Uchaguzi 2020 Lissu ni mtu jasiri, jaribio lolote la kuiba kura zake litaleta shida

Uchaguzi 2020 Lissu ni mtu jasiri, jaribio lolote la kuiba kura zake litaleta shida

Nimesema jana!! Katika umri wangu na uZoefu wangu ikiwemo kusoma historia ya Tanzania. Nchi hii haijawai pata mwanasiasa kiwango cha Tundu Antiphas Lissu.

Si Kambona, si kolimba, Si Njelu kusaka na G55 yao, si mtikila, si tuntemeke sanga , si aboud Jumbe, si Maalim Seif, Mbowe, Lipumba, Magufuli, si Juma Duni Haji , Zi zitto, si Nyerere wala si kikwete.

Lissu ni alama ya kitu cha kipekee sana kwenye siasa za Tanzania. Ni alama kweli ya haki, uhuru, amani, upendo na kubwa zaidi Lissu ni kielelezo cha kutumia akili na si nguvu katika kusimamia kweli unaloliamini bila kujali matokeo yatakuwaje! Kitendo cha yeye mwenyewe jana kuongoza katika kusimamia analolitetea tena kwenye mazingira magumu vile( Mbele ya askari waliosheheni Silaha za kivita) huku akisimamia msimamo wake hadi mwisho kushinda ni kielelezo cha kipekee sana kwa jinsi gani huyu mtu ni special.

Jana Lissu kafanya kampeni kubwa sana, maana hata wale waliodhani angeshindwa mwishoni walipigwa na butwaa.

Lissu sio tu ni binadamu, ni binadamu na nusu

Lissu sio tu mwana siasa ni mwana siasa na nusu

Lissu sio tu mtu wa haki ni mtu wa haki na nusu

Hongera Lissu!!

Watanzania wote kwa pamoja tunasema Shkamoo!!
Lisu ni debe tupu lile!
 
Ccm lzm waibe kura, na Wana mbinu nyingi.

Saivi wanakusanya id za kura hasa za akina mama, wanachukua kopi, wanasema watazitumia kuwapa mikopo. Inasemekana hizo zinatumika kwa ajili ya kura za vituo hewa vya kupigia kura vya chama
Lisu hana kura za kuibiwa!

Kawavunja moyo sana watu baada ya kuwa kibaraka zile kauli zake za faragha
 
Bado awajaona kitu, washaonywa Lissu sio mzima kichwani; ngoja huu uchaguzi uishe hilo swala litakuwa dhahiri by December.
 
Chadema wakiweza kuweka mawakala kila kituo cha kupigia kura wameshinda.Ccm wanachotegemea ni kuingiza kura kwenye vituo...

NEC wanategea kufanya figisu ktk siku ya kuhesabu kura...

NEC na polisi hawatoweza kuzuia nguvu ya umma endapo vurugu zikitokea ktk vituo vya uchaguzi na ambavyo vipo sehemu mbalimbali tz..
 
Bado awajaona kitu, washaonywa Lissu sio mzima kichwani; ngoja huu uchaguzi uishe hilo swala litakuwa dhahiri by December.
Kunywa maji tu mwana Lumumba. Lissu sio saizi yenu. Naona ameshawapoteza vibaya 😂😂
 
Polee sana mwana Lumumba. Najua hadi kichwa kinakuuma unavyowaza mtaweza vipi kumkabili Lissu [emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Lisu kashashindwa mkuu!

Najua wewe mwenyewe unalifahamu hili kwamba lisu hawezi kuvuka 20% sema ndio hivyo huwezi kukiri kwamba mtapigwa!

Anyway baada ya oktoba 28 najua kiswahili kitabadirika tu.
 
Kunywa maji tu mwana Lumumba. Lissu sio saizi yenu. Naona ameshawapoteza vibaya 😂😂
Yeye kwenye kichwa chake campaign alizokuwa anafanya kipindi cha kutafuta wadhamini anadhani ilikuwa mbinu ya akili kweli wakati watu waliamua kumfumbia macho tu ajisikie yupo salama nyumbani.

Eti anaenda kutembelea masoko hivi anadhani jeshi la polisi limejaza viazi kama wafuasi wa CDM.
 
NEC wanategea kufanya figisu ktk siku ya kuhesabu kura...

NEC na polisi hawatoweza kuzuia nguvu ya umma endapo vurugu zikitokea ktk vituo vya uchaguzi na ambavyo vipo sehemu mbalimbali tz..
Figisu zipi? Wakati Lisu hana kura za kufanyiwa figisu?
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]Lisu kashashindwa mkuu!

Najua wewe mwenyewe unalifahamu hili kwamba lisu hawezi kuvuka 20% sema ndio hivyo huwezi kukiri kwamba mtapigwa!

Anyway baada ya oktoba 28 najua kiswahili kitabadirika tu.
Kila siku nakwambia izo asilimia 20 weka kwa Magufuli. Amini amini nakwambia, Magufuli hashindi uchaguzi wa mwaka huu
 
Yeye kwenye kichwa chake campaign alizokuwa anafanya kipindi cha kutafuta wadhamini anadhani ilikuwa mbinu ya akili kweli wakati watu waliamua kumfumbia macho tu.

Eti anaenda kutembelea masoko hivi anadhani jeshi la polisi limejaza viazi kama wafuasi wa CDM.
Nakushauri tena ndugu. Kunywa tu maji mengi!! Lissu atakuua kwa pressure 😂😂😂😂
 
Kwa nini mnamfanyia figisu kama hana kura za kuibiwa???[emoji23][emoji23][emoji3][emoji23]
Figisu zipi?

Jana mme prove kwamba nyie ni teeth less dogs! Mnabweka ila kuuma hamuwezi!
Yani mikwara yote ile mmemuacha Lisu amapigwa na jua pale kiluvya kwa masaa 8? Kweli?

Lisu sasa atakuwa kajifunza
 
Kila siku nakwambia izo asilimia 20 weka kwa Magufuli. Amini amini nakwambia, Magufuli hashindi uchaguzi wa mwaka huu
Mkuu najua huwezi kukiri kushindwa!

Ila Lisu hatapata zaidi 20%
 
Nakushauri tena ndugu. Kunywa tu maji mengi!! Lissu atakuua kwa pressure 😂😂😂😂
Hiyo pressure itaanza kumdhuru Lissu kabla yangu. Hivi mtu anatembea na magari plate number zimewekwa jina lake, huyu mzima kweli kama sio kutafuta ugomvi na polisi.

Mwambieni ukweli Magufuli ni raisi na anaenda shinda uchaguzi asuburi aone campaign yake itakavyorudi. Aache kushindana na Magufuli personal atoweza hiyo vita yaani jamaa wana mvumilia kweli sio kwamba anaogopwa.
 
Figisu zipi?

Jana mme prove kwamba nyie ni teeth less dogs! Mnabweka ila kuuma hamuwezi!
Yani mikwara yote ile mmemuacha Lisu amapigwa na jua pale kiluvya kwa masaa 8? Kweli?

Lisu sasa atakuwa kajifunza
Huzioni figisu mnazomfanyia??? Kama sisi ni toothless god mgemzuia mgombea wetu kwa masaa 9 jana alafu mkaja kuufyata????

Kwani tulikwambia kuwa Kuna shida kwa yeye akikaa masaa 8 katika kudai haki yake??
 
Hiyo pressure itaanza kumdhuru Lissu kabla yangu. Hivi mtu anatembea na magari plate number zimewekwa jina lake, huyu mzima kweli kama sio kutafuta ugomvi na polisi.

Mwambieni ukweli Magufuli ni raisi na anaenda shinda uchaguzi asuburi aone campaign yake itakavyorudi. Aache kushindana na Magufuli personal atoweza hiyo vita yaani jamaa wana mvumilia kweli sio kwamba anaogopwa.
Nyie mliyoweka plate no za CCM akili zenu ziko sawa kweli??
 
Back
Top Bottom