Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Lema: Mh. Rais, Vyama vya siasa sio uadui

Ni active member lakini sio verified user, na hawezi kuwa verified kwani hana uwezo kujenga hoja kwenye uwanja huru. Anaweza kujenge hoja na kejeli anapokuwa mbele ya polisi na vyombo vingine vya dola. Umewahi kumuona kwenye midahalo zaidi ya kuhutubia kama kasisi?
Kumbe haya mawe yote tunayo mpondaga humu hua yanampata.....[emoji15] [emoji45]
 
Je ni Lema yeye anaruhusiwa kuombea wenzie kifo ? Anahubiri asichokitenda, kati ya watu ambao wanafanya siasa za kupandiki chuki na uchochezi CDM wanaongeza, wako tayari hata kuombea mtu afe ila vivyo hivyo wako vizuri sana ku play victim card. Godbless J Lema acha unafiki.

Alieombewa kufa ni nani huyo..? Maana naona umekazana tu hapa, kaombea watu kifo.. Hebu mtaje huyo alieombewa kifo na Lema..
 
Lema alikuwa anamuombea Rais kifo miezi michache iliyopita, tena kwa mbwembwe na kejeli unamuombea binadamu mwenzio asifikishe 2020, leo kwa unafiki anajidai kuhubiri upendo, huu unafiki Godbless J Lema unautoa wapi ?

Acha kujitoa ufahamu, unaweza kumuombea mtu kifo ana akafa? Kuna binadamu mwenye nguvu ya kumuombea mwingine kifo ana akafa kweli? Ungeniambia alimpiga risasi akapona ningekuelewa.
 
Mnahangaika na huyo raisi...
Kauli zake za kijinga jinga ndio zitumike dhidi yake next time.
Watanzania wanatakiwa wajue walichagua mtu wa aina gani.
Haina haja ya kuomboleza na kumsihi mtu ambaye yupo doomed.
 
Mh Rais Magufuli nakusalimu.

Nimetoka Magereza hivi karibuni ambako nilikuwa huko kwa zaidi ya miezi minne kwa kunyimwa masharti ya dhamana kwa dhamana iliyokuwa wazi.

Mh Rais, nimeona kwenye vyombo vya habari leo kuwa kwamba wale Wabunge waliokuwa wanataka kunisalimia nilipokuwa Magereza kuwa ni wasaliti wa chama cha CCM, Mh Rais wengi walinisalimia , Wachungaji , Masheikh, Wabunge na Viongozi mbali mbali , sidhani kama hatua hii ilikuwa ni usaliti isipokuwa upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yoyote haswa wakati wa matatizo.

Mh Rais , nimeogopa sana kwa kauli hii yako , je Taifa linakwenda wapi , hivi kweli sisi Wabunge ni maadui? kama viongozi tutafikiri utengano ni moja ya njia ya kuimarisha vyama vyetu , basi bila shaka tutakuwa tunalitendea Taifa ubaya .

Dhambi hii ikikomaa basi ni hakika kwamba lugha za udini ,ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa , ni muhimu sasa tukajenga utamaduni wa kuimiza mshikamano wa Kitaifa bila kujali itikadi kama kweli tunawapenda masikini na wanyonge wa Nchi hii .

Nawaomba Wabunge wenzangu walionijali wakati niko magereza wasijisikie vibaya kwani walifanya jambo jema na muhimu kwa wakati muhimu sana katika maisha yangu , ninatarajia kuwa Spika wa Bunge atatoa kauli juu ya kauli yako .

Mh Rais wakati wa Msiba wa Christina Lissu dada yake na Mh Tundu Lissu nilikuona katika msiba ule wewe na Mama yetu Mke wako , je Mh Rais na wewe ulikuwa unasaliti Chama chako ?

Mh Rais neno la Mungu linasema , Wapendeni maadui zenu , waombeni wanaowauzi , wabarikini wanaowaonea kwani kufanya hivi ni kuishi kwa thawabu za Mwenyezi Mungu .

Mungu akubariki sana , natumaini Mh Rais sitakamatwa leo kwa ujumbe huu mfupi .


Godbless J Lema (MB)
Kwa sisi Wakatoliki tupo kwenye mwezi wa toba Kwaresma, imani yetu inatufundisha kusamehe hata walio adui zetu kwa kipindi hiki, na mtukufu Rais nj mkatoliki mwenzangu.

Bahati mbaya tuna Askofu mnafki kama Pengo mambo haya anveyafanya Kikwete kwa sababu ya uislamu wake basi ungesikia matamko mazito ya TEC na Kardinali mwenyewe na waraka wake wa kichungaji.

Kwakuwa wewe una chanel nyingi za kusikilizwa kwa wadhifa wako, nashauri copy ya waraka huu imfikie Kardinali Pengo, Tec, na ile kamati ya viongozi wa dini ya amani.

Kamwe usitalajie Sheikh mnafiki kama sheikh mkuu wa mkoa Darisalama kuinuwa mdomo wake kukemea hili, Bakwata ndio kabisa GSM wanawajengea ghorofa.

Wacha niishie hapa maana Watanzania wote wameufyata kwa mtu mmoja, ngoja na miye nikapapalie migomba yangu.
 
Mh Rais Magufuli nakusalimu.

Nimetoka Magereza hivi karibuni ambako nilikuwa huko kwa zaidi ya miezi minne kwa kunyimwa masharti ya dhamana kwa dhamana iliyokuwa wazi.

Mh Rais, nimeona kwenye vyombo vya habari leo kuwa kwamba wale Wabunge waliokuwa wanataka kunisalimia nilipokuwa Magereza kuwa ni wasaliti wa chama cha CCM, Mh Rais wengi walinisalimia , Wachungaji , Masheikh, Wabunge na Viongozi mbali mbali , sidhani kama hatua hii ilikuwa ni usaliti isipokuwa upendo ambao ni muhimu kwa binadamu yoyote haswa wakati wa matatizo.

Mh Rais , nimeogopa sana kwa kauli hii yako , je Taifa linakwenda wapi , hivi kweli sisi Wabunge ni maadui? kama viongozi tutafikiri utengano ni moja ya njia ya kuimarisha vyama vyetu , basi bila shaka tutakuwa tunalitendea Taifa ubaya .

Dhambi hii ikikomaa basi ni hakika kwamba lugha za udini ,ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa , ni muhimu sasa tukajenga utamaduni wa kuimiza mshikamano wa Kitaifa bila kujali itikadi kama kweli tunawapenda masikini na wanyonge wa Nchi hii .

Nawaomba Wabunge wenzangu walionijali wakati niko magereza wasijisikie vibaya kwani walifanya jambo jema na muhimu kwa wakati muhimu sana katika maisha yangu , ninatarajia kuwa Spika wa Bunge atatoa kauli juu ya kauli yako .

Mh Rais wakati wa Msiba wa Christina Lissu dada yake na Mh Tundu Lissu nilikuona katika msiba ule wewe na Mama yetu Mke wako , je Mh Rais na wewe ulikuwa unasaliti Chama chako ?

Mh Rais neno la Mungu linasema , Wapendeni maadui zenu , waombeni wanaowauzi , wabarikini wanaowaonea kwani kufanya hivi ni kuishi kwa thawabu za Mwenyezi Mungu .

Mungu akubariki sana , natumaini Mh Rais sitakamatwa leo kwa ujumbe huu mfupi .


Godbless J Lema (MB)

Ila Lema nawe uache unafiki.

Uwe unachunga kauli zako.

 
Lema fanya yako..Jimboni hakuna maji ya uhakika wala umeme!Miundo mbinu ya shida na vijana wengi hawana ajira!Ila kila siku una deal unarukia yasiyokuhusu..Fanya yako na shughulikia kero za wananchi wako!Period
Acha siasa zako rahisi wewe. Wewe ndio unajua kero za wananchi? Hopeless propaganda in the making.
 
Alieombewa kufa ni nani huyo..? Maana naona umekazana tu hapa, kaombea watu kifo.. Hebu mtaje huyo alieombewa kifo na Lema..
Acha unafiki, haujui Lema amekaa Kisongo kwa kesi ipi ?
Yeye yuko radhi kumuombea Rais afe ila analia lia hapa kuhusu kusalimiwa tu, kweli Nabii Lema ana nyumbu wengi.
 
Lema fanya yako..Jimboni hakuna maji ya uhakika wala umeme!Miundo mbinu ya shida na vijana wengi hawana ajira!Ila kila siku una deal unarukia yasiyokuhusu..Fanya yako na shughulikia kero za wananchi wako!Period
Siyo kazi ya mbunge kutafutia vijana ajira wewe, muulize Rais wako tangu ameingia madarakani ametoa ajira ngapi zaidi ya watu kupoteza ajira?
 
Acha kujitoa ufahamu, unaweza kumuombea mtu kifo ana akafa? Kuna binadamu mwenye nguvu ya kumuombea mwingine kifo ana akafa kweli? Ungeniambia alimpiga risasi akapona ningekuelewa.
Hayo muulize Nabii Lema, yeye ndio alikuwa anasema kwa mbwembwe na kejeli kuwa Rais atakufa kabla ya 2020, leo analia lia kwa sababu ya kuto kusalimiwa tu. Unafiki utamuumiza Lema.
 
Mna wakati mgumu sana upinzani safari hii msipo simama pamoja na kuweka tofauti zenu pembeni sijui hali itakuwaje
Watanzania ndio wanawakati mgumu siyo wapinzani huko ni kujitia tu upofu wa kisiasa. Taifa linapokuwa la chuki, visasi n.k. tutaumia wote hatasalia mtu hata asiyekuwa na chama.
 
Kumpenda mtu isiwe one way traffic!

Yaani kutaka wewe tu upendwe lakini hutaki wewe kuwapenda wengine.

Hata kumuombeA mtu mabaya sio upendo achilia mbali kutaka watu wasisalimiane .

Mbona hatukuona huo upendo au ushauri kwenye hii habari?

LINK==> CCM wazungumzia uamuzi wa wabunge wa UKAWA kutowasalimia

LINK==> Saed Kubenea ataka wabunge wa UKAWA wenye wapenzi wao CCM wawasuse

Ama kweli mkuki kwa Nguruwe ni mtamu...

It's very easy to act as victim wakati wewe ndiye aggressor.

Inanikumbusha kwenye football ambapo mchezaji anamtemea mate mchezaji mwingine ambapo yule aliyetemewa mate anapatwa na hasira na kurusha kofi au ngumi. Referee ataona mwenye makosa ni yule aliyerusha kofi au ngumi na hapohapo atampatia kadi nyekundu.
kwahiyo unataka kutueleza Rais yuko sahihi?
 
Asante sana kwa ujumbe wenye busara na hekima Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless J Lema .
Dhambi hii ikikomaa basi ni hakika kwamba lugha za udini ,ukanda na ukabila hazitaacha kukomaa , ni muhimu sasa tukajenga utamaduni wa kuimiza mshikamano wa Kitaifa bila kujali itikadi kama kweli tunawapenda masikini na wanyonge wa Nchi hii
 
Back
Top Bottom