Kwenye kila shule kuna yule Mwalimu mnoko shuleni kwenu alikuwa anaitwa nani?

Kwenye kila shule kuna yule Mwalimu mnoko shuleni kwenu alikuwa anaitwa nani?

Kuna kichwa Mwaza sec kilikuwa kinaitwa Shija au Ndondocha. Mshkaji yuko kama baba ubaya wa kwenye gazet. Jamaa alikuwa mkudaa haijapata tokea.
 
Kamwambie baba yako nimekutana na 'Linyambuuta' S/M ya Mazoezi Masebe...
Unachapwa bakora unaambiwa andika namba 11,111,111,111 hizo numericals ndio idadi ya mboko utakazolambishwa...hapo kosa ni kupiga kelele au utoro. No wonder wengi wamekuwa hawapendi shule
 
Mr Dengea-Njombe sec

Mr Komba Midlands high school, huyu komba alinikamata na simu halafu nikaitupa km jiwe kwenye majani kisha nikamkana sina simu aisee alishindwa kuamini macho yake
Akataka kunichapa bakora nikamgomea akasalimu amri


Siku nyingine niliamua kumfanyia fujo ambayo kamwe hatoweza kusahau
Baada ya kuzidi unoko nilitafuta namba yake ya simu kwa mabinti kisha nikamtumia Tafadhali nipigie km 800 za tigo enzi hizo zilikuwa hazina idadi na mbaya zaidi km cm haipo hewani zinakaa pending ukiwasha tu zinaanza kumiminika basi kila akikaa simu yake inaingia tafadhali nipigie mpaka akanppigia simu sikupokea akatuma msg kuwa niwaambie tigo simu yangu inamtumia tafadhali nipigie ovyo,nikamuongeza zingine 400 akatupa na line..
 
wazee wa kigonsera watakua wanamjua ticha mmoja kajange aka JUNGI
 
Mkuu Ndelio ndani ya mwembetogwa hapo aliwahi kuwarusha washkaji kichura chura katikati ya stand kuu pale iringa walikua wametoroka shuleni
 
kuna mwalimu alikua anaitwa kavuye[R.I.P] SHINGATINI SEC mwanga[usangi]huyu jamaa alikua noma,teacher sijui alikua mchawi, alikuwa head master then mgomo miaka ya 97 akachomolewa na mgomo sababu ya ukuda wake, unaambiwa alishikiwa bunduki na mzee mmoja tajiri anaitwa mekzedeki,digi akageuka kuwa mnazi teteteteh. alikuwa na vijana wake amewatoa thame huko mamba miamba vijeba haswaa ndo anawatumia kama viongozi.
baada ya miaka kadhaa akarudi kama discipline master hahah, asee watu tulinyooka anaweza kuja bwenini saa nane usiku kuitisha rokoo....ila na shukuru alinisaidia maana nisinge kuwa leo hapa, ningekuwa njangili la kutupwa.
 
Back
Top Bottom