Licha ya Rais kujitahidi kuchapa kazi lakini bado Wananchi hawamuelewi!

Licha ya Rais kujitahidi kuchapa kazi lakini bado Wananchi hawamuelewi!

Anajichanganya yeye mwenyewe.

1. Anafukuza wamachinga bila kuwa na sehemu za kutosha kuwaweka, anataka wakale wapi?
2. Anafukuza wamasai ili kufurahisha mwarabu
3. Anafanya teuzi za ajabu ajabu. Sasa mtu kama Kingai alifaa kuwa na nafasi ile?
4. Anakumbatia wabunge 19 walioko bungeni kinyume cha katiba
5. Hana ubunifu wa vyanzo vya mapato, yeye kutwa kucha anakopa tu anakopa tu
6. Anatuwekea tozo na kodi za ajabu ajabu, Tozo kwenye miamala ya simu, tozo tukitoa pesa zetu benki, anatulipisha kodi ya jengo la mwenye nyumba pindi tukinunua LUKU
7. Anatangaza kutuongezea mishahara kwa 23.3% halafu anaenda kutuongezea buku kumikumi, kisha anaichukua juu kwa juu tukitoa pesa benki.
8. Sisi tunataka katiba mpya, yeye anajifanya kuunda tume mpya ya Mukandala wakati Jaji Warioba alishamaliza kazi!

Sasa mtu kama huyu tutaanzia wapi kumuelewa kwa mfano?

1. Wamachinga hawajafukuzwa isipokuwa waliambiwa wasizonge hifadhi za barabara.

2. Hajafukuza Wamasai isipokuwa wamepunguzwa na kuhamishwa waliokaribu au ndani ya hifadhi ya ngorongoro.

3. Kwenye Teuzi hapo sina chakuchangia, kwani ni ishu ya mtazamo wa mtu na mtu. Kwako anaweza kuwa mzuri Kwa mwingine akawa Mbaya.
Kuhusu kufuata sheria Kama ameteua waliopindisha sheria basi amekosea.

4. Wabunge 19 wapo chini ya mhimili wa Bunge na sio serikali.

5. 😂😂 Vyanzo vya mapato alivyobuni ikiwemo Tozo umeona Watanzania wakipiga mayowe. Akibuni vingine zaidi watu watajiua walahi😂

6. Tozo ndio ubunifu aliouona unaweza fanyika Kwa urahisi na Kwa watu wengi yaani kila mtu ni rahisi kuchangia nchi kupitia tozo Kama tuu atatumia Simu, Luku, bank n.k

7. 😀😀😀 Hapo sina chakumtetea.

8. Pia kwenye Katiba mpya sina cha kumtetea.
 
Alisema yeye na JPM kitu kimoja lakini alipoingia tuu akaanza kufyeka watu wa JPM kuanzia kule Madawa ya kulevya, Kalemani, Polepole, Bashiru, mpaka kina.mbuge. wengi hapo ndio waliposhindwa kumuelewa falsafa yake ni ipi
 
1. Wamachinga hawajafukuzwa isipokuwa waliambiwa wasizonge hifadhi za barabara.

2. Hajafukuza Wamasai isipokuwa wamepunguzwa na kuhamishwa waliokaribu au ndani ya hifadhi ya ngorongoro.

3. Kwenye Teuzi hapo sina chakuchangia, kwani ni ishu ya mtazamo wa mtu na mtu. Kwako anaweza kuwa mzuri Kwa mwingine akawa Mbaya.
Kuhusu kufuata sheria Kama ameteua waliopindisha sheria basi amekosea.

4. Wabunge 19 wapo chini ya mhimili wa Bunge na sio serikali.

5. 😂😂 Vyanzo vya mapato alivyobuni ikiwemo Tozo umeona Watanzania wakipiga mayowe. Akibuni vingine zaidi watu watajiua walahi😂

6. Tozo ndio ubunifu aliouona unaweza fanyika Kwa urahisi na Kwa watu wengi yaani kila mtu ni rahisi kuchangia nchi kupitia tozo Kama tuu atatumia Simu, Luku, bank n.k

7. 😀😀😀 Hapo sina chakumtetea.

8. Pia kwenye Katiba mpya sina cha kumtetea.
4. Rais ni sehemu ya bunge!
Sehemu nyingine ya bunge ni general assembly.

Rais licha ya kuwa ni mkuu wa serikali lakini bado pia ni mkuu wa nchi!
 
Sabato Njema!

Tangu Rais arithi kiti cha Urais mwaka Jana hajapumzika wala sijasikia Kama alipata likizo. Anachapa kazi, Leo yupo huku kesho yupo Kule. Anachapa kazi.

Lakini licha ya jitihada zake zote katika kulitumikia taifa hili bado Wananchi hawamuelewi.

Hii inasababishwa na nini? Kuna yeyote anaweza kutuambia sababu ya hayo?

Mimi nikajiuliza maswali haya labda ni sehemu ya sababu;

1. Je ni Kwa sababu yeye sio mwanaume?

2. Je ni kutokana na gharama za maisha kupanda maradufu?

3. Je, ni maneno au Ile minong'ono kuwa nchi imerudi kuwa Shamba la Bibi?

4. Je, ni Kwa sababu Vijana hawana Ajira za uhakika Hali inayowafanya wakate tamaa?

5. Je, ni Kwa sababu aliowateua wanajulikana vibaya Kwa wananchi?

Unafikiri nini KIFANYIKE ili Wananchi wamkubali au wakubali kazi zake?

Taikon yeye msimamo wake ni kuwa;
i. anasapoti Rais au kiongozi yeyote apendaye HAKI,

ii. Asiye mroho, Mlafi wa Mali,
iii. Asiyejigeuza mungumtu, anayekubali kukosolewa,
iv. Anayeheshimu watu na kuwatumikia na sio wao wamtumikie.
v. Anayekemea na kuhakikisha Wezi wa Mali za nchi wanapewa Haki Yao ikiwa ni pamoja na adhabu Kali Kwa mujibu wa sheria.
vi. Atakayefanya Raia wasitawaliwe na Wageni. Wasigeuzwe Watumwa katika nchi Yao wenyewe.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Makamba, Mwigulu, Nape wana gundu kwenye utawala wake. Awafute kazi haraka sana.
 
Watoto hawawezi kumwelewa baba anayeenda shambani kila siku, lakini nyumbani njaa kali. Kuhusu wasaidizi wake, hilo nalo limesababisha watu wasimwelewe.. unateua watu wenye taswira mbaya kwa jamii unategemea nn
 
Anajichanganya yeye mwenyewe.

1. Anafukuza wamachinga bila kuwa na sehemu za kutosha kuwaweka, anataka wakale wapi?
2. Anafukuza wamasai ili kufurahisha mwarabu
3. Anafanya teuzi za ajabu ajabu. Sasa mtu kama Kingai alifaa kuwa na nafasi ile?
4. Anakumbatia wabunge 19 walioko bungeni kinyume cha katiba
5. Hana ubunifu wa vyanzo vya mapato, yeye kutwa kucha anakopa tu anakopa tu
6. Anatuwekea tozo na kodi za ajabu ajabu, Tozo kwenye miamala ya simu, tozo tukitoa pesa zetu benki, anatulipisha kodi ya jengo la mwenye nyumba pindi tukinunua LUKU
7. Anatangaza kutuongezea mishahara kwa 23.3% halafu anaenda kutuongezea buku kumikumi, kisha anaichukua juu kwa juu tukitoa pesa benki.
8. Sisi tunataka katiba mpya, yeye anajifanya kuunda tume mpya ya Mukandala wakati Jaji Warioba alishamaliza kazi!

Sasa mtu kama huyu tutaanzia wapi kumuelewa kwa mfano?
Umesema kweli! Aisee Kingai?
 
Nchi imemshinda hii, wengine tunaangalia tu anavyoteua watu wa hovyo kumsaidia, rushwa imekithiri, tozo karibia kila unachofanya kwa kutumia pesa yako, hakuna solutions kwenye issues zinazomgusa mwananchi, upotevu mkubwa wa rasilimali fedha..nk.

Kwanza kuongozwa na ke, hili ni kosa kubwa sana. Hata the most democratic nation halijawahi kuongozwa na ke.
 
5. Je, ni Kwa sababu aliowateua wanajulikana vibaya Kwa wananchi?
Sasa Mtu kama Nape, Mwigulu, January and the like unatarajia Kitu Gani? It is something to do with the system, CCM regime! Na next week TOZO ni kwenye PEDI
 
Wengi tu tunamuelewa sema tunazibwa midomo tunasubr Hilo sanduku la kura na sisi tuongee
 
Nchi imemshinda hii, wengine tunaangalia tu anavyoteua watu wa hovyo kumsaidia, rushwa imekithiri, tozo karibia kila unachofanya kwa kutumia pesa yako, hakuna solutions kwenye issues zinazomgusa mwananchi, upotevu mkubwa wa rasilimali fedha..nk.

Kwanza kuongozwa na ke, hili ni kosa kubwa sana. Hata the most democratic nation halijawahi kuongozwa na ke.
Akili zako ziko kwenye mapumbu tu maana ndiyo unAmzidi mwanamke! Kwani Angela Merkel wa Ujerumani au Margaret Thatcher wa Uingereza walikuwa wanaume?
 
Sabato Njema!

Tangu Rais arithi kiti cha Urais mwaka Jana hajapumzika wala sijasikia Kama alipata likizo. Anachapa kazi, Leo yupo huku kesho yupo Kule. Anachapa kazi.

Lakini licha ya jitihada zake zote katika kulitumikia taifa hili bado Wananchi hawamuelewi.

Hii inasababishwa na nini? Kuna yeyote anaweza kutuambia sababu ya hayo?

Mimi nikajiuliza maswali haya labda ni sehemu ya sababu;

1. Je ni Kwa sababu yeye sio mwanaume?

2. Je ni kutokana na gharama za maisha kupanda maradufu?

3. Je, ni maneno au Ile minong'ono kuwa nchi imerudi kuwa Shamba la Bibi?

4. Je, ni Kwa sababu Vijana hawana Ajira za uhakika Hali inayowafanya wakate tamaa?

5. Je, ni Kwa sababu aliowateua wanajulikana vibaya Kwa wananchi?

Unafikiri nini KIFANYIKE ili Wananchi wamkubali au wakubali kazi zake?

Taikon yeye msimamo wake ni kuwa;
i. anasapoti Rais au kiongozi yeyote apendaye HAKI,

ii. Asiye mroho, Mlafi wa Mali,
iii. Asiyejigeuza mungumtu, anayekubali kukosolewa,
bado mnachokonoa
iv. Anayeheshimu watu na kuwatumikia na sio wao wamtumikie.

v. Anayekemea na kuhakikisha Wezi wa Mali za nchi wanapewa Haki Yao ikiwa ni pamoja na adhabu Kali Kwa mujibu wa sheria.
Hii iliwahikosekana Tanzania? Haki kwa watuhumiwa na mijizi ya rasilimali zetu?
vi. Atakayefanya Raia wasitawaliwe na Wageni. Wasigeuzwe Watumwa katika nchi Yao wenyewe.
Unamjua mjomba wewe? Baada ya Nyerere, Magufuli pia aliona hili. Karibu maraisi wote isipokuwa Awamu hii...haileweki.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Rais Samia ni mtu wa vitendo sana kuliko sifa, ni mpenda haki na siyo mtu wa DHULUMA. Kikubwa anafanya kazi zake vizuri kwa ajili ya wananchi wa Tanzania. Wala hafanyi kwa ajili ya kutaka abakie madarakani mwaka 2025.

Kama hatutamtaka mwaka 2025 naamini atakaa pembeni lakini hawezi kufanya ule UHAYAWANI wa Magufuli wa kuiba chaguzi za vitongoji za 2019 na uchaguzi Mkuu wa 2020. Tuko mikono salama na Rais SSH

Wakati ndiyo utasema tusubiri 2025
 
Mama Samia anachapa Kazi hila tatizo la nchi ni Ccm tu na hakuna Kazi ngumu ya kuongoza wananchi wanaowaza ngono na Pombe 24/7
 
Back
Top Bottom