Huwa na mashaka sana na wewe kama kweli unataka kuona upinzani nchi hii unaimarika.
Akili imeanza kuwajia..na Membe aende wapi?
Ndugu acha kuongea utumbo basi, hueleweki kabisa. Hoja yako ni nini hasa? Unashindwaje kufahamu kwamba Serikali hii ya CCM haina tofauti na ile ya NDULI IDD AMIN DADAA?Kesi siyo kigezo cha kumzuia mgombea wa Chadema kugombea iwapo chama kitarally behind him.
Kitendo cha kuwapa CCM option kuwa Chadema ina wasiwasi na ugombea wa Lissu kitawafanya CCM wamshughulikie Lissu kweli kupitia mahakama. Lakini kama Chsdema itasema kuwa huyu ndo mgombea pekee tuliye naye hatuna mwingine, basi serikali ya CCM haitomshughulikia kwa sababu kufanya hivyo kutaondoa credibility ya zoezi zima la uchaguzi kitu ambacho Magufuli anakiogopa sana, ili aweze kupata mikopo ma misaada nje ya nchi na kujaribu kujenga taswira kuwa alishinda kihalali na hivyo hatamshughulikia Lissu kumdiscredit kugombea.. Lakini hili linawezekana tu kama chama kitatuma meseji kuanzia sasa kuwa huyu ndo likely candidate wao!
Ila Chadema wakionyesha wasiwasi kwenye candidacy ya Lissu basi serikali ya CCM itacapitalize ktk hilo kumshughulikia kweli
Lissu alishasema chama wakinipa nafasi ya kupepeprusha bendera.Sisi sio Kama ccm hata angechukua fomu pekeake angepigiwa kura za Ndio/hapana Kama kwa Sumaye uchaguzi uliopita.Kwa hiyo wengi kuchukua fomu haimaanishi kwamba hawamtaki Lissu Wala Mwenyekiti kuchukua fomu haimaanishi Lissu hakubariki.Hii Ndio demokrasia nanhata nafasi za ubunge wa ndani Kuna wabunge ambao huwadhanii wanaweza kupigwa chini kutokana na Sina ya watu wakakao wachallenge kwenye majimbo.
ACT wazalendo pia Wana nafasi ya kusimamisha mgombea wakitaka Ila sio Lissu.Lissu hahami kwenda popote.Lissu anaweza kugombea Tena Cha CDM miaka mitano ijayo.Usitake kuleta siasa za uchonganishi hapa
Ndugu acha kuongea utumbo basi, hueleweki kabisa. Hoja yako ni nini hasa? Unashindwaje kufahamu kwamba Serikali hii ya CCM haina tofauti na ile ya NDULI IDD AMIN DADAA?
Ukweli mchungu
Huko CCM nani atachukua fomu kupimana misuli na "yesu" wenu?Huku kufarijiana Mkuu,,, mimi MWANA Chadema Damu na Mifupa,,,,Picha lishaonekana Lissu hatakiwi CHADEMA,,ANATAKIWA NYALANDU AU MBOWE,,,,,,Ila wote hawauziki kama. TUNDU ANTIPAS LISSU,,,Tena NYALANDU ndo mweupee kabisa ,,,,
We ni bureee KABSA....HUNA TOFAUTI NA MAMA BHOKEJe Edwin Mtei anataka Lissu awe mgombea?
Jiandae tu kisaikolojia Lisu hatateuliwa na chadema Kuna issues nyingi Lisu kachemka
Nani kakuambia Mbowe hana nia ya kugombea uraisKila dalili ndani ya Chadema zinajionyesha, brother Lissu wenye Chadema yao hawakutaki ugombee urais kupitia chama hicho. Wangekutaka wangekupa hata signal ya kuwa wako nyuma yako katika kinyang'anyiro hiki.
Kuna sauti mitandaoni Godbless Lema anasema "umeanza kujiweka katika tune ya ugombea urais", yaani umeshaanza kujiaminisha kuwa wewe ni mgombea, hii ni dalili ya kwanza kwamba brother bado hauna baraka za wenye chama chao kugombea.
Pili, kitendo cha Mwenyekiti kuchukua fomu wakati tunajua by all means hana nia ya urais, sisi tunajua na yeye anajua, inalenga kufanya mahesabu yako ndani ya Chadema kupata hiyo nafasi kuwa ngumu, maana kiukweli mwenyekiti anaungwa mkono kuliko wewe ndani ya Chama, na there is no way unaweza kumshinda mbele ya wajumbe kwenye mkutano mkuu.
Kitendo cha Msingwa naye kuchukua fomu wakati naye tunafahamu fika hawezi kumchallenge Magufuli head on ni dhahiri umewekwa mtu kati, chance zako za kuwa mgombea zimeminywa kutokana na move hizi tunazoziona.
Nguvu zilezie zilizoamua Dr Slaa asiwe mgombea mwaka 2015 unfortunately ndiyo hizo hizo it seems zinataka usigombee this time.
Wewe Lissu, watu wana biashara zao, wana mipango yao ya hela pembeni, wengine siasa ni mtaji, unadhani wakipewa dili wakuzuie usigombee wanaumia chochote?
Aisee utakatwa kupitia mchakato feki ndani ya chama utakaopewa jina la demokrasia na wewe utashangaa!
Sisi wananchi tunajua wewe na Membe ndiyo mlioutaka Urais mapema kabisa na tunawajua na tunaamini. mmoja kati yenu ndo angeweza kumchallenge jiwe, Yaani Membe ndani ya CCM na wewe nje ya CCM.
Karata ya Membe huko CCM imeshatolewa mchezoni kimafia, umebaki wewe nje ya CCM. na lazima uchezewe mchezo uleule lakini hukohuko ndani ya upinzani! Kuna kitu kigumu mbele ya Fedha?
Sasa jiandae, kama unautaka Urais uwe tayari kushusha Tanga na kupandisha Tanga kwa kwenda ACT.
Kuna kila dalili ya wenye Chadema yao kwenye chama chako hawajawa na msimamo kuwa wewe uwe mgombea!
Endelea kujipanga na ujiandae kisaikolojia. Wewe unaweza kuwa real, lakini kuna baadhi ya watu uchaguzi ni dili.
Kwani akiomba urais lazima apate? Mini maana ya kuwa na baraka za uongozi Wa chama?Lifanyikalo gizani linawekwa hadharani
Lissu akiisikia clip hii inabidi akae afikirie mara mbilimbili
Kama alidhani ana baraka za uongozi wa Chadema kupeperusha bendera ya chsma hicho kwenye uraisi basi ajipange upya. This is not the case!
Siyo kuudhi pale ndio akili yake ilipoishia,!Mbowe anaudhii sanaa
Mimi natamani aje wakati ameshateuliwa kugombea urais na kampeni zinaanza Kama kesho tuone wa kumkamta?hao CCM sometimes mnawapa sifa wasizostahili na ndo maana wanaharibu nchi yetu
Kwahiyo makosa yaliyoko ccm yanahalalisha yanayofanyika chadema?Huko CCM nani atachukua fomu kupimana misuli na "yesu" wenu?
Subiri vikao vitaamua Mkuu, ukijiita chama cha demokrasia vumilia, shida kubwa ya chadema kila mtu kambale, nidhamu Ni zero. Wagombea watano tu mnalalamika, wangekuwa 42 so mgepasuka.Huku kufarijiana Mkuu,,, mimi MWANA Chadema Damu na Mifupa,,,,Picha lishaonekana Lissu hatakiwi CHADEMA,,ANATAKIWA NYALANDU AU MBOWE,,,,,,Ila wote hawauziki kama. TUNDU ANTIPAS LISSU,,,Tena NYALANDU ndo mweupee kabisa ,,,,