Ligi ya Morrison na Simba kwenye suala 'Release letter' imefikia patamu

Ligi ya Morrison na Simba kwenye suala 'Release letter' imefikia patamu

Unajua kusoma?? wapi hapo imeandikwa WAMEACHANA NAE?
Soma aya ya kwanza na yapili na yamwisho
Kwahiyo kaishaitwa kusaini mkataba mpya baada ya awali unaoishia? Mchezaji hajaachwa inakuaje unamtakia heri ktika safari yake mpya ya soka?
 
Maana yake timu nyingi ambazo zinacheza champions league haziwezi kumsajili kwa kuogopa kutomtumia huko,maana yake anakosa timu za maana kuchezea hapa Afrika

Huko ni kumkomoa mchezaji ambaye alitumia jasho na damu ktk kuichezea timu yako na kwasasa kama hauna matumizi yake hauna haja ya kuziba riziki yake
Alivyokua akitumia jasho na damu alikua analipwa mapumbuh au hela ambazo nazo zinapatikana kwa jasho na damu?
 
Kwani ile barua waliandika simba ilijielezaje? Simba si wamesema wameachana na Morrison asa kama umeshasema mmefikia makubaliano ya kuachana kwanini wasimpe talaka yake?View attachment 2267389
Simba haikutamka kumuachilia BM3, hiyo barua inaeleza kumtakia mapumzuko mema na kila la kheri katika safari yake ya kimpira.

Kuianza safari yake nyingine katika maisha yake ya kimpira ni pamoja na ku-clear kisha kusaini katika team nyingine legally na sio kiholea kama mnavyotaka.

Sheria lazima ifuatwe kwa manufaa ya taasisi na mchezaji husika, huu uswahili wa kuendesha taasisi kwa hisia na fadhila ndo uliiyumbisha team yenu.
 
Simba wako sahihi kukausha.
Kikanuni, Mchezaji anaetaka kuondoka hana haki ya kuomba Release Letter.

Club mpya inayomtaka mchezaji ndio inayotakiwa kutoa taarifa ya nia ya kumuhitaji mchezaji, kisha iombe release letter. (Yanga haina mahusiano mema na Simba ndio maana inapata ugumu)
Hii inaitwa waleteeeeeeeeee😂😂😂
 
Maana yake timu nyingi ambazo zinacheza champions league haziwezi kumsajili kwa kuogopa kutomtumia huko,maana yake anakosa timu za maana kuchezea hapa Afrika

Huko ni kumkomoa mchezaji ambaye alitumia jasho na damu ktk kuichezea timu yako na kwasasa kama hauna matumizi yake hauna haja ya kuziba riziki yake
akipewa sasahivi atacheza timu gani? kama inamtaka kwanini wasimnunue?
 
Unasema mpaka kifo kiwatenganishe!A mere joke!Teh!
Mkatana uheshimiwe bwana. Tatizo utopolo much known ukijumlisha kejeli za zungu poro roporopo sasa waje tu kuomba release letter. Sema yanga hawawez kuja wanapenda vya bure. Ndio maana hata wakongo wao awamu iliyopita hawakushiriki CAF CL kwa maana walishindwa kuvunja mikataba wakasubiria mpaka iishe
 
Kwahiyo kaishaitwa kusaini mkataba mpya baada ya awali unaoishia? Mchezaji hajaachwa inakuaje unamtakia heri ktika safari yake mpya ya soka?
Mkataba ukiisha kuna mawili kama timu inakutaka mnakaa mezani kuzungumzia terms mpya kama haikutaki inakuacha uende kama free agent
NB: MKATABA UKIISHA
 
Simba haikutamka kumuachilia BM3, hiyo barua inaeleza kumtakia mapumzuko mema na kila la kheri katika safari yake ya kimpira.

Kuianza safari yake nyingine katika maisha yake ya kimpira ni pamoja na ku-clear kisha kusaini katika team nyingine legally na sio kiholea kama mnavyotaka.

Sheria lazima ifuatwe kwa manufaa ya taasisi na mchezaji husika, huu uswahili wa kuendesha taasisi kwa hisia na fadhila ndo uliiyumbisha team yenu.
Anayekomolewa hapa ni Morrison, nakumbuka kuna ishu ilitokea zamani kati ya Yanga nadhani na Dante. Yanga hawakumuingeza mkataba Dante wakawa wanapigana danadana tu na hawakusema kama hatutokuongezea mkataba. Hivyo akajikuta mkataba umeisha na dirisha la usajili limeshafungwa.

Hili litatokea kwa Morrison, dirisha la usajili CAF limebakiza siku tisa tu lifungwe. Bila shaka mkataba wa Morrison unatamatika na sijui kama wamekaa mezani kwaajili ya kuongeza mkataba.

Kama haijafanyika hilo, maanake huenda Morrison akakosa timu ya kuchezea mashindano ya kimataifa.
 
Mchezaji hajaachwa inakuaje unamtakia heri ktika safari yake mpya ya soka?
Safari mpya baaada ya mkataba kuisha, maana yake Simba haina nia yaku-renew mkataba baada ya huu kuisha, so avumilie au club nyingine ilete offer mezani
 
MM KAMA SHABIKI SIHAFIKI KUKOMOANA. KAMA HANA MANUFAA UNAFANYA HIVYO ILI NINI? UKIMWACHIA SASA NA UKAMWACHIA WAKATI MKATABA UTAKAPOISHA TOFAUTI NI NN KATIKA CLUB?
 
Simba wangempa tu hiyo Reliase Latter.
Wangemsikiliza kama bado wanamtaka basi wa wangesema tu ili awe na amani.
Kama hawataki wamwachie tu kwani akija Yanga Simba itakosa nini?

Ngoja niombe kazi ya kuwa Mshauri wa Simba Sports.
 
Anayekomolewa hapa ni Morrison, nakumbuka kuna ishu ilitokea zamani kati ya Yanga nadhani na Dante. Yanga hawakumuingeza mkataba Dante wakawa wanapigana danadana tu na hawakusema kama hatutokuongezea mkataba. Hivyo akajikuta mkataba umeisha na dirisha la usajili limeshafungwa. Hili litatokea kwa Morrison, dirisha la usajili CAF limebakiza siku tisa tu lifungwe. Bila shaka mkataba wa Morrison unatamatika na sijui kama wamekaa mezani kwaajili ya kuongeza mkataba. Kama haijafanyika hilo, maanake huenda Morrison akakosa timu ya kuchezea mashindano ya kimataifa.
Kwani maingizo yenu mapya msimu uliopita mangapi yakihusika kwenye mpira wa kimataifa ?

Kama kweli Yanga inamtaka ni either imsajili sasa kwa kufuata taratibu au isubirie mkataba wake uishe imsajili.

Haya mengine ni kupiga kelele zisizo na maana kwasababu Simba Sc kama taasisi haina kosa lolote hapo kisheria.
 
Back
Top Bottom