Kwanini watu wa mikoani wanapenda kusalimia salimia?

Kwanini watu wa mikoani wanapenda kusalimia salimia?

Habari wana JF

Niko shamba kwa mitikasi ya hapa na pale, yaani kila mtu anasalimia, kwa siku unasalimiwa zaidi ya mara 200

Mambo ya kijinga sana na ni code za kishamba sana, unakuta una mawazo yako mtu ana ku-distract alafu cha ajabu hakujui na hiyo salamu haijengi chochote.

Kwa hesabu ya kawaida energy unayotumia kujibu watu 200 ukii-conserve unaweza ukafanya jambo kubwa la msingi.

Tusalimie watu tunaowajua na tuwe tunamaanisha, vinginevyo tunachoshana. Mmesikia nyinyi wapori pori?
Kuna Miafrika mitaahira inafikri kuiga mila za Wazungu ndio maendeleo hayo! Utakuwa umelelewa kwenye li familia la hovyo hovyo, pengine la Singo mazafanta!
 
Fikiria upo katika mazingira ya ugenini,umepatwa ajali unataka kusema watu wakuache mpaka waje wanaokujua ? Acha maringo salimia watu
huko mikoani na vijijini watu wamekua wabaya zaidi, kama una experience ya kusafiri omba Mungu usipate tatizo.
 
Kuna Miafrika mitaahira inafikri kuiga mila za Wazungu ndio maendeleo hayo! Utakuwa umelelewa kwenye li familia la hovyo hovyo, pengine la Singo mazafanta!
Jibu hoja mkuu, ujinga unaondolewa na elimu, usione aibu kuwa mjinga, njoo utibiwe
 
Usiwe hivyo mkuu, jifunze kuishi kulingana na mazingira.itikia salamu hizo Wala usichoke ikiwezekana Anza wewe ukiwakuta.

Watu wako very hospitality, hukaribisha chochote bila kinyongo au kumjaribu mtu, hawana unafiki
Muache ajifanye anajua watamsusa mpaka atashangaa. Yaani huyu ni mshamba kweli kweli. Yaani hapo kajiona mjanjaa
 
Ni kama mimi tu, shikamoo zimekuwa nyingi mpaka kero. Naamkiwa mpaka na vijana wakubwa. Naamkiwa mpaka kwenye sms. Kwenye bus unaambiwa "mzee onyesha tiketi". Unajiuliza hii ni mzee ya kishkaji au ndio uzee tayari?!

Nilikuwa naboreka ila hakuna jinsi. Ila kwa vile sijafikisha 40 bado nakula kula ujana

Uzee ndio huo Mzee 😂😂😂

Wazee wenyewe haelewi imekuaje kuaje wamekuwa wazee kwani wanaona walizaliwa juzi tuu hapa. Yaani hawaelewi kabisa
 
Mkuu, muda ni fedha, uwezi tumia nusu ya siku yako kuulizana mambo ya kipuuzi, mtu anakuuliza haujambo wakati uko road, ungekua na shida si ungekua hospital au rumande. Tumia kichwa kufikiri siyo kusukia rasta madam
Kama muda ni hela na unautumia vizuri leo umefika kwenye hizo fedha
 
Hakuna hoja yoyote hapo zaidi ya ushamba na ulimbukeni. Mtu yeyote aliyestaarabika na mwenye exposure hawezi kuja na hoja kama hii. Wewe uko shamba ambako watu wanaishi as a community, na unapita tu lakini unaona wanachokifanya sio sahihi. Huo ni ushamba uliopitiliza.
Kwa hivyo ukiwa shamba ukaona watu wanakunya vichakani na wewe ukanye vichakani, siyo kuwajengea vyoo? Is it? Hapo ndipo akili yako ilipofikia mwisho?
 
Umenikumbusha kabila la WANYIHA huko mbozi mkoa wa songwe. Yaani lazima mtu akusalimie salamu ndefu then akwambie pole na kazi, Sasa mimi hicho kipindi hata kazi sina, nabaki kushangaa tu ni kazi gani hii nayopewa nayo pole?? Au hawa watu wananipaga kazi za usiku bila kujua, Maana nao ni wataalam kwelikweli Hawa wanyiha
 
Kwa hivyo ukiwa shamba ukaona watu wanakunya vichakani na wewe ukanye vichakani, siyo kuwajengea vyoo? Is it? Hapo ndipo akili yako ilipofikia mwisho?
Mfano gani huo sasa mkuu, salamu ina shida gani? sisi huku vijijini tunaishi kama ndugu na wote tunafahamiana. Lazima tujuliane hali, hata kama napita nje ya nyumba ya mtu nitamuita nimsalimie. Tukiona mgeni ni kama tumemuona ndugu yetu, na ukiwa na shobo wanakushangaa sana. Huwa tunapokea wageni toka mikoa mingine na kupitia salamu wanakuwa sehemu yetu. Hata hao volunteer toka nje wakija, wanajiblend kirahisi kupitia salamu. Wewe wala hutokaa huko sana, salimia watu, then utarudi ulikotoka. Huwezi lazimisha mabadiliko kwa namna hiyo.
 
Umenikumbusha kabila la WANYIHA huko mbozi mkoa wa songwe. Yaani lazima mtu akusalimie salamu ndefu then akwambie pole na kazi, Sasa mimi hicho kipindi hata kazi sina, nabaki kushangaa tu ni kazi gani hii nayopewa nayo pole?? Au hawa watu wananipaga kazi za usiku bila kujua, Maana nao ni wataalam kwelikweli Hawa wanyiha
Nimecheka kwa nguvu sana, ni code za kipori pori sana
 
Hakuna hoja yoyote hapo zaidi ya ushamba na ulimbukeni. Mtu yeyote aliyestaarabika na mwenye exposure hawezi kuja na hoja kama hii. Wewe uko shamba ambako watu wanaishi as a community, na unapita tu lakini unaona wanachokifanya sio sahihi. Huo ni ushamba uliopitiliza.
NAKAZIA
 
Mfano gani huo sasa mkuu, salamu ina shida gani? sisi huku vijijini tunaishi kama ndugu na wote tunafahamiana. Lazima tujuliane hali, hata kama napita nje ya nyumba ya mtu nitamuita nimsalimie. Tukiona mgeni ni kama tumemuona ndugu yetu, na ukiwa na shobo wanakushangaa sana. Huwa tunapokea wageni toka mikoa mingine na kupitia salamu wanakuwa sehemu yetu. Hata hao volunteer toka nje wakija, wanajiblend kirahisi kupitia salamu. Wewe wala hutokaa huko sana, salimia watu, then utarudi ulikotoka. Huwezi lazimisha mabadiliko kwa namna hiyo.
Mkuu, huwezi lazimisha mimi nitafakari au kuchakata vitu au mambo kwa namna yako, wewe amini unacho aminini na mimi naaamini ninacho amini
 
Habari wana JF

Niko shamba kwa mitikasi ya hapa na pale, yaani kila mtu anasalimia, kwa siku unasalimiwa zaidi ya mara 200

Mambo ya kijinga sana na ni code za kishamba sana, unakuta una mawazo yako mtu ana ku-distract alafu cha ajabu hakujui na hiyo salamu haijengi chochote.

Kwa hesabu ya kawaida energy unayotumia kujibu watu 200 ukii-conserve unaweza ukafanya jambo kubwa la msingi.

Tusalimie watu tunaowajua na tuwe tunamaanisha, vinginevyo tunachoshana. Mmesikia nyinyi wapori pori?
Hii sio sawa. Kijijini wanajua thamani ya Salam. Acha tuendelee na utamaduni wetu.
 
Back
Top Bottom