Lipi ni sawa, kumfukuza kijana wako hapo kwako ili akaanze maisha yake au kumwacha azeekee hapo kwako?

Njia zote mbili ni sio sahihi,
,......njia sahihi ni KUMUANDAA mtoto mapema ili aweze kujitegemea, pia kumshika mkono na kuwa nae bega kwa bega anapoanza kujitegemea,...... kumfukuza ni kumuweka kwenye HATARI zaidi ya uwezo wake, kwani dunia imechafuka mno, na KUMUACHA tu nyumbani ni KUMDEKEZA na kumuweka katika hatari ya kushindwa kukabiriana vizuri na changamoto za dunia, pindi atakapokuwa peke yake,....
 
Mi pia mkuu,wanangu wawili wa kiume ntawapa banda langu moja waanzie maisha, mi mshua wangu alikuwa hitra kabisa,alitufukuza home tukiwa na twenty years tu
 
Home bana mambo hayakuwa mazuri kabisa ko sikufukuzwa wala kuandaliwa cho chote zaidi ya kujiongoza mwenyewe nikaondoka home.
Ila leo hii alhamdulilah mambo yako sawa.
Bora nimuandae kuliko nimtimue.
Ila kitu sitaki ni akae bila kufanya kazi na kaanza kunielewa kwa kujitunzia akiba ila kingine majukum lazima akutane nayo mapema.
 
Mpe basic za kumsaidia kuanza maisha km unacho otherwise angalia asijeenda uza madawa ya kulevya au wale wasioonekana
 
Kwamba mnajenga nyumba kubwa kwa tabu alafu baadae mnafukuza vijana? Hii hapana wakuu
😆😆Inategemea aisee. kuna mzee alikuwa na vijana kibao hapo kwake sasa wakawa hawaelewani basi hapo home ikawa mambo vululuvululu. madogo walikuwa na varangati muda wowote kinawaka. kila wakati nyumba ya moto. mzee akaona hawa wanantania akawafukuza wote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…