Kwanini wazazi wa siku hizi wako 'obsessed' sana na ufaulu wa Division One kwa watoto wao?

Acha aminisha ndoto za zamani dunia imebadirika saivi
Kivipi imebadilika kuwa dunia haihitaji rubani aliyefaulu mitihani? Dunia haihitaji daktari aliyefaulu mitihani? Haihitaji wakili aliyefaulu mitihani? Haihitaji mhasibu au mchumi aliyefaulu mitihani?
 
Sio kilaza ana division one point saba, kwa mawazo na akili kama zako sio kilaza kabisa, ni genious kabisa na hakuna mtu kwenye ukoo wenu amewahi kupata hiyo ufaulu lakini kwetu sisi wenye akili kubwa huyu mtoto sio genious.
Umepigilia msumari penyewe. Tanzania tumeingia kwenye mfumo mbaya sana na kuja kutoka hapo ni kazi na itahitaji nguvu kubwa na akili. Hili ni tatizo na kinachofanyika sasa hivi shuleni ni wanafunzi kukaririshwa ili washinde mitihani. Mambo ya kuelewa wanachofundishwa yamewekwa pembeni. Sasa hivi kila shule inahijitahidi kutumia ''mbinu mbadala'' ili ifaulishe na kusifiwa. Na wanafunzi nao wanajitahidi kutumia ''mbinu mbadala'' ili wafaulu. Matokeo yake ni kuwa tutakuwa na ''wataalam'' wasio na utaalam wowote na watanzania kushindani kwenye soko la ajiri itakuwa ngumu sana. Kinachotakiwa sasa hivi ni kufumua mfumo wote wa elimu na kutahini ili turudi kwenye mwelekeo mzuri. Mitihani ya mwisho inatakiwa iwe sehemu ndogo ya kutahini wanafunzi.
 
Kivipi imebadilika kuwa dunia haihitaji rubani aliyefaulu mitihani? Dunia haihitaji daktari aliyefaulu mitihani? Haihitaji wakili aliyefaulu mitihani? Haihitaji mhasibu au mchumi aliyefaulu mitihani?
Kwani wewe ulikua unahoji nini mkuu?
Hao waliopata division one si ndio viongozi wako wanao kutoza kodi na wewe unalilia ama sio wewe. Sasa unawezaje kujilinganisha na waliopata division one kuwa huoni impact na huku ndio wanakutawala na kukupangia kila kitu? Wenye division one ndio wanaongoza nchi, ndio wanaokutibu, hivi jitu limefeli vibaya o level na advance linaweza kusomea udaktari? na kukutibu? Linaweza kufanya upasuaji?
 
kwa hiyo wewe mkuu unaka kutwambia kwamba mtu aliyepata division one o level na advance hana maarifa? mpaka uanze kumfanyia usaili. Labda ungezungumzia wafanyiwe usaili wenye degree. Lakini sio hizo level mbili. nadhani umesoma olevel na advance na unazijua vizuri.
 
Kwa hiyo madaktari wetu na mainjinia wa Tanesco na Madereva wa mabasi na marubani wetu wamekariri masomo? Hawajui practicals? Mafundi ujenzi je? Wamekariri masomo?
Wengi sio tu wamekariri, bali mfumo wetu hauwaruhusu kuja na kitu kipya au kuhoji.

Angalia historia ya mtu anaitwa Erasto Mpemba, aligundua - alitukumbusha- kitu kinaitwa Mpemba-Aristotle effect. Aristotle alikiandika hiki kitu miaka kama 2500 iliyopita, kikaja kusahaulika na ulimwengu wa sayansi.

Kitu chenyewe ni kwamba, katika mazingira fulani ya kugandisha maji, maji ya moto yanaganda kwa haraka zaidi ya maji baridi, kitu ambacho kinaonekana kuwa counter-intuitive, kwa sababu maji ya baridi yapo karibu zaidi kufikia temperature ya kuganda kuliko maji moto.

Erasto Mpemba aligundua hilo, kwa sababu alikuwa anafanya kazi ya kugandisha barafu na kuuza, tulikuwa tunaita asikirimu.
Shuleni walipewa jaribio linalofanana na hilo, mwalimu akategemea majibu kama ya kitabuni, Mpemba akamuonesha practically kwamba majibu yanayotegemewa kitabuni si halisi. Mwalimu alim dismiss Erasto Mpemba kwa miaka kadhaa, mpaka akaja mzungu kwenye program moja. Erasto Mpemba wakati huo mtoto tu, bado alikuwa na hamu ya kuchunguza zaidi, akaona Watanzania hawamuelewi, akamfuata huyo mzungu. Akamuelezea alivyofanya experiment na matokeo yake yalivyokuwa tofauti na kitabu. Mzungu akamsikiliza, wakafanaya majaribio, wakaona kweli Mpemba yuko right. Papers zikawa published. Hiki kitu kiliwazingua wansayansi kuanzia miaka hiyo ya sitini mpaka wamepata jibu hivi karibuni


Kwa nini walimu wa Erasto Mpemba hawakumsikiliza na kufuatilia experiment yake kwa umakini? Kwa nini ilibidi Erasto Mpemba amfuate mzungu ili asikilizwe? Kuna kina Erasto Mpemba wangapi huko vijijini ambao wamezimwa ideas zao kwa sababu hawajapata mzungu?
Unapozima ideas za vijana wadogo mashuleni, wakikua wakubwa watapata wapi nguvu za kuondokana na dunia ya kukariri na kuanza kuhoji mambo?

Unaweza kunisoma kirahisi kwamba nasema watu wetu hawana akili ya kuhoji. La hasha, sina maana ya kusema hivyo.Tuna watu wenye akili sana.

Kuna mtu aliuliza, wako wapi kina Newton na Einstein wa Africa? Ina maana watu wote wa Africa hakuna wenye akili kama hizo?

La hasha, wapo wengi tu.Wameminywa na utamaduni. Utamaduni wa mambo kufanywa kwa "amri kutoka juu". Utamaduni wa "mkubwa hakosei".Utamaduni wa "funga kombe mwanaharamu apite".

By the time mtu anafika kuwa Engineer na Doctor huko, anakuwa kashafundishwa self censorship.Anafanya kazi ndani ya office politics, kwa kukariri.Akianza kuhoji na kuleta innovation tu anapigwa daflao.

Zaidi ya watu, tuna tatizo la mfumo na utamaduni.

Ndiyo maana ukitafuta vitu vipya tunavyogundua, ni vichache na katika hivyo vichache, vyenye impact kwenye kutatua matatizo katika maisha ya kila siku ni vichache zaidi.
 
Mkuu nina uhakika hujafika chuo

Hujapata one

Advance hujafika

O level ulikunja sifuri nzuri

Unawaonea wivu madogo wanaopasua div one kwa sasa


Tulia dawa ikuingiee


Nani alikwambia usisome kenge weweee
😂😂😂😂Imebidi nicheke.

Mkuu umeamua kunichamba kama mama Gwajima.

Nashukuru sana mkuu. Ila ungetakiwa upewe unaibu waziri wa afya ushirikiane na mama Gwajima kuchamba watu.
 
Sikuwa na maana hiyo. Nilitumia kusaili kama ku- question ubora wa hizo divisheni one jambo ambalo linaturudisha kule kwenye mfumo mzima wa elimu. Nimesharekebisha. Ukisoma tena pengine utapata nilichokuwa najaribu kusema..
 
Kuna watu tulikuwa nao huku, very bright fellows. Wakaamua kurudi nyumbani kujaribu kubadili mambo.

Wamejikuta badala ya kubadili mambo, kwa kiasi kikubwa wao ndiyo wamebadilika kukubali mfumo.

Sasa hivi wengine wanataka kurudi tena US.

Mimi nawaambia mlikosea kurudi kabla ya kuusoma mchezo vizuri.

Tuna matatizo ya kimfumo na kiutamaduni.
 
Kila kizazi kinataka kijiione kilikua bora kuliko kilichopita
 
Mimi Auncle wangu ni computer engineer hajarudigi mpaka leo yupo Texas huko, na kampuni alizozifanyia kazi katika top leve ni zifuatazo, Philips, BP, Schlumburger (ambayo ndio yuko kwa sasa) ana hela chafu hana hata mpango wa kurudi kwenye ardhi yetu ya udogo mwekundu.
 
Sikuwa na maana hiyo. Nilitumia kusaili kama ku- question ubora wa hizo divisheni one jambo ambalo linaturudisha kule kwenye mfumo mzima wa elimu. Nimesharekebisha. Ukisoma tena pengine utapata nilichokuwa najaribu kusema..
Ukienda U.S, CANADA lazima utoke. Waafrika tuna akili hata huu mfumo wetu wa elimu ni mzuri na unaendana na dunia inavyo kwenda changamoto kubwa ni mazingira yetu ya kujifunzia ni magumu. Hatuna vitendea kazi vya kujufunzia.
 
Ukifanya kazi top level IT Marekani, unaweza kurudi Tanzania ukakuta hakuna kazi ya kufanya ya kutumia ujuzi wako.

Tanzania bado hata hatujaweka legal framework ya kueleweka ya mambo ya IT .

Kwa sababu hakuna mifumo iliyo sophisticated hivyo, na hata ukitaka kuanzisha private practice hakuna uchumi wa kutosha.

Na hata ukisema utafute projects interesting za kuanzisha Tanzania, hata za non-profit tu kusaidia jamii, ambazo ukiwa makini huwezi kukosa, hiyo attitude ya serikali kuanzia kodi, rushwa, wizi, mpaka kukubali teknolojia mpya, kwa mtu aliyezoea kufanya kazi Marekani, itakufanya uchoke mwenyewe.

Mimi nilipeleka proposal serikalini tuachane na proprietary software, tutumie open source, tupunguze gharama za software license.

Project ilikuwa nzuri sana, ina breakdown nzuri sana. Wakubwa hawakuipenda. Kwa sababu inainekana wanapolipa software license ndiyo wanapata cha juu hapo hapo. Ukiwapa software za bure hawapati sehemu ya kula cha juu!

Huyo Uncle wako naweza kumuelewa vizuri sana, kwa sababu mimi mwenyewe nishafanya kazi kama hizo naongoza project kubwa dunia nzima. Najiuliza hivi hii kazi ningekuwa Tanzania ningeweza kufanya kweli?
 
N Ni kweli mkuu,
 
Aisee Ilboru wametia fora, nimehesabu Division one za point 7 ziko 47, haha daah.
 
Kule Arusha Kuna Vocational secondary school nafikiri hiyo Ni nzuri hasa ukizingatia kuwa Ni Private.
 
Unaposema maisha mazuri unamaanisha nini? Mwenzio anazungumzia uwezo wa mtoto kupambanua mambo,kuhoji,nk. Jibu kitaalam usijibu km ligi mkuu
 
Humu hatuongezi kitu kichwani,hatuchambui hoja,tunabishana tu,yaani tupo kishabiki tu.
 
Kwa hiyo madaktari wetu na mainjinia wa Tanesco na Madereva wa mabasi na marubani wetu wamekariri masomo? Hawajui practicals? Mafundi ujenzi je? Wamekariri masomo?
Hao wote uliowataja walipata dvn one kwani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…