Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Maelezo yako ni mazuri ila Mimi naamini Mungu anaipenda sana Tanzania licha ya mabaya yote tunayoyatenda . Kuhusu umaskini wetu sababu zake ni nyingi lakini kubwa ninaloliona ni mgawanyo mbaya wa raslilimali ambazo zinawanufaisha wachache...
Ila awe mwenye kujali utu, asiye na upendeleo wala ubaguzi, huyo anayo nafasi ya kutupelela mbele.
 
Kuna wakati najiuliza tumemkosea nini Mungu wetu mpaka huu umasikini wa watanzania upo kwa miaka 60 sasa licha ya Mungu kuibariki nchi hii kwa kuipa raslimali karibu kila mkoa lakini wananchi wake ni masikini wa kutupwa?

Raslimali zilizopo Tanzania hakuna nchi ya kufanana nayo Afrika Mashariki na kati.

Viongozi wetu kwa miaka 60 ni wale wale chama ni kile kile lakini wameshindwa kuzitumia raslimali tulizopewa na mungu kuwaondolea umaskini wananchi wake, badala yake wameamua kuwatoza kodi za maumivu na kukopa nje mpaka deni la taifa limefika tril 71 lakini umaskini upo pale pale.

Binafsi naanza kuamini Tanzania tuna tatizo na Mungu ni wakati kama taifa kufanya maombi na kuombana msamaha kwa maovu tuliyofanyiana ili Mungu arudishe upendo wake kwa nchi tupate maendeleo na wananchi wanufaike na kuondokana na umaskini kwa kutumia raslimali alizotupa Mungu.

Kuna watu wapo magerezani kwa miaka kwa kesi za kuonewa, kuna watu wamepigwa risasi, wamepotea, wameuawa kwa uonevu tu.
Yote hayo Mungu hapendi na hasira ya Mungu huwa ni mateso kwa watu.
Wewe umefanya jitihada gani kujikwamua?

Bila kuwa na akili hata uwe unalala kwenye dhahabu utaishia kuwa maskini.
 
Kila binadamu amezaliwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yake yaani hahitaji kufundishwa.

Fanyeni kazi tafuta hela acha kutegemea watu watakupa pesa
Vijana wanakusikia ujue, wakianza kukushimukia kama mwewe hata sikutetei, kwani mwenyewe ulikataa kuwepo miongoni mwa maskini 🤔
 
Hii Nchi ina mazombi na walalamishi Sana, badala ya kuji convene wakiona changamoto waende kwenye mamlaka za serikali Ili watatue wanaishia kulalama na kulaumu, useless.
 
Tatizo la nchi hii ni matumizi makubwa ya serikali, angalia kuanzia Rais mpaka wakuu wa idara, mishahara mikubwa, marupurupu, na mengine bado magari n.k
Umesahau ujenzi wa mahekalu ya viongozi wanaostaafu pamoja na mafao yao yaliyonona. Pamoja na hayo yote matibabu yao tunayagharamia.

Kuna kikundi kidogo kinachoishi kama wako Switzerland.
 
Kama uko katikati ya masikini,wewe pia ni masikini wa kutupwa. Hakuna cha nini wala nini,hata ujifanye kukataa wewe ni kimasikini tu.
Nitake radhi.

Umasikini ni kushindwa kumudu basic needs.

Mahitaji yangu yote ninayapata kikamilifu. Malazi bora, mavazi, chakula.

Sasa iweje uniite masikini?
 
Wewe ndiye bilionea nani hapa nchini? Au umevembewa machalari umekuja kuharisha hapa mtandaoni.Mtoa mada anaongelea nchi kwa ujumla wewe unaleta porojo zako ambazo hakuna hata anayezitambua hapo kwenye ukoo wenu.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Nimejibu nilichoulizwa.

Mtoa mada kasema Watanzania ni masikini.

Nikamjibu kwamba siyo wote masikini. Mimi siyo moja wapo ya hao masikini anaowasema.

Kwani utajiri ni kuwa na mabilioni tu?
 
Nitake radhi.

Umasikini ni kushindwa kumudu basic needs.

Mahitaji yangu yote ninayapata kikamilifu. Malazi bora, mavazi, chakula.

Sasa iweje uniite masikini?
Hiyo kanuni ya kwako peke yako. Kanuni za kwako peke yako ziwage nyumbani kwako tu. Kanuni za dunia zinaeleweka,zina vigezo vyake. Na nchi kuitwa ni nchi masikini,maana yake wananchi wake asilimia kubwa ni masikini. Mfano Tanzania matajiri wanaweza kuwa 10% tu. Hiyo itaitwa masikini.
 
Nitake radhi.

Umasikini ni kushindwa kumudu basic needs.

Mahitaji yangu yote ninayapata kikamilifu. Malazi bora, mavazi, chakula.

Sasa iweje uniite masikini?
Kwa mtazamo wako wew ni masikani na Kama ni mbunge Basi nyie ndio chanzo Cha huu umasikini na ufukara uliopo. Elewa kwamba umasikini ni neno ambalo ni husianishi na vitu vingine. Usifikirie kuhusu hivyo vyakula, mavazi na malazi.

Fikiria mbali kuhusu Uhuru wa kifedha, kuigusa jamii inayokuzunguka, Uhuru wa kufikiri, kupatwa fursa za kuchangamana na jamii nyingine, kupatwa vitu vinavyokuondolea sonono, ushiriki wako kwenye kujenga taifa, nkz
 
Hiyo kanuni ya kwako peke yako. Kanuni za kwako peke yako ziwage nyumbani kwako tu. Kanuni za dunia zinaeleweka,zina vigezo vyake. Na nchi kuitwa ni nchi masikini,maana yake wananchi wake asilimia kubwa ni masikini. Mfano Tanzania matajiri wanaweza kuwa 10% tu. Hiyo itaitwa masikini.
Bila shaka akisoma maelezo haya, lazima atafuta akaunti yake ya JF. Analeta ubinafsi kweli masuala mapana ya maslahi ya taifa? Pathetic!
 
Kwa mtazamo wako wew ni masikani na Kama ni mbunge Basi nyie ndio chanzo Cha huu umasikini na ufukara uliopo. Elewa kwamba umasikini ni neno ambalo ni husianishi na vitu vingine. Usifikirie kuhusu hivyo vyakula, mavazi na malazi. Fikiria mbali kuhusu Uhuru wa kifedha, kuigusa jamii inayokuzunguka, Uhuru wa kufikiri, kupatwa fursa za kuchangamana na jamii nyingine, kupatwa vitu vinavyokuondolea sonono, ushiriki wako kwenye kujenga taifa, nkz
Hawezi kuelewa, because amezaliwa kwenye upigaji, amekulia kwenye upigaji na asipobadilika, atazeekea kwenye upigaji!
 
Ttzo ni vyama pinzani vya siasa visivyo imara ndo vinasababisha yote haya yatokee
Leo ukiitoa CCm madalakani utampa nchi nan
Chadema chama kina zaidi ya miaka 20 hakina ofisi hakina katiba, chama cha ukanda
TLP ni yale yale
CUF kila sku wanagombea vyeo
ACT bado wapya
NCCR chama ya mbatia na akijui kinataka nn nchi au CCM b
 
Back
Top Bottom