Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Pre GE2025 Lissu: CHADEMA ipo nusu kaputi, Mbowe hataki kupambana na Samia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kinachonisikitisha kuhusu suala lote hili ni kuwa "it is so unnecessary". CDM walikuwa katika sehemu nzuri ya kuingia katika hiyo hatua anayoizungumzia Lissu. Sasa hivi watu wamebaki wakishughulukiana na kumuacha yule anayewasababishia maumivu yote waliyonayo. Na kwa huzuni kubwa naweza kusema kuwa aliyesababisha yote haya ni Lissu na sio mwingine.

Amandla...
Haahaa kasababisha yepi mkuu shujaa wa mtandao I?😂
 
Hili mtaruka mtatua lkn lipo wazi ya kwamba lissu anaendeshwa kama drone ktk swala hili na rafiki yake kipenzi msigwa wa ccm
Haahaa kama ni fact acha tu aendeshwe, lakini lissu ndo mpango mzima kwa sasa chadema
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama na Bado unasema uongozi umekwama. Si wewe ni kiongozi mzito ndani ya Chama Tena unayetakiwa kumsaidia Mwenyekiti!!! Ebu tueleze ulichukua hatua gani kumsaidia Mwenyekiti na Mwenyekiti akakataa msaada wako? Au ulikuwa umenyamaza badala ya kumsaidia, ili aharibu nawe upate upenyo wa kumuangamiza kiuongozi?

Ebu fafanua!
Hivi unajua maana ya makamu?😂😂😂
 
Sawa tuseme kuwa Lissu ndio aliyotaka lakini hayakutokea. Kwa mtazamo wangu ni kuwa hakuwa pragmatic. Unapoingia katika maadiliano hauwezi kung'ang'ania kupata kila kitu unachotaka. Mtu yeyote anajua kuwa hamna namna CCM watakubali Covid 19 waondolewe maana wao ndio wanalipa legitimacy Bunge lao. Bila wao hakuna upinzani, na bila upinzani kamati nyingi za Bunge zisingeweza kuundwa. Hicho ni kilima ambacho CCM wlikuwa wako tayari kufia. Sasa kama katika matakwa yao yote, ni hilo tu ndio halijafanikiwa sioni sababu ya kumtuhumu Mbowe kuwa njia yake ilishindwa.

Mbowe kwa kukubali kuingia katika majadiliano, aliwapa CCM kmba ya kujinyongea. Sasa hivi CCM haiwezi kuituhumu CDM kuwa ni chama cha vurugu na hakiko tayari kukaa mezani kwa majadiliano. Hatua ya Mowe ndio imeupa uhalali hatua anayozungumzia Lissu kufuata.

Sijui ni mimi tu lakini nimemsikia Mbowe akisema kuwa CCM haikuonyesha utayari kuhusu suala la Covid 19, Katiba Mpya na Tume ya Uchaguzi. Kujitoa kwa CDM katika tume na kamati zilizoanzishwa kama sehemu ya mchakato wa vitu hivi ni ishara tosha kuwa wanataka mabadiliko ya dhati na si ya kiini macho.

Mimi nisichoelewa ni way forward ipi amayo CDM inatakiwa kuonyesha. Kama wananchi wanajifungia ndani wakiona askari wanafanya mazoezi au usafi hamna litakalo fanikiwa. Mimi sidhani kama Mbowe anapinga watu kuchukua hatua kali zaidi. Ndio maana Bavicha walipotaka kulianzisha Mbeya na wakakamatwa hakusita kwenda kusimama nao.

Inawezekana Lissu ana point lakini hatua na maneno yanaharibu kuliko kujenga. Kwangu mimi anaonyesha dalili za unafik unafik ambao sio mzuri. Karibu yote anayoyasema ni furaha kwa CCM ambao naamini wanamuogopa zaidi Mbowe kuliko Lissu. Sio bure kumsikia Steve Mengele akimpongeza Lissu. Sio bure kusikia watu wakidai kuwa Msigwa ndie anayembeba Lissu. Sio bure kusikia tetesi kuwa mwisho wa safari yake ni kujiunga na CCM. Aidha, sio bure kusikia tuhuma kuhusu ubadhirifu wa Mbowe zikija kwa kasi. Ni Lissu ndio anayapa oxygen haya yote.

Lissu ana nguvu sana ya ushawishi lakini kwenye hili amekurupuka. Nahisi ameanza kuamini kuwa yeye ni zaidi ya chama na viongozi wenzake. Mawazo kama hayo hayana afya kwa chama chake maana apende asipende kuna wengi wamepitia mengi na Mbowe na wana imani kubwa nae. Matendo na maneno yake yana wa alienate hao watu.

Timu ya Mbowe na Lissu ni formidable na CCM wanajua hilo. Bahati mbaya inaelekea Lissu haoni hilo na anaamini yeye ndie Stelin peke yake.

Amandla...


..Tundu Lissu hakupinga Chadema kuingia ktk maridhiano.

..Kilichotokea ni Lissu kupinga danadana na ubabaishaji waliokuwa wakifanya Ccm wakati wa maridhiano.

..Maridhiano yalikuwa yanahusu mambo kama Tume Huru, Katiba Mpya, etc na imethibitika kwamba Ccm walikuwa wanawapotezea muda Chadema kupitia maridhiano, na ACt na wengine kupitia kikosi kazi.

..Kwa maoni yangu chama kinahitaji kujipanga upya, na kurudi kwa wananchi kwa ari kubwa zaidi.
 
Kwamba Lissu anashikiwa akili na msigwa?
Unajua Mbowe anapewa support na dola ya kupambana na Lissu? Tulia uione show ya lissu
Kwenye sakata hili Mbowe anasapoti kutoka ikulu.. huyu sio kiongozi bali ni mpiga dili tu.
 
Lakini Wakuu hii Strategy ya "NO REFORMS NO ELECTIONS" yale Mafisiemu si yanashangilia?!

Mnaonaje Jemadari Lissu atufafanulie zaidi maana Uchaguzi ujao mimi nataka uwe Jino kwa Jino wakituibia tunaingia Mabarabarani.
Mwisho wako ni key board kamwe huwezi kuingia barabarani.
 
Nilipofika kwenye mass mobilisation nimeacha kusoma. Upinzani hasa Chadema wana kazi ya zaida ya kufanya ili kuitoa ccm madarakani. Ni vipi chama kitafanya mass mobilisation wakati tangu wameruhisiwa kufanya mikutano wameshindwa kuekeza sera zao kama chama badala yake wamekuwa wakiikosoa serekali tena kwa kejeli na kurukia rukia mambo. Karen hii ya 21 chama cha siasa kinafanya siasa kama za enzi za kudai uhuru, . Chadema ili ijikwamue hapo ilipo inataka viongozi wataoweza kuzungumzia sera zaidi kuliko mambo yao binafsi , watu wanahitaji kumuona kiongozi atakayeweza kuwasemea zaidi kuliko kiongozi anayepata nafasi na kuzungumzia mambo yake binafsi na kueneza chuki dhidi ya watu wengine.

Watanzania kwa asili ni watu wasiopenda fujo, na kama kuna kiongozi yeyote atataka kutumia njia hii atafeli mapema sana, nakumbuka Chadema ya Dr. Slaa na kina Zito Kabwe ilikuwa ni Chadema ya hoja zenye mashiko kwa taifa na ndio maana watu walikipenda sana chama walio wanachama na wasio wanachama viongozi wale walikuwa wakizungumzia mambo ya kitaifa zaidi na sio mambo binafsi, leo hii sioni mtu wa karba ya Dr. Slaa na Zito Kabwe ndani ya Chadema. Wasipoangalia kwa makini ACT atakwenda kunyakua nafasi yao. Tuwe wa kweli kwa hali ilivyo sasa Chadema ni vigumu mzaleondo kutoka chama kingine akajiunga nao, kutokana na wao kwa sasa hawana sera shawishi.
 
Back
Top Bottom