Kwanini watumishi wengi wa Serikali wana hali duni kiuchumi?

Kwanini watumishi wengi wa Serikali wana hali duni kiuchumi?

Habari za kazi wanajamvi...
Kiuhalisia swala la watumishi kuwa na madeni kila kona ni jambo la kawaida sanaaa... na hili linanipa maswali mengi sana bila majibu kwasababu watumishi wa vyeo vya juu na kwa uchache wanahali nzuri ya kiuchumi ila wengi hawana haki nzuri Tatizo liko wapi..?? Na nini kifanyike kutatua swala hilii??
Nakaribisha mawazo yako ili wote tujifunze ili iwe msaada kwa watumishi wa serikali na wasio watumishi wa serikali.
Inategemea upo sekta ipi ya serikalini
 
Habari za kazi wanajamvi...
Kiuhalisia swala la watumishi kuwa na madeni kila kona ni jambo la kawaida sanaaa... na hili linanipa maswali mengi sana bila majibu kwasababu watumishi wa vyeo vya juu na kwa uchache wanahali nzuri ya kiuchumi ila wengi hawana haki nzuri Tatizo liko wapi..?? Na nini kifanyike kutatua swala hilii??
Nakaribisha mawazo yako ili wote tujifunze ili iwe msaada kwa watumishi wa serikali na wasio watumishi wa serikali.
Suala liko hivii...

Mtu akipata ajira ya kwanza, anataka kuishi "ki-tumishi". Atakopa hela fasta bank au saccos ili anunue ndinga, abadilishe gheto kiaina na akijiongeza kidogo anunue plot. Wakati huo wote anaendelea kujiachia kulingana na hobby yake..akija kushtuka mzigo umekata ndani ya mwezi,anaendelea kula bata kwa mkopo kwa kuwa kaishaaminiwa na jamii kwa kipindi kifupi, slip yake ambayo imekatwa lile rejesho anaitumia tena kulipia madeni kule maeneo yake. Hali inakuwa hivyo kila mwezi, mshahara hautoshi! Baada ya miaka 2,3 ana-top-up kwenye ile taasisi yake au anauza deni kwenye taasisi nyingine, akikaza anainua kidogo kule kwenye plot alafu anarekebisha ndinga kwa kuwa ishaanza kuzingua (kama bado anayo), mchele mwengine anajiachia kiaina, huku makato yakiwa yameongezeka na ameishakariri sauti na shift za Customer care wa Umoja loan, Nipige tafu, Bustisha, kwenye mzao n.k.. Usisahau pia ana majukumu ya kifamilia! Kwa kweli PESA HAZIMTOSHI!
 
Ni kwa sababu matumizi yetu yanazidi kipato af mambo mengi tumezungukwa na masikini wengi mno na wengine hatuna choyo lazima tuwafurahishe tuombwe pesa
Hapo kuna ukweli fulani hivi. Enzi zetu za Mwalimu Nyerere mfanyakazi wa serikali alikuwa hawazii kuwa na gari lakini leo hii kijana akishapata ajira tu anakwenda kuchukua mkopo wa gari na hajui kwamba pale ni kujifilisi tu.

Pia atataka maishaa makubwa kuliko kiwango chake na mpango wa kuweka akiba hana hata kidogo wakati umri ndiyo unakwenda.

Aidha humu vijana wengi hujisifia mipango yao ya kando na fedha wanazohonga hao akina dada bila ya kujali familia.
Vijana amkeni na muhakikishe munasave hata kama ni shilingi elfu kumi kwa mwezi siyo usubiri pension tu.
 
Dah umekomenti kibwege Sana ila Ni ukweli Mchungu...Tumezunguzwa na waombaji na kuwanyima Ni ngumu Sana...hapo kutoboa Ni mbinde
Kwa mfano mimi binafsi bado mwajiriwa mpya per diem yangu bado 80k tuombe mpya ya mama irudi ya 150k...sasa imagine niko field ya siku 14...
Mahitaji yangu
Lodge 20000 kwa siku
Chakula na maji 15000 kwa siku
Ukaombwa home uchangie rambirambi lets say 50000
Hapo bado una familia nyumbani umeiachaje..bando,

Haya kama ndo mlevi ukienda tu bar ukisema unywe bia zako tano ukalale mara kaja mlevi mwenzako ili kumfurahisha ushamnunulia bia tatu yaani vijana changamoto nyingi bado hujaopoa demu...ebu nambie home unarudi na nini katika hio million maana ume save sana labda laki mbili...ukirudi home ma bill yanakusubiri...kumbuka mshahara ulishaukopeaga hivyo kama laki saba unakatwa hata laki nne kila mwezi...yaani ni maisha ya kipumbavu kbs
 
Hapo kuna ukweli fulani hivi. Enzi zetu za Mwalimu Nyerere mfanyakazi wa serikali alikuwa hawazii kuwa na gari lakini leo hii kijana akishapata ajira tu anakwenda kuchukua mkopo wa gari na hajui kwamba pale ni kujifilisi tu.

Pia atataka maishaa makubwa kuliko kiwango chake na mpango wa kuweka akiba hana hata kidogo wakati umri ndiyo unakwenda.

Aidha humu vijana wengi hujisifia mipango yao ya kando na fedha wanazohonga hao akina dada bila ya kujali familia.
Vijana amkeni na muhakikishe munasave hata kama ni shilingi elfu kumi kwa mwezi siyo usubiri pension tu.
Kweli aseee tena naonea sana huruma hawa wa local government ambao sio wakuu wa idara.hawana posho za kueleweka


Ila hata sisi wa serikali kuu kidogo ingelikuwa heri posho mpya za mama zingerudi zile za 150k wilayani kwa taasisi zote za wizara kidogo hata ukitumia 50000 safarini unaweza kusave laki kwa siku...ila hizi za 80k
 
Toka lini mwajiri akakulipa kiasi kikubwa cha pesa

1. Mwajiri anakulipa fedha ya kufanya uweze kula.

2. Uweze kununua nguo nadhifu ili uwavutie wengine kuajiriwa.

3. Uweze kupata matibabu ya kawaida

4. Uweze kujenga kibanda sio nyumba ya maana ili uweze kuishi humo na kufuga mabata, kulima mchicha.

5. Utapata mikopo yenye riba kubwa ili uwe mtumwa wa kudumu.

6. Ukionekana una mishe binafsi za kukuingizia kipato au kumiliki mali kama magari nyumba nzuri wanakuundia zengwe ili waweze kuharibia ramani zako.
Kwa ujumla kuajiriwa ni utumwa flani unafichwa na mshahara mdogo.
Kuajiriwa ni kimbilio la waoga wa maisha
....Umemaliza....
 
Kwaiyo wakikopeshwa na Serikali, Serikali haita wakata kila mwezi kulipia mikopo yao?
Benki mdanyakazi akikopa 10 ml. ndani ya miaka 7 atakatwa katiba milioni 20. Sasa hii maana yake ni kwamba huyo mdanyakazi angekopeshwa bila riba za hovyo angeweza kupata million 20.
Kwa kupewa 20 badala ya 10
Au milioni 15 badala ya 30 hapo hataweza kutatua mipango yake mingi kwa wakati mmoja.
Ni kukopa tu ili usolve hili. Sometimes kukopa mkopo juu ya mkopo ni wizi wa wazi kabisa sema tu shida zinapelekea mtumishi aweke mkopo juu ya mkopo.
Kama wewe mtumishi nadhani umenielewa,
 
Kuna mzee mmoja niliwahi kutana naye 2009 wakati nilipoenda kupiga kimeo cha computer maintenance
kwenye wizara yao wakati tumekaa baada ya kazi kwisha katika kupiga stori akaniambia unajua kwanini sisi wafanya kazi wa serikali hatuna maisha ? nikamwambia sijui.. akaniambia.. Ni kwasababu tukiwa humu ofisini tunakuwa kama wafu vile akili zinakuwa zimepofushwa, akili ya kuzalisha katika ziada nje ya ofisi inatoweka katika kipindi chote cha utumishi wako, pili hii michezo ya kuiba iba hela za selikali unafanya watumishi wengi kuishi kwenye laana sana si kwa mtumishi anayeiba hizo hela tu mpaka familia yake, tatu ukiwa ofisi za serikali ukaanza kuishi maisha ya anasa, kushiriki vitendo vya ushirikina utaishi maisha ya kimaskini au utakufa kwa ajali au ugonjwa wenye uchungu sana hata kama ulikuwa na cheo cha juu..
Hizo ndo point na ile mentally kwamba mwisho wa mwezi si ntapata tu ...kuna watu Wana safari daily ila pesa haikai wao ni hanasa tu .

Nimeenda kijijini Kuna ticha yuko early 30's ana nyumba na pikipiki nje kwake ana kiduka cha kusogezee siku ana mke ni WA kawaida hanaga skendo na anapendwa ..

Uncle wangu ni mwalimu wa msingi hapo mtwara mjini ana nyumba mbili hata miaka 50 bado hajafika ,na anapokaaa kachimba kisima anauza maji maana huko alipo ni town ila maji ya shida Tena sio mbali ni mjini hapo hapo kwa bajaji kutoka mkanared(chipuputa) au town kabisa mpaka hapo ni jero tu.
 
Asilimia kubwa ya waajiriwa ni masikini kuanzia ngazi ya familia,hebu fikiria kijana amepata ajira familia yote inamtegemea yeye asomeshe wadogo zake,awatunze wazazi wake malazi mavazi chakula lote ni jukumu lake na mshahara wenyewe ni laki 4 au 6 unategemea atafanya savings zipi? Ndio maana madukani wanaongoza kwa madeni.
 
Asilimia kubwa ya waajiriwa ni masikini kuanzia ngazi ya familia,hebu fikiria kijana amepata ajira familia yote inamtegemea yeye asomeshe wadogo zake,hawatunze wazazi wake malazi mavazi chakula lote ni jukumu lake na mshahara wenyewe ni laki 4 au 6 unategemea atafanya savings zipi? Ndio maana madukani wanaongoza kwa madeni.
Lawama kibao bado ndugu eti waje hapo kuwasomesha wazazi wanakufanya kitenga uchumi
 
Mimi nimejaribu kuwasemea waajiriwa tu wa Tanzania ambao wanakufa wakiwa na miaka 30 na kuzikwa wakiwa na miaka 60 , yaani watumishi wana mizigo ya madeni na ndio maana wengi huishia kua wezi tu wa mali ya umma
Sasa kama hujui hao watumishi wa hali ya chini hawapati hata huo mwanya wa
 
Habari za kazi wanajamvi...
Kiuhalisia swala la watumishi kuwa na madeni kila kona ni jambo la kawaida sanaaa... na hili linanipa maswali mengi sana bila majibu kwasababu watumishi wa vyeo vya juu na kwa uchache wanahali nzuri ya kiuchumi ila wengi hawana haki nzuri Tatizo liko wapi..?? Na nini kifanyike kutatua swala hilii??
Nakaribisha mawazo yako ili wote tujifunze ili iwe msaada kwa watumishi wa serikali na wasio watumishi wa serikali.
Wanafanya top up sana kwenye mikopo wanayokopa yaani Kuna Wengine wakija ku topup mpaka tunawashauri wasifanye hivyo. Moshahara Yao midogo sana na wengi wanazaa kwa kushindana na bahati mbaya wengi wanazaa wapiga kuraaaa
 
Kwa mfano mimi binafsi bado mwajiriwa mpya per diem yangu bado 80k tuombe mpya ya mama irudi ya 150k...sasa imagine niko field ya siku 14...
Mahitaji yangu
Lodge 20000 kwa siku
Chakula na maji 15000 kwa siku
Ukaombwa home uchangie rambirambi lets say 50000
Hapo bado una familia nyumbani umeiachaje..bando,
Ikiwa wewe ni mwajiriwa mpya huwezi kupata hiyo 150k (kwa Principal 1 na kwenda mbele) kwa hivyo usiipangie kazi ya field buree.....

  • hiyo lodge ya elfu 20 sijui utaitoa wapi kwa sasa na utakapoipata basi hata mashuka hawaoshi hao utalala na kunguni.
  • vyakula na hivyo vyengine labda utakula kwa mama ntilie, lakini jihadhari usije harisha ukiwa kazini....
 
Habari za kazi wanajamvi...
Kiuhalisia swala la watumishi kuwa na madeni kila kona ni jambo la kawaida sanaaa... na hili linanipa maswali mengi sana bila majibu kwasababu watumishi wa vyeo vya juu na kwa uchache wanahali nzuri ya kiuchumi ila wengi hawana haki nzuri Tatizo liko wapi..?? Na nini kifanyike kutatua swala hilii??
Nakaribisha mawazo yako ili wote tujifunze ili iwe msaada kwa watumishi wa serikali na wasio watumishi wa serikali.
Nyongeza ya mshahara tatizo
 
Ikiwa wewe ni mwajiriwa mpya huwezi kupata hiyo 150k (kwa Principal 1 na kwenda mbele) kwa hivyo usiipangie kazi ya field buree.....

  • hiyo lodge ya elfu 20 sijui utaitoa wapi kwa sasa na utakapoipata basi hata mashuka hawaoshi hao utalala na kunguni.
  • vyakula na hivyo vyengine labda utakula kwa mama ntilie, lakini jihadhari usije harisha ukiwa kazini....
Ile rate walitupa mkuu na hata sasa nazani wanapewa taasisi nyingi chini ya maliasili na utalii rafiki zangu wanasema wanalipwa hio 150k na kwa marafiki zamgu wa ruwasa pia wanalipwa 130k na tumeajiriwa nao hata miaka mitatu bado.
 
Back
Top Bottom