Kwanini watu wa mikoani wanapenda kusalimia salimia?

Kwanini watu wa mikoani wanapenda kusalimia salimia?

Kiufupi sijaona tatizo lolote kwenye salamu, ingawa mleta mada anaweza kuona yupo sahihi ila si vyema kwa kuwa ameingia kwa watu wenye utamaduni huo. Itikia salamu then endelea na mambo yako. Nyodo unazozionyesha kwa watu hazifai, vinginevyo ujihakikishie unajitosheleza kwa Kila kitu na hautowahitaji hao watu kwa lolote lile.. Inawezekana akipata changamoto akiwa kwa watu pori (kama alivyowaita) ataleta watu wake kutoka Dar waje wamsaidie
Ndio maana nikamwambia huyo no limbukeni na hajatembea. Binafsi nilikuwa sisalimii watu lakini baada ya kukaa na wapoli Poli nimejifunza kusalimia watu.

Kuna siku tulienda na jamaa yangu sehemu wakati wa kurudi tukapotea Giza likaingia alafu Piki Piki ikaisha mafuta. Ikabidi tutembee kufika sehemu tukasikia mbwa wanabweka ikabidi twende kwa kufuata sauti za mbwa maana giza lilikuwa tororo kufika kwenye mji jamaa akatumulika na tochi, sikumfahamu huyo jamaa Lakini yeye alikuwa ananifahamu;
Ilibidi nimuulize mbona ananifahamu alafu simfahamu. Akanikumbusha Kwa kuniuliza wewe si ndio ulipoteza ufungu wa gari nyeupe nikamwambia ndio Mimi; jamaa akatuuliza mnashida gani tukamweleza akachukua mafuta akatupa tukapewa na maziwa tukanywa.
Wakati tunaondoka akasema nimekupa mafuta kwa sababu hujisikii, unasalimia watu na lift unatoa. Akatuelekeza njia tukasepa

Imagine kama ningekuwa kama mleta mada siku hiyo ingekuwa je?
 
Habari wana JF

Niko shamba kwa mitikasi ya hapa na pale, yaani kila mtu anasalimia, kwa siku unasalimiwa zaidi ya mara 200

Mambo ya kijinga sana na ni code za kishamba sana, unakuta una mawazo yako mtu ana ku-distract halafu cha ajabu hakujui na hiyo salamu haijengi chochote.

Kwa hesabu ya kawaida energy unayotumia kujibu watu 200 ukii-conserve unaweza ukafanya jambo kubwa la msingi.

Tusalimie watu tunaowajua na tuwe tunamaanisha, vinginevyo tunachoshana. Mmesikia nyinyi wapori pori?
Wewe mwenyewe umeanza kwa kutusalimia "habari wana jf"... Utatupotezea muda wetu kukujibu na pia haitasaidia.😀
Nb: Salaam ndio mwanzo wa kujuana
 
wee bwege kweli yani.dar pamekushinda kutafuta umeenda mkoa unataka kupeleka ujinga wako huko?siungebaki dar ambapo watu hawana habari hata najirani tuu.kiufupi ndio Mana hujafanikiwa dar nihuo ujeuri wako.salimia watu utapata na kujua vingi vya faida ndezi we.
You are so bitter
Huli ukashiba au?
 
Kwa jibu hili ulikuwa na maada Gani sasa kupost thread ya namna hii, si ungebaki na Imani yako tu kama ulilijua Hilo. Umeleta mada ukitegemea attention na support lakini imekuwa vice versa umekutanishwa na vikombe
Umebaki kupaniki tu
Mkuu, umeuliza swali la muhimu sana. Ukileta uzi humu JF, ina maana unahitaji mjadala na kupata mtazamo na uzoefu wa members wengine. Lengo ni kujifunza na kuwekana sawa. Sasa mleta mada anataka kutudictate badala ya kuacha mjadala uende vyema
 
Wewe mwenyewe umeanza kwa kutusalimia "habari wana jf"... Utatupotezea muda wetu kukujibu na pia haitasaidia.😀
Nb: Salaam ni ndio mwanzo wa kujuana
Hakuna hoja kwenye Uzi wake Bali ni majigambo tu na kujiona yeye ndio kontawa ulimwengu huu. Kaanza na salamu ya nini hapa wakati anaikemea? Au anatujua sisi hadi atusalimu??
 
Habari wana JF

Niko shamba kwa mitikasi ya hapa na pale, yaani kila mtu anasalimia, kwa siku unasalimiwa zaidi ya mara 200

Mambo ya kijinga sana na ni code za kishamba sana, unakuta una mawazo yako mtu ana ku-distract halafu cha ajabu hakujui na hiyo salamu haijengi chochote.

Kwa hesabu ya kawaida energy unayotumia kujibu watu 200 ukii-conserve unaweza ukafanya jambo kubwa la msingi.

Tusalimie watu tunaowajua na tuwe tunamaanisha, vinginevyo tunachoshana. Mmesikia nyinyi wapori pori?
Mtuache,usitake tuige tabia zenu huko,kila kukicha kila mtu yuko mbio,barabarani utadhani anafukuzwa,huo muda wa kusalimia atautoa wapi...
 
Back
Top Bottom