Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
MAHOJIANO YA LISSU NA VOICE OF AMERICA (VOA)

VOA: Nini kimetokea na uongozi wa sasa?

Lissu: Umekuwa madarakani kwa miaka 20 na muafaka tunatakiwa kufanya mabadiliko ya lazima ili tuweze kupeleka chama mbele.

VOA: Plani yako nini kama ukiwa M’kti, unapeleka chama vipi?

Lissu: Hapa tulipo, tupo kwenye mkwamo mkubwa wa kisiasa. Mabadiliko ambayo tumezungumza kwenye maridhiano na Rais Samia Suluhu Hassan kwa takribani miaka miwili, hakuna matunda yoyote. Njia ya kutoka hapa ni uongozi Mpya uje na uonyeshe na ukipeleke chama kwenye muelekeo tofauti. Kama maridhiano hayajafanya kazi, tuna nini mbadala?

Tunatakiwa tufanye mass mobilization (Nguvu Ya Umma) ili kukiongoza chama kwenye kuliamsha Taifa na kuunganisha nguvu na asasi za kiraia, vyama vya siasa, ili tuweze kuleta mabadiliko makubwa ya kidemokrasia ili tuweze kulazimisha mabadiliko.

VOA: Kwa hiyo, Tunaweza kusema kuna tofauti kati yako na M’kiti (Mbowe) Juu ya namna ya kukipeleka chama mbele?

Lissu: You are right on the money (Umepiga sehemu sahihi kabisa). Nadhani tuna tofauti ya kimsingi kabisa namna ya kukipeleka Chama mbele

VOA: Kumekuwa na mengi yanaendelea Kati ya serikali na chama chako, kuna wanachama wenu wamekuwa wanatekwa na hatujaona hatua kubwa kutoka kwenye chama chako

Lissu: Hiyo ndio hoja ya msingi kabisa. Hoja ni kuwa chama kinaonekana kime-paralyze (kipo nusu kaputi) kwa sababu M’kiti wa sasa haonekani kutaka kupambana na Samia.

M’kti Hataki kubomoa daraja na uongozi wa Samia. Viongozi wetu na wanaharakati wametekwa na wengine kuuwawa kwa namna za kikatili. Wanachama wetu, viongozi wetu wa Wilaya nao wametekwa na kupotezwa.

Yote haya yanatokeo ni wazi tumerudi kwenye zama za Giza za Magufuli. Na uongozi wa chama unaonekana kutokujua namna ya kutoka kwenye mkwamo huu. Kwa hiyo, nina gombea kwa sababu tunatakiwa kutoka kwenye huu mkwamo

VOA: Umesema No Reforms, No Election. Unaweza elezea hili?

Lissu: Tumekuwa na uchaguzi wa serikali za vijiji, vitongoji na mitaa kama wiki mbili au tatu zilizo pita. Ilikuwa ni MAJANGA! (total disaster!). Ulikuwa ni uchaguzi mbaya kuliko wa 2020 kwa minajili ya manipulation ya uchaguzi kwa kiwango cha kitaifa. Kama hili litakuwa kawaida kwenye chaguzi zetu, ni wazi kwetu kuwa hawapo (CCM) tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani. Kwa hiyo, kama hawapo tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani, kwa nini tushiriki chaguzi zijazo?

Kwa hiyo, tumeamua (CHADEMA) ili turudi kwenye uchaguzi, lazima tulazimishe mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Kwa hiyo, msimamo wetu ni: tupiganie mabadiliko, tukisha pata mabadiliko, tutakuwa tayari kushirki chaguzi. Tunasimama kwenye No reforms, No Election.

VOA: Pia, Unataka mabadiliko ndani ya CHADEMA pamoja na ukomo wa uongozi?

Lissu: Kabisa, Hatuwezi kupambana na udicteta wa Samia kama sisi ndani tupo tulivyo sasa. Kwa hiyo, lazima tusafishe nyumba yetu kwanza.

Lazima tusafishe matendo yetu kabla hatuja pambana na uongozi wa Samia. Kama hatuta jisafisha, itakatisha tamaa watu wetu na tutashindwa kupambana na tatizo kubwa ambalo limekuwa linatuathili la utawala wa Samia Suluhu Hassan

VOA: Mr. Lissu, thank you very much!

TunduALissu: Thank you for having me on your program.
Hii video/audio yake iko wapi mtandaoni?
 
..Tundu Lissu hakupinga Chadema kuingia ktk maridhiano.

..Kilichotokea ni Lissu kupinga danadana na ubabaishaji waliokuwa wakifanya Ccm wakati wa maridhiano.

..Maridhiano yalikuwa yanahusu mambo kama Tume Huru, Katiba Mpya, etc na imethibitika kwamba Ccm walikuwa wanawapotezea muda Chadema kupitia maridhiano, na ACt na wengine kupitia kikosi kazi.

..Kwa maoni yangu chama kinahitaji kujipanga upya, na kurudi kwa wananchi kwa ari kubwa zaidi.
Wanachotakiwa kufanya chadema kwanza kuaminika kwa umma na baada ya hapo kuuamsha
 
Wanachotakiwa kufanya chadema kwanza kuaminika kwa umma na baada ya hapo kuuamsha

..sasa ni nani wa kukipeleka chama kwa umma ili kiaminike, na umma uhamasike?

..Mbowe amefanya kazi kubwa, lakini nadhani sasa hivi amechoka.

..Hata hamasa ya kufanya shughuli za chama haonyeshi kuwa nayo.

..Na sisemi hivyo kwa kumlaumu Mbowe. Miaka 30 ya kufanya siasa za kiharakati ni lazima mhusika atachoka kiakili, na kimwili.
 
Busara imuongoze Mbowe ampishe Lissu!.
Ana mikakati thabiti ya kupambana na ma ccm, Mbowe toka apewe ule msamaha na Samia amekuwa hana tofauti na mtu aliyehongwa tuu...kawa mpoleee sn dhidi yake!.
Pia umri umesonga, woga umeingia
 
..sasa ni nani wa kukipeleka chama kwa umma ili kiaminike, na umma uhamasike?

..Mbowe amefanya kazi kubwa, lakini nadhani sasa hivi amechoka.

..Hata hamasa ya kufanya shughuli za chama haonyeshi kuwa nayo.

..Na sisemi hivyo kwa kumlaumu Mbowe. Miaka 30 ya kufanya siasa za kiharakati ni lazima mhusika atachoka kiakili, na kimwili.
Uko sahihi. Lakini,Lisuu asimlaumu! Lawama hazisaidii. Mbowe amewekwa mahabusu muda mrefu tuu kwa ajili ya Chama. Mmesahau mara hii. Nashauri Vikao vikae,Mbowe abaki kwenye Ulezi au cheo kingine. Bado Chama kinamhitaji.
 
Uko sahihi. Lakini,Lisuu asimlaumu! Lawama hazisaidii. Mbowe amewekwa mahabusu muda mrefu tuu kwa ajili ya Chama. Mmesahau mara hii. Nashauri Vikao vikae,Mbowe abaki kwenye Ulezi au cheo kingine. Bado Chama kinamhitaji.

..ukisikiliza majibu ya Lissu kutokana na maswali ya waandishi wa habari ametoa kauli za kumheshimu Mbowe.

..lakini unapogombea uongozi ktk hatua ya awali ni lazima kama mgombea ujitofautishe na mtangulizi / aliyeko ktk nafasi.
 
..ukisikiliza majibu ya Lissu kutokana na maswali ya waandishi wa habari ametoa kauli za kumheshimu Mbowe.

..lakini unapogombea uongozi ktk hatua ya awali ni lazima kama mgombea ujitofautishe na mtangulizi / aliyeko ktk nafasi.
Hakika.
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama na Bado unasema uongozi umekwama. Si wewe ni kiongozi mzito ndani ya Chama Tena unayetakiwa kumsaidia Mwenyekiti!!! Ebu tueleze ulichukua hatua gani kumsaidia Mwenyekiti na Mwenyekiti akakataa msaada wako? Au ulikuwa umenyamaza badala ya kumsaidia, ili aharibu nawe upate upenyo wa kumuangamiza kiuongozi?
Ebu fafanua!
Makamu mwenyekiti hana nguvu
 
..Tundu Lissu ametoa maelezo kwamba kilichokuwa masharti ya kufanyika kwa mazungumzo ya maridhiano, ndio kimegeuzwa na Ccm kwa udanganyifu kuwa mafanikio au matokeo ya maridhiano.


..katika maelezo yake Lissu anasema kabla ya mazungumzo Chadema waliweka masharti kwamba Mbowe aachiwe, mamia ya mahabusu wa Chadema waachiwe, Covid 19 waondolewe, mikutano ifunguliwe, na mengine. Baada ya hayo kufanyika ndipo CCM na Chadema walitakiwa kuanza kuzungumza kuhusu namna ya kubadili sheria, na mifumo, ili maovu na ukatili uliotokea hapo awali usijirudie.

..Kwa hiyo Lissu sio mpinga maridhiano, ila ni mpinga uongo na ulaghai wa CCM kuhusu maridhiano.

..Tofauti kati ya Lissu na Mbowe ni kwamba ilimchukua muda mrefu zaidi Mbowe kukata shauri kwamba CCM hawakuwa na nia njema katika maridhiano.


..Jambo lingine kwa maoni yangu naona Mbowe anakosea ni kutojitokeza kwa Watanzania na kueleza kwa bayana nini kilijitokeza mpaka kupelekea maridhiano kuvunjika.

..Kuna ombwe katika kuwahabarisha wananchi nini kimetokea katika maridhiano, what is the way forward.

..Jambo lingine ni kwamba pamoja na mikutano kufunguliwa lakini hazionekani jitihada za kutosha kwa Chadema kwenda kwa wananchi. Sijui kama viongozi wamechoka, kuna jambo lingine linasababisha hali hiyo.
Mbowe ni tapeli wa siasa za Tanzania
 
Hapana.
Kwa kukufahamu kwa michango yako humu JF, niseme tu kwamba, kwa heshima kubwa sikubaliani na wewe katika hili la Mbowe kuwa 'pragmatic'. Kuna zaidi ya 'pragmatism' inayo tawala akili zake baada ya hayo mazungumzo ya Maridhiano na mtu aliye mlaghai kwa uwazi kabisa na kumchota akili zake.
Tabia ya Mbowe na namna yake ya uongozi baada ya hayo mazungumzo ilibadilika kabisa na wala haijarudia tena kama ilivyo kuwa huko siku za nyuma.
Nasema hivyo kwa dalili mbali mbali alizo onyesha Mbowe mwenyewe.
Kwa mfano, mara yangu ya kwanza kabisa kumtilia mashaka Mbowe ni ile hotuba yake aliyo itoa na ikawekwa humu JF, wakati alipo tembelea huko ughaibuni na kuzungumza na wanao itwa diaspora. Maelezo yake kwenye hotuba ile yalionyesha kabisa kuwa yeye ni mtu wa Samia moja kwa moja na asinge penda watu waseme chochote kumhusu huyo mama. Hiyo hotuba itakuwa mahali, humu humu JF. Ikilazimu kuitafuta tutafanya hivyo.

Pili, kuna swala la COVID-19 Bungeni. Mbowe hata siku moja hajawahi kuwa muwazi jinsi hao mabinti walivyo ingia bungeni. Kama swala hili alisha litolea msimamo, basi inawezekana sikuupata. Hii ni aina ya uongozi usio tofautiana sana na huu tunao ushuhudia ndani ya CCM, siyo uongozi wa kuwa 'pragmatic.'.

Hata baada ya Samia kudhihirisha waziwazi jinsi alivyo mwacha kwenye mataa; wakati alipo amua wazi kuwa hakuna mabadiliko yoyote ya maana juu ya waliyo kuwa CHADEMA wakiyadai, e.g., Tume Huru ya Uchaguzi na Marekebisho ya sheria muhimu za kufanya chaguzi ziwe na maana, Mbowe hajasimama kama yule Mbowe alivyo kuwa kabla ya kuwekwa mfukoni na mama wa Kizimkazi. Kama kuna hotuba yoyote aliyo itoa Mbowe juu ya jambo hili, naomba unikumbushe; binafsi sijawahi kumsikia kinaga ubaga, kama ilivyo kuwa kawaida yake huko zamani.

Pamoja na kwamba Samia katumia njia za ulaghai na hadaa huko mwanzo wa utawala wake, ili aonekane kuwa ni tofauti na Magufuli; lakini matendo yake yote matokeo yake hayakutofautiana na aliyo kuwa akifanya Magufuli. Lengo limekuwa ni lile lile la kuidhoofisha CHADEMA
Lakini hata Samia mwenyewe alipoona arudie njia zile zile za Magufuli za kutesa na kuua wanachama na wapenzi wa CHADEMA, umemsikia au kumwona Mwenyekiti wa chama akisimama mbele kama zile siku za Magufuli? Hii 'pragmatism' imekuwa ni tatizo?

Mwisho mkuu 'Fundi Mchundo', kwa maoni yangu ni kama nina muelewa Mwenyekiti Mbowe katika mabadiliko yake haya ya uongozi chini ya serikali ya mama Samia Suluhu Hassan na CCM anayo iongoza. Nadhani 'pragmatism' unayo izungumzia wewe, chimbuko lako litakuwa hapa. Mwenyekiti Mbowe ni muumini mkubwa wa mtindo wa uchumi anao usimamia Samia Suluhu Hassan. Kwa upande huo sioni namna Mbowe anavyo weza kupingana na Samia. Yale mazungumzo ya mardhiano, bila shaka yalijikita zaidi kwenye maswala wanayo kubaliana upande huu na kukubaliana kuwa watakuwa upande mmoja. Na pengine, ni kweli Samia alikuwa amenuia kulegeza kidogo kwenye eneo la kuwasulubu CHADEMA, hadi ilipo bainika kuwa huko ndani ya CHADEMA kulikuwa na vichwa ngumu ambao Mbowe hakuonekana kuwa na uwezo wa kuwadhibiti. Na kwa upande wa Samia mwenyewe, lile kundi la Magufuli na wahafidhina wengine likawa linamzidi nguvu Samia mwenyewe na mipango yake na mwenzie wa CHADEMA. Sote tume shuhudia alivyo babaika huyu mama kwa teuzi na tenguzi zisizo na kikomo.
Bila shaka kukawa na mipango ya kuyaepuka makundi haya kwa pande zote mbili; kwamba CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe washirikiane wakati mahususi utakapo wadia ili waungane mithili ya yale tunayo yaona kila mara huko nchi jirani yakitokea wakati wa chaguzi zao.
Kwa hiyo, wakati sahihi ndio huu. Kwa CHADEMA, mnyukano ndio huo, kuelekea kwenye Mwenyekiti kuiwasilisha CHADEMA yake kwa Suluhu Hassan. Lisilo julikana bado, ni kama kwenye hili pia Mwenyekiti anaweza kuwa kaingizwa choo cha kike? Maana ule uchafuzi wa serikali za mitaa sioni kama Samia atamhitaji Mbowe kwa sababu yoyote ile.

Mwenyekiti Mbowe amekengeuka, na asipo stuka, CHADEMA ndiyo hivyo inaanza msambaratiko. Sioni jinsi Mbowe atakavyo weza tena kuisimamizsha na kuwa imara aking'ang'ania kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
Mbowe angekua na akili kidogo ilitakiwa apumzike bila kelele
 
Hapana.
Kwa kukufahamu kwa michango yako humu JF, niseme tu kwamba, kwa heshima kubwa sikubaliani na wewe katika hili la Mbowe kuwa 'pragmatic'. Kuna zaidi ya 'pragmatism' inayo tawala akili zake baada ya hayo mazungumzo ya Maridhiano na mtu aliye mlaghai kwa uwazi kabisa na kumchota akili zake.
Tabia ya Mbowe na namna yake ya uongozi baada ya hayo mazungumzo ilibadilika kabisa na wala haijarudia tena kama ilivyo kuwa huko siku za nyuma.
Nasema hivyo kwa dalili mbali mbali alizo onyesha Mbowe mwenyewe.
Kwa mfano, mara yangu ya kwanza kabisa kumtilia mashaka Mbowe ni ile hotuba yake aliyo itoa na ikawekwa humu JF, wakati alipo tembelea huko ughaibuni na kuzungumza na wanao itwa diaspora. Maelezo yake kwenye hotuba ile yalionyesha kabisa kuwa yeye ni mtu wa Samia moja kwa moja na asinge penda watu waseme chochote kumhusu huyo mama. Hiyo hotuba itakuwa mahali, humu humu JF. Ikilazimu kuitafuta tutafanya hivyo.

Pili, kuna swala la COVID-19 Bungeni. Mbowe hata siku moja hajawahi kuwa muwazi jinsi hao mabinti walivyo ingia bungeni. Kama swala hili alisha litolea msimamo, basi inawezekana sikuupata. Hii ni aina ya uongozi usio tofautiana sana na huu tunao ushuhudia ndani ya CCM, siyo uongozi wa kuwa 'pragmatic.'.

Hata baada ya Samia kudhihirisha waziwazi jinsi alivyo mwacha kwenye mataa; wakati alipo amua wazi kuwa hakuna mabadiliko yoyote ya maana juu ya waliyo kuwa CHADEMA wakiyadai, e.g., Tume Huru ya Uchaguzi na Marekebisho ya sheria muhimu za kufanya chaguzi ziwe na maana, Mbowe hajasimama kama yule Mbowe alivyo kuwa kabla ya kuwekwa mfukoni na mama wa Kizimkazi. Kama kuna hotuba yoyote aliyo itoa Mbowe juu ya jambo hili, naomba unikumbushe; binafsi sijawahi kumsikia kinaga ubaga, kama ilivyo kuwa kawaida yake huko zamani.

Pamoja na kwamba Samia katumia njia za ulaghai na hadaa huko mwanzo wa utawala wake, ili aonekane kuwa ni tofauti na Magufuli; lakini matendo yake yote matokeo yake hayakutofautiana na aliyo kuwa akifanya Magufuli. Lengo limekuwa ni lile lile la kuidhoofisha CHADEMA
Lakini hata Samia mwenyewe alipoona arudie njia zile zile za Magufuli za kutesa na kuua wanachama na wapenzi wa CHADEMA, umemsikia au kumwona Mwenyekiti wa chama akisimama mbele kama zile siku za Magufuli? Hii 'pragmatism' imekuwa ni tatizo?

Mwisho mkuu 'Fundi Mchundo', kwa maoni yangu ni kama nina muelewa Mwenyekiti Mbowe katika mabadiliko yake haya ya uongozi chini ya serikali ya mama Samia Suluhu Hassan na CCM anayo iongoza. Nadhani 'pragmatism' unayo izungumzia wewe, chimbuko lako litakuwa hapa. Mwenyekiti Mbowe ni muumini mkubwa wa mtindo wa uchumi anao usimamia Samia Suluhu Hassan. Kwa upande huo sioni namna Mbowe anavyo weza kupingana na Samia. Yale mazungumzo ya mardhiano, bila shaka yalijikita zaidi kwenye maswala wanayo kubaliana upande huu na kukubaliana kuwa watakuwa upande mmoja. Na pengine, ni kweli Samia alikuwa amenuia kulegeza kidogo kwenye eneo la kuwasulubu CHADEMA, hadi ilipo bainika kuwa huko ndani ya CHADEMA kulikuwa na vichwa ngumu ambao Mbowe hakuonekana kuwa na uwezo wa kuwadhibiti. Na kwa upande wa Samia mwenyewe, lile kundi la Magufuli na wahafidhina wengine likawa linamzidi nguvu Samia mwenyewe na mipango yake na mwenzie wa CHADEMA. Sote tume shuhudia alivyo babaika huyu mama kwa teuzi na tenguzi zisizo na kikomo.
Bila shaka kukawa na mipango ya kuyaepuka makundi haya kwa pande zote mbili; kwamba CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe washirikiane wakati mahususi utakapo wadia ili waungane mithili ya yale tunayo yaona kila mara huko nchi jirani yakitokea wakati wa chaguzi zao.
Kwa hiyo, wakati sahihi ndio huu. Kwa CHADEMA, mnyukano ndio huo, kuelekea kwenye Mwenyekiti kuiwasilisha CHADEMA yake kwa Suluhu Hassan. Lisilo julikana bado, ni kama kwenye hili pia Mwenyekiti anaweza kuwa kaingizwa choo cha kike? Maana ule uchafuzi wa serikali za mitaa sioni kama Samia atamhitaji Mbowe kwa sababu yoyote ile.

Mwenyekiti Mbowe amekengeuka, na asipo stuka, CHADEMA ndiyo hivyo inaanza msambaratiko. Sioni jinsi Mbowe atakavyo weza tena kuisimamizsha na kuwa imara aking'ang'ania kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
Asante sana Mkuu kwa kunijibu kwa heshima inavyotakiwa ingawa unatofautiana na mimi. Nashukuru sana kwa heshima uliyonipa. Na mimi nitakujibu kwa heshima abayo kwa kweli unastahili.
Mimi sikubaliani na wewe kwa sababu zifuazo:
1.Mtu pragmatic ni mtu strategic zaidi ya kuwa tactician. Ana uwezo wa kuangalia picha kubwa na kukubali kushindwa sehemu nyingine ili mradi anajua siku ya siku atafikia malengo yake.
2. Mbowe alikuwa na haki ya kukataa kuingia katika majadiliano na CCM kwa sababu ndio kwanza alikuwa ametoka lupango alipowekwa kwa miezi saba wakati kesi yake ya ugaidi ikisikilizwa. Kesi ambayo hukumu yake ni kifo na viongozi wa juu walituhakikishia kuwa kuna ushahidi wa kutosha wa kumkuta na hatia. Ni lazima alikuwa ana hasira na hakuwa na imani kuwa haki itatendeka kutokana na yaliyompata. Angeweza kususa, kukaa nyumbani na kuendeleza mpambano kwenye mitandao na barabarani. Lakini wote tunajua muitiko wetu watanzania bara linapokuja suala la kupambania haki yetu hasa wakati kulikuwa na zuio la mikutano ya aina yeyote. Au angeweza kuingia katika majadiliano ili zuio la mikutano liondolewe, wanachama na wafuasi wa CHADEMA walio ndani watolewe, waanze kupokea ruzuku ili mzigo wa kuendesha chama upunguzwe, viongozi wenzake waliokuwa nje ya nchi wahakikishiwe usalama wao pindi watakaporudi, viongozi ambao walinyimwa stahili zao walipwe. Na yote haya alifanikiwa. Angesusa ili ajipatie sifa za haraka haraka asingefanikiwa kitu. Kumsifia Samia wakati ule ilikuwa ni namna ya kumfanya asibadili mawazo maana ndani ya CCM hoja ya maridhiano ilikuwa inapingwa sana. Na pengine, alikuwa na matumaini kuwa Mheshimiwa Rais akipata ushirikiano atatambua kuwa hakuna haja ya siasa za kibabe.
2. Ulitaka aseme nini zaidi ya kuwafukuza katika chama hao Covid 19? Mnyika amesema wazi kuwa hakuna barua au fomu kutoka kwake iliyowapendekeza. Mimi nahisi wakina Halima waliwekewa presha kubwa ili kufikia uamuzi ule. Nahisi walimuambia Mbowe kuhusu hizo presha nae aka sympathize nao. Aidha, alitegemea kuwa angeweza kuwashauri wenzake wawe na huruma nao. Lakini alipopima joto na kuona kuwa huruma ya aina yeyote haina nafasi hakusita kuunga mkono msimamo wa wengi na kuwatimua. Hiyo ndio pragmatism. Hapo hapo hajaficha kuwa bado ana ukaribu na wakina Halima kibinadamu. Ndio maana aliwaalika wazi wazi kwenye shughuli za kuchangia kanisa lake kijijini kwao. Alifanya hivyo kama Mbowe na sio kama Mwenyekiti Mbowe.
3. CCM isigeweza kukubali kwa namna yeyote kuwatoa wakina Halima bungeni maana legitimacy ya Bunge ingepotea. Ingekuwa ni ku commit suicide baada ya kufanya juhudi za ziada kuwaingiza Bunge. Si Lissu au mtu mwingine angeweza kubadili ukweli huu. Mbowe alitambua hili.
4. Mbowe ni Mwenyekiti wa CDM na msimamo wa CDM kuhusu Katiba Mpya, Tume Huru ya Uchaguzi umewekwa wazi na Mbowe na viongozi wenzake. Viongozi wote wa CDM ( akiwemo Lissu) wana wajibu wa kuyazungumzia masuala haya na wamefanya hivyo. Chadema na taasisi zake zimeandaa mafunzo na makongamano kwa wanachama wao kila mahali. Sijui wangeweza kufanya nini zaidi ili wawaridhishe. Kwa kusema kweli hoja ya kuwa Mbowe amenunuliwa haina mashiko maana tunaona jinsi yeye na wenzake wanavyoendelea kusumbuliwa. Kama hiyo ni kweli basi ina maana Mbowe haumizwi na yaliyowapata wanachama wenzake waliopotea na kuuawa? Kwenye hilo hamumtendei haki.
5. Wakati Msigwa ameanzisha vita ya kumbomoa Mbowe Lissu alikaa kimya. Hata pale watu waliposema kuwa Lissu ndie anayempa kiburi Msigwa alikaa kimya. Wakati wa uchaguzi wa ndani wa CDM, Lissu akatoa shutuma za uwepo wa pesa chafu ndani ya CHADEMA zenye lengo la kuwanyima fursa watu makini wenye moyo wa kupigania haki za wananchi. Wengi tulihisi kuwa alikuwa anamzungumzia Msigwa. Na kweli Msigwa akapigwa stop. Matokeo yake kakimbilia CCM ambako kajipa cheo cha jemadari wa mapambano dhidi ya Mbowe na Chadema. Sijamsikia Lissu akisema lolote kuhusu mambo anayofanya Msigwa. Tofauti kabisa na anavyokuwa mkali kwenye suala la Covid 19 ambao toka wafukuzwe hawajawahi kutoa matamko yeyote kubeza chama chao cha awali. Hii ni moja ya sababu zinazonifanya nimtilie shaka Lissu. Naona kama sifa zimemuingia kichwani na kujiona kama Mussa wa wayahudi.
Naona niishie hapa. Asante tena kwa kuibua hoja kiungwana.

Amandla...
 
Back
Top Bottom