LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji

LBL: Pyramid Scheme Inayowatapeli Watu kwa Kisingizio cha Uwekezaji

Status
Not open for further replies.
Njooni FIC huku hakuna utapeli kampuni imesajiliwa yaani unabet kupigwa hamna
 
Umewahi ona you tube wanalazimisha ulete watu wa kujiunga?
Umejuaje kuwa wanalazimisha,kwanini wewe?wakati kila msanii anatangaza kuwa tembelea YouTube account yangu Kuna tofauti gani,kujenga team ni priority ya mtu,in my case najenga platform za muda 120 days 100 days.wakisepa na Kijiji poa,last year niliwekeza kwenye mitaji ya wakulima elnino ikaja hapo kati lakini mtaji ulirudi na mwaka huu Kuna mvua kidogo,hivyo ndivyo Dunia inaenda ,Haina utulivu kabisa. Hata TBL wako na hard time this time sababu watu hawana mapenzi na bia Tena wemebadiri mwelekeo wanapenda Serengeti product na product ndogondogo za take away,ni swala la muda tuu utajua kuwa AI inaleta vitu vingi vipya kama vile Ask na Chatgtp.Technology is running the world.
 
Hawa jamaa wajanja sana. Sio matapeli. Wanakwambia wanakupa faida 2% kwa siku alafu Hela yako wanaenda izalisha kwa at least 10%-15%. Wakiwa na hiyo mitaji yenu yote mliowakusanyia, kutengeneza 10% kwa siku sio issue. Sio wapigaji
Unaweza kunisaidia inavyowezekana kuzalisha asilimia kumi ya mtaji kwa siku.
 
Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko la makampuni yanayodai kutoa fursa za uwekezaji wa mtandaoni, lakini kwa uhalisia ni matapeli wa hali ya juu. Moja ya makampuni haya ni, ambalo limekuwa likiwahadaa watu kwa mfumo wa Pyramid Scheme — utapeli wa kifedha unaojificha chini ya kivuli cha uwekezaji.

LBL ni Pyramid Scheme, Si Uwekezaji wa Kweli
LBL linadanganya watu kuwa wanaweza kupata faida kubwa kwa kuwekeza kiasi kidogo cha pesa na kuwashawishi wengine kujiunga. Mfumo wake unategemea kusajili watu wapya ambao hulipa pesa zao kwa wale waliowatangulia badala ya kufanya biashara halali. Hii ni tabia ya kawaida ya Pyramid Scheme, ambapo faida inapatikana tu endapo watu wapya wataendelea kuingia kwenye mfumo.

Mbinu wanazotumia Kutapeli watu
  1. Ahadi za Faida Kubwa kwa Muda Mfupi — Wanadanganya kuwa unaweza kuongeza pesa zako kwa haraka bila juhudi yoyote.
  2. Motisha kwa Kusajili Watu Wengine — Ili upate “faida,” unalazimika kuwaleta watu wengine, jambo linalothibitisha kuwa si biashara halali.
  3. Matumizi ya Ushuhuda wa Uongo — Wanatumia video na picha za watu wakidai kuwa wamepata mafanikio, ilhali ni sehemu ya mbinu za kushawishi watu zaidi.
  4. Hakuna Bidhaa Halisi Inayouzwa — Biashara yoyote halali lazima iwe na bidhaa au huduma inayoeleweka. LBL haifanyi hivyo, inaendeshwa kwa mfumo wa mlolongo wa udanganyifu.
Kwa nini LBL ni Hatari?
  • Mfumo wake hudumu kwa muda mfupi kabla ya kuanguka na watu kupoteza pesa zao.
  • Walioko juu tu ndio hunufaika, lakini wanachama wapya huishia kulia baada ya kuliwa pesa zao.
  • Serikali nyingi zimekuwa zikifungia makampuni ya aina hii kwa sababu ni kosa la jinai kuendesha Pyramid Scheme.
USIJINGE! CHUKUA HATUA MAPEMA
Ikiwa umeshawahi kushawishiwa kujiunga na LBL, usiweke pesa zako hata kidogo. Ikiwa tayari umeshaingia, tafuta namna ya kutoka mapema kabla hujapoteza zaidi. Onyo watu wengine kuhusu utapeli huu ili tusiruhusu matapeli kuendelea kueneza hadaa zao.

View attachment 3225058
Mpaka leo kuna Wajinga wanapigwa hela zao na utapeli huu wa DECI.
Kweli wajinga ndio waliwao
 
Wacha watapeliwe wao
Wakitapeliwa wewe unapata hasara gani?
Hata kama ni kweli ni kampuni ya kitapeli sidhani kama kuna unalolipoteza
Wacha watapeliwe watajifunza kupambana na yanayowahusu
We huna tofauti na mchawi
 
Kwa ufupi haya ni kweli ni makampuni ya kitapeli ,kwangu binafsi nimejiunga na LBL na F.I.C tangu mwaka jana na pesa niliyowekeza imesharudi sahivi nakula tu pesa zao na najua siku moja watasepa na kijiji hivyo nipo makini na sijaongeza pesa tena maana najua muda wowote watapotea.
 
Umejuaje kuwa wanalazimisha,kwanini wewe?wakati kila msanii anatangaza kuwa tembelea YouTube account yangu Kuna tofauti gani,kujenga team ni priority ya mtu,in my case najenga platform za muda 120 days 100 days.wakisepa na Kijiji poa,last year niliwekeza kwenye mitaji ya wakulima elnino ikaja hapo kati lakini mtaji ulirudi na mwaka huu Kuna mvua kidogo,hivyo ndivyo Dunia inaenda ,Haina utulivu kabisa. Hata TBL wako na hard time this time sababu watu hawana mapenzi na bia Tena wemebadiri mwelekeo wanapenda Serengeti product na product ndogondogo za take away,ni swala la muda tuu utajua kuwa AI inaleta vitu vingi vipya kama vile Ask na Chatgtp.Technology is running the world.
SAWA, UMEELEWEKA.
HIYO MICHONGO YENU NINYI WAJANJA.
ENDELEENI KUPIGA MPUNGA BOSS.
 
Kwa ufupi haya ni kweli ni makampuni ya kitapeli ,kwangu binafsi nimejiunga na LBL na F.I.C tangu mwaka jana na pesa niliyowekeza imesharudi sahivi nakula tu pesa zao na najua siku moja watasepa na kijiji hivyo nipo makini na sijaongeza pesa tena maana najua muda wowote watapotea.
Mkuu FIC ndo ikoje tukapigwe na huku
 
Halafu hata sio watu wapya wanaotapeliwa, wale wale waliotapeliwa kwenye kampuni ya kalyinda ndo hawa wamejazana kwenye LBL,

Walio wengi ni wale walokole wanaoishi kwa kuombewa na manabii na mitume wao, Kuna watu nchi hii wanaamini wanaweza kufanikiwa bila kutumia akili bali kulia makanisani na kutapeliwa sadaka na hao manabii

Watu waliozoea kutapeliwa sadaka, wanaowatapeli wananunua magari na kuishi kifahari lakini watapeliwa kutwa wanaombewa ili wapate magari na mali. Hao watu ukiwaeleza kuwa LBL ni utapeli wanakuona wewe hamnazo, Kiukweli Tanzania ina wajinga wengi sana

Niko nafanya mpango wa kutengeneza application/Mfumo kama wa LBL najua nitawapata tu watanzania wajinga niwapige pesa.

NB: Kuwa tajiri huitaji kuwa na huruma na mtu unaemwibia
Unishtue mkuu, tuungane tuwapige.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom