mungu na useme ninaweza, nitaweza lazima nitaweza,`` alisema na kuongeza kuwa, mafanikio yake yametokana na kujiamini na kumtanguliza Mungu mbele.

Bw. Mengi ambaye ni Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda na Biashara (CTI), alisema wakati anaanza biashara, hakuwa na mtaji kabisa lakini alijitahidi kukopa na kuanza kutengeneza kalamu nyumbani kwake.

Alisema woga ni adui mkubwa katika biashara na imekuwa ikisababisha watu wengi kushindwa kabla ya kuanza.

Aidha, aliwaasa wanafunzi hao kukumbuka kusaidia jamii watakapopata fedha na kwamba hiyo ndio njia pekee ya kurudisha shukrani kwa Mungu na kwa wananchi.

``Ukifa hutaulizwa mali uliyojilimbikizia bali namna ulivyoitumia kusaidia wenye shida, kwa hiyo mkipata mjitahidi kusaidia wenye shida,`` alisema.

Kwa upande wake, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Bw. Daudi Mwakawogo, alipongeza jitihada za Bw. Mengi katika kupambana na rushwa.

Alisema Bw. Mengi amekuwa akitoa misaada bila ubaguzi wowote na kwamba amekuwa akisaidia waumini wa dini mbalimbali.

Alimwelezea kuwa ni mwanamazingira aliye mstari wa mbele na kwamba mpaka sasa amewezesha kupanda miti milioni 23 hapa nchini.

SOURCE: Nipashe
 
CCM wamesoma haya? Maan JK anaendelea kupanga mbinu za kuomba na kula pesa kwa jina la Tanzania masikini kumbe Nchi ni tajiri sana ila masikini ni Watanzania na hazina yetu imejaa mapesa ila kwa ajili ya wachache.
 
Hivi karibuni kumekuwa na kauli mbali mbali kinzani zinazotolewa na viongozi and other dignitaries together with some influencial people, prominent businessmen as well as politicians!

Kauli hizi ni wazi kuwa zimetolewa wakati ambapo nchi yetu pamoja na bara letu kwa ujumla tukiwa kwenye wakati ambao inabidi tutafakari tunachokifanya,tulikotokea na tunakoelekea!

Nauliza kama Tanzania ni masikini ama tajiri kutokana na kauli zinazopingana kutoka kwa:

1)Mh Rais

2)Mh Mbunge wa Karatu Dk Slaa

3)Reginald Mengi

Mh Rais wakati wa uzinduzi wa barabara alisema "Tanzania ni Masikini"

Mengi naye alipokuwa akihutubia wawakilishi kutoka Nigeria alisema.."Tanzania ni Tajiri"

Dk Slaa naye huko Bungeni wakati wa kudai Mkapa alipe kodi naye alisema.."Tanzania ni Tajiri"

Ndugu zangu wana jf what is what?

Lipi tuamini and why?

And if not then why not?
 
``Nchi hii ni maskini, ujenzi huu unagharamiwa na fedha za wananchi, epukeni kuingia gharama mara mbili, kwani wanaofanya hivyo wanakuwa wanyonya damu,`` alisema.
Hiyo ni kauli ya Mh Rais wakati wa ufunguzi wa barabara!
 
Nadhani tofauti kubwa ya misemo yote hii miwili ilikuwa ni ktk tofauti za ARDHI na WATU..
Mheshimiwa rasi alikuwa akizungumzia WATU hali Mengi na Dr. Slaa walikuwa wakizungumzia ARDHI... sasa swala la kujiuliza kinachounda Tanzania ni ARDHI ama WATU!...
 
Nadhani tofauti kubwa ya misemo yote hii miwili ilikuwa ni ktk tofauti za ARDHI na WATU..
Mheshimiwa rasi alikuwa akizungumzia WATU hali Mengi na Dr. Slaa walikuwa wakizungumzia ARDHI... sasa swala la kujiuliza kinachounda Tanzania ni ARDHI ama WATU!...

Tanzani ni nchi tajiri yenye watu masikini. Inajumuisha kauli zote za watu watatu Kikwete, Slaa na Mengi?
 
Halafu wanatudanganya wananchi kuwa nchi ya Tanzania maskini, si kweli, kama maskini wawekezaji wasingekuja kuwekeza... hiki ni kiini macho ili wananchi wasiwe na ufahamu`` alisisitiza Dk. Slaa.

Dk Slaa akilonga huko kwenye haus of paliamenti...Kauli inayopingana vikali na ile ya Mh Rais!
 
Waafrika wameainishwa kuwa ni maskini na wamebakia kuimba kama kasuku sisi ni fukara wakati rasilimali zao zinaporwa ukiwemo utajiri wa madini. Lakini hawajawahi kujiuliza mbona bara letu ni tajiri lakini tunaendelea kuwa maskini,`` alisema.

Reginald Mengi akilonga na wawakilishi kutoka Nigeria....Kauli ambayo inakinzana na ile ya rais kwa kuendeleza kilio kuwa sisi ni masikini!
 
Aliwataka wananchi kujiuliza mbona Tanzania au Nigeria ni tajiri sana lakini watu wake ni maskini.
Ndugu Mengi aliongeza!
 
Tanzani ni nchi tajiri yenye watu masikini. Inajumuisha kauli zote za watu watatu Kikwete, Slaa na Mengi?
Umasikini aliouzungumzia Mh Rais ni wa watu ama wa rasilimali/kipato?

Maana alikuwa akizungumzia kuhusu gharama za ujenzi wa barabara:

Issue ambayo technically ina angukia kwenye miundo mbinu.


Hivyo then kuwa satisfied na ukweli kuwa ni nyenzo muhimu kwa maendeleo ya nchi yetu.

Nyenzo ambayo watendaji wake wako infected na gonjwa hatari!

Nyenzo ambayo imeingiliwa na gonjwa hatari dhidi ya maendeleo..UFISADI!

Je kuna Haja ya Mh Rais kutoa ufafanuzi pale anaposema Tanzania ni masikini?
 
Tanzania ni nchi tajiri, lakini tuna viongozi mafisadi ambao wanajali matumbo yao na hivyo kuutumia utajiri wa Tanzania kujitajirisha wao na familia zao kupitia rasilimali tulizonazo na mikataba mibovu wanayoidhinisha.

Miaka ya karibuni tumesikia baadhi ya viongozi wakiwa na migodi yao ambayo wameipata katika mazingira ya kutatanisha. Hao waliosaini mikataba mibovu ya uchimbaji dhahabu ni mashareholders wa Barrick ambapo kila kampuni hiyo ikifanya vizuri thamani ya shares zao huongezeka lakini Watanzania hatuoni manufaa yoyote ya dhahabu yetu..
 
Tanzania ni nchi tajiri, lakini tuna viongozi mafisadi ambao wanajali matumbo yao na hivyo kuutumia utajiri wa Tanzania kujitajirisha wao na familia zao kupitia rasilimali tulizonazo na mikataba mibovu wanayoidhinisha.
Kauli yako itakuwa inapingana na mh rais!
 
I second "Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini".

Ukichukulia utajiri in terms of rasilimali kama madini, ardhi nzuri, ufukwe wa bahari, vyanzo vya maji na vitu vingine vingi basi Tanzania ni nchi tajiri.

Ukichukulia kipato na hali ya maisha ya wananchi Tanzania ni nchi masikini.

Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini, partly kwa sababu ya uongozi mbovu unaojumuisha ufisadi aliousema vizuri Bubu hapo juu.
 
Kauli yako itakuwa inapingana na mh rais!

Siyo kauli yangu tu inayopingana naye hata utendaji wake tangu achaguliwe kama Rais naupinga na nadhani na Watanzania wengi hawaridhishwi na utendaji wake. Maisha bora kwa kila Mtanzania, hadi hii leo hatujayaona. Billioni za Kikwete hazikuwa na manufaa yoyote kwa Watanzania, ari mpya nguvu mpya na kasi mpya wote tunajua matokeo ya hili, ahadi za kuipitia mikataba ya uchimbaji dhahabu ambayo inalalamikiwa na Watanzania kwamba haina maslahi kwa nchi yetu hadi hii leo hakuna chochote kilichofanyika. Kwa kifupi ni ZERO!
 
I second "Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini".

Ukichukulia utajiri in terms of rasilimali kama madini, ardhi nzuri, ufukwe wa bahari, vyanzo vya maji na vitu vingine vingi basi Tanzania ni nchi tajiri.

Ukichukulia kipato na hali ya maisha ya wananchi Tanzania ni nchi masikini.

Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini, partly kwa sababu ya uongozi mbovu unaojumuisha ufisadi aliousema vizuri Bubu hapo juu.
Kauli ya Mh rais wewe umeielewa kivipi?
Naomba tusaidiane hapo.
Kumbuka alikuwa akizungumzia uwezo wa serikali kuwekeza kwenye miundo mbinu pamoja na infrastructures kwa ujumla!
 
Umasikini aliouzungumzia Mh Rais ni wa watu ama wa rasilimali/kipato?
Maana alikuwa akizungumzia kuhusu gharama za ujenzi wa barabara!

Jmushi1,

Statements zote ni sahihi, Tanzania na Afrika kwa ujumla ni tajiri kwa maana ya resources kama ardhi, madini, mafuta nk. Lakini watu wake ni maskini kwasababu tumeshindwa kutumia akili zetu kutengeneza added values kutoka kwenye hizo resources zetu.

Umaskini uko kwenye vichwa vyetu, akili zetu, fikra zetu nk. Hata tukipata uongozi bora sana bado itachukua miaka mingi kwa Watanzania kuwa matajiri. Ni rahisi kubadili uongozi lakini ni ngumu sana kubadili culture ya uvivu
na kutokuwajibika ambayo imejengeka Tanzania na Afrika. Sisemi Waafrika ni wavivu, maana wakija huku nje wanajituma kweli kweli.

Culture yetu ndio ya kimaskini, culture ya kukimbilia majibu rahisi na common sense. Culture ambayo haitufanyi tukae chini na kuwaza nje ya our comfort zone. Kuibadili hii itatuchukua muda mrefu sana na juhudi kubwa mno kuanzia level ya individuals mpaka kwenye viongozi wa nchi.

Ndio viongozi wa Afrika wameiba mabilioni ya resources zetu lakini mimi siamini kama ndio chanzo cha umaskini wetu. Matatizo yetu yanaenda ndani zaidi. Mwalimu Nyerere alijaribu kushughulikia kiini cha matatizo ya Watanzania lakini bahati mbaya akachagua siasa mbaya na chama kushika hatamu mpaka ikafikia mahali ambapo hakuwa challenged na hivyo kudumaa kama viongozi wetu wengine.
 
Jmushi1,

Statements zote ni sahihi, Tanzania na Afrika kwa ujumla ni tajiri kwa maana ya resources kama ardhi, madini, mafuta nk. Lakini watu wake ni maskini kwasababu tumeshindwa kutumia akili zetu kutengeneza added values kutoka kwenye hizo resources zetu.

Umaskini uko kwenye vichwa vyetu, akili zetu, fikra zetu nk. Hata tukipata uongozi bora sana bado itachukua miaka mingi kwa Watanzania kuwa matajiri. Ni rahisi kubadili uongozi lakini ni ngumu sana kubadili culture ya uvivu
na kutokuwajibika ambayo imejengeka Tanzania na Afrika. Sisemi Waafrika ni wavivu, maana wakija huku nje wanajituma kweli kweli.

Culture yetu ndio ya kimaskini, culture ya kukimbilia majibu rahisi na common sense. Culture ambayo haitufanyi tukae chini na kuwaza nje ya our comfort zone. Kuibadili hii itatuchukua muda mrefu sana na juhudi kubwa mno kuanzia level ya individuals mpaka kwenye viongozi wa nchi.

Ndio viongozi wa Afrika wameiba mabilioni ya resources zetu lakini mimi siamini kama ndio chanzo cha umaskini wetu. Matatizo yetu yanaenda ndani zaidi. Mwalimu Nyerere alijaribu kushughulikia kiini cha matatizo ya Watanzania lakini bahati mbaya akachagua siasa mbaya na chama kushika hatamu mpaka ikafikia mahali ambapo hakuwa challenged na hivyo kudumaa kama viongozi wetu wengine.
If thats the case then wewe na mh rais mnaimba kama kasuku?
This is according to this;
``
Waafrika wameainishwa kuwa ni maskini na wamebakia kuimba kama kasuku sisi ni fukara wakati rasilimali zao zinaporwa ukiwemo utajiri wa madini. Lakini hawajawahi kujiuliza mbona bara letu ni tajiri lakini tunaendelea kuwa masikini
R.Mengi
 
If thats the case then wewe na mh rais mnaimba kama kasuku?
This is according to this;
``
R.Mengi

Jmushi1,

Mimi nakubaliana na Mengi pia. Ni muhimu kwa mtu mmoja mmoja kuchukia umaskini na kuanza kufanya mabadiliko ya kweli kuelekea kupambana na huo umaskini. Hapo ndipo culture inaingia, kupambana na hiyo culture ya kusema sisi ni maskini na kuendelea kubweteka na kuwa ombaomba.

Zaidi ya hapo kuna yale mambo ambayo wote kwa pamoja na kama taifa kunaweza kuwa na sera za maana za kuwahakikishia hawa Watanzania wanakuwa na nyenzo bora za kupambana na umaskini wao.

Hakuna haja ya kuimba umaskini bila kuchukua hatua. Mengi aliona hiyo nafasi na kapambana kadri inavyowezekana kujiletea maendeleo yeye mwenyewe na jamii ya Tanzania.

Sasa ni wajibu wa Watanzania wengine pia kuiga mifano ya akina Mengi.
 
Back
Top Bottom