Lipi ni sawa, kumfukuza kijana wako hapo kwako ili akaanze maisha yake au kumwacha azeekee hapo kwako?

Lipi ni sawa, kumfukuza kijana wako hapo kwako ili akaanze maisha yake au kumwacha azeekee hapo kwako?

Njia zote mbili ni sio sahihi,
,......njia sahihi ni KUMUANDAA mtoto mapema ili aweze kujitegemea, pia kumshika mkono na kuwa nae bega kwa bega anapoanza kujitegemea,...... kumfukuza ni kumuweka kwenye HATARI zaidi ya uwezo wake, kwani dunia imechafuka mno, na KUMUACHA tu nyumbani ni KUMDEKEZA na kumuweka katika hatari ya kushindwa kukabiriana vizuri na changamoto za dunia, pindi atakapokuwa peke yake,....
 
Kwa maisha magumu na heka heka za kutokua na kazi maalum niliopitia baada ya kufukuzwa ,na Mzee kwangu nitakua tofauti sana, mwanangu wa kiume akae tu home hata akipata na vitukuu hapa sawa
Maisha ya kujitegemea bila kua na msaada au support yeyote kwa ndg mabaya sana unaweza kujikuta kibaka bila kupenda

Napenda sana mfumo wanaoutumia baadhi ya kabila kama wairaq kwao mtoto wa kiume akifikisha umri wa kuoa anakatiwa ngombe za kutosha then anaenda kujitafuta
Mi pia mkuu,wanangu wawili wa kiume ntawapa banda langu moja waanzie maisha, mi mshua wangu alikuwa hitra kabisa,alitufukuza home tukiwa na twenty years tu
 
Home bana mambo hayakuwa mazuri kabisa ko sikufukuzwa wala kuandaliwa cho chote zaidi ya kujiongoza mwenyewe nikaondoka home.
Ila leo hii alhamdulilah mambo yako sawa.
Bora nimuandae kuliko nimtimue.
Ila kitu sitaki ni akae bila kufanya kazi na kaanza kunielewa kwa kujitunzia akiba ila kingine majukum lazima akutane nayo mapema.
 
Kwa jamii nyingi kijana akishapata umri basi anaonekana ameshakuwa mkubwa na hastahili tena kuwepo hapo kwako mzazi na mara ingine kama ataendelea kuwepo, basi atakereshwa almradi aondoke akaanze kujitegemea na s'tyms haya yanafanyika bila hata kujali kama mhusika ana ajira au la.

Wengi wanadai kumwondoa kijana kunaichangamsha akili yake kumfanya kijana ajitambue zaidi aache kujibweteka aongeze juhudi za kupambania maisha n.k.

Hii ni tofauti kwa jamii zingine hasa za kimwambao. Wao kijana hakui kwa mzazi. Mandhari mzazi yu hai basi mtoto atabaki kuwa mtoto tu, maisha yake yote. Huko kijana anaweza kuishi na wazazi hadi akapata wajukuu na pengine hata kuzeekea na hata kufia akiwa
hapohapo kwa wazazi.

Haya mambo wakuu yamekaaje?

Je, ungependa kumwona kijana wako katika taswira ipi kati ya izo mbili hapo juu?
Mpe basic za kumsaidia kuanza maisha km unacho otherwise angalia asijeenda uza madawa ya kulevya au wale wasioonekana
 
Kwamba mnajenga nyumba kubwa kwa tabu alafu baadae mnafukuza vijana? Hii hapana wakuu
😆😆Inategemea aisee. kuna mzee alikuwa na vijana kibao hapo kwake sasa wakawa hawaelewani basi hapo home ikawa mambo vululuvululu. madogo walikuwa na varangati muda wowote kinawaka. kila wakati nyumba ya moto. mzee akaona hawa wanantania akawafukuza wote.
 
Back
Top Bottom