Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Tarehe: 15/04/2015 Tanzania ni nchi ya pili kwa uchumi mkubwa miongoni mwa nchi wanachana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ni ya kumi na mbili kwa uchumi mkubwa barani Afrika. Kilimo ndiyo uti mgongo wa Taifa kikiajiri takribani nusu wananchi wake wenye uwezo wa kufanyakazi. Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 34 ya watanzania wanaishi katika mstari wa umaskini. Nchi imekuwa katika mapinduzi ya kiuchumi tangu mwaka 1985 ambapo Tanzania inaachana na uchumi unaomilikiwa na dola na kuacha uchumi umilikiwe na soko. Tanzania ina ukubwa wa km2 947,303, ikiwa na watu milioni 47.4 kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2014. Taarifa za Wikipedia kuhusu uchumi wa Tanzania zinasema, pato la taifa kwa mwaka 2014 limetajwa kuwa Dola za Kimarekani Bilioni 41.33 huku kipato cha mtu mmoja mmoja ni Dola 1,813 kwa mwaka. Tanzania imejaaliwa kuwa na vivutio kadhaa vya utalii ikiwa na pamoja na mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, Mlima Kilimanjaro. Pia ina Ziwa Tanganyika linaloaminika kuwa na urefu kuliko yote barani Afrika. Vilevile Ziwa Victoria na Nyasa yanayoaminika kuwa miongoni mwa maziwa makubwa barani Afrika yanapatikana Tanzania. Kuna mito kadhaa mikubwa, maporomoko ya ardhi, majumba ya makumbusho, mbuga za wanyama, majengo ya kihistoria katika miji ya Bagamoyo, Kilwa, Zanzibar na kwingineko. Haya yote yanaweza kuvutia mamilioni ya watalii toka kona mbalimbali za dunia na kuliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni. Kwa mfano, mwaka 2012 Tanzania ilipokea watalii 1.043.000 ambao waliingizia taifa Sh bilioni 56. Hivyo, licha ya kuchangia fedha kwenye pato la taifa, kama utatangazwa ipasavyo utalii unaweza kutoa mchango mkubwa katika ukuaji uchumi wa taifa na kutoa fursa nyingi zaidi za ajira kwa vijana. Tanzania pia ina utajiri mkubwa wa madini ya aina mbalimbali yakiwemo yanayopatikana Tanzania pekee yaani madini ya Tanzanaiti. Kadhalika, chuma na makaa ya mawe yamethibitika kuwepo sehemu mbalimbali ya ardhi ya Tanzania. Taifa linaweza pia kunufaika na madini ya Urani katika kutekeleza shughuli zake za maendeleo. Ikiwa inapak ana na nchi zisizo na bahari yaani (Land Locked Countries) kama DRC, Malawi, Zambia, Zimbabwe nk Tanzania inayo nafasi kubwa ya kunufaika kiuchumi kwa kutumia fursa ya kuwa na bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na Zanzibar. Nchi hizo hutumia bandari nchini Tanzania kupitishia mizigo yake toka ughaibuni na kadhalika kusafirisha ng’ambo mazao yanayozalishwa nchini mwao hivyo kutoa nafasi ya nchi kunufaika kiuchumi. Ripoti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ya Novemba 2013, Tanzania ina ekari milioni 44 zinazofaa kwa kilimo. Kati ya hizo, ekari milioni 14 zinazolimwa na wakulima wadogo huku ekari milioni 1.5 zinatumika kwa kilimo cha biashara. Taarifa toka Mpango wa Taifa wa Umwagiliaji yaani (National Irrigation Master Plan) zinasema kuwa jumla ya ekari milioni 29.4 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Taarifa hiyo inasema hata hivyo, ni ekari 450,392 tu sawa na asilimia 1.53 zinazotumika hivi sasa kwa kilimo cha umwagiliaji nchini. Licha ya viwanda kuchangia asilimia 22.2 ya pato la taifa viwanda vingi hivi sasa vimekufa na vinavyoendelea kubinafsishwa kwa wageni hugeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa huku mashine na mitambo ikiuzwa kwenye chuma chakavu. Hali hii imefanya malighafi za viwanda zinazozalishwa nchini zisafirishwe kwa ajili ya matumizi ya viwanda nje ya nchi hali inayochangia pia uduni wa bei ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi. Takwimu za sensa ya mifugo ya mwaka 2012 inaonesha kuwa Tanzania ina ng’ombe 21,400,889. Ng’ombe 21,125,251 wanafugwa na wakulima wadogowadogo Tanzania Bara huku 155,624 wakifugwa na wafugaji kama hao Zanzibar. Ng’ombe wengine 120,014 wanafugwa kwenye mashamba makubwa yaliyopo Tanzania Bara. Takwimu za Sensa ya Mifugo za mwaka 2008, Tanzania ina mbuzi 15,085,150 huku idadi ya kondoo ikiwa ni 5,715,549. Mapinduzi makubwa katika matumizi ya mazao ya mifugo kama nyama, ngozi, sufu, kwato na kadhalika yanahitajika nchini ili kutoa fursa ya sekta hii kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi na mendeleo ya Taifa. Jambo ambalo hadi sasa watanzania linawatatiza na kuibua dukuduku la kutaka kufahamu Zaidi ni kuwa licha ya fursa zilizopo, zilizotajwa hapa kwa ufupi na nyingine ambazo hatujaweza kuzitaja: KWA NINI TANZANIA BADO NI MASKINI???
Jumatano April 15 saa nne usiku katika kituo cha Channel Ten atakuwepo Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi) David Kafulila na wageni wengine kujadili mada hii kupitia kipindi kipya cha Mada Motto. usikose.
 
Tarehe: 15/04/2015 Tanzania ni nchi ya pili kwa uchumi mkubwa miongoni mwa nchi wanachana wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ni ya kumi na mbili kwa uchumi mkubwa barani Afrika. Kilimo ndiyo uti mgongo wa Taifa kikiajiri takribani nusu wananchi wake wenye uwezo wa kufanyakazi. Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 34 ya watanzania wanaishi katika mstari wa umaskini. Nchi imekuwa katika mapinduzi ya kiuchumi tangu mwaka 1985 ambapo Tanzania inaachana na uchumi unaomilikiwa na dola na kuacha uchumi umilikiwe na soko. Tanzania ina ukubwa wa km2 947,303, ikiwa na watu milioni 47.4 kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2014. Taarifa za Wikipedia kuhusu uchumi wa Tanzania zinasema, pato la taifa kwa mwaka 2014 limetajwa kuwa Dola za Kimarekani Bilioni 41.33 huku kipato cha mtu mmoja mmoja ni Dola 1,813 kwa mwaka. Tanzania imejaaliwa kuwa na vivutio kadhaa vya utalii ikiwa na pamoja na mlima mrefu kuliko yote barani Afrika, Mlima Kilimanjaro. Pia ina Ziwa Tanganyika linaloaminika kuwa na urefu kuliko yote barani Afrika. Vilevile Ziwa Victoria na Nyasa yanayoaminika kuwa miongoni mwa maziwa makubwa barani Afrika yanapatikana Tanzania. Kuna mito kadhaa mikubwa, maporomoko ya ardhi, majumba ya makumbusho, mbuga za wanyama, majengo ya kihistoria katika miji ya Bagamoyo, Kilwa, Zanzibar na kwingineko. Haya yote yanaweza kuvutia mamilioni ya watalii toka kona mbalimbali za dunia na kuliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni. Kwa mfano, mwaka 2012 Tanzania ilipokea watalii 1.043.000 ambao waliingizia taifa Sh bilioni 56. Hivyo, licha ya kuchangia fedha kwenye pato la taifa, kama utatangazwa ipasavyo utalii unaweza kutoa mchango mkubwa katika ukuaji uchumi wa taifa na kutoa fursa nyingi zaidi za ajira kwa vijana. Tanzania pia ina utajiri mkubwa wa madini ya aina mbalimbali yakiwemo yanayopatikana Tanzania pekee yaani madini ya Tanzanaiti. Kadhalika, chuma na makaa ya mawe yamethibitika kuwepo sehemu mbalimbali ya ardhi ya Tanzania. Taifa linaweza pia kunufaika na madini ya Urani katika kutekeleza shughuli zake za maendeleo. Ikiwa inapak ana na nchi zisizo na bahari yaani (Land Locked Countries) kama DRC, Malawi, Zambia, Zimbabwe nk Tanzania inayo nafasi kubwa ya kunufaika kiuchumi kwa kutumia fursa ya kuwa na bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara na Zanzibar. Nchi hizo hutumia bandari nchini Tanzania kupitishia mizigo yake toka ughaibuni na kadhalika kusafirisha ng’ambo mazao yanayozalishwa nchini mwao hivyo kutoa nafasi ya nchi kunufaika kiuchumi. Ripoti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ya Novemba 2013, Tanzania ina ekari milioni 44 zinazofaa kwa kilimo. Kati ya hizo, ekari milioni 14 zinazolimwa na wakulima wadogo huku ekari milioni 1.5 zinatumika kwa kilimo cha biashara. Taarifa toka Mpango wa Taifa wa Umwagiliaji yaani (National Irrigation Master Plan) zinasema kuwa jumla ya ekari milioni 29.4 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Taarifa hiyo inasema hata hivyo, ni ekari 450,392 tu sawa na asilimia 1.53 zinazotumika hivi sasa kwa kilimo cha umwagiliaji nchini. Licha ya viwanda kuchangia asilimia 22.2 ya pato la taifa viwanda vingi hivi sasa vimekufa na vinavyoendelea kubinafsishwa kwa wageni hugeuzwa kuwa maghala ya kuhifadhia bidhaa huku mashine na mitambo ikiuzwa kwenye chuma chakavu. Hali hii imefanya malighafi za viwanda zinazozalishwa nchini zisafirishwe kwa ajili ya matumizi ya viwanda nje ya nchi hali inayochangia pia uduni wa bei ya bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi. Takwimu za sensa ya mifugo ya mwaka 2012 inaonesha kuwa Tanzania ina ng’ombe 21,400,889. Ng’ombe 21,125,251 wanafugwa na wakulima wadogowadogo Tanzania Bara huku 155,624 wakifugwa na wafugaji kama hao Zanzibar. Ng’ombe wengine 120,014 wanafugwa kwenye mashamba makubwa yaliyopo Tanzania Bara. Takwimu za Sensa ya Mifugo za mwaka 2008, Tanzania ina mbuzi 15,085,150 huku idadi ya kondoo ikiwa ni 5,715,549. Mapinduzi makubwa katika matumizi ya mazao ya mifugo kama nyama, ngozi, sufu, kwato na kadhalika yanahitajika nchini ili kutoa fursa ya sekta hii kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi na mendeleo ya Taifa. Jambo ambalo hadi sasa watanzania linawatatiza na kuibua dukuduku la kutaka kufahamu Zaidi ni kuwa licha ya fursa zilizopo, zilizotajwa hapa kwa ufupi na nyingine ambazo hatujaweza kuzitaja: KWA NINI TANZANIA BADO NI MASKINI???
Jumatano April 15 saa nne usiku katika kituo cha Channel Ten atakuwepo Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi) David Kafulila na wageni wengine kujadili mada hii kupitia kipindi kipya cha Mada Motto. usikose.

CCM ACT hoyeeeeee!

Mnatumia elimu ndogo ya watanzania kuwarubuni ili muendelee kutawala? Siku zenu zimefikia mwisho, maandishi yamechorwa ukutani, ushindwe muda wote huo kuwawajibisha mafisadi, upange mipango miovu dhidi ya raia wenzako; eti gafla ubadilike kuwa malaika mlinzi waooo!

Mungu hadhihakiwi, huwezi kumtumia shetani (evil ways) kuleta baraka, yeye ni mwongo na baba wa huo. But we shall see whose words count, Tanzania njema ni lazima na wala fisadi hawezi kanyaga Ikulu mwaka huu!
 
Majibu yatapatikana leo katika kipindi cha Mada Motto kinachorushwa na Channel Ten kuanzia saa nne usiku. Wageni ni Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
 
Wakuu naomba tujadiliane maada hapo juu. Aliyewahi kuwa kiongozi safi na mzalendo wa chama cha magamba amewahi kusema kwamba ili nchi iendelee ( ipate maendeleo) inahitaji vitu ninne, navyo ni:
1. Aridhi
2. Watu
3. Siasa safi
4. Uongozi bora.
Sasa ni miaka zaidi ya hamsini sasa bado tuna shule za tope na kuezekwa kwa nyasi. Tunashuhudia mafoleni sehemu nyingi za nchi hususani Dar eS salaam kana kwamba nchi haikuwa na planning au projections na wakati huo huo sensa wamefanya karibu kila muongo, sasa sifahamu hizo sensa zilikuwa za nini. Tatizo nini? Je hatuna aridhi? Mbona kuna mapori yenye rutuba ambayo hata hayahitaji mbolelea hayajaguswa? Au tatizo ni watu? Kama tatizo ni watu mbona nchi ina watu weye nguvu na wanafanya kazi kwa bidii sana lakini bado umasikini umewaandama? Au pengine tatizo ni siasa safi? Magamba ndio wenye dhamana na nchi toka uhuru, hivi ni kweli chama cha magamba hakina sera zenye siasa safi za kuleta maendeleo katika nchi? Au labda tatizo ni uongozi bora? Kama ni hilo, mbona magamba wanakemeana wanapogawana mabilioni ya pesa wanazotuambia hazina mwenyewe na wanafanya hivi kwa sababu shule zinafungwa kwa kukosa chakula? Mbona hatuoni wakipeana vyeo kwa kujuana (nepotism), mbona wanatutarifu mamilioni ya wanayotumia kwenda kutanua huku duniani kwa visingizio vya kwenda kutafuta maendeleo, mbona hatujawahi kusikia mambo ya ufisadi ambayo hata Ibilis shetani hawezi akafayafanya, mbona ombwe la uongozi halionekaniki katika nchi yetu, mbona tuna dira safi ya maendeleo, mbona tuna viongozi safi na wazalendo ambao wapo kwa masirahi ya umma sio kwa ajiri yao na ndugu zao wa damu, mbona kuna demokrasia safi, tume huru ya uchaguzi ambayo wadau wote wa siasa wanauwakilishi, mbona hatuna rushwa katika nchi? Mbono vyombo vya dora hususani polisi hawana upendeleo, wapo kulinda masilahi ya jamii na sio kundi fulani la watawara mafisadi? Waheshimiwa tatizo nini, ebu tujadiliane.
 
Hiki chama cha Kijani Kinafanya hii nchi shamba la Bibi wamejisahau kabisa Kila anaeingia madarakani anaona kama karisishwa mali na baba yake.
 
Nashukuru wanabodi kutoa michango yenu kuhusu maada ya umasikini tulionao. Nimejaribu kusoma kwa makini kila hoja na jinsi inavyojengwa. Namnukuu mmoja alivyosema, '' We are poor because we lack the correct attitude. We lack the will to comply with and teach these functional principles of rich & developed societies''.'' ...The difference is the attitude of the people, framed along the years by the education & the culture''. Nimeichukua hii nukuu kwa vire nimeiona kama ndio tatizo tulilo nalo as a hindrance to development. Prem P. Bhalla kwenye kitabu chake cha Magnetic Personality, anasema, '' you are what your basic characteristics, which you inherited from your parents, have made you when they reacted with the circumstances and the environment in which you have grown up''. Ninachotaka kukisema hapa ni kuwa culture iliyotulea ni ya kibaraghara. Niutamaduni usio na discipline, ni utamaduni usio na uzalendo, ni utamaduni ambao ni inhumanity, utamaduni wa wizi, utamaduni wa kutotii sheria, ni culture ambayo ni extravagant. Ndio maana mwizi aliyeiba hela za umma akifika kwao anapokewa kama shujaa. Hivi ndivyo minds/atitudes zetu zilivyo. Kwa msingi huo ndio maana umasikini bado tunao mpaka leo hii zaidi ya miaka hamsini. Sasa kama tatizo ni hilo, nani mwenye wajibu wa kuhahakikisha jamii inajengwa upya? Jibu ni jepesi, ni wale tuliowapa mamlaka ya kutoongoza (magamba). Sasa kwanini wanashindwa, ni wazi kuwa UONGOZI NI MBAYA, unanuka.
 
popote duniani hakuna serikali inayogawa hela kwa watu wake ili wawez kujikimu maisha. serikali huwapa watu wake elimu bora ili wao wenyewe wajiletee maendeleo. julius nyerere. je viongoz wetu wanaotaka uongoz wanaelewa hilo? sasa ni wakati wa kuwauliza kama wana mawazo hayo sio kuwaza sacoss kila siku na ujasiria mali nje ya hapo hawana wazo mbadala
 
zawadi kubwa na murua serikali inaweza kuwapa watu wake ni elim bora tu si bora elimu kwa sasa serikali ya nchi yetu inawapa watoto wa nchi yake bora elimu je umaskin utatoka au unaongezeka
 
Kwa wana ccm,nijibuni haya nakila jibu ujue lipo swali tena la kwanini?Jibu lake pia lipo swali kwa nini?Moja,kwa nini nchi ni maskini?Kwanini tunaishi chini ya dola kwa siku?
Tatu:kwanini wanafunzi wakaa chini?
Nne:kwanini wazazi walala chini hospital?
Nne:kwanini wanafunzi walofaulu kwenda kidato cha tano wakose nafasi kisa chakula? Ni machache tu naukumbuke kila jibu utalonipa mbele yake lipo swali kwanini..?
Mfano,ukijibu sababu watanzania niwavifu ...nakuuliza kwa nini?
 
Jaman nimeamua kuandika haya kuwauliza wanaccm kwa ujumla kuwa kwann kila wakati wanajinasibu kuondoa umaskin wa watanzania lakin hauishi.Je ni kwamba wanaccm wameshindwa kuondoa umaskini wetu na wanashindwa kukir hilo...??Mpaka lin ccm watakiri kuwa watanzania wameondokana na umaskin....???Tafakari muhim sana.....
 
Afyao
Elimu
Ajira
mabasi ya kasI hatupandi kivuko tutapiga mbizi nauli hatuna
 
Jaribu hata kutumia akili kidogo

Afya
Kuna zahanati zmejengwa kila kata na Serikali tukufu ya ccm
Zimemaliza kero za wakina mama wanaitembea umbali mrefu keende kutafuta matibab
Waalize ndugu zako wanaokaa vijijin watakuambia
Tena raia wanaishukuru tu serikali

Elimu
Jmn kuhusu suala la elimu
hata kama ww ni kipofu huwezi kusema eti serikali haijafanya kitu kuhusu serikali

Compare shule za sekondari zilijuwa ngap wakati jk anaingia madarakan
Na leo shule hizo ziko ngap na zmesaidia vipi kupunguza idad ya watu wanaoishia shule ya msingi.
Hapa katikati palijitikeza tatzo la ukosef wa maabara na walimu wa kutisha
lakin serikal tukufu ya ccm imelifix hilo na kama unakumbuka
Juz juz kulikuwa na shinikizo la ma DC ambao maabara hazjakamilika wakamilishe na wamefanikiwa

Ajira
Serikali yetu imejitahidi kwa kias chake katika suala la ajira
Kwa kuapply njia zifuatazi
1.kuongeza vyuo vya elimu ya Ufundi kwa vutendi kama veta
Na vyuo mbali mbali vya maendeleo ya jamii
Hivyo kupunguza tatzo la ajira

2 . kupitia wizara zake mbalimbali
kama wizara ya elimu ambayo imekuwa mstar wa mbele katka kutoa ajira mbalimbali


Mabasi yaendayo kasi


mradi huo umeshajamilija
Na bashukuru serikali yetu imetimiza hilo na uzinduz ulikuwa jana
Hilo sitalizungumzia maana mmejionea wote
 
unaongelea tatizo la maabara wakati walimu na wananchi ndio wamechangishwa pesa ya maabara huku bilioni 324 za escrow zilizofisadiwa na serkal ya ccm zingetosha kabisa kumaliza tatizo la maabra nchini,ubora wa elimu ndio unaouongelea au wingi wa majengo ya shule bila elimu bora? umesema kuhusu ajira serkal imeongeza vyuo vya ufundi,hebu fafanua hapo vyuo vya ufundi vimepunguzaje tatizo la ajira?




Atleast unaonekana unahitaji kujifunza kitu
Saafi

Suala la vyuo vya mafunzo kwa vitendo limepunguza kwa kiasi kikubwa suala la ajira jana ufuatavyo

1. Wanafunzi wa vyuo guvyo
Mfano veta
Wamekuwa wakifundishwa elimu ya kujiajiri
Mfano ufundi

Ambapo wakitoka hapo hawahitaji kusubiri kuajiriwa na mtu bali wabajiajiri wenyew
Na ndio sera za nchi nyingi zilizo endelea
Wanasema
Kabla hujawaza kuajiriwa
Waza kuajiri watu elfu kumi
nadhan kijana utafanikiwa sana
 
Back
Top Bottom