Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
MAHOJIANO YA LISSU NA VOICE OF AMERICA (VOA)

VOA: Nini kimetokea na uongozi wa sasa?

Lissu: Umekuwa madarakani kwa miaka 20 na muafaka tunatakiwa kufanya mabadiliko ya lazima ili tuweze kupeleka chama mbele.

VOA: Plani yako nini kama ukiwa M’kti, unapeleka chama vipi?

Lissu: Hapa tulipo, tupo kwenye mkwamo mkubwa wa kisiasa. Mabadiliko ambayo tumezungumza kwenye maridhiano na Rais Samia Suluhu Hassan kwa takribani miaka miwili, hakuna matunda yoyote. Njia ya kutoka hapa ni uongozi Mpya uje na uonyeshe na ukipeleke chama kwenye muelekeo tofauti. Kama maridhiano hayajafanya kazi, tuna nini mbadala?

Tunatakiwa tufanye mass mobilization (Nguvu Ya Umma) ili kukiongoza chama kwenye kuliamsha Taifa na kuunganisha nguvu na asasi za kiraia, vyama vya siasa, ili tuweze kuleta mabadiliko makubwa ya kidemokrasia ili tuweze kulazimisha mabadiliko.

VOA: Kwa hiyo, Tunaweza kusema kuna tofauti kati yako na M’kiti (Mbowe) Juu ya namna ya kukipeleka chama mbele?

Lissu: You are right on the money (Umepiga sehemu sahihi kabisa). Nadhani tuna tofauti ya kimsingi kabisa namna ya kukipeleka Chama mbele

VOA: Kumekuwa na mengi yanaendelea Kati ya serikali na chama chako, kuna wanachama wenu wamekuwa wanatekwa na hatujaona hatua kubwa kutoka kwenye chama chako

Lissu: Hiyo ndio hoja ya msingi kabisa. Hoja ni kuwa chama kinaonekana kime-paralyze (kipo nusu kaputi) kwa sababu M’kiti wa sasa haonekani kutaka kupambana na Samia.

M’kti Hataki kubomoa daraja na uongozi wa Samia. Viongozi wetu na wanaharakati wametekwa na wengine kuuwawa kwa namna za kikatili. Wanachama wetu, viongozi wetu wa Wilaya nao wametekwa na kupotezwa.

Yote haya yanatokeo ni wazi tumerudi kwenye zama za Giza za Magufuli. Na uongozi wa chama unaonekana kutokujua namna ya kutoka kwenye mkwamo huu. Kwa hiyo, nina gombea kwa sababu tunatakiwa kutoka kwenye huu mkwamo

VOA: Umesema No Reforms, No Election. Unaweza elezea hili?

Lissu: Tumekuwa na uchaguzi wa serikali za vijiji, vitongoji na mitaa kama wiki mbili au tatu zilizo pita. Ilikuwa ni MAJANGA! (total disaster!). Ulikuwa ni uchaguzi mbaya kuliko wa 2020 kwa minajili ya manipulation ya uchaguzi kwa kiwango cha kitaifa. Kama hili litakuwa kawaida kwenye chaguzi zetu, ni wazi kwetu kuwa hawapo (CCM) tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani. Kwa hiyo, kama hawapo tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani, kwa nini tushiriki chaguzi zijazo?

Kwa hiyo, tumeamua (CHADEMA) ili turudi kwenye uchaguzi, lazima tulazimishe mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Kwa hiyo, msimamo wetu ni: tupiganie mabadiliko, tukisha pata mabadiliko, tutakuwa tayari kushirki chaguzi. Tunasimama kwenye No reforms, No Election.

VOA: Pia, Unataka mabadiliko ndani ya CHADEMA pamoja na ukomo wa uongozi?

Lissu: Kabisa, Hatuwezi kupambana na udicteta wa Samia kama sisi ndani tupo tulivyo sasa. Kwa hiyo, lazima tusafishe nyumba yetu kwanza.

Lazima tusafishe matendo yetu kabla hatuja pambana na uongozi wa Samia. Kama hatuta jisafisha, itakatisha tamaa watu wetu na tutashindwa kupambana na tatizo kubwa ambalo limekuwa linatuathili la utawala wa Samia Suluhu Hassan

VOA: Mr. Lissu, thank you very much!

TunduALissu: Thank you for having me on your program.
Mabadiriko ni muhimu sana, vinginevyo tutakuwa kama nyani tu, alivyoishi babu hata kitukuu kinaishi kama babu. Kama dunia inabadilika lazima watu, mifumo, tabia , taratibu na mbinu zibadirike ili kufikia malengo kulingana na mshindani wako
 
MAHOJIANO YA LISSU NA VOICE OF AMERICA (VOA)

VOA: Nini kimetokea na uongozi wa sasa?

Lissu: Umekuwa madarakani kwa miaka 20 na muafaka tunatakiwa kufanya mabadiliko ya lazima ili tuweze kupeleka chama mbele.

VOA: Plani yako nini kama ukiwa M’kti, unapeleka chama vipi?

Lissu: Hapa tulipo, tupo kwenye mkwamo mkubwa wa kisiasa. Mabadiliko ambayo tumezungumza kwenye maridhiano na Rais Samia Suluhu Hassan kwa takribani miaka miwili, hakuna matunda yoyote. Njia ya kutoka hapa ni uongozi Mpya uje na uonyeshe na ukipeleke chama kwenye muelekeo tofauti. Kama maridhiano hayajafanya kazi, tuna nini mbadala?

Tunatakiwa tufanye mass mobilization (Nguvu Ya Umma) ili kukiongoza chama kwenye kuliamsha Taifa na kuunganisha nguvu na asasi za kiraia, vyama vya siasa, ili tuweze kuleta mabadiliko makubwa ya kidemokrasia ili tuweze kulazimisha mabadiliko.

VOA: Kwa hiyo, Tunaweza kusema kuna tofauti kati yako na M’kiti (Mbowe) Juu ya namna ya kukipeleka chama mbele?

Lissu: You are right on the money (Umepiga sehemu sahihi kabisa). Nadhani tuna tofauti ya kimsingi kabisa namna ya kukipeleka Chama mbele

VOA: Kumekuwa na mengi yanaendelea Kati ya serikali na chama chako, kuna wanachama wenu wamekuwa wanatekwa na hatujaona hatua kubwa kutoka kwenye chama chako

Lissu: Hiyo ndio hoja ya msingi kabisa. Hoja ni kuwa chama kinaonekana kime-paralyze (kipo nusu kaputi) kwa sababu M’kiti wa sasa haonekani kutaka kupambana na Samia.

M’kti Hataki kubomoa daraja na uongozi wa Samia. Viongozi wetu na wanaharakati wametekwa na wengine kuuwawa kwa namna za kikatili. Wanachama wetu, viongozi wetu wa Wilaya nao wametekwa na kupotezwa.

Yote haya yanatokeo ni wazi tumerudi kwenye zama za Giza za Magufuli. Na uongozi wa chama unaonekana kutokujua namna ya kutoka kwenye mkwamo huu. Kwa hiyo, nina gombea kwa sababu tunatakiwa kutoka kwenye huu mkwamo

VOA: Umesema No Reforms, No Election. Unaweza elezea hili?

Lissu: Tumekuwa na uchaguzi wa serikali za vijiji, vitongoji na mitaa kama wiki mbili au tatu zilizo pita. Ilikuwa ni MAJANGA! (total disaster!). Ulikuwa ni uchaguzi mbaya kuliko wa 2020 kwa minajili ya manipulation ya uchaguzi kwa kiwango cha kitaifa. Kama hili litakuwa kawaida kwenye chaguzi zetu, ni wazi kwetu kuwa hawapo (CCM) tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani. Kwa hiyo, kama hawapo tayari kuwa na uchaguzi wa ushindani, kwa nini tushiriki chaguzi zijazo?

Kwa hiyo, tumeamua (CHADEMA) ili turudi kwenye uchaguzi, lazima tulazimishe mabadiliko ya mfumo wa uchaguzi.

Kwa hiyo, msimamo wetu ni: tupiganie mabadiliko, tukisha pata mabadiliko, tutakuwa tayari kushirki chaguzi. Tunasimama kwenye No reforms, No Election.

VOA: Pia, Unataka mabadiliko ndani ya CHADEMA pamoja na ukomo wa uongozi?

Lissu: Kabisa, Hatuwezi kupambana na udicteta wa Samia kama sisi ndani tupo tulivyo sasa. Kwa hiyo, lazima tusafishe nyumba yetu kwanza.

Lazima tusafishe matendo yetu kabla hatuja pambana na uongozi wa Samia. Kama hatuta jisafisha, itakatisha tamaa watu wetu na tutashindwa kupambana na tatizo kubwa ambalo limekuwa linatuathili la utawala wa Samia Suluhu Hassan

VOA: Mr. Lissu, thank you very much!

TunduALissu: Thank you for having me on your program.
Nimesikiliza hayo mahojiano ila sikusikia chadema ipo nusu kaputi.
Maybe i overlooked.
#CRITICAL THINKER.
 
Muulize lissu anackuwa controlled na msigwa QUOTE="CHIEF PRIEST, post: 52249981, member: 658193"]
Wewe jamaa ni mpuuzi huyu Msigwa labda ni basha wako unamsifia sana atakuwa anakupiga mashine.
[/QUOTE]
 
Lissu ndiye mwenyekiti wa CHADEMA ajaye, tumechoka kuongozwa na kilaza.
 
Siungi mkono mbowe kuendelea na uenyekiti lakini naona pia hatari kubwa ya Lisu kuwa mwenyekiti.
 
Lissu na machine kubwa ,angekuwa ni mwanachama mwingine nadhani Mzee Mbowe angekuwa ameshachuka hatua za kumfukuza kwenye hii kampuni yake.Hakika mzee Mbowe kayakanyaga,
🤪🤪🤪🤪😂😂😂😂😂😂🤪🤪
 
..Tundu Lissu hakupinga Chadema kuingia ktk maridhiano.

..Kilichotokea ni Lissu kupinga danadana na ubabaishaji waliokuwa wakifanya Ccm wakati wa maridhiano.

..Maridhiano yalikuwa yanahusu mambo kama Tume Huru, Katiba Mpya, etc na imethibitika kwamba Ccm walikuwa wanawapotezea muda Chadema kupitia maridhiano, na ACt na wengine kupitia kikosi kazi.

..Kwa maoni yangu chama kinahitaji kujipanga upya, na kurudi kwa wananchi kwa ari kubwa zaidi.
Yote ni sawa. Ninachopinga ni "the way he went about it". Alichokifanya ni badala ya kuonyesha tatizo lilikuwa CCM amemgeuza Mbowe kuwa ni tatizo. Sasa hivi kelele ni Mbowe must go sio CCM must go. Ukimya wake kwenye suala hili kunaashiria anakubalia hizo kelele.

Wakati John McCain alikuwa anagombea urais alijizolea sifa alipomzima shabiki wake aliyekuwa anamsemea ovyo Obama. Lissu anatakiwa kuweka wazi kuwa tofauti yake na Mbowe ni approach na sio personal. Kama bado anamheshimu Mbowe angeliweka hili wazi. Lakini kama hamheshimu na anamuona ni mwizi n.k. aende full blast kama walivyofanya wakina Lijualikali, Msigwa n.k. Ni vigumu kuamini kuwa hakuhusika katika fujo alizokuwa akizifanya Msigwa kabla ya kuondoka.

Labda anayofanya sasa hivi ni pre emptive ili ikiwekwa wazi uhusika wake katika kumchimba Mbowe ionekane anafanyiwa hivyo kwa sababu amediriki kuona sumu.

Kwangu mimi baada ya Slaa, Halima na Msigwa hamna kitakacho nishangaza.

Amandla...
 
Mbowe ni pragmatic. Kabla ya mazungumzo ya maridhiano ( ambayo inaelekea Lissu aliyapinga) kulikuwa na zuio la mikutano ya hadhara. Kulikuwa na mamia ya wanachama na wafuasi wa CDM waliokuwa ndani ambapo wengine walikuwa mpaka na kesi za mauaji. Mazungumzo hayo ndio yaliyopelekea zuio la mikutano ya hadhara kuondolewa na wengi waliokuwa ndani kesi zao kufutwa na wengi waliokuwa wameenda uhamishoni kurudi. Hayo sio mafanikio madogo. Sidhani kama yangepatikana njia mbadala aliyoitaka Lissu.
Lakini pamoja na mafanikio hayo Mbowe ametangaza wazi kuwa hana imani kuwa CCM wana nia nzuri na maridhiano. Huo umekuwa ndio msimamo wa chama chake na ndio maana hayo mazungumzo hayajaendelea. Kudai kuwa imani yake ya maridhiano ni kikwazo kwa Lissu ni uongo.

Amandla...
Hapana.
Kwa kukufahamu kwa michango yako humu JF, niseme tu kwamba, kwa heshima kubwa sikubaliani na wewe katika hili la Mbowe kuwa 'pragmatic'. Kuna zaidi ya 'pragmatism' inayo tawala akili zake baada ya hayo mazungumzo ya Maridhiano na mtu aliye mlaghai kwa uwazi kabisa na kumchota akili zake.
Tabia ya Mbowe na namna yake ya uongozi baada ya hayo mazungumzo ilibadilika kabisa na wala haijarudia tena kama ilivyo kuwa huko siku za nyuma.
Nasema hivyo kwa dalili mbali mbali alizo onyesha Mbowe mwenyewe.
Kwa mfano, mara yangu ya kwanza kabisa kumtilia mashaka Mbowe ni ile hotuba yake aliyo itoa na ikawekwa humu JF, wakati alipo tembelea huko ughaibuni na kuzungumza na wanao itwa diaspora. Maelezo yake kwenye hotuba ile yalionyesha kabisa kuwa yeye ni mtu wa Samia moja kwa moja na asinge penda watu waseme chochote kumhusu huyo mama. Hiyo hotuba itakuwa mahali, humu humu JF. Ikilazimu kuitafuta tutafanya hivyo.

Pili, kuna swala la COVID-19 Bungeni. Mbowe hata siku moja hajawahi kuwa muwazi jinsi hao mabinti walivyo ingia bungeni. Kama swala hili alisha litolea msimamo, basi inawezekana sikuupata. Hii ni aina ya uongozi usio tofautiana sana na huu tunao ushuhudia ndani ya CCM, siyo uongozi wa kuwa 'pragmatic.'.

Hata baada ya Samia kudhihirisha waziwazi jinsi alivyo mwacha kwenye mataa; wakati alipo amua wazi kuwa hakuna mabadiliko yoyote ya maana juu ya waliyo kuwa CHADEMA wakiyadai, e.g., Tume Huru ya Uchaguzi na Marekebisho ya sheria muhimu za kufanya chaguzi ziwe na maana, Mbowe hajasimama kama yule Mbowe alivyo kuwa kabla ya kuwekwa mfukoni na mama wa Kizimkazi. Kama kuna hotuba yoyote aliyo itoa Mbowe juu ya jambo hili, naomba unikumbushe; binafsi sijawahi kumsikia kinaga ubaga, kama ilivyo kuwa kawaida yake huko zamani.

Pamoja na kwamba Samia katumia njia za ulaghai na hadaa huko mwanzo wa utawala wake, ili aonekane kuwa ni tofauti na Magufuli; lakini matendo yake yote matokeo yake hayakutofautiana na aliyo kuwa akifanya Magufuli. Lengo limekuwa ni lile lile la kuidhoofisha CHADEMA
Lakini hata Samia mwenyewe alipoona arudie njia zile zile za Magufuli za kutesa na kuua wanachama na wapenzi wa CHADEMA, umemsikia au kumwona Mwenyekiti wa chama akisimama mbele kama zile siku za Magufuli? Hii 'pragmatism' imekuwa ni tatizo?

Mwisho mkuu 'Fundi Mchundo', kwa maoni yangu ni kama nina muelewa Mwenyekiti Mbowe katika mabadiliko yake haya ya uongozi chini ya serikali ya mama Samia Suluhu Hassan na CCM anayo iongoza. Nadhani 'pragmatism' unayo izungumzia wewe, chimbuko lako litakuwa hapa. Mwenyekiti Mbowe ni muumini mkubwa wa mtindo wa uchumi anao usimamia Samia Suluhu Hassan. Kwa upande huo sioni namna Mbowe anavyo weza kupingana na Samia. Yale mazungumzo ya mardhiano, bila shaka yalijikita zaidi kwenye maswala wanayo kubaliana upande huu na kukubaliana kuwa watakuwa upande mmoja. Na pengine, ni kweli Samia alikuwa amenuia kulegeza kidogo kwenye eneo la kuwasulubu CHADEMA, hadi ilipo bainika kuwa huko ndani ya CHADEMA kulikuwa na vichwa ngumu ambao Mbowe hakuonekana kuwa na uwezo wa kuwadhibiti. Na kwa upande wa Samia mwenyewe, lile kundi la Magufuli na wahafidhina wengine likawa linamzidi nguvu Samia mwenyewe na mipango yake na mwenzie wa CHADEMA. Sote tume shuhudia alivyo babaika huyu mama kwa teuzi na tenguzi zisizo na kikomo.
Bila shaka kukawa na mipango ya kuyaepuka makundi haya kwa pande zote mbili; kwamba CCM ya Samia na CHADEMA ya Mbowe washirikiane wakati mahususi utakapo wadia ili waungane mithili ya yale tunayo yaona kila mara huko nchi jirani yakitokea wakati wa chaguzi zao.
Kwa hiyo, wakati sahihi ndio huu. Kwa CHADEMA, mnyukano ndio huo, kuelekea kwenye Mwenyekiti kuiwasilisha CHADEMA yake kwa Suluhu Hassan. Lisilo julikana bado, ni kama kwenye hili pia Mwenyekiti anaweza kuwa kaingizwa choo cha kike? Maana ule uchafuzi wa serikali za mitaa sioni kama Samia atamhitaji Mbowe kwa sababu yoyote ile.

Mwenyekiti Mbowe amekengeuka, na asipo stuka, CHADEMA ndiyo hivyo inaanza msambaratiko. Sioni jinsi Mbowe atakavyo weza tena kuisimamizsha na kuwa imara aking'ang'ania kuwa Mwenyekiti wa chama hicho.
 
Na hapa ndipo tatizo linapoanzia. Chadema wameiga mambo mengi sana ya ccm, na hivyo kukifanya chama hiki kisiwe na tofauti kubwa sana na ccm kiutendaji na mwenendo wake.
Kuna mazuri ya kuiga, toka huko CCM, lakini naona CHADEMA hawayafanyi hayo. Kwa mfano Namna CCM ilivyo jiimarisha hadi huko mitaani kwenyewe. Muundo huu wange utilia nguvu CHADEMA; hata hiyo Dola inayo tegemewa na CCM kuwabakisha madarakani isinge mudu kudhibiti nguvu za wananchi nchi nzima.
 
Back
Top Bottom