Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Ndugu mwanajukwaa! Hili swali laweza kua na majibu lukuki, Me naliona gumu kwasababu ya wingi wa majibu.Hayati mwalimu baba taifa aliwahi kusema ili taifa liendelee lazima tuwe na watu, ardhi na siasa safi. Lakini hivi vyote havipo? Kama tuna rasilimali watu, rasilimali materials, tatizo nini? Nchi za wenzetu zinatuacha kwa mbali ilihali awali tulikua ktk level moja.Tusaidiane kulijibu hili swali pengine miongoni mwetu twaweza kua na majibu sahihi zaidi. Ivi angekuepo mwalim Nyerere tungekua hapa tulipo kweli?Asingetoa ushauri wake kwa watengeneza sera na mipango wakamuelewa?
 
Ndugu mwanajukwaa! Hili swali laweza kua na majibu lukuki, Me naliona gumu kwasababu ya wingi wa majibu.Hayati mwalimu baba taifa aliwahi kusema ili taifa liendelee lazima tuwe na watu, ardhi na siasa safi. Lakini hivi vyote havipo? Kama tuna rasilimali watu, rasilimali materials, tatizo nini? Nchi za wenzetu zinatuacha kwa mbali ilihali awali tulikua ktk level moja.Tusaidiane kulijibu hili swali pengine miongoni mwetu twaweza kua na majibu sahihi zaidi. Ivi angekuepo mwalim Nyerere tungekua hapa tulipo kweli?Asingetoa ushauri wake kwa watengeneza sera na mipango wakamuelewa?

Ndugu kwanza nikupongeze kwa ufafanuzi wako. Tatizo kubwa kwetu leo ni mtindo wa kiutendaji tunaotumia miaka nenda rudi. Wenzetu waliokwisha gundua siri hii wana msemo wao: "You cannot teach an old god new tricks"-"huwezi mfundisha mbwa mzee/aliyezeeka mbinu mpya za uwindaji." Ulimwengu tunaoishi umebadilika sana nasi ilitupasa kubadilika nao kadri ya mahitaji.

Ila ninasikitika sana mtindo wetu wa kiutendaji umepitwa na wakati. Tusisahau kuwa maendeleo yeyote yale huharakishwa na siasa safi na wazi. Siasa za chama tawala kwa sasa si safi na wazi. Ni sawa na mbwa mzee.

Tazama haya kwa ufupi utajua ninacho maanisha;

1. Je ni sawa kwa nchi kama yetu karne hii kwa kiwango cha uhuru wa miaka 50 kuwa omba omba?

2. Je, ni sawa kwa nchi yetu na rasilimali zake kuendelea kupata huduma za kijamii chini ya kiwango? Ni haki kwa viongozi wa serikali kupata huduma hizo nje ya nchi. Huu ndiyo utawala bora na wawazi?

3. Je, inaingia akilini kweli hadi leo utendaji uliokuwa madarakani zaidi ya 50 kuendelea kuwarubuni wananchi kwa ahadi hewa? Mfano tu swala la umeme. Hata kwa mambo madogo tu kuyatatua inakuwa shida. Kipimo cha maendeleo siyo takwimu kwenye makaratasi, bali ni maisha halisi wa watu katika uchumi ule. Je, unafuu huo upo?

Siasa safi na uwazi ndiyo tatizo kubwa hapa Tanzania. Siasa za kulindana na kulinda maslahi binafsi zinaliteketeza Taifa. Mfano wa karibu ni mchakato wa katiba. Je, kunauhakisi wa siasa safi na za uwazi? Hatima yake ni nini?
-Mwendelezo wa utendaji zeeka
-Mwendelezo wa wachache kufaidi raslimali za Taifa
-Kukithiri kwa ukuaji wa umaskini
-Ongezeko la rushwa
-Kutoweka kwa utu wa kibinadamu
-Mwisho machafuko yalisiyo kwisha.
 
Naunga mkono hoja......!

Mkuu unaweza kuwa una RASILIMALI nyingi !!! Lakini usipojituliza na ku Plan na kuweka uaAminifu mbele yote itapotea na kuwenda hewani...pppuuuuffff !! Mifano mizuri :- Singapore,dubai,KulaLumpur,Bahrain,Banglore,Swissterland, NK Trophs
 
Last edited by a moderator:
Mkuu unaweza kuwa una RASILIMALI nyingi !!! Lakini usipojituliza na ku Plan na kuweka uaAminifu mbele yote itapotea na kuwenda hewani...pppuuuuffff !! Mifano mizuri :- Singapore,dubai,KulaLumpur,Bahrain,Banglore,Swissterland, NK Trophs

Kaka uko sahihi kabisa,hapo kwenye mifano ongezea Israel wana mivita kila siku lakini bado wanaishi comfortable,Holland wametengeneza inchi kavu kwa ku-squeeze bahari na wanatumia eneo hilo kulima na shughuli za viwanda.....,sisi tunabaki tunalialia tu hali ngumu wakati maeneo makubwa tunayo mashamba ya kufa mtu,vijana wasomi yaani sijui tufanyeje.

Alafu mkuu nimegundua tatizo lingine sisi vijana sio wabunifu,serambovu zisizotekelezeka na vijana wengi wanaharaka ya kupata utajiri haya nayo ni vikwazo vya maendeleo kwa nchi yetu.
 
Kaka uko sahihi kabisa,hapo kwenye mifano ongezea Israel wana mivita kila siku lakini bado wanaishi comfortable,Holland wametengeneza inchi kavu kwa ku-squeeze bahari na wanatumia eneo hilo kulima na shughuli za viwanda.....,sisi tunabaki tunalialia tu hali ngumu wakati maeneo makubwa tunayo mashamba ya kufa mtu,vijana wasomi yaani sijui tufanyeje.

Alafu mkuu nimegundua tatizo lingine sisi vijana sio wabunifu,serambovu zisizotekelezeka na vijana wengi wanaharaka ya kupata utajiri haya nayo ni vikwazo vya maendeleo kwa nchi yetu.
Mkuu nakuombea kwa Moula karimu akupe Uzima na Furaha, Maana umegusia Ujana na upotofu wa mawazo.....
Pia Umegusia nchi ya Holland baada ya yote RUZUKU na 50% ya bajeti yetu inatoka kwao !! hiyo inaonyesha taswira fika.!!
Sisi kwa kulalamika na kulaumu ndiyo wenyewe!
ubarkiwe
 
Mkuu nakuombea kwa Moula karimu akupe Uzima na Furaha, Maana umegusia Ujana na upotofu wa mawazo.....
Pia Umegusia nchi ya Holland baada ya yote RUZUKU na 50% ya bajeti yetu inatoka kwao !! hiyo inaonyesha taswira fika.!!
Sisi kwa kulalamika na kulaumu ndiyo wenyewe!
ubarkiwe

Amen, Ubarikiwe na wewe pia mkuu.
 
Kama watanzania wataendelea na ushabiki wa kijinga wa kuchagua viongozi wenye historia ya ufisadi na wizi; kama watanzania wataendelea kuwasifu na kuwaheshimu wezi wa mali ya umma na wakwepa kodi; kama watanzania tutaendelea kutumiwa na wanasiasa kufikia maslahi yao; tutaendelea kuwa maskini.

Lazima tutambue kuwa ni vyema tukachagua viongozi wazuri wa kuongoza juhudi zetu za maendeleo, viongozi wenye kuzingatia mazingir mapana ya nchi. Viongozi hao lazima wawe tayari kupiga vita rushwa, ufisadi na ubadhirifu. wawe tayari kuongoza nchi kwa uwazi na uwajibikaji.

Tukiweza kuamka sasa tukachagua viongozi makini kuanzia ngazi ya serikali za mitaa, madiwani, wabunge na rais, nchi itapiga hatua na tutaondoa umaskini. tukiendekeza ushabiki na kuchagua viongozi wa kisiasa kwa kujali kupewa fedha, chakula, pombe na nguo, tutaendelea kubaki maskini.
 
Ni ukweli usiopingika kua Tanzania imejaliwa kula a in a ya utajiri madini ya kila a in a hadi madini pekee duniani yaani tzanite, makaa ya mawe, mafuta, gesi, chuma (iron deposits), vivutio vya utalii kama vile milima eg Kilimanjaro, mbuga za wanyama, ardhi ya kutosha na yenye rutuba, mito na misitu ya asili vyote hivi vingepatiwa Sera na utekelezaji mzuri basis tz ingekuwa HEAVEN badala take tz is a HELL na tajiri wa kuomba omba misaada nje hasa misaada yenye mashart magumu ya kuplunder utajiri wetu.

Na sasa utajiri tulio nao wa kuomba omba misaada unaishiaishia kutokana na rushwa tens kwa kiwango cha juu kabisa UFISADI madhara ya kuwa tegemezi no makubwa sana kwa tz na watz kwa ujumla isipokua kwa wajanja mafisadi wachache wanaolindwa na serikali na watz wasipogutuka tutaishia pabaya sana kwani ujinga wa wawatanzania umekua ndio mtaji wa ccm na Sera za serikali yao mbovu, yenye viongozi dhaifu kupindukia haijawahi kutokea duniani.

Sasa kashfa ngap tz,? Mauaji, ukiukwaji wa haji za bndmu, kuminywa kwa democrasia, Richmond,IPTL/ESCROW, biashara haramu, utawala mbovu, nk.

Yote hayo yanaitafuna nchi yetu and those fools are comfortable and busy smiling at the world, hapana hapana watznia sasa wekezeni ktk mabadiliko walau kukipumzisha ccm mbona kuna kustaafu lakini hiki chama kizee hatukistafishi? CCCM kuna viongozi wazuri na watendaji wazuri sana lakini mfumo wa rushwa rushwa unawameza nap wanaishia kua corrupt haimaanishi kua vyama vngine ndo kuna malaika lakini kuwapga chino ccm kutawafanya watakaoiongoza nchi wasijiwekee hati miliki kua nchi hii ni yao peke yao watajua kua IPO siku kuna kuwajibishwa na wenye nchi ambao no wananchi pale panapotokea uzembe tkt utendaj, coz kwa sasa ccm na watawala pamoja na familia zao wako juu ya sheria hili ndo mama mambo yanafanyika kienyeji enyeji tu sheria na taratibu zinapindishwa ili kuwalinda na kulinda maslahi ya familia zao, maskini watz walio wengi hawayajui hayo ingawa tkt hali ngumu ya maisha. Sijui wapi hii tz inaelekea.

Ona sasa na huko tunakokimbilia kuomba hiyo misaada nako tumeharibu wafadhili nap wamechoshwa na huu ufisadi uliokithiri utajiri wetu umetushinda kuutumia tumekimbilia kW wenzetu ngoja sasa watz watakufa kwa kukosa madawa, barabara jazitatengenezwa, wanafunzi hawatasoma vzuri na huduma nyingi ztacease kwa ubovu wa Sera na wasimamizi wa Sera hizo, kwa ujumla nchi IPO ktk machafuko makubwa ingawa sio ktk physical war, with wangu kwa watanzania wenzangu we are late but not very very late tuamue kukua ktk mabadiliko kW maendeleo ya Tanzania yetu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Tanzania na laana ya rasilimali

JAMHURI ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) imetumbukia katika vita ya wenyewe kwa wenyewe kutokana na utajiri wake wa rasilimali, yakiwemo madini aina ya coltan, yenye kutumika kutengenezea simu na kompyuta.

Aina hizo za madini yenye kutumika kutengenezea vifaa vya Kinshasa vya kielekroniki yameguliwa hivi karibuni nchini pia, ni katika Kijiji cha Ngualla, Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.

Mafuta, almasi na dhahabu nayo yamegeuka kuwa laana kwa mataifa mbali mbali barani Afrika yakiwemo Nigeria, Sudan ya Kusini, Siera Lion, Somali na Angola.

Baada ya kugunduliwa kwa rasilimali gesi nchini katika miaka ya hivi karibuni, Wataalamu wa uchumi na maendeleo wanajiuliza,

"Jee, gesi na madini kuwa Neema au laana kwa Tanzania na nchi zingine tajiri wa rasilimali barani Afrika!"

Profesa wa Uchumi wa Maendeleo (development economics), katika Shule ya Biashara, Uchumi na Sheria, Chuo Kikuu cha Gothenburg nchini Sweden, Ola Olsson anaiangali neema iliyolishukia Bara la Afrika katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni, katika jicho la jinsi rasilimali hizo zitakavyotumika kujenga uchumi endelevu na kujitegemea kwa mataifa hayo, na sio kunufaisha kikundi kidogo cha watawala.

Prof. Olsson alitoa mtazamo wake huo hivi karibuni katika Mkutano wa Nane wa Mwaka wa Mpango wa Mazingira kwa Maendeleo Endelevu (EFD Policy Day) wakati akitoa mada kuhusu Siasa ya Uchumi ya uendelezaji rasilimali (Political Economy of Natural Resource Exploitation) uliofanyika katika Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.

Kufanikiwa katika matumizi ya rasilimali yenye tija kwa taifa na wananchi wake, jambo moja la msingi lazima lifanyike, na kwa mujibu wa Profesa huyo wa Uchumi wa Maendeleo, inatakiwa kuwepo kwa uwazi katika mfumo nzima wa uendelezaji rasilimali hizo.

"Transparency is crucial to avoid devastating scenarios. Governments should publish all revenues, whereas firms should publish all payments they make to governments for natural resources. So the people can judge whether revenues are used for sustainable development," anasema Prof. Olsson katika mada yake ya uwazi msingi kwa ukuaji endelevu na uhuru kwa Afrika.

Tafsiri isiyo rasmi, Prof Olsson anasema uwazi ni jambo la msingi kukwepa kutumbukia katika majanga mbali mbali yatokanayo na uchimbaji rasilimali. Serikali lazima zitangaze mapato yote, vile vile makapuni nayo lazima yatangaze malipo yote wanayotoa serikalini kutokana na mapato yatokanayo na rasilimali. Ili watu waweze kuamua iwapo mapato hayo yanatumika kwa maendeleo endelevu.

Kukosekana kwa uwazi katika uendelezaji wa rasilimali, mapato na matumizi yake inaelezwa kuwa msingi wa migogoro inayoibuka na kuendelea kuwepo katika nchi nyingi za Kiafrika zenye rasilimali, yote ikitokana na uchu wa kumiliki mapato yatokanayo na rasilimali hizo kwa manufaa binafsi.

Mapigano yanayotokana na rasilimali hizo ni kwa maslahi binafsi na sio maendeleo ya taifa na watu wake, na hatimaye kuibuka kwa vikundi vya kiharamia, ambavyo hutumia mgongo wa wananchi, kwamba vinapigania maslahi ya wananchi wakati ukweli ni kwamba vinapigania maslahi yao binafsi.

Prof. Olsson anaamini kuwa Tanzania kwa sasa inayo mifumo imara, na kwamba nchi yenye mifumo imara huwa na demokrasia bora na utawala bora.

Nani amiliki rasilimali nchini;

Pamoja na uwepo wa mifumo bora, Profesa huyo wa Uchumi wa Maendeleo anashauri njia iliyo bora katika umiliki wa rasilimali hiyo, na anaitaja ushirika wa pamoja wa Watanzania na makampuni ya nje (joint venture).

Mtaalamu huyo ambaye pia ni mshauri wa Benki ya Dunia anasema ni hatari kuyaachia kuyaachia makampuni am kubwa ya kimataifa pekee kuendeleza sekta hiyo, kutokana na utamaduni wa makampuni duniani wa kuzingatia zaidi utengezaji faida maradufu.

Mfumo huo sio mpya, ndio unaotumika na mataifa makubwa dunia pamoja na ule wa dola. Uchuguzi unaonyesha kuwa umiliki wa makampuni kumi makubwa dunia ni ama, umma au serikali (public or state ownership).

Ni kweli gesi kuibadili Tanzania !!

Kugunduliwa kwa gesi nchini kumebadili mitazamo ya watu, hususani viongozi, wengi wakiutazama ugunduzi huo kama dawa pekee ya umasikini uliopo, kwamba gesi iliyogunduliwa itaweza kuibadili nchi ndani ya kipindi kifupi.

Mwananchi mmoja wa mjini Mtwara, akitoa ushuhuda wa vurugu zilizojitokeza baada ya kuanza mchakato wa ujenzi wa bomba la gesi kwenda jijini Dar es Salaam, aliwalaumu baadhi ya viongozi wa juu nchini akisema waliwaeleza kuwa gesi iliyopatikana kwenye bahari huko Kusini kuibadili Mtwara, itakuwa kama Dubai ndani ya muda mfupi.

Mtazamo huo unaweka matumaini yote kwenye rasilimali hiyo ya gesi, na ni mtazamo ambao unawalemaza wananchi, ambapo hutelekeza shughuli zao za kiuchumi wakiamini kuna utajiri wa gesi, hivyo hawana haja ya kuhangaika tena.

Mkurugenzi Mkuu wa Mpango wa Mazigira kwa Maendeleo Endelevu (Environmental for Development EFD), Prof Gunnar Kohlin anatahadharisha dhidi ya mtazamo huo, akisema gesi pekee haiwezi ibadili Tanzania, bali itafanya vizuri zaidi kwa kutumia vyanzo vingine vya uchumi, akitumia mfano wa nishati ya umeme ambapo anasema bado umeme uzalishwao kutokana na maji, jotoardhi, upepo na jua unao nafasi katika uchumi wa nchi.

Pamoja na tahadhari hiyo dhidi ya utekelezaji wa nyanja zingine za kiuchumi kwa sababu tu ya kupatikana kwa gesi, Prof. Gunnar pia anatahadharisha juu ya kasi katika utafutaji na uchimbaji gesi, akisema ni vema uendelezaji gesi nchini ukafanywa taratibu na kwa awamu.

"It is wise to do it slowly, no need of rush," anasema Prof. Gunnar katika mahojiano yake na Raia Mwema.

Mtazamo wa utegemezi katika rasilimali gesi unachangiwa zaidi na soko la bidhaa hiyo duniani, ambapo nchi za Kiafrika huendelea kuwa wasafirishaji wa malighafi na wapokeaji wa malipo yatolewayo na wanunuzi.

Kutokana na utamaduni huo, ukuaji wa uchumi wa nchi za Kiafrika, Tanzania ikiwemo, hutegemea zaidi bei kwa rasilimali zake katika soko la dunia ambalo ndilo huamua bei ya kununulia. Na hapa ndipo Mtaalamu huyo wa Uchumi na Maendeleo, Olsson anapohoji,

"Nini kitatokea katika uchumi wa nchi hizi pale bei inapoporomoka!"

Ni wazi kwamba, mtazamo huo unaendeleza utegemezi wa nchi za Kiafrika kwa Mataifa yaliyoendelea yenye kuwekeza barani humu.

Mfano hai katika utegemezi wa bei ya soko la Dunia ni Zambia ambayo wakati bei ya shaba ilipokuwa juu uchumi wake ulikuwa imara, lakini ukaporomoka katika kasi ya kutisha baada ya kuporomoka kwa bei ya madini hayo katika soko la Dunia.

Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamo wa Rais, Mazingira, Dr. Binilith Mahenge, Tanzania inaendelea kujifunza kutokana na uzoefu wa nchi zingine ili kupata njia zilizo bora zaidi katika matumizi ya utajiri utokanao na rasilimali hiyo ya gesi.

Hatua ya serikali kutumia uzoefu wa mataifa mengine, ni katika kukabiliana na laana Itokanayo na uwepo wa utajiri wa rasimila, kama ilivyojitokeza katika mataifa yaliyotangulia kuendeleza rasilimali hiyo.

"Tunajifunza kutokana na uzoefu uliopo kwenye nchi zingine, tunafanyia kazi njia za kuepukana na tatizo hili," alisema Dr. Mahenge katika mahojiano na Raia Mwema alipotakiwa kuelezea mtazamo wa serikali katika kukabiliana na tatizo hilo maarufu kama "resource curse."

Chanzo: raiamwema
 
Laiti mungu angetupa upendo waafrica tukapendana wazungu wangekuja kutuomba msaada wa rasilima na chaku,tatizo la waafrica wengi tunapendana kwa macho lkn miyoyoni mwetu ni giza chuki na ubinafsi umetujaa,huwa tabia halis ya mwafrica anapenda jirani yake awe na njaa au matatizo ili aweze kumtumikisha kwa faida yake,ndugu zangu tubadilikeni ss ni binaadamu kama wazungu pia,tofauti ni rangi tu,kwa kifupi wote tunaenda msani,amani iwe pamoja nanyi.
 
Rekebisha mkuu 'kutoomba' ndio nini?kwa nini usitulie unapoandika mkuu?kwani unakimbizwa na panyaroad**?
 
Wachumi wa Tanzania tuelimisheni kuhusu hili.

Nimekuwa nikijiuliza ni kwa nini Tanzania ni Nchi masikini mpaka sasa?.

Nauliza swali hilo kwa sababu Nchi hii ina Rasilimali nyingi sana.

Mojawapo ya Raslimali tulizo nazo ni Madini, Mbuga za Wanyama, Gesi, Ardhi yenye Rutuba, Mlima Kilimanjaro na nyingine nyingi.

Sasa ninachojiuliza ni kwa nini Nchi yetu ni Maskini na Rasilimali zote hizo?.

Nawaomba Wachumi watujibie swali hili ili wengi wanaojiuliza tupate majibu.
 
Jibu hili hapa:-
[h=3]‘Watanzania 99 wanamiliki Sh193 bil Uswisi'[/h]
madola.jpg
 
Wachumi wa Tanzania tuelimisheni kuhusu hili.

Nimekuwa nikijiuliza ni kwa nini Tanzania ni Nchi masikini mpaka sasa?.

Nauliza swali hilo kwa sababu Nchi hii ina Rasilimali nyingi sana.

Mojawapo ya Raslimali tulizo nazo ni Madini, Mbuga za Wanyama, Gesi, Ardhi yenye Rutuba, Mlima Kilimanjaro na nyingine nyingi.

Sasa ninachojiuliza ni kwa nini Nchi yetu ni Maskini na Rasilimali zote hizo?.

Nawaomba Wachumi watujibie swali hili ili wengi wanaojiuliza tupate majibu.
It all boils down to poor governance.
Lakini kitu kimoja kinachoweza kutukwamua ni miundombinu. Kila sekta ya uchumi itakua endapo tutajenga miundombinu (bandari, reli, barabara na umeme)
 
Hatuna miundo mbinu wakati tumelala au niseme bado tumelala wezetu miaka ya 1920 walianza kutengeneza barabara za uhakika ili kuunganisha biashara.
 
Mleta mada sijakuelewa unasema hii nchi ni masikini au wananchi walio wengi ndio masikini..?
 
mleta mada sijakuelewa unasema hii nchi ni masikini au wananchi walio wengi ndio masikini..?
 
Mojawapo ya Raslimali tulizo nazo ni Madini, Mbuga za Wanyama, Gesi, Ardhi yenye Rutuba, Mlima Kilimanjaro na nyingine nyingi.
Hivi vitu ulivyotaja sivyo vinavyoleta maendeleo kwani hata Mwalimu alishataja kuwa inatakiwa siasa safi, ardhi, uongozi bora na watu.
Lakini hata hivi vikiwepo huenda visisaidie sana, cha muhimu sana ni AKILI. Hata ukimiliki milima Kilimanjaro mia na hata madini yakawa juu ya ardhi badala ya kuchimbwa hatakusaidia chochote kama akili hazitoshi. Na akili sio kama kura za kupitisha katiba mpya (ya Chenge na Sitta) kwamba 'zitatosheshwa'.

Kwa maana hiyo tumekuwa masikini either kwa sababu wengi wetu hatuna akili au tunazo lakini hatuzitumii. (observation ya kwanza ni relevant zaidi nadhani).

 
Back
Top Bottom