Tetesi: Lissu kufanya mapinduzi CHADEMA kuwavuta Mwabukusi, Dkt Slaa na Mpina

Tetesi: Lissu kufanya mapinduzi CHADEMA kuwavuta Mwabukusi, Dkt Slaa na Mpina

Pafukapo moshi ujue kuna moto,

Za chini ya kapeti Makamu Mwenyekiti wa Chadema yupo, kwenye harakati za chini kwa chini kutaka kumpindua mwenyekiti na kukiongoza chama kama mwenyekiti.

Kikao chao cha siri inasemakana ameona Mbowe ni kikwazo chama kukamata dola hata kama sio kukamata ila chama kuendeshwa kiharakati zaidi kuliko uongozi wake Mbowe, ambaye chama kinafanya siasa za uoga .

Na inasemekana wanamtuhumu Mh Mbowe kuwa chama kimepokea mabilioni ili kutimiza matakwa ya kuwaweka wale watu wasio na siasa kali za kiharakati, hivyo makamu mwenyekiti kama atafanikiwa kuchukua madaraka amepanga kumvuta mwabukusi kama makamu wake, na katibu ni Dkt. Slaa.

Sisi tulio nje tunasema wacha wapasuane pesa haijawahi muacha mtu salama!

Chadema na ife kabisa Act ichukue nafasi!
Sawa.
 
Ni kupiga kura kwa wingi wastani wa umri unawabeba wapinzani!
Kura kwa tume ipi, hii ambayo mwenyekiti wa ccm anapanga na genge lake matokeo yaweje kwa kushirikiana na vyombo vya Dola?
 
Kura kwa tume ipi, hii ambayo mwenyekiti wa ccm anapanga na genge lake matokeo yaweje kwa kushirikiana na vyombo vya Dola?
Tume imebadilishwa jina maana kwa takwa la wananchi kama wewe sasa ni tume huru ya uchaguzi hamasisha wengine mkajaze sanduku mzilinde kura zenu!
 
Tume imebadilishwa jina maana kwa takwa la wananchi kama wewe sasa ni tume huru ya uchaguzi hamasisha wengine mkajaze sanduku mzilinde kura zenu!
Watu wajinga ndio watajitokeza kupiga kura kwa tume kubadilishwa jina.
 
CCM badala ya kuongelea suala la mwenyekiti wenu kukimbia hoja ya kikotoo kwenye sherehe za Mei mosi, mnaleta umbeya usio na mashiko 🤔
Halafu unakuta hao vuvuzela wa ccm wengine ni watumishi na wanalia lia na kikokoto na umasikini wao baada ya kustaafu.
Leo Samia kawakimbia Arusha lakini shida zao wakigeuka nyuma wanataka kina Heche, Lema, Lissu nk ndio waeasemee!
Ni kama wamelishwa limbwata na ccm
 
Pafukapo moshi ujue kuna moto,

Za chini ya kapeti Makamu Mwenyekiti wa Chadema yupo, kwenye harakati za chini kwa chini kutaka kumpindua mwenyekiti na kukiongoza chama kama mwenyekiti.

Kikao chao cha siri inasemakana ameona Mbowe ni kikwazo chama kukamata dola hata kama sio kukamata ila chama kuendeshwa kiharakati zaidi kuliko uongozi wake Mbowe, ambaye chama kinafanya siasa za uoga .

Na inasemekana wanamtuhumu Mh Mbowe kuwa chama kimepokea mabilioni ili kutimiza matakwa ya kuwaweka wale watu wasio na siasa kali za kiharakati, hivyo makamu mwenyekiti kama atafanikiwa kuchukua madaraka amepanga kumvuta mwabukusi kama makamu wake, na katibu ni Dkt. Slaa.

Sisi tulio nje tunasema wacha wapasuane pesa haijawahi muacha mtu salama!

Chadema na ife kabisa Act ichukue nafasi!
Bado tu mnatumiaga mbinu hii ya propaganda uchwara za miaka 47?

Huu uwendawazimu wenu wa kujaribu ku - baffle mgogoro ndani ya CHADEMA hujitokeza kila zinapokaribia chaguzi kuanzia 2005, 2010, 2015 na zaidi ilikuwa 2020...

kipara kipya unadhani una akili utaiweza kuicheza ngoma ya CHADEMA wewe na wenzako maana style ya propaganda ni ileile na watu ni walewale tangu miaka ileeeeeee na ilishashindikana!!
 
Bado tu mnatumiaga mbinu hii ya propaganda uchwara za miaka 47?

Huu uwendawazimu wenu wa kujaribu ku - baffle mgogoro ndani ya CHADEMA hujitokeza kila zinapokaribia chaguzi kuanzia 2005, 2010, 2015 na zaidi ilikuwa 2020...

kipara kipya unadhani una akili utaiweza kuicheza ngoma ya CHADEMA wewe na wenzako maana style ya propaganda ni ileile na watu ni walewale tangu miaka ileeeeeee na ilishashindikana!!
Mtu mwenye maarifa angekaa kimya akachimba undani wa jambo ,nyumba inatekea!
 
Mpaka unatamani kurudisha kadi ya chama lakini unasema yawezekana itafika siku chama changu kitakomaa kwa siasa za ukomavu.
 
Mimi Mwashambwa Lucas Nasema acha wapinduane tu mpaka na ikibidi hata wagawane mbao ili kila mtu aende na mbao zake kwake kukokea moto kwa ajili ya kuota kupata joto.
Lucas uteuzi ni mgumu sana ndugu yangu lakini upambanie. Kwa akili yako kabisa unaamini ujumbe huu ni kweli? Basi utakuwa umewaza kwa namna ya ajabu sana kukubali hili jambo kama la kweli.
 
Kabisa, sio hasira ndogo. Wenye muda wa kupoteza kushiriki huo ushenzi uitwao uchaguzi wanaruhusiwa.
Mbona wana usubiri kwa hamu kubwa na shauku wanasema wanatayarisha vichinjio!
 
Pafukapo moshi ujue kuna moto,

Za chini ya kapeti Makamu Mwenyekiti wa Chadema yupo, kwenye harakati za chini kwa chini kutaka kumpindua mwenyekiti na kukiongoza chama kama mwenyekiti.

Kikao chao cha siri inasemakana ameona Mbowe ni kikwazo chama kukamata dola hata kama sio kukamata ila chama kuendeshwa kiharakati zaidi kuliko uongozi wake Mbowe, ambaye chama kinafanya siasa za uoga .

Na inasemekana wanamtuhumu Mh Mbowe kuwa chama kimepokea mabilioni ili kutimiza matakwa ya kuwaweka wale watu wasio na siasa kali za kiharakati, hivyo makamu mwenyekiti kama atafanikiwa kuchukua madaraka amepanga kumvuta mwabukusi kama makamu wake, na katibu ni Dkt. Slaa.

Sisi tulio nje tunasema wacha wapasuane pesa haijawahi muacha mtu salama!

Chadema na ife kabisa Act ichukue nafasi!
Umeandika utumbo mtupu, halafu wakati mwingine habari zenye kuvuta hisia za watu muwe mnaandika kwa weledi basi.
 
Back
Top Bottom