Liberata Mulamula: Rais Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana

Liberata Mulamula: Rais Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana

Kuna kitu kimoja ambacho nakichukia kupita kiasi katika maisha yangu ya U-Tanzania. Hiki ni kauli za Polisi au wanasiasa pale ambapo wanajaribu kuficha au kupotosha ukweli ambao ukiwekwa wazi wananchi wataona wanavyokiuka haki za msingi za Watanzania, wanavyokandamiza demokrasia au hata wanavyofanya uhalifu kama wanasiasa au polisi.

Nadhani mmesikia kauli za polisi za "waliuwawa katika mapambano makali ya silaha na polisi na hakuna askari aliyejeruhiwa", "aliuwawa na kitu cha ncha kali tunafanya uchunguzi", "alikufa kwa kujaribu kuruka toka kwenye gari akiwa na pingu" nk.

Na pia kauli za wanasiasa kama "kama hutaki tozo nenda Burundi"; "kama huna nauli piga mbizi"nk.

Sasa leo nimekutana na kauli ya Waziri wa Mambo ya Nchi za nje, Liberata Malamula, akijaribu kueleza kwa nini mkutano kati ya Raisi Samia na wapinzani haukutokea. Anasema "Raisi Samia alipanga kukutana na wapinzani lakini ratiba zikaingiliana". Hivi huu mkutano ulikuwa ufanyike kwa muda gani, miezi sita mfululizo?

Ni wazi kwamba hawa watu wanapotoa hizi kauli wanaona sisi Watanzania ni wajinga, hatuna akili na tanakubali lolote tutakalowaambiwa.

Kwa kiingereza huwa ni ni falsafa ya "insulting Tanzanians' intelligence"

Napenda kwa mara nyingine niwaambie Polisi na Wanasiasa jambo moja, kwamba mtitutukane Watanzania, msidhani kwamba hatuna aiki, na msione upole wetu na utunzaji wetu wa hali ya amani nchini kuwa ni watu ambao tupotupo tu kama mazezeta. Uvumilivu wa kutukanwa una mipaka yake, na mnatutukana sana kwa hizi kauli zenu.

Hizi ni kauli zinafanya niwachukie wanasiasa na polisi kwa kiwango cha juu kabisa, kwa kuwa ni kauli ambazo naziona kama matusi kwa Watanzania. Ninavyozitafsiri mimi ni kwamba mnatoa kauli kama hizo eidha kwa kuwa nyie hamna uwezo wa kufikiri, au kwa kuwa mnadhani sisi Watanzania hatuna uwezo wa kufikiri. Jitafakarini sana. Tanzania ya 2021 sio Tanganyika ya 1961. We are not naive - you are disgustingly naive.


Tulishasema kuna watu wengi walikuwa wananufaika na uhasama. Wametumia mwanya huu kupata pesa za kunua vitu kama teknologia ya kurekodi watu, kununua wapinzani...... wote hawa watakosa kazi
 
Uwe na heshima kwa Mheshimiwa Rais wetu. Ni Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, sio samia.

Amandla...
Heshima haiombwi wala kulazimishwa bali inatengenezwa na matendo yako.

Kwa ukigeugeu wake, maneno yake kuwa tofauti na matendo yake, nani atamheshimu? Hapa ndani atasifiwa na kuheshimiwa na wanafiki, watu wajinga, na wanaojikomba kwake kutafuta teuzi, lakini siyo na watu wenye good free brain. Huko nje amekwishaanza kudharaulika sana, na ataendelea kuwa hivyo.
 
ni bola hajaongea nao kwanza,maana Kama angeongea nao,halafu inakuja kugundulika mwejekiti wao ni gaidi suspect,nadhani ingeleta taswira ya sintofahamu zaidi.nadhani wadukuzi walimtonya mama asikutane nao Kuna Mambo wameyadukua kwa Mr hai si shwari kukutana nao kwa Sasa!
Hao wote ni satanic syndicate. Wasubiri malipo yao hapa Duniani na ahera. Mmoja wa washauri wake wa siri, ameuawa jana. Maisha ya Duniani ni mafupi sana, jitahidi utende wema. Unakuja wakati utaomba ungerudi kwenye nafasi uliyokuwepo ili ukafute uovu wako, lakini hutaupata.
 
J
Hao wote ni satanic syndicate. Wasubiri malipo yao hapa Duniani na ahera. Mmoja wa washauri wake wa siri, ameuawa jana. Maisha ya Duniani ni mafupi sana, jitahidi utende wema. Unakuja wakati utaomba ungerudi kwenye nafasi uliyokuwepo ili ukafute uovu wako, lakini hutaupata.
Nani huyo?
 
ni bola hajaongea nao kwanza,maana Kama angeongea nao,halafu inakuja kugundulika mwejekiti wao ni gaidi suspect,nadhani ingeleta taswira ya sintofahamu zaidi.nadhani wadukuzi walimtonya mama asikutane nao Kuna Mambo wameyadukua kwa Mr hai si shwari kukutana nao kwa Sasa!
Umeishia darasa la ngapi? Siku hizi JF imekuwa kokoro. Limekusanya hata watu ambao hawajui kuandika vizuri. Ile JF ya Home of great minds inazidi kupotea.
 
Hivi kweli kwa akili za Hawa viongozi tutapata maendeleo kweli,siasa za kishamba zinalingamiza Taifa.
Laana kubwa ya Taifa hili, ni kukosa viongozi wenye uwezo. Kwenye uongozi wapo low minds ambao hawawezi kuipeleka nchi mbele.
 
Vichaka vya kujificha mtavipata vingi tu-
Leta hoja ujibiwe, sio unajiumauma. CHADEMA wameweka mambo yao wazi. Wanakamatwa, wanauwawa, wanapotezwa, wanateswa, wamekomaa kwenye reli. Hawana kichaka cha kujificha, wala hawana haja wala mpango. Sasa Serikali mara oohh, tutakutana na wapinzani. Mara oooh, chokochoko zimeanza, wananchi wapuuzeni hao, wana pa kukimbilia na wana hela za kujitibia tukiwajeruhi. Mara ooohhh, tulitaka kukutana nao, ratiba ilibana. Ni nani hasa anayejificha vichakani? Siyo CHADEMA , ni Samia na serikali yake
 
Kuna mawili. Kwanza, kwa bahati mbaya tumejenga jamii ambayo wanaofika kwenye ngazi za juu za uongozi sio ambao ni bora zaidi baina yetu kiuwezo na kifikra. Hata pale wanaporuhusu wenye fikra sahihi kufikia nafasi za uongozi, wananyimwa uhuru wa kufanya kazi kwa ubora na uwezo wao. Ni tokenism, wanawekwa huko ili watumikie maslahi ya wanaowaweka.
Pili, kwa muda sasa, wanaotuongoza hawatuheshimu. Mkataba wa viongozi na wanaoongozwa, na mahusiano baina ya pande hizo mbili sio mahusiano respectful. Kiongozi anapozungumza na umma, kichwani kwake anamuona mtu duni kwake kifikra. Kwa namna moja wanaweza kuwa sahihi kwa sababu kiwastani, uwezo wa kufikiri wa average Tanzanian uko chini ukilinganishwa na ule wa average kiongozi. Matokeo yake ni kauli unazozizungumzia za polisi na wanasiasa. Kwa namna fulani, hii state of affairs inaakisi kukosa kwao uwezo wa kuongoza na pengine ni hali ambayo wanai encourage kwa sababu inawanufaisha. Isingekuwa hivyo, ungeona sauti za wenzetu wenye fikra sahihi na uwezo wa kufanya mijadala inayohoji hizi kauli za viongozi zikipewa nafasi zaidi kwenye vyombo vyetu habari ili hata wale wasio na uwezo wajifunze. Na pia ubora wa elimu wanayopewa watoto wetu usingekuwa ulipo.
 


Pichani, Mzalendo akiwa Mazungumzoni na Beberu .

Hivi wenzetu ni kwamba wanatuoni ujinga wetu lakin wanatupotezea na kutucheka sana.
 
Samia aendelee kuonea wapinzani kwa sababu kashika Bunduki na Mabomu,wala siye hatuna shida ya kukutana na Samia,hana faida yoyote kwa Taifa aende zake huko
Basi ni bora hata aseme wazi, sina mpango wa kukutana na mtu yeyote. Lakini wanapokuja na utumbo wa maelezo kama huu wanatuletea harufu mbaya tu, hata kama sisi sio watu wa upinzani. Waelewe kwamba haya ni masuala yanahusu nchi yetu, hawa Wapinzani ni Watanzania pia, sio wapinzani wa kutoka Burundi wanakotaka twende. Wapinzani wakichachamaa tunaoathirika ni Watanzania wote.
 
Basi ni bora hata aseme wazi, sina mpango wa kukutana na mtu yeyote. Lakini wanapokuja na utumbo wa maelezo kama huu wanatuletea harufu mbaya tu, hata kama sisi sio watu wa upinzani. Waelewe kwamba haya ni masuala yanahusu nchi yetu, hawa Wapinzani ni Watanzania pia, sio wapinzani wa kutoka Burundi wanakotaka twende. Wapinzani wakichachamaa tunaoathirika ni Watanzania wote.
Hahaha umeongea ukweli
 
Wanaofaidika na hizi distractions ni wengi mkuu.

Ufalme ni gharama sana, Natamani Rais Samia angejua hilo. Amezungukwa na watu wajanja sana.
Mie sidhani kama amezungukwa na watu wajanja kiasi hicho. Hata kama waliomzunguka ni wajanja kwa kiasi fulani, inawezekana kabisa tatizo basi ni yeye kutotambua ujanja wa watu waliomzunguka. Sasa tuna neno linalosema mtu wa namna hiyo ni nani.
 
Wapinzani nawafananisha na abiria ndani ya boti wotw tupo safarini halafu anatokea abiria mmoja anaanza kutoboa boti mpinzanianaanza kufurahia kama zuzu kana kwamba hajui kitakachokuja kutokea kitawakumba wote........
 
Back
Top Bottom