Uchaguzi 2020 Lema: Msafara wa mgombea Urais, Tundu Lissu washambuliwa vibaya katika Ofisi ya CHADEMA Wilayani Hai, Kilimanjaro

S

Sawa Mkuu Wangu...

Yatadhihirika tu,kuwa hayo Ni Maigizo...

Hizo ni SETUPS TU ili Nganga Itimie...

Zile BARUA Za Hague SI ndio Preamble....
Hayo mambo ya barua ya nini kama haki ya watu haichezewi ?!. Mara ni kanda maalumu ya fujo. Lakini udhamini umeenda bila vurugu iweje hai kwa Sabaya ?!. Mmefanya siasa miaka mitano mfululizo hukuona fujo za wana Cdm . Wao kutafuta tu wadhamini hamtaki ?!
 
Ccm mpya wajinga sana
 
But ikumbukwe kuwa OCD nae anahusika kwenye hilo tukio
 
WEWE NDO sabaya Eti unaandika utumbo gani Vijana wa Lumumba wajinga sana !.Hasara amekula mzazi wako
Mimi SI Sabaya na Kama Ni Utumbo Andaa Ndizi Ujinome...

Nimekuwekea Majina Ya Mabeberu Wanaowasukuma..unanishambulia Mimi Mkuu?!!

Kalaghabaho Mkuu Wangu,Ukipata Ndizi Mshale itakuwa mwakeπŸ‘πŸ‘
 
Mapapa kvp akati mmoja wa hao vijana ameshasema kuwa, walitumwa na DC pamoja na OCD na waliahidiwa kulipwa elfu 20 kila mtu...

NB:Yani mtu unaamua kurisk maisha yako kisa elfu 20 kwelii
Na huenda hata wasilipwe wakadhulumiwa wapuuzi Sana hawa vijana wenzetu.
 
Nakunga mkono mkuu huu ni mda wa kushikamana tusiseme vijana wamehogwa wala nini. kipindi hiki ndo kipindi cha watu kuchomwa sindano za sumu na zenye maumivu makali.
Africa hakuna upinzani wa kweli hata kidogo, vyama vingi vya upinzani huwa vina pata Good support kutoka kwa MABEBERU na muda mwingine wapinzani kutumia ufinyu wa mawazo ya wananchi kama mtaji wa kuonekana kuwa wanaonewa na serikali iliyo madarakani
Tushikamane wote kwa pamoja kulijenga taifa letu. Wagombea wote watowe hoja za kujenga na si kubomowa, penye kukosowa wakosowe na kusema nini kifanyike kuepuka hayo makosa penye kupongeza papongezwe na si kutukanana majukwani.
 
Lissu na zitto Ni wapinzani
Kazi Yap ni kupinga
Unataka wafanye kzi gani tofauti na hiyo?
Wakianza kuunga mkono tutawauliza kuna haja gani ya wao kuwa wapinzani?
Fikiri, sehemu zote walikopita hakukuwa na mapanga na marungu ila wakayabeba hai? Kwann? Njia ya mwongo in fupi, kama wanahubirj raisi hajafanya kitu na vitu vinaonekana kuanzisha vita si suluhu. Tuwe makini na hii amani.
Una uhakika walikuwa na hizo silaha au umekaririshwa na hao jamaa zako?

Hata kama ni kweli walikuwa na hizo silaha kama unavyodai, je kilikuwa na shida gani kutoa ripoti polisi ndio washughulikie hilo suala?

Sasa hao vijana walipoanza kurusha mawe, je hao mnaodai walikuja na mapanga sijui vipi wangejibu mapigo unadhani hali ingekuwaje?

Utu uzima ni kutumia akili yako kupambanua mambo sio kuamini kila unaloambiwa. Hivi kweli kama hao watu walikuja na hizo silaha na lengo ilikuwa kuzitumia kufanya fujo kama ulivyoaminishwa, kitu kimewazuia wasizitumie?
 
Ndio uende kuwakataa kwenye sanduku la kura!
 
πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘πŸ‘
 
Mbowe naye alifanyiwa hivihivi tena mbele ya vyombo vya dola lakini hata sisimizi hakukamatwa kwa tukio hilo pamoja na tukio kufanyika mbele ya vyombo vya dola ambavyo vinakibali cha kisheria kukamata makosa yanayofanyika mbele yao.

Kilekile kimejirudia tena kwa mtindo uleule mbele ya vyombo vilevile vya dola vyenye wajibu wa kuzuia uhalifu kama huu lakini hakuna aliyekamatwa,kinachosubiriwa ni kuambiwa kuwa viachiwe vyombo vya dola vifanye uchunguzi wake wakati vilikuwa na nafasi ya kuzuia tukio lisitokee na kukamata watuhumiwa hapohapo.

Kwa ukimya huu wa vyombo vya dola wakutokuwajibika kwa jambo ambalo siyo mara moja kutokea na linalowahusu viongozi wanaoipinga CCM moja kwa moja linatoa taswila kuwa wapangaji wa matukio haya ni wale wa chama tawala na chama chao na ndio wanaotaka kuifuta amani ya nchi hii.
 
Chama changu twendeni kwenye mikutano yetu na mapanga hutaona mpumbavu yeyote akileta upumbavu tatizo tunaenda kama kanisani, tuache mzaha hawa wakijani washageuka muumiani tuache malalamiko.
Huu ni muda wa jino Kwa jino ndo heshima itapatikana huu muda si wa kuambiana ati ukipigwa shavu la kulia mgeuzie la kushoto, akikupora ardhi mpe na ng'ombe Kwa kufanya hivyo wewe utaenda peponi huyo dhulmati atakwenda motoni.
Siku moja green guard wakija vamia mkutano wetu halafu angalau watano wakaondoka bila vichwa hutaona tena huu upuuzi
 

Ukweli hali hii inasikitisha sana.
Sasa kama walikuja kumsikiliza Lissu, wakaona hotuba yake ilikuwa tofauti na walivyo tegemea, na wanasema hao chadema walikuja na marungu, mawe na visu, je hayo mabango waliyoshika yaliandikwa baada ya vujo kuanza au kabla ya vujo?

Sabaya ni janga naatagharimu mahisha ya hao wananchi waliokubali kununuliwa kwa 20,000/=.

Kama Rais ndiye aliyemweka, basi ni vizuri kwa sasa afikirie tofauti, vinginevyo watu wataamini yanayosemwa kuwa Rais ndiye aliyemtuma kufanya hivyo.
 
Vijana waliopandikizwa wanaweza kufanya fujo mbele ya polisi na wakaachwa tu waendelee kuleta fujo? Hivyo ndivyo akili yako inakutuma?

Hao Polisi Wanaweza Pia Wakawa Na Malengo Tofauti ....

Usikariri Mzee...

Kalaghabaho
 
Ndio siasa,vumilieni!
Wakisema hamjafanya kitu ni kazi yenu kuwambia watu mmefanya, lakini pia watu wakiona mlichokifanya moja kwa moja watawapuuza wanaosema hamjafanya kitu maana tayari wanaona kwa macho yao.

Pia uvumilivu kwenye maneno ya kisiasa ni muhimu sana. Kama vile wenzenu wanavyowavumilia mnapowaita ni vibaraka wa mabeberu, mara sijui wametumwa kuja kuuza nchi yote wanayavumilia. Hivyo mnapaswa na nyie kuvumilia hivyo hivyo hata wakiwaita nyie ni madikteta vumilia ndio siasa tuliyoichagua.

Kikubwa ni kujitahidi kuwashawishi wapiga kura wasiwachague.

Kufanya fujo kwakweli hiyo sio afya hata kidogo maana upande wa pili wakiamua kujibu mapigo hakutakuwa na mshindi wote tutapoteza.

Tusikubali kuingia kwenye mtego huu. Tutaumia wengi hata wale tusiokuwa na upande wowote kwenye siasa.

Jamani tuipende nchi yetu, tuilinde, vyama hivi ni vya kupita tu lakini nchi yetu ni muhimu kuliko hivi vyama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…