Clever505
JF-Expert Member
- Jul 27, 2020
- 1,183
- 2,256
Hii ya kufanya kosa Kisha unajificha kwenye makosa ya wengine ili kosa lako lisionekane sio poa kabisa, yaani unalazimisha makonda aonekane hajafanya kosa kisa wengine wanatembea na watoto wadogo, wanaiba pesa za uma, ushoga?Hakuna Mahali alipomdhalilisha Mtu kwenye ule mkutano wa Wanakamati wa Halmashauri na Wananchi Mkoani Manyara Longido.
Akichoongea RC Makonda ndio maneno ya kawaida tunayotumia watu wengi na yamezoeleka sana wakati unapotaka kusisitiza Jambo na halijawahi kuwa Udhaliliashaji kwenye lugha na mila zetu.
Watu wasitake kukuza mambo.
Mtu hata kama humpendi basi usimsakizie mambo ambayo hayapo.
Kusema tu Usiongee na mimi kama mchumba wako ndio ionekane ni kosa hadi watu walishikie Bango?
Hebu tuwe serious tujikite kwenye mambo yenye tija.
Mbona nyinyi mnaiba pesa za umma na za hao hao wakina Mama na watoto hadi wanakufa mahospitalini kwa kukosa huduma bora.
Mbona nyinyi mnafanya mambo ya matusi mnatembea na watoto wadogo, wengine hadi kuwadhalilisha kingono?
Mbona nyinyi wengine mnafanya hadi vitendo vichafu hadi aibu kuvisema hapa ikiwemo Ushoga na usagaji?
Makonda Paul Piga kazi achana na hawa waganga njaa.
Makonda namkubali kinoma ila anapokosea aambiwe, kwani kulikuwa na ulazima kusema vile!? Hata kama una cheo kikubwa jaribu kuheshimu wa chini yako