Kwanini watu hawawapi watoto wao majina haya?

Kwanini watu hawawapi watoto wao majina haya?

Umenikumbusha huko meru miaka fulani kuna Dogo nakumbuka alikuwa wanamuita Frimasoniii, Darasani unasikia "Frimasoni Elias Kibeda" "Nipo mwalimu"
 
Kuna dogo mmoja alikuwa anaitwà yuda
Nakuapia hakika yule dogo alikuwa na tabia za kuwasnitch wana balaa..

Kitu sio kitu kawasnitch yaani ata mkipewa assignment yy anawahi kupeka kwa lecture faster kuliko nyinyi ili tu muonekane wazembe na mmechelewa...
Majina kweli yanaumba..
Nimecheka sana,
Huyu YUDA anafanana na Rafik wangu wa udogoni na shule ya msingi.....
Ali itwa NASIBU,
Sijawai kua na rafik mbinafsi kama Huyu....
Ntaeleza matukio yake kadhaa.....

Kuna siku tulikua tunatembea mitaa flani tukapita mtaa mmoja kulikua na Mbwa mkali sana...NASIBU akamchokoza......

Mbwa akaanza kutukimbiza Kwa speed kali tuka Anza kutimua mbio balaa Mimi nikamzidi speed NASIBU nikawa mbele......NASIBU KUONA ivyo akanipigia Ngwala Kwa makusud kabisa nikadondoka na yeye akadondika😊.....Nikapata wazo fasta kumrushia Mbwa michanga NDIO ikawa pona pona yetu......

Kuna siku Moja jion Ali iba Bata dume kwao akanidanganya akaniletea home nimhifadhie wanarekebisha banda.....kwakua home sisi tulikua tunafuga Nika mkubalia bila kuwa ambia nyumbani...akinambia kua Kwao hakukua na nafasi.. Mimi bila kujua Nika muhifadhi...... Jion kindumbwe ndumbwe...kaja na mama Ake huku anatandikwa balaa kua kaiba Bata na kamleta nyumbani kwetu...
yule Bata ule mchana akapotea Bata wana mtindo wa kutoroka ivyo na hatukumuona tena....
Mama Ake akawa na mdomo sana ilibidi mama angu ampe Bata mwingine....

Wakati Tupo darasa la sita alimwandikia mwanafunzi barua kumtongoza ikadakwa na jamaa mmoja kiherehere sana A.K.A mdomo wa kuku😊🤓
Jamaa akaipelekwa Kwa mwalimu wa darasa..
Alipo kua anahojiwa na mwalimu akanitaja Mimi ndie nilie msaidia kuchora Yale maua ya makopa kopa (love)........wakati hata sikua nahusika.....hili zoezi likashindikana🤓🤓 for sure nasib alipenda kupata matatizo akiwa na Mimi.....

Na matukio mengi sana na Huyu jamaa Kwa Sasa ngoja ni ishie hapo🤓🤓🤓🤓
 
Umenikumbusha huko meru miaka fulani kuna Dogo nakumbuka alikuwa wanamuita Frimasoniii, Darasani unasikia "Frimasoni Elias Kibeda" "Nipo mwalimu"
Haahaa 😂😂🤣🤣 Kuna watu watakuja hapa watasema Chai......
 
Kuna siku niliona Insta kuna wazazi Baba na Mama wamevaa jezi za Yanga wamebeba mtoto wao mchanga huku wamepiga picha na Mayele halafu wakaandika mtoto anaitwa Fiston Mayele.

Ujue niliwashangaa eeh!
Umbumbumbu. Enzi hizo Ali Kiba ndo anatamba kwenye music, kuna dada mmoja kijijini (RIP) kazaa mtoto wa kiume kampa jina Alikiba! Hakujua kuwa ni majina mawili yeye kaunga!
 
Back
Top Bottom