Lazaro Nyalandu: Tatizo kubwa la CHADEMA ni Uongozi wa juu, CCM imejaliwa mfumo

Lazaro Nyalandu: Tatizo kubwa la CHADEMA ni Uongozi wa juu, CCM imejaliwa mfumo

Tatizo la Chadema ni uongozi,tatizo la CCM ni nini? hadi ukakimbia uko na kuacha ubunge?
MaCCM yameamua kumdaharirisha tu, hiyo ni Ng’ombe yao wameikata mkia tayari.
Kila anaerudi ccm , anaandaliwa media press na nilazima aimbe Mbowe.. Mbowe..! Ndio wampe cheo..😂😂
 
NYALANDU HANA NGUVU NA HAKUA NA NGUVU YA KUMSHINDA LISSU.

UPEPO WA LISSU HATA MAGUFULI NA VYOMBO VYAKE VYA USALAMA, WALIUOGOPA

1619995695950.png
😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Huyu Nyalandu alimkimbia jiwe! lililotaka kumsaga saga kwa kushiriki ujambazi wa mali asili zetu! CDM walikukaribisha kukuepusha na mkono wa jiwe ili akikufuata useme ni SIASA. Unatakiwa uwashukuru
Kama alikuwa jambazi wa maliasili zetu, kwanini Chadema walimpokea?
 
Kama wapinzani watakuwa kila ukikaribia uchaguzi wanapokea makapi-kapi ya chama tawala, basi safari ndefu ya demokrasia itafuata. Nadhani sio kosa kuwapokea bali utafiti wa kumchangua mtu uwe wa kina, na wala asipewe majukumu ndani ya uongozi hadi miaka 5 - 10 imalize.

Akifikisha miaka 10 na bado hajarudi ndio tunaweza kuanza kumuamini kama ana nia kweli ya kujiunga na upande mwengine. Unajua ni vigumu mtu kubadili chama, maana sera za hivi vyama ziko tofauti. Mtu anaweza vipi leo yuko CCM/kada - kesho CDM tena kiongozi wa juu!

Vyama vya upinzani lazima mtafakari vizuri, hii imekalia kama vile mna pupa kidogo katika kufikia malengo.
 
Akiwa 360 Clouds ameliongea hili leo na yuko live mpaka sasa,anasema tatizo lipo kwenye uongozi. Amesema wanachama wa chini kabisa hawana tatizo kabisa ,matumaini yao yanaharibiwa na uongozi wa juu.

Angalizo: Mbowe uongozi wako umeshindwa vibaya sana, achia ngazi

==================

“Nilipoenda nchi ya ugenini (CHADEMA) wimbo ulikuwa haumbiki kwa namna ambavyo nilikuwa naangalia matukio, ilipotokea Mheshimiwa Rais anaumwa kuna baadhi ya viongozi walijitolea wakasema huyu hafai aondoke tufurahi, ilikuwa inanikwaza kupita kiasi”

“Niliposafiri kwenda Chato kuzika mashambulizi ambayo yalikuwa yananipata, hayakutoka kwa wana-CCM, hayakutoka kwa wana-CHADEMA wa kawaida, yalitoka kwa baadhi wenye msimamo mkali, unamshambuliaje mtu alieenda kuzika kiongozi wake wa nchi?"

“Wakati wa matatizo ya Lissu mimi binafsi sikujali kwamba ni CHADEMA, nilimuona ni Mtanzania ni kiongozi mwenzangu kule Singida, nakumbuka hata Mhe Rais alienda pia kumuona. Lakini wanachama wa CCM kuanzia Rais hadi viongozi hakuna aliepiga simu au kututukana”

“Kuna mitihani ilitokea kwenye uchaguzi, kulikuwa na chaguzi za aina mbili, moja ilikuwa kupigiwa kura kwenye kamati, tunaenda kwenye Baraza Kuu. Kwenye Kamati Kuu Nyalandu alipata 100%, nilimgaragaza kweli kweli, kilichotokea viongozi wakasema Nyalandu asije akawa kama Lowassa”

“Uchaguzi wa mgombea ubunge Singida Kaskazini, wajumbe wamefika usiku ule kuanzia saa kumi na mbili watu wananipigia simu wananiambia mbona mgombea Urais wako hakutaki anasema kidogo umkoseshe kugombea Urais kule Dar es Salaam”

“Wana-CHADEMA watu wa kawaida wengi ni watu wazuri, ni watu ambao wanatamani nchi bora, ambacho wanawazidi wana-CCM wewe itisha mkutano watakuja kwa mguu, watatoka walikotoka, watajitolea katika hali ambayo hutoamini”

“Siasa sio matusi, siasa sio kukoseana heshima, sio kutukana kiongozi wa nchi, siasa sio kuwatukana wale unaotofautiana nao, ni kusema hoja zako mbadala”

“Chama Cha Mapinduzi kimejaliwa mfumo, kilivyotengeneza itifaki ya chama, namna ambavyo walitengeneza mfumo wa kutoa dukuduku zako, mfumo wa kuchaguana. Kina strength ya mfumo, naamini imani ya watu tukipeleka kwa public, mwananchi wa kawaida anatoa kura” -
Herding behavior is an occurrence of thoughtful people suspending individual reasoning because of fear 'Unyumbu ama kujitoa ufahamu'
 
“Kuna mitihani ilitokea kwenye uchaguzi, kulikuwa na chaguzi za aina mbili, moja ilikuwa kupigiwa kura kwenye kamati, tunaenda kwenye Baraza Kuu. Kwenye Kamati Kuu Nyalandu alipata 100%, nilimgaragaza kweli kweli, kilichotokea viongozi wakasema Nyalandu asije akawa kama Lowassa”

Kwa kweli hapo Chadema waliona mbali sana kwamba tusimpe Nyalandu Madaraka kwani atakuwa kama Lowassa. Kwani sasa walisema uongo?
 
Akiwa 360 Clouds ameliongea hili leo na yuko live mpaka sasa,anasema tatizo lipo kwenye uongozi. Amesema wanachama wa chini kabisa hawana tatizo kabisa ,matumaini yao yanaharibiwa na uongozi wa juu.

Angalizo: Mbowe uongozi wako umeshindwa vibaya sana, achia ngazi

==================

“Nilipoenda nchi ya ugenini (CHADEMA) wimbo ulikuwa haumbiki kwa namna ambavyo nilikuwa naangalia matukio, ilipotokea Mheshimiwa Rais anaumwa kuna baadhi ya viongozi walijitolea wakasema huyu hafai aondoke tufurahi, ilikuwa inanikwaza kupita kiasi”

“Niliposafiri kwenda Chato kuzika mashambulizi ambayo yalikuwa yananipata, hayakutoka kwa wana-CCM, hayakutoka kwa wana-CHADEMA wa kawaida, yalitoka kwa baadhi wenye msimamo mkali, unamshambuliaje mtu alieenda kuzika kiongozi wake wa nchi?"

“Wakati wa matatizo ya Lissu mimi binafsi sikujali kwamba ni CHADEMA, nilimuona ni Mtanzania ni kiongozi mwenzangu kule Singida, nakumbuka hata Mhe Rais alienda pia kumuona. Lakini wanachama wa CCM kuanzia Rais hadi viongozi hakuna aliepiga simu au kututukana”

“Kuna mitihani ilitokea kwenye uchaguzi, kulikuwa na chaguzi za aina mbili, moja ilikuwa kupigiwa kura kwenye kamati, tunaenda kwenye Baraza Kuu. Kwenye Kamati Kuu Nyalandu alipata 100%, nilimgaragaza kweli kweli, kilichotokea viongozi wakasema Nyalandu asije akawa kama Lowassa”

“Uchaguzi wa mgombea ubunge Singida Kaskazini, wajumbe wamefika usiku ule kuanzia saa kumi na mbili watu wananipigia simu wananiambia mbona mgombea Urais wako hakutaki anasema kidogo umkoseshe kugombea Urais kule Dar es Salaam”

“Wana-CHADEMA watu wa kawaida wengi ni watu wazuri, ni watu ambao wanatamani nchi bora, ambacho wanawazidi wana-CCM wewe itisha mkutano watakuja kwa mguu, watatoka walikotoka, watajitolea katika hali ambayo hutoamini”

“Siasa sio matusi, siasa sio kukoseana heshima, sio kutukana kiongozi wa nchi, siasa sio kuwatukana wale unaotofautiana nao, ni kusema hoja zako mbadala”

“Chama Cha Mapinduzi kimejaliwa mfumo, kilivyotengeneza itifaki ya chama, namna ambavyo walitengeneza mfumo wa kutoa dukuduku zako, mfumo wa kuchaguana. Kina strength ya mfumo, naamini imani ya watu tukipeleka kwa public, mwananchi wa kawaida anatoa kura” -

Nyalandu anatakiwa akapimwe akili kwanini,kwasababu, Mara anakimbia ubunge,mara anataka tena uRais,mara anataka tena ubunge alio ukimbia. Mara anakimbia CCM anakimbilia Chadema,mara anakimbia chadema anakimbilia CCM.

20210427_193657.jpg
 
Ukweli ni kwamba MwanaCCM hawezi maisha ya upinzani. Narudia tena hawezi! Wao wamezoea kuwekewa mezani kila aina ya cheo na anasa. Wamezoea kupiganiwa na vyombo vya dola, na NEC. Aliyeonja pepo ya CCM hawezi maisha nje ya pepo ya CCM. Narudia tena, hawezi hata kidogo.
 
Mlio jirani na Nyalandu mniulizie, ni kwa nini anaonekana hajiamini kwa kile anachokisema? kwani kalazimishwa kutembelea vituo vya radio na kusema hayo ayasemayo?

Kwani akikaa kimya tu anapungukiwa nini?
 
Back
Top Bottom