Lissu: Dola za Kimarekani Milioni 42 (takribani Tsh. Bilioni 100) zilikutwa nyumbani kwa Magufuli baada ya kufariki

Kiasi chote hicho cha pesa kilikutwa nyumbani kwa Magufuli, ina maana alikiweka kwa siri hata mke wake na wengine wa familia yake hawakujua...
Mada hii itakuwa na uhai au sifa stahili kufanyiwa kazi ktk akili endapo maswali haya uliyouliza yatajibiwa.vinginevyo ni uzushi kama uzushi mwingine tu.
 
Magufuli alikuwa akiishi ktk nyumba za serikali Dsalaam na Dodoma.

Maeneo hayo mawili ndipo kuna uwezekano fedha hizo zilipatikana na huenda zilipatikana wakati wa kuhamisha familia yake, ili kutoa nafasi kwa familia ya Raisi mpya.
Nyumba yoyote anayokwenda raisi iwe yake binafsi au ya serikali; walinzi wake lazima waikague kila chumba kuhakikisha ipo secure.

Sasa hizo hela alikuwa anazificha wapi, anapokuwa akienda huko. Tena wanaenda kabla yeye mwenyewe ajafika, $42m sio hela unazoweza zificha zisionekane.

Porojo tu, raisi ata anapoenda ata nje ya nchi kuna watu wanatangulia kukagua anapofikia siku kadhaa kabla ya yeye kufika.
 
Niliwahi kushauri, threads za tuhuma za kuchafua watu humu, kwa hearsay ziendane na uthibitisho usiotia shaka, usikute mtoa tuhuma anatafuta a honorary exit ili akiitwa kuthibitisha, huyooo....
Umejuaje ana amani. Umejuaje amepumzika wakati dunia inajua alilkufa.

Au ndiyo kuongea bila uthibitisho!

Magu alikuwa mwizi km Majizi mengine ya CCM.

Alichofanya Jiwe Ni kupunguza idadi ya walaji.

Hakuna CCM msafi.
 
Kama Lissu ni muongo, wamshitaki kwa uongo kesi iende mahakamani aoneshe ushahidi wake.

Watawala wasipomshitaki, wamekubali Lissu anasema kweli na wameogopa atatoa ushahidi zaidi ikiwa kesi itafuka mahakamani.
Tundu Lissu ana historia ya kusema uongo.

Alishawahi kudai kuwa huyu mlinzi wa Magufuli naye alikufa kwa COVID-19. Alidai hivyo akiwa anahojiwa Voice of America





Video hii hapa. Anzia dakika ya 21:14 - 21:40.


Kwenye video anatoa kabisa na maelezo ya muonekano wa jamaa alivyo, rangi yake, na anaweka wazi kabisa kuwa siyo yule mpambe wa kijeshi. Ni yule mlinzi.

Huyu mlinzi wa Magufuli hakuwa amekufa wakati Tundu Lissu anatoa madai yake hapo VOA.

Jamaa alikuwepo mpaka kwenye mazishi Chato.



Kauli za Tundu Lissu siyo za kuaminiwa mazima, hususan ikija kwenye mambo yamhusuyo Magufuli, which is understandable.

Lissu is severely jaundiced when it comes to Magufuli. And I’m not saying this to defend Magufuli. I’m just giving my objective observations here.

I know our judicial system is a shit show. But I’d still love to see someone drag Lissu to court and sue him for this so at least we can see what kind of evidence he has about his allegations.

I’m not saying it can’t happen but I find it hard to believe that Magufuli would stash $42 million in his house only to be found out after he died.

Nani alizihesabu hizo hela? Nani aliziona hizo hela?

Na aliingiaje nyumbani kwa Magufuli? Aligonga hodi mlangoni na wao wakamfungulia tu na akaingia akaanza kuzihesabu?

Dola milioni 42 ni nyingi bana.

Tundu Lissu ni lazima atoe ushahidi zaidi ya hayo maneno yake.
 
Nasema hivi, mfungulieni kesi mahakamani mjue mbivu mbichi.

Kama muongo, waongo wapate funzo. Kama mkweli, tujue ukweli kwa ushahidi utakaopitiwa na mahakama na kufanyiwa uchambuzi wa kisheria.

Vinginevyo, mmekubali tuhuma.

Mtu kuwa na historia ya kusema uongo, if that is indeed the case, haimaanishi kila atakachokisema kitakuwa uongo.

After all, even a broken clock can be right twice a day.

Investigate every case on its own, do not deflect an issue with ad hominem logical fallacy.

There us such a thing as "the problemnof induction"
 

..nimesema uwezekano fedha hizo zilionekana wakati wa zoezi la kuhamisha familia ya Magufuli toka ktk makazi ya Raisi.
 
Tutake kutafuta ukweli kwa kutumia mantiki badala kubishana na Lisu hovyo hovyo.
Tumuulize kuhusu pesa hizo kukutwa nyumbani, tusihangaike na biashara, bank account au mali nyingine.
Yeye kazungumzia habari ya nyumbani.
 
Mfungulieni kesi mahakamani?

Mimi sihusiki na chochote. Naona hujaelewa vizuri nilichoandika.

Nimesema hivi, Lissu ana historia ya kusema uongo. Hivyo, mimi binafsi nahitaji zaidi ya hayo maneno yake maana alishawahi kudanganya waziwazi [iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya] kwenye kituo cha habari cha kimataifa.

Nimesema pia ningependa kuona anaburuzwa mahakamani ili tuweze kuona ana ushahidi gani wa hayo madai yake.

Mimi binafsi sijali kama Magufuli alikuwa na hayo mahela nyumbani kwake au la.
 
Magufuli alikuwa anafanya biashara gani nahiyo bilioni 98 hapo nyumbani kwake?

..biashara yake ilikuwa Uraisi wa Tz.

..hivi mmesahau mabulungutu ya pesa aliyokuwa akitembea nayo na kuyagawa alivyokuwa akijisikia?

..sasa kuna ajabu gani mtu wa aina hiyo kukutwa amejaza mapesa nyumbani kwake?

..wasiwasi wangu uko ktk kiwango cha fedha inachodaiwa zilikuwa nyumbani.


..lakini sishangazwi na madai kwamba kuna fedha, tena nyingi, zilikutwa nyumbani kwa Magufuli, IKULU.
 
Kwa nini hujali kama Magufuli alikuwa na hizo hela ama la?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…