shimboni mene
JF-Expert Member
- Sep 11, 2022
- 264
- 290
Eti ellor..we fungo aisee!Spelling ellor
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Eti ellor..we fungo aisee!Spelling ellor
Stelling error or spelling endoplasmEti ellor..we fungo aisee
Eti ellor..we fungo aisee!
China wana demokrasia ipi?UAE wana demokrasia ipi?maana huko kute wawekezaji wamejaaa tele mpaka wanamwagika...Wawekezaji wanawekeza sehemu ambayo kuna demokrasia. Ndo Mana wakati wa dictator jpm wawekezaji walikuwa wanakimbia kwa speed ya 5G aliposhtuka akaanza kuwabembeleza akina rostam but too late
Kodi zinakusanywa kwa ajili ya nini ?? Mavieite ?!!Mifumo huundwa na wananchi, hivyo wananchi imara vivyo hivyo mifumo.
Tatizo kubwa ni raia kufikiria kuwa kuna watu wa kuwajengea nchi yao.
Wananchi imara watasimamia kodi yao itumike ipasavyo.Kodi zinakusanywa kwa ajili ya nini ?? Mavieite ?!!
Hakika kabisa!Wananchi imara watasimamia kodi yao itumike ipasavyo.
Kama wananchi wote watajielewa, matumizi mabaya ya kodi yao hayatakuwepo.
Duh !!CCM imebaki kasha tu la kubebea kila takataka. Akitokea mmoja wao mwenye nia hasa ya kulichoma moto hilo kasha, mambo yatanyooka vizuri tu!
Tatizo ni hilo moja la kupatikana mTanzania huyo, au kundi dogo la waTanzania wenye nia hiyo.
CCM ya siku hizi ni huyo mtu mmoja aliyeko juu, basi. Na kwa bahati mbaya sana kwa waTanzania, huyo anayekuwepo huko juu ya kasha, ni huyo huyo anayelitumia kasha kujaza uchafu zaidi kwenye kasha lenyewe..
.Tanzania haiji endelea hata siku moja kwa kuwa na Rais Legelege, mpiga porojo,chuma ulete,mpenda starehe,mdekezaji,mwivi,fisadi,asiyejiamini, anayeendeshwa na watu kadhaa.
Nchi italiwa, itafisaidiwa kodi na mikopo. Wezi watakumbatiwa na kutamba kwenye korido za Ikulu. Maskini wana maskinika, watanyanyaswa na kukamuliwa.
Nchi italala mafisadi wataota pembe na wanasiasa uchwara watafanya ujasiliasiasa. Hawa watakuwa wakipewa kiziba mdomo na kuendelea kuacha Serikali kama hiyo ijikite kuota mizizi. Utaona watakavyopishana ikulu na kutoa matamko ya kuunga mkono juhudi.
Maskini watatumika kupangwa kama ngazi ili wanasiasa njaa wafikie sehemu za juu za utukufu. Maisha yatabaki yale yale. Asiye nacho hata kile kidogo alichodhani anacho atanyang'anywa na kitapelekwa kwa aliye nacho. Huyo ataongezewa.
Masheikh,Mapadre,Wachungaji,Maaskofu,Maulamaa,Maimam hawa watakuwa na posho yao nao watajiunga katika kusifu na kuabudu. Nchi itakuwa gizani. Kila mtu ata Chukua Chake Mapema. Maana atakula kwa urefu wa Kamba yake.
Na akimaliza majani yaliyo kwenye urefu wa kamba yake atahamia maeneo ambayo ni ya wenzie. Atakata na kamba awe huru zaidi katika kula.
Tutagundua HATA BAADA YA KUMALIZA KUNYWA MTORI CHINI KUNA MIFUPA TU.
Mimi naungana nawe katika haya uliyoandika hapa, hasa namba moja na tatu. Namba mbili inahitaji kufanyiwa marekebisho kidogo tu..
Ili afilika iendelee, yafuatayo ni lazima yafanyike.
1.
Ipitishwe sheria ya kunyongwa hadi kufa kwa yeyote atakaye husika na ufisadi, wizi na ubadhirifu wa mali za umma. Wakinyongwa kikamilifu watu wawili watatu, nchi inanyooka. Hii italeta hofu kwa wahusika wasione kodi zetu ni shamba la bibi. Rejea China, hii imewasaidia sana.
2.
Mishahara na marupurupu ya viongozi wa serikali ipunguzwe kwa mgawanyo wa 10. Mfano mbunge analipwa 12M, alipwe 1.2M. Hii itafanya wapiga dili wasigombee nafasi za uongozi kwani hakuna tena maslahi. Watakaogombea nafasi hizo ni wale wenye nia ya dhati ya kuwa viongozi. Mfano halisi mshahara wa raisi wa china ni kama 4.5M kwa mwezi lakini nchi za afilika, maraisi wanalipwa............Lakini unaweza kuniuliza mishahara midogo si itasababisha wakwibe zaidi? Rejea point namba moja.
3.
Kuwe dira/sera ya taifa ambayo haitegemei raisi gani yuko madarakani. Ili mtu, kampuni, taasisi au taifa lisonge mbele, lazima liwe na dira, mwelekeo. Huwezi kufika kama hujui unaenda wapi. Ni ajabu sanaa afilika haina dira! Huyu ubinafsishaji, anayemfuatia kilimo kwanza, yule viwanda na biashara, anayekuja utalii etc etc. Ni kama genge la vichaa ambao hawajui wanafanya nn. Mfano mdogo, ni miaka 60 tangu tupate uhuru lakini hatuna maji ya uhakika wala umeme wa uhakika! Kama tangu tupate huru, nchi ingekuwa na malengo hata ya miaka 10 kumaliza tatizo 1 kati ya haya, leo yangekuwa historia.
100% correctNapingana na wewe kwa asimilia kubwa kwangu mimi naona ili inchi iendelee inahitaji MIFUMO imara ya uongozi wa nchi. Rais wetu asiwe yeye ni ndiyo kila kitu, yeye awe dira, yeye awe mteuzi wa kila mmoja - yeye yeye kila kona hapana.
Kwa mfumo huu ukipata Rais ambaye hana uwezo unaiingiza nchi kwenye matatizo makubwa mno; mfano hai ni kwa nchi yetu hakuna check and balance - nchi inaongowa kwa mawazo ya upande mmoja kitu ambacho ni makosa makubwa mno.
100% correct.
Ili afilika iendelee, yafuatayo ni lazima yafanyike.
1.
Ipitishwe sheria ya kunyongwa hadi kufa kwa yeyote atakaye husika na ufisadi, wizi na ubadhirifu wa mali za umma. Wakinyongwa kikamilifu watu wawili watatu, nchi inanyooka. Hii italeta hofu kwa wahusika wasione kodi zetu ni shamba la bibi. Rejea China, hii imewasaidia sana.
2.
Mishahara na marupurupu ya viongozi wa serikali ipunguzwe kwa mgawanyo wa 10. Mfano mbunge analipwa 12M, alipwe 1.2M. Hii itafanya wapiga dili wasigombee nafasi za uongozi kwani hakuna tena maslahi. Watakaogombea nafasi hizo ni wale wenye nia ya dhati ya kuwa viongozi. Mfano halisi mshahara wa raisi wa china ni kama 4.5M kwa mwezi lakini nchi za afilika, maraisi wanalipwa............Lakini unaweza kuniuliza mishahara midogo si itasababisha wakwibe zaidi? Rejea point namba moja.
3.
Kuwe dira/sera ya taifa ambayo haitegemei raisi gani yuko madarakani. Ili mtu, kampuni, taasisi au taifa lisonge mbele, lazima liwe na dira, mwelekeo. Huwezi kufika kama hujui unaenda wapi. Ni ajabu sanaa afilika haina dira! Huyu ubinafsishaji, anayemfuatia kilimo kwanza, yule viwanda na biashara, anayekuja utalii etc etc. Ni kama genge la vichaa ambao hawajui wanafanya nn. Mfano mdogo, ni miaka 60 tangu tupate uhuru lakini hatuna maji ya uhakika wala umeme wa uhakika! Kama tangu tupate huru, nchi ingekuwa na malengo hata ya miaka 10 kumaliza tatizo 1 kati ya haya, leo yangekuwa historia.