Kwanini watoto wa viongozi wa umma hawasomi shule za umma?

Kwanini watoto wa viongozi wa umma hawasomi shule za umma?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Watoto na wajukuu wa viongozi wakuu wa umma (Rais, Marais wastaafu, mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya, wabunge, wakurugenzi wa wilaya, wakuu wa mashirika ya umma, wakuu wa chama tawala, nk) hawako kwenye shule za umma wanazozijenga na kuziongoza kwanini? Ni watoto na wajukuu wa wakulima, wafugaji na watumishi wadogo wa umma wanaosoma kwenye shule za umma. Kuna nini kwenye shule za umma? hakuna nini kwenye shule za umma kulinganisha na shule wanakopeleka watoto wao? Ni sawa?

Hali hii iendelee hivihivi au kuna kitu kifanyike?
 
Watoto na wajukuu wa viongozi wakuu wa umma (Rais, Marais wastaafu, mawaziri, wakuu wa mikoa na wilaya, wabunge, wakurugenzi wa wilaya, wakuu wa mashirika ya umma, wakuu wa chama tawala, nk) hawako kwenye shule za umma wanazoziongoza kwanini? Ni watoto na wajukuu wa wakulima, wafugaji na watumishi wadogo wa umma wanaosoma kwenye shule za umma.

Hali hii iendelee hivihivi au kuna kitu kifanyike?
Hizo zisizo za umma nani atasoma sasa kama wote wakienda huko?!
 
Ndiyo ujue Sasa shule za umma hazikidhi mahitani ya soko.zipo Kwa ajili ya kutengeneza tabaka la kutawaliwa.mtoto wa kiongozi kama rais utamkuta anasoma nje na ikiwa hapa ndani atakuwa anasoma internation na siyo hivi vi medium vya milioni Moja na nusu Hadi mbili. Na wakimaliza shule wanachotewa tu pesa waanzishe biashara na siyo kuajiriwa na ikiwa kuajiriwa lazima iwe kuanzia ukurugenzi,ubunge,uwaziri n.k.mnaosoma hizi kayumba ndiyo wengi wanaangukia ualimu,askari nurse nik
 
Ni kwa sababu hizo shule zimejengwa mahsusi kwa ajili ya watoto wa masikini! Na siyo matajiri wakkwemo hao watoto wa wanasiasa wanaojilimbikizia mali kutokana na kodi za wananchi masikini.

Watoto wa wanasiasa wanasoma Ulaya, Marekani, Feza, St Francis, nk.
 
Hizo zisizo za umma nani atasoma sasa kama wote wakienda huko?!
siku moja nyuma nilikwenda ofisini kwa mo, nikakuta maji ya kunywa ya chupa ya brand nyingine badala ya maji yake ya masafi. Tangu siku hiyo na mimi niliyakataa maji ya masafi maana sikujuwa yalikuwa yana nini hadi mwenye nayo hayanywi.

Lazima tuchunguze kwa kina kwanini watoto na wajukuu wa viongozi ambao ndio watunga sera na watunga sheria hawapeleki watoto na wajukuu wao kwenye shule hizi, zina nini?
 
Kuna siku wabunge walichachamaa kweli lugha ya kisawahili iendelee kufundishwa primary, eti tutapoteza utamaduni wetu, nikacheka sana maana najua hakuna mtoto wa mbunge anayesoma huko, wanawachora wananchi tu
Mkuu kiswahili ndio lugha ya taifa kufundishwa shuleni ni wajibu,lakini kujifunza lugha ya kiingereza kama tunavyojifunza katika masomo mengine kama hesabu,chemia na mengine kwa kuwa kiswahili ni changa hahijitosherezi kwenye nyanja nyingine.
Matokeo yake hata kazi ya udereva vijana wetu kupata kazi Saudia,Iraq,Bahrain,Kuwait, Qatar, UAE,hawapati kwa kuwa communication skills wanataka English tena basic.Lakini Kenya na Uganda wako madereva kwa maelfu.
 
Mkuu kiswahili ndio lugha ya taifa kufundishwa shuleni ni wajibu,lakini kujifunza lugha ya kiingereza kama tunavyojifunza katika masomo mengine kama hesabu,chemia na mengine kwa kuwa kiswahili ni changa hahijitosherezi kwenye nyanja nyingine.
Matokeo yake hata kazi ya udereva vijana wetu kupata kazi Saudia,Iraq,Bahrain,Kuwait, Qatar, UAE,hawapati kwa kuwa communication skills wanataka English tena basic.Lakini Kenya na Uganda wako madereva kwa maelfu.
Mkuu namaanisha masomo mengine kama sayansi kufundishwa kwa mtaala wa kiswahili, afu wakifika form 1 wanabadilishiwa GIA angani
 
Back
Top Bottom