Uchaguzi 2020 Lissu, kuna kila dalili wenye CHADEMA yao hawakutaki ugombee urais, kama vipi twen'zetu ACT Wazalendo

Uchaguzi 2020 Lissu, kuna kila dalili wenye CHADEMA yao hawakutaki ugombee urais, kama vipi twen'zetu ACT Wazalendo

Kesi siyo kigezo cha kumzuia mgombea wa Chadema kugombea iwapo chama kitarally behind him.

Kitendo cha kuwapa CCM option kuwa Chadema ina wasiwasi na ugombea wa Lissu kitawafanya CCM wamshughulikie Lissu kweli kupitia mahakama. Lakini kama Chsdema itasema kuwa huyu ndo mgombea pekee tuliye naye hatuna mwingine, basi serikali ya CCM haitomshughulikia kwa sababu kufanya hivyo kutaondoa credibility ya zoezi zima la uchaguzi kitu ambacho Magufuli anakiogopa sana, ili aweze kupata mikopo ma misaada nje ya nchi na kujaribu kujenga taswira kuwa alishinda kihalali na hivyo hatamshughulikia Lissu kumdiscredit kugombea.. Lakini hili linawezekana tu kama chama kitatuma meseji kuanzia sasa kuwa huyu ndo likely candidate wao!

Ila Chadema wakionyesha wasiwasi kwenye candidacy ya Lissu basi serikali ya CCM itacapitalize ktk hilo kumshughulikia kweli
Ndugu acha kuongea utumbo basi, hueleweki kabisa. Hoja yako ni nini hasa? Unashindwaje kufahamu kwamba Serikali hii ya CCM haina tofauti na ile ya NDULI IDD AMIN DADAA?
 
Kumbe na wewe umeligumdua hilo? Huyu jamaa nadhani anayumiwa na wenzetu upande wa act
Lissu alishasema chama wakinipa nafasi ya kupepeprusha bendera.Sisi sio Kama ccm hata angechukua fomu pekeake angepigiwa kura za Ndio/hapana Kama kwa Sumaye uchaguzi uliopita.Kwa hiyo wengi kuchukua fomu haimaanishi kwamba hawamtaki Lissu Wala Mwenyekiti kuchukua fomu haimaanishi Lissu hakubariki.Hii Ndio demokrasia nanhata nafasi za ubunge wa ndani Kuna wabunge ambao huwadhanii wanaweza kupigwa chini kutokana na Sina ya watu wakakao wachallenge kwenye majimbo.

ACT wazalendo pia Wana nafasi ya kusimamisha mgombea wakitaka Ila sio Lissu.Lissu hahami kwenda popote.Lissu anaweza kugombea Tena Cha CDM miaka mitano ijayo.Usitake kuleta siasa za uchonganishi hapa
 
Ndugo MOTN, mengi ulitoyasema yana ukweli , na usiwasikilize wala kuwajibu hao bendera kama akina Salary Slip.

Naomba nikusahihishe au nikuongezee UKWELI mchezo ulivyo mpana kuliko unavyouona.

Lissu alikuwa mmoja wa waliotumia Nguvu zilizoamua Dr Slaa asiwe mgombea mwaka 2015 unfortunately ndiyo hizo hizo zitakazo muangusha naye. Mtego wa Panya....,

Zaidi ya hivyo hata ACT hawantaki, kuna mpango wa pamoja kati ya Mbowe na Zitto kuhakikisha wanamzima Lissu, Zitto anamchukia sana Lissu zaidi ta Mbowe, Mama yake Zitto alipifariki watu waliowashawishi chadema wasihudhurie mazishi ya mama Zitto, ambaye alikuwa mjumbe wa kamati kuu ya chadema, walikuwa Dr Slaa na Lissu ndio waliokuwa wakali sana.

Pia wenye Chadema na hata Zitto wanaogopa Lissu akibahatika akawa raisi , basi atakuwa mkali zaidi ya JPM, na hatawasikiliza wala kupokea ushauri.

LISSU, fursa aliyokuwa nayo ni kujiunga na NCCR au vyama vingenevyo, na nina uhakika kwa nguvu zake pekee atakiunua chama chochote atakachojiunga nacho.
 
Huku kufarijiana Mkuu,,, mimi MWANA Chadema Damu na Mifupa,,,,Picha lishaonekana Lissu hatakiwi CHADEMA,,ANATAKIWA NYALANDU AU MBOWE,,,,,,Ila wote hawauziki kama. TUNDU ANTIPAS LISSU,,,Tena NYALANDU ndo mweupee kabisa ,,,,
Huko CCM nani atachukua fomu kupimana misuli na "yesu" wenu?
 
Jiandae tu kisaikolojia Lisu hatateuliwa na chadema Kuna issues nyingi Lisu kachemka

Amechemka kwenye mambo gani labda. Na kwanini cdm hawakumuambia mpaka atangaze nia ya kugombea?
 
Kila dalili ndani ya Chadema zinajionyesha, brother Lissu wenye Chadema yao hawakutaki ugombee urais kupitia chama hicho. Wangekutaka wangekupa hata signal ya kuwa wako nyuma yako katika kinyang'anyiro hiki.

Kuna sauti mitandaoni Godbless Lema anasema "umeanza kujiweka katika tune ya ugombea urais", yaani umeshaanza kujiaminisha kuwa wewe ni mgombea, hii ni dalili ya kwanza kwamba brother bado hauna baraka za wenye chama chao kugombea.

Pili, kitendo cha Mwenyekiti kuchukua fomu wakati tunajua by all means hana nia ya urais, sisi tunajua na yeye anajua, inalenga kufanya mahesabu yako ndani ya Chadema kupata hiyo nafasi kuwa ngumu, maana kiukweli mwenyekiti anaungwa mkono kuliko wewe ndani ya Chama, na there is no way unaweza kumshinda mbele ya wajumbe kwenye mkutano mkuu.

Kitendo cha Msingwa naye kuchukua fomu wakati naye tunafahamu fika hawezi kumchallenge Magufuli head on ni dhahiri umewekwa mtu kati, chance zako za kuwa mgombea zimeminywa kutokana na move hizi tunazoziona.

Nguvu zilezie zilizoamua Dr Slaa asiwe mgombea mwaka 2015 unfortunately ndiyo hizo hizo it seems zinataka usigombee this time.

Wewe Lissu, watu wana biashara zao, wana mipango yao ya hela pembeni, wengine siasa ni mtaji, unadhani wakipewa dili wakuzuie usigombee wanaumia chochote?

Aisee utakatwa kupitia mchakato feki ndani ya chama utakaopewa jina la demokrasia na wewe utashangaa!

Sisi wananchi tunajua wewe na Membe ndiyo mlioutaka Urais mapema kabisa na tunawajua na tunaamini. mmoja kati yenu ndo angeweza kumchallenge jiwe, Yaani Membe ndani ya CCM na wewe nje ya CCM.

Karata ya Membe huko CCM imeshatolewa mchezoni kimafia, umebaki wewe nje ya CCM. na lazima uchezewe mchezo uleule lakini hukohuko ndani ya upinzani! Kuna kitu kigumu mbele ya Fedha?

Sasa jiandae, kama unautaka Urais uwe tayari kushusha Tanga na kupandisha Tanga kwa kwenda ACT.

Kuna kila dalili ya wenye Chadema yao kwenye chama chako hawajawa na msimamo kuwa wewe uwe mgombea!

Endelea kujipanga na ujiandae kisaikolojia. Wewe unaweza kuwa real, lakini kuna baadhi ya watu uchaguzi ni dili.
Nani kakuambia Mbowe hana nia ya kugombea urais
 
Chadema wagombea watano tu Wa urais maneno yanaanza, hivi vipi mngekuwa kama ccm waliokuwa na wagombea 42? nini maana ya demokrasia? Jambo LA msingi haki itendeke kwenye vikao vya chama.Atakayepata kura nyingi asimamishwe Vila kujali wadhifa wake.Binafsi naamini hili andiko halina nia njema kwa chadema.
 
Lifanyikalo gizani linawekwa hadharani

Lissu akiisikia clip hii inabidi akae afikirie mara mbilimbili

Kama alidhani ana baraka za uongozi wa Chadema kupeperusha bendera ya chsma hicho kwenye uraisi basi ajipange upya. This is not the case!
Kwani akiomba urais lazima apate? Mini maana ya kuwa na baraka za uongozi Wa chama?
 
Pamoja na kununua vyama vya kina Lipumba na mbatia, naona Ccm aka gambas bado mko njia panda, baada ya kuona waliochukua fomu ya urais cdm wako wengi, sasa mnaianza kuweweseka, inafahamika wazi jiwe hataki kuwa na mpinzani kwenye kiti cha urais, sasa kitendo cha kujitokeza wagombea wengi mnaona dhahiri namna ya kuzuia cdm kusimamisha mgombea wa urais itakuwa ngumu, ndio mnakuja na hizi propaganda zenu uchwara.
 
Mimi natamani aje wakati ameshateuliwa kugombea urais na kampeni zinaanza Kama kesho tuone wa kumkamta?hao CCM sometimes mnawapa sifa wasizostahili na ndo maana wanaharibu nchi yetu

Mkuu acha hasira, kwani akija na akakamatwa nini kitatokea? Kumbuka hakamatwi na ccm, bali maagizo ya ccm ndio yanamkamata kupitia vyombo vya dola. Kama kuna mahali tulipobugi ni kwa kufundishwa siasa za kikondoo na kina Lowassa na Sumaye, eti tuache harakati na tufanye siasa za hoja. Matokeoa yake chaguzi zote za marudio tulizoshiriki tumepoteza, na zile tulizosusia wamejitangaza wapendavyo.

Hivi majuzi uchaguzi wa serikali za mitaa ndio wametuona wachumba kabisa, wamejitangaza wanavyotaka na hakuna lolote tumewafanya. Wangalau Lissu ndio namuona anaweza kuamsha ile hamasa ya siasa za kuheshimiana. Viongozi madictator huwa hawaogopi siasa za hoja, huwa wanaogopa siasa za misuguano tu.
 
Huko CCM nani atachukua fomu kupimana misuli na "yesu" wenu?
Kwahiyo makosa yaliyoko ccm yanahalalisha yanayofanyika chadema?

Humo vichwani mwenu uwa mmejaza takataka gani?
 
Huku kufarijiana Mkuu,,, mimi MWANA Chadema Damu na Mifupa,,,,Picha lishaonekana Lissu hatakiwi CHADEMA,,ANATAKIWA NYALANDU AU MBOWE,,,,,,Ila wote hawauziki kama. TUNDU ANTIPAS LISSU,,,Tena NYALANDU ndo mweupee kabisa ,,,,
Subiri vikao vitaamua Mkuu, ukijiita chama cha demokrasia vumilia, shida kubwa ya chadema kila mtu kambale, nidhamu Ni zero. Wagombea watano tu mnalalamika, wangekuwa 42 so mgepasuka.
 
Ngoja tuone hili picha mwisho wake bt nahisi wengine wamechukua form ili watengeze cv wengi tu wanahamu na ubunge wao
 
Back
Top Bottom