Lissu, na Wanaharakati kuweni makini mtapeleka Mbowe jela hamna mnachomsaidia kwenye kesi yake

Napenda tu sheria. Mahakama zetu ziwe huru na sheria zisipindishwe. Haya ya kulambana miguu sio endelevu
 

Kwani Lisu na Chadema Ni mke wa Mbowe? Mbowe si yupo Jela, si mtu mzima, anaweza Omba msamaha ndani ya dakika akatoka!

Kinachotafutwa hapa Ni suluhisho la Kudumu, Hivi unafikiri Mbowe Mjinga? Familia yake haimshauri? Kabisa ?

Kuna watu wameumbwa Kama Mbowe na wako hivyo siku zote na wataendelea Kuwa hivyo milele yote, Hakuna namna wala cha kuwafanya, na Wapo tayari kufa!
 
Sasa hata mkimpeleka huyo Mbowe jela kwa kesi ya kupika, mtapata faida gani! Zaidi tu mnaendelea kudarauliwa na Watanzania wenye akili timamu
Watanzania wenye akili timamu hawawezi Chaggadema
 
Unadhani kukaa jela hata siku moja ni mchezo! Nebda kajaribu! Nadhani huyu bwana keshajifunza kuwa mihemko huwa mwisho wake ni majuto!

Mbowe kukaa jela kwake siyo big deal kivile! Ameamua kujitoa sadaka kutetea kile anacho kiamini, kwa ajili ya Taifa lililo bomoka. Hata mimi ningefikia hatua kama ya kwake, ningekaa tu.
 
Napenda tu sheria mahakama zetu ziwe huru na sheria zisipindishwe. Haya ya kulambana miguu sio endelevu
Ni kweli, ila mfumo wa mahaka zetu si mfumo wa huru. kwasababu kuna connection ya kua under contro na muhimili mwingine, shida ipo hapo. Ifikie mahala kwa mazingira hayo kuwe na 50/50.. serikali inatumia nguvu na mamlaka yake isionekana imetoa boko na Mbowe nae anataki haki.. kuna ushindani hapo.. ila mwenye nguvu ni serikali.. mda usipotee busara itumukie wasilambane miguu.. mbowe awe huru akiwa clear na serikali nayo ichomoke kwa maslahi ya taifa.. 50/50 ila kukishakuwa na maneno mengi kila mtu anasema yes kuna pressure ya haki itendeke ila nao wanajiuliza how?
 
Haki haiombwi, hata kenge huonekana mbishi Kwa kuonewa, anaamini katika kuipata haki yake
 
Watanzania wenye akili timamu hawawezi Chaggadema

Huna tofauti yoyote ile na Luten Urio. I remember you once upon the time! Siku hizi umekuwa kama kituko vile. Lazima utakuwa na wewe ulibinywa sehemu na akina Goodluck.

By the way mimi si Chadema. Mimi ni Mtanzania (Mtanganyika) tu Mzalendo.
 
Huna tofauti yoyote ile na Luten Urio. I remember you once upon the time! Siku hizi umekuwa kama kituko vile. Lazima utakuwa na wewe ulibinywa sehemu na akina Goodluck.

By the way mimi si Chadema. Mimi ni Mtanzania (Mtanganyika) tu Mzalendo.
Makengeza lazima atoke na mimba

 
Athari za risasi 16 siyo mchezo, huku ukiwa umedhulumiwa haki zako za ubunge na matibabu umenyimwa. Tuendelee kumuombea kwa Mungu apate utulivu wa akili ili achague mambo ya kuongea.

Kweli Magufuli alimuibua Tundu Lissu kura za Oktoba 2020, ila naona Lissu anaweza kuwa DIKTETA mbaya sana kuliko Magufuli. Mungu katuepusha kutoka kwa wote wawili.

Huwezi kuanika mambo uliyoongea na Rais kwenye vyombo vya habari unless umetumwa naye.
 
Hivi huyu Lissu si ndio mlitaka awe raisi wetu...?
 
Reactions: Tui
Jibu lao ni kufuata sheria bila mihemko na kushinikizwa. Hivyo tu itaonekana haki imetendeKa. Ndugu kumbuka kesi hii itakua reference kwenye kesi zijazo. Tusiposisitiza matumizi sahihi ya sheri tukawekeza kwenye kubembeleza, wapo watakaoumizwa na kunyimwa hakizao kwa kukosa wabembelejai/watakaowabembelezea. Sheria na uhuru wa mahakama zetu ndio viwe vita yetu kuu kwa maslahi mapana ya watanzania.
 
Giza lizidipo kukaribu na kucha!

Giza lizidipo pambazuko huwa Karibu.

Mwenyezi Mungu anapendezwa na haki .
 
Subiri wenye akili High Court wakupe majibu. Maana unaleta ushabiki wa Simba na Yanga.
 
Lissu sio kiongozi mzuri..yaani angekuwa mtulivu mbowe angetoka mapema Sana.. lakini kwa ubabe huu wa Lissu na ujuwaji..mbowe atakaa Sana
Ni kweli mbowe Hana kosa.. lakini yupo gerezani Sasa..zitumike mbinu zote kumtoa mbowe..ujuwaji hausaidii chochote..
 
Kumbe maneno ya Lissu yanaweza kuathiri upatikanaji wa haki mahakamani.
 
Kuna watu hawataki kusikia Haya ulichokiandika hapa wengi low mind tu ndio wakurupukagi
 
Pamoja na lawama kwa TAL Je kuna sehemu yoyote Jaji wenu kanukuu vifungu na sheria gani ambayo imetumika kuwaona FAM na wenzake wanakesi ya kujibu? Nadhani ni Tanzania pekee hapa hakuna kesi kuna maagizo. Kurasa 1500 kashindwa hata kusoma kifungu katia maamuzi utadhani anasoma gazeti la SANI. Hii lawama itakuja kummaliza SSH kisiasa vibaya sana kuna wahuni wanamtengenezea kizimba.
 
Pamoja na wewe kuwa lawyer unaamini kuwa mahakama itafanya maamuzi kwa kutegemea nani anasema nini kwenye media?

Kama ndivyo vyombo vya haki na maamuzi vinavyofanya kazi ktk nchi hii basi kunahitajika kuuhuisha kila idara na mihimili yote.
 
Mbowe kukaa jela kwake siyo big deal kivile! Ameamua kujitoa sadaka kutetea kile anacho kiamini, kwa ajili ya Taifa lililo bomoka. Hata mimi ningefikia hatua kama ya kwake, ningekaa tu.
Nenda huko jela kaunge juhudi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…