Leo ilipaswa kuwa mwaka 2031, Error katika upangaji wa Calender imetufanya tuwe 2024

Leo ilipaswa kuwa mwaka 2031, Error katika upangaji wa Calender imetufanya tuwe 2024

uthibitisho wake utaupata ukiangalia jinsi vitu vyote vilivyokua aligned perfectly, kuanzia tu kwenye mwili wako jinsi unavyofanya kazi kwa viungo kushirikiana zaidi ya mashine, mfano unaweza kupokea mawimbi ya sauti ukajua ujumbe na ukajibu

jinsi jinsia mbili ya kike na ya kiume zinavyoshirikiana kwa kutaka in nature kabisa na kuzaa,, in nature tuu jinsi utavyomlinda mtoto au uzao wako

jinsi tukivyokuta mazingira yapo tayari, kuna oxygen, maji na kilakitu dawa na virutubisho vyote vinavyoendana na mwili

kama hizo factors hizi chache hazikuaminishi kua Mungu yupo...

Je factors kama unazoziongelea ambazo pia ukiziangalia ni dhahiri kwamba zimezidiwa mashiko zitakuaminishaje kwamba hayupo ?
Kwanza kabisa, vitu haviko perfect. Watu wanazeeka, wanaumwa, wanakufa.Wanajamba, wanakunya, wanapata njaa. Vitu vinaoza. Hiyo si perfection.

Pili, vitu kuwa perfect si uthibitisho kwamba Mungu yupo, ni uthibitisho kwamba vitu viko perfect. Ukimuingiza Mungu hapo ni non sequitur logical fallacy.

Tatu, kama vitu kuwa na complexity ni ushahidi kuwa vimeumbwa, huyo Mungu naye ni complex, yeye naye kaumbwa ?

Hiyo hoja yako inathibitisha Mungu hayupo, haithibitishi Mungu yupo.
 
Mkuu ili ujue Mungu yupo au hayupo fanya zoezi dogo tu ziba pua na mdomo usipumue kwa lisaa limoja tu ukitoka hapo utapata jibu mujarabu kabisa

Usijibu hoja yangu hadi ufanye ivo kwanza hiyo ndio njia pekee ya kujua kama kweli Mungu yupo au hayupo ahsante
Sasa kuziba pua kunathibitishaje Mungu yupo?

Ukiziba pua hivyo utakufa.

Kifo ni uthibitisho kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Hoja yako ni uthibitisho kwamba Mungu hayupi, si uthibitisho kwamba Mungu yupo.
 
Kwa nini tuanze kuhesabu miaka tangu alipozaliwa Yesu?
Roma Locuta, Causa Finita
Kwa vyovyote kwa kuwa wote tupo katika sayari moja na ulimwengu mmoja, ilikuwa ni lazima kutafuta standard moja. Wenye akili zao wakapanga standard za kutumika, wasio na akili wakalazimika kufuata standard hizo
 
Roma Locuta, Causa Finita
Kwa vyovyote kwa kuwa wote tupo katika sayari moja na ulimwengu mmoja, ilikuwa ni lazima kutafuta standard moja. Wenye akili zao wakapanga standard za kutumika, wasio na akili wakalazimika kufuata standard hizo
Kwa hiyo umekubali kwamba hii ni mipango ya watu tu, na hizo habari za Mungu kuwapo ni sehemu ya habari hiyo hiyo ya kutaka kuwapangia watu wote wafuate standard moja tu?
 
Kwa hiyo umekubali kwamba hii ni mipango ya watu tu, na hizo habari za Mungu kuwapo ni sehemu ya habari hiyo hiyo ya kutaka kuwapangia watu wote wafuate standard moja tu?
upangaji wa calender hauna uwezo wowote wa kuonyesha kwamba Mungu yupo au Hayupo,
Yaani hakuna uhisiano kabisa. hata ingekwepo calender moja,
 
Kwa hiyo umekubali kwamba hii ni mipango ya watu tu, na hizo habari za Mungu kuwapo ni sehemu ya habari hiyo hiyo ya kutaka kuwapangia watu wote wafuate standard moja tu?
Tuliumbwa na Mungu kuwa na utashi wa kuyatawala mazingira yetu

Mwanzo 1:27-28
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
 
upangaji wa calender hauna uwezo wowote wa kuonyesha kwamba Mungu yupo au Hayupo,
Yaani hakuna uhisiano kabisa. hata ingekwepo calender moja,
Kwa sababu Mungu mjuzi wa yote mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwapo, kusingekuwa hata na haja na kuonesha Mungu yupo.

Kwa sababu kila mtu angejua Mungu yupo bila utata, kufundishwa wala mjadala.
 
Tuliumbwa na Mungu kuwa na utashi wa kuyatawala mazingira yetu

Mwanzo 1:27-28
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
Hatujaumbwa na Mungu na hatuyatawala mazingira yetu.

Na hiyo Biblia unayoinukuu ni kitabu kimeandikwa na watu tu, kina uongo mwingi sana. Nikikuwekea msururu wa contradictions zilizo ndani ya Biblia huwezi kuzimaliza kuzitatua.

Bisha.
 
Sasa kuziba pua kunathibitishaje Mungu yupo?

Ukiziba pua hivyo utakufa.

Kifo ni uthibitisho kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Hoja yako ni uthibitisho kwamba Mungu hayupi, si uthibitisho kwamba Mungu yupo.
Bado hujafanya nilichokuambia fanya kwanza halafu urudi tena
 
Bado hujafanya nilichokuambia fanya kwanza halafu urudi tena
Wewe huwezi kufanya fikra dhahania.

Hata nikifanya hicho ulichoniambia, hakitathibitisha Mungu yupo, kitathibitisha Mungu hayupo.

Unaelewa hilo?
 
Wewe huwezi kufanya fikra dhahania.

Hata nikifanya hicho ulichoniambia, hakitathibitisha Mungu yupo, kitathibitisha Mungu hayupo.

Unaelewa hilo?
Nakuapia ukifanya lazima utapata jibu hiyo ni practical based evidence ya kujua kama kweli kuna Mungu au hakuna fanya uone
 
Hatujaumbwa na Mungu na hatuyatawali mazingira yetu.
Na hiyo Biblia unayoinukuu ni kitabu kimeandikwa na watu tu, kina uongo mwingi sana. Nikikuwekea msururu wa contradictions zilizo ndani ya Biblia huwezi kuzimaliza kuzitatua.
Bisha.
Sihitahi kubishana. Endelea tu kupinga uamuzi wa kuhesabu miaka kwa utaratibu wa BC na AD. Mimi kwa elimu yangu ya hesabu, unapozungumzia magnitude ya fundamental quantities of physics, ni lazima uwe na reference point. Mass, Time na Length huwezi kuziexpress bila reference. Hawa walioamua kupima miaka (Time), waliona reference yao iwe ni mwaka wa kuzaliwa Kristu. Unaruhusiwa pia kutafuta namna tofauti ya kuelezea hilo, lakini fundamental quantities za physics zitabaki kuwa ni Mass, Time na Length. Ni sawa tu na convention ya boiling point ya maji kuwa 100 oC, au density ya maji kuwa 1g/cc
 
Kwa sababu Mungu mjuzi wa yote mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwapo, kusingekuwa hata na haja na kuonesha Mungu yupo.

Kwa sababu kila mtu angejua Mungu yupo bila utata, kufundishwa wala mjadala.
mimi nikichogundua, ni kua wewe unahitaji kuona vitu fulani kama hivyo unavyosema ndo uamini yupo, ila sasa Mungu yeye ana namna yake nyingine kabisa ambayo wewe kwa ulivyotaka iwe ndo haiendani,

hata hivyo akili ya binadamu japo unaweza kuona umefikiria kwa kina hadi mwisho, kumbe ndo inapoweza kuishia lakini vitu vingine vinahitaji ufikiri beyond and beyond ambapo pia kwa capacity ya ubongo wa binadamu haiwezekani

ndo maana wanasayansi kuna mambo mengi hawawezi kuyaelezea na hawajui mechanisim yake,

hawawezi hata kuzuia mtu asizeeke, hawawezi kutengeneza hata seli moja ikafanya kazi,

ukishindanisha ufahamu wako na kuweka conclusion hivo ni kama kushindanisha maji ya kwenye kikombe au bakuli na bahari

Mwanadamu amepewa akili ili aweze kuyatawala mazingira yake, ila pia ina limit yake sanasana inafanya vitu kutokana na experience na memory,

ila vitu ambavyo hawezi kugi experience physically kama uwepo wa Mungu,
ndo hapo kunakua na ubishani.
 
Zamani kalenda iliyokua ikitumika ilikua haiendani na mzunguko wa dunia kuizunguka jua, kwa hiyo majira yakawa yanabadilika mfano mwaka huu mvua zinanyesha mwezi wa 7, mwaka ujao zinanyesha mwezi wa 12, na kadhalika. Hii ni kwa sababu kalenda ilikua inapishana na jinsi dunia inavyozunguka jua.

Mwaka 45 KK (kama tunavyoujua kwa sasa), Julius Caesar alipanga kalenda upya ili iendane na mzunguko wa dunia. Akaweka mfumo wa kuwa na mwaka mrefu wenye siku 366 kila baada ya miaka mitatu yenye siku 365. Akaweza kupata wastani wa mwaka wenye siku 365.25 ambao ukawa unaendana na mzunguko wa dunia kwa kiasi kikubwa. Hii kalenda inaitwa Kalenda ya Julian.

Karne ya 6, takriban mwaka 525 BK, kulikuwa na mwanafunzi wa dini anayeitwa Dionysius Exiguus ambaye alianzisha mfumo wa kuhesabu miaka kutokana na mwaka aliozaliwa Yesu. Baada ya uchambuzi na mahesabu alizofanya, mwaka aliozaliwa Yesu aliuita 1 BK (Anno Domini), 2 BK, 3 BK, na kadhalika. Mwaka mmoja kabla ya kuzaliwa Yesu aliuita 1 KK (Before Christ), 2 KK, 3 KK, na kadhalika.

Kabla ya hapo, miaka ilihesabiwa kutokana na matukio, utawala, na kadhalika. Kwa Dola ya Kirumi, miaka ilihesabiwa kutokana na kuzaliwa kwa Dola ya Roma. Mfano mwaka 45 KK ambapo Julius Caesar alirekebisha kalenda ulikua ukijulikana kama mwaka 709. Kwa hiyo iliendelea kuhesabiwa hivyo hadi takriban mwaka 525 BK ambapo mfumo wa huyo mwanafunzi wa dini ukaanza kusambaa wa kuhesabu kuanzia mwaka aliozaliwa Yesu.

Kalenda ya Julian bado ilikua na makosa kwa kiasi fulani. Mwaka 1582 ikazaliwa kalenda mpya iliyorekebisha makosa kwenye Kalenda ya Julian, inaitwa Kalenda ya Gregorian. Hii kalenda tunayotumia sasa inaitwa Kalenda ya Gregorian ilianzishwa na Papa Gregory XIII mwaka 1582 ili kurekebisha mpangilio uliokuwepo kwenye Kalenda ya Julian. Kalenda ya Julian ilikuwa na wastani wa siku 365.25, ila kiuhalisia dunia inatumia siku 365.2424 kumaliza mzunguko wake kuzunguka jua. Kwa hiyo kutokana na Kalenda ya Julian, baada ya muda mrefu mzunguko wa dunia unapishana na kalenda.

(kafatilie mabadiliko yaliyofanywa ila siku 10 zikapunguzwa)

Kwanini Sasa Sio 2024?​

  1. Mwanafunzi wa dini aliyeanzisha mfumo wa kuhesabu miaka kwa kuzingatia mwaka aliozaliwa Yesu aliupanga mwaka aliozaliwa Kristo kuwa 1 BK. Mwaka kabla ya 1 BK aliuita 1 KK, kwa hiyo hakuna mwaka sifuri, maana yake ni lazima kuna mwaka umerukwa hapo kati.
  2. Kutokana na teknolojia ya sasa, wanasayansi wa anga (astronomers) wanaweza kuunda tena nafasi ya vitu vya anga: sayari, nyota, na kadhalika kama vilivyoonekana miaka mingi iliyopita. Kutokana na vitabu vya Injili vinavyoelezea kuzaliwa kwa Kristo, Injili ya Mathayo inaongelea kuonekana kwa nyota juu ya anga la Bethlehem ambayo iliwaongoza wanajimu. Kutokana na astronomia, mwaka 1 BK hakukuwa na nyota wala kitu chochote kilichoonekana angani. Ila mwaka 7 KK sayari Saturn na Jupiter zilikingiliana mara tatu ndani ya miezi tisa juu ya anga la Bethlehem (planetary conjunction), kitu kinachofanya ikiangaliwa kutoka duniani inaonekana kama nyota inayong'aa sana.

Kwanini 7 KK ni Muhimu Zaidi Licha ya Kuwa Conjunction ni Kawaida Kutokea?​

Conjunction ya 2 KK ya Jupiter na Venus iliyoonekana kama nyota inayong'aa sana Bethlehem, haina umuhimu sana kwa sababu ilitokea mara moja mwaka 2 KK na imewahi kujirudia sehemu mbalimbali baada ya miaka fulani. Mfano 66 BK, hata mwaka 2021 pia kulikuwa na conjunction ya Jupiter na Saturn.

Umuhimu wa Triple Conjunction ya 7 KK​

  1. Conjunction ya 7 KK imejirudia mara tatu ndani ya mwaka mmoja, Triple Conjunction, na haijawahi kujirudia kutokea hivyo tena (mara tatu ndani ya mwaka mmoja).
  2. Kutokana na Injili ya Mathayo, nyota iliwaongoza wanajimu watatu kutoka sehemu mbali mbali kwenda Bethlehem (ambazo pia zilikuwa ni mbali sana na Bethlehem). Conjunction ya 2 KK ilionekana mara moja tu hivyo isingeweza kuwaongoza. Conjunction ya 7 KK ya Saturn na Jupiter imeonekana mara 3 ndani ya miezi tisa, kwa hiyo ni likely kuwaongoza wanajimu kutoka sehemu ya mbali.
(ukitaka kujua zaidi fuatilia triple conjunction of Saturn and Jupiter of 7 KK)

Kwa hiyo, kulingana na astronomia ya kisasa, upangaji wa miaka kwa kadiri ya mwanafunzi wa dini Dionysius Exiguus ulikuwa na makosa ya miaka 7 ambayo inaweka huu mwaka kuwa 2024 badala ya 2031.

Ambacho Huenda Hukukijua Kabla​

Tarehe inayofuata baada ya tarehe 4/10/1582 ni tarehe 15/10/1582. Yaani baada ya tarehe 4 ilifuata tarehe 15 (kutokana na kuhama kutoka kutumia Kalenda ya Julian kwenda kwenye Kalenda ya Gregorian). Pia kwa mtazamo mwingine utaona ni jinsi gani Roma na Kanisa Katoliki limekuwa na nguvu na ushawishi kwenye mifumo tunayotumia hadi sasa.
CHAI
 
mimi nikichogundua, ni kua wewe unahitaji kuona vitu fulani kama hivyo unavyosema ndo uamini yupo, ila sasa Mungu yeye ana namna yake nyingine kabisa ambayo wewe kwa ulivyotaka iwe ndo haiendani,

hata hivyo akili ya binadamu japo unaweza kuona umefikiria kwa kina hadi mwisho, kumbe ndo inapoweza kuishia lakini vitu vingine vinahitaji ufikiri beyond and beyond ambapo pia kwa capacity ya ubongo wa binadamu haiwezekani

ndo maana wanasayansi kuna mambo mengi hawawezi kuyaelezea na hawajui mechanisim yake,

hawawezi hata kuzuia mtu asizeeke, hawawezi kutengeneza hata seli moja ikafanya kazi,

ukishindanisha ufahamu wako na kuweka conclusion hivo ni kama kushindanisha maji ya kwenye kikombe au bakuli na bahari

Mwanadamu amepewa akili ili aweze kuyatawala mazingira yake, ila pia ina limit yake sanasana inafanya vitu kutokana na experience na memory,

ila vitu ambavyo hawezi kugi experience physically kama uwepo wa Mungu,
ndo hapo kunakua na ubishani.
Kitu cha msingi kabisa ni kwamba, napinga uwepo wa Mungu si kwa sababu mimi nataka kuona vitu fulani.

Hili si suala langu mimi binafsi, hizi ni hoja zilizokuwepo maelfu na maelfu ya miaka kabla mimi sijazaliwa.

Ni suala la logical consistency. Unaelewa logical consistency ni nini?

Yani imeandikwa Mungu yupo, mtaona cha bluu, halafu mnaona chekundu, hamuoni cha bluu. Mnahoji, mbona tuliambiwa tutaona cha bluu halafu tunaona chekundu, huyo Mungu yupo kweli?

Hapo nikihoji, si suala langu tu, ni suala la logical consistency.

Mpaka sasa hujathibitisha Mungu yupo.
 
Sihitahi kubishana. Endelea tu kupinga uamuzi wa kuhesabu miaka kwa utaratibu wa BC na AD. Mimi kwa elimu yangu ya hesabu, unapozungumzia magnitude ya fundamental quantities of physics, ni lazima uwe na reference point. Mass, Time na Length huwezi kuziexpress bila reference. Hawa walioamua kupima miaka (Time), waliona reference yao iwe ni mwaka wa kuzaliwa Kristu. Unaruhusiwa pia kutafuta namna tofauti ya kuelezea hilo, lakini fundamental quantities za physics zitabaki kuwa ni Mass, Time na Length. Ni sawa tu na convention ya boiling point ya maji kuwa 100 oC, au density ya maji kuwa 1g/cc
Hata habari ya reference ya mwaka wa kuzaliwa Kristu wamekosea.

Ndiyo point ya uzi huu.

Na wamekosea kwa sababu hizi ni habari za watu tu, Mungu hayupo. Angekuwapo, angewaongoza wasikosee tangu mwanzo.
 
Kitu cha msingi kabisa ni kwamba, napinga uwepo wa Mungu si kwa sababu mimi nataka kuona vitu fulani.

Hili si suala langu mimi binafsi, hizi ni hoja zilizokuwepo maelfu na maelfu ya miaka kabla mimi sijazaliwa.

Ni suala la logical consistency. Unaelewa logical consistency ni nini?

Yani imeandikwa Mungu yupo, mtaona cha bluu, halafu mnaona chekundu, hamuoni cha bluu. Mnahoji, mbona tuliambiwa tutaona cha bluu halafu tunaona chekundu, huyo Mungu yupo kweli?

Hapo nikihoji, si suala langu tu, ni suala la logical consistency.

Mpaka sasa hujathibitisha Mungu yupo.
ahaa kumbe wewe umeamua tu kuamini hayupo kwasababu ya logic

kuna vitu vingi sayansi haina Majibu

hili ni mojawapo
 
Back
Top Bottom