Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki


Unapaswa kuwa na Ubongo was maiti ili umuamini lisu kichaa

USSR
 
Kwamba afe muda wote na pesa ziwepo tu zimekaa. Hivi anaijua billioni 100 huyo?
 
Imekuwa tabia ya baadhi ya watawala wa Afrika. Wa Malawi naye ilikuwa hivyo hivyo.

Ni jambo lililosikika sana, kuwa mara tu baada ya kifo, waliokuwa wanafanya kazi ya kupeleka pesa, ndio walioenda kuvunja nyumba na kuzikomba zote. Waluzipeleka wapi, hata hatujui. Na hao walifurahia sana kifo cha Magufuli maana kwao ilikuwa ndio mwanzo wa utajiri mkubwa.

Mungu, ukuu wake ni wa ajabu sana. Historia inaonesha watawala waliojilimbikizia utajiri mkubwa, na mara nyingi siyo kutokana na mapato halali, hawakupata nafasi ya kuutumia.

Tanzania ya Nyerere, ya viongozi waliotosheka, imepotea.

Kama wana wa Mungu, tunachotakiwa kufanya ni kumwombea msamaha kwa Mungu. Mema yake yakawe sababu ya yeye kuupokea msamaha wa Mungu. Kama Yesu aliwasamehe na kuwaombea msamaha wauaji wake (Baba uwasamehe kwa kuwa hawajui watendalo) basi nasi twastahili kuiga mafundisho yake kwa vitendo. Lakini waliozichukua hizo pesa wanastahili kuzirejesha hazina, la sivyo, laana ijuu ya vichwa vyao.
 
Kwani alishafanya biashara hii msikitini,ahaaaaa

Nimeipenda hii sentensi
 
Ulitakiwa uwe ulishatiwa Kitanzi umekunya kabisa
 
Lissu hajui siasa ni mchafuzi nafiki lengo lake kutaka Chadema isikubalike Geita

Kwa nini anajua mwenyewe

GEITA Magufuli ni household name Kawapelekea maendeleo vitu kibao hata umwite mwizi hawakuelewi. Nilikuwa kule wakasema hata waseme mwizi aliiba atujengee hospitali nzuri,uwanja wa ndege, mbuga, Crdb nk na pia yule kabila yetu.

Kuna watu wakabila kama wasukuma, wachaga, wanyakyusa na wahaya? Lissu kachemka msukuma huwezi mtukana Msukuma mwenzie hadharani akakubali huo ujinga hata kama unayemtukana alikosea kweli huuliza kwa nini aje atutukanie Msukuma mwenzetu nyumbani kwetu yaani Geita au Chato?

Matusi ya hadharani kule hawajazoea hasa ukitukana mtu kabila yao wa eneo hilo ni kama kilimanjaro.Lisu haelewi kabisa kuwa lipi aseme wapi na lipi asiseme

Anaua Chadema kwa wasukuma huyo

kuna Tetesi kuwa anajua 2025 Chadema hawatamteua kuwa mgombea uraisi anataka kuhamia ACT wazalendo. Kwa hiyo kabla kuhama anataka kuua Chadema kanda ya ziwa

Lisu hajui eneo lipi aseme nini .Anachoongea mdomoni .Mdomo wake hauna connections na ubongo.

Geita au Chato waweza ponda Magufuli? Au uende mwanasiasa Hai halafu umponde Mbowe hutoboi kwenye kura
 
Labda alivyoenda yeye ndio amefanya utafiti kazikuta..mbona hakutueleza kwenye ile mikutano waliyokuja na kauli mbiu ya kumchana magu wakakosa watu wakaachana kabla ya kurudi na DP world.
 
Kupekuliwa nyumban kwa Magufuli mi sioni ni hoja, madam hakuwa Tena rais lazima security wafanye clearance mambo ya nchi yasije fika mikono isiyo salama
 
CCM team Samia wajanja sana wanavunja ngome ya CHATO kwa kuitumia CHADEMA then baadae wakishawaaminisha kwamba bwana yule alikuwa fisadi basi itakuwa rahisi sana wao kumalizia tu.
Kosa moja halihalalishi mengine.
 
Labda alivyoenda yeye ndio amefanya utafiti kazikuta..mbona hakutueleza kwenye ile mikutano waliyokuja na kauli mbiu ya kumchana magu wakakosa watu wakaachana kabla ya kurudi na DP world.
Lisu yeye chochote anachosikia juu ya Magufuli anaropoka! Mazwazwa nao wanalala nae mbele kushangilia!
Lakini hutamsikia akiongelea ufisadi wa Kikwete na Riziwani!
Hivi Lisu ashindwe kujua habari za Magufuli aje aseme leo! Hizo ni habari za kusikia na kuropoka!
 
Kama Lissu ni muongo, wamshitaki kwa uongo kesi iende mahakamani aoneshe ushahidi wake.

Watawala wasipomshitaki, wamekubali Lissu anasema kweli na wameogopa atatoa ushahidi zaidi ikiwa kesi itafuka mahakamani.
 
Utaelewa tu. Serikali ina mkono mrefu
Samia alivyotaka kumchafua Magufuli tokea mwanzo wa utawala wake ashindwe kulisema hata kama sio yeye machawa wake akina Nape washinde kumwandika hata tweeter au kumzodoa Bashiru au Pole pole kwa jinsi alivyowasumbua mpaka kumpa ubalozi!
 
Kwani uongo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…