Lissu: Nilipokaimu Umakamu, haki za kikatiba zilikataliwa kujadiliwa vikaoni na Mwenyekiti!

Lissu: Nilipokaimu Umakamu, haki za kikatiba zilikataliwa kujadiliwa vikaoni na Mwenyekiti!

Akizungumza na Watanzania kupitia katika mtandao wa clubhouse mheshimiwa Lissu amejibu maswali mengi aliyoulizwa na Watanzania. Miongoni mwa mambo aliyoulizwa ni kuhusu faida za maridhiano zilizoelezwa na mwenyekiti Mbowe. Akijibu swali hilo, Ndugu Lissu akasema, anashangaa ndugu Mbowe kuwatangazia wananchi kuwa haki zao za kikatiba kama vile haki ya kufanya mikutano, kufuta kesi za kubambikiwa eti ni matunda ya maridhiano. Lissu akasema kuwa hayo ni haki zao za kikatiba NI NON-NEGOTIATABLE AT THE FIRST PLACE (yaani si jambo la kukaa vikaoni na kujadili eti hizo haki wapeweje)

Mheshimiwa Lissu akasema kuwa , Yeye alipokutana na Samia kule Brussels alimwambia wazi kuwa kwanza afungulie haki zao za kikatiba kisha baada ya hapo ndo wazungumze maridhiano. Mheshimiwa Lissu akasema kuwa kwake maridhiano siyo kupewa kilicho chao kwa mujibu wa katiba, bali maridhiano ni kukubaliana namna ya kufanya REFORMS ZA MSINGI za KATIBA MPYA na SHERIA FAIR ZA UCHAGUZI. Hiyo ndo definition ya maridhiano kwa mujibu wa Lissu.

Lissu akasema, Mwenyekiti alipokuwa kwenye kikao cha baraza la wazee huko Zanzibar alikiri wazi kuwa Mardhiano yalikuwa ni FAILURE na akasema wenzie walioyapinga toka mwanzo walikuwa sahihi, sasa anashangaa leo Mwenyekiti anayapongeza maridhiano kuwa eti yalikuwa mazuri.

Mheshimiwa Lissu akaeleza kuwa Serikali/CCM walikataa mambo ya msingi yote ambayo CHADEMA walitaka kuwa ndio yawe maridhiano halisi, tena waliyakataa kwa barua siyo kwa maneno matupu. Sasa inakuwaje leo Mwenyekiti anasema eti maridhiano yalikuwa ni mafanikio?


Wakati huohuo Ndugu Lissu akampongeza na kumshukuru mheshimiwa Mbowe kwa huduma yake kwa chama, kwa kujitolea kwa namna nyingi sana kukisaidia chama. Hata hivyo Mheshimiwa Lissu akasema, kila mwanachama wa CHADEMA kwa nafasi yake wamakichangia chama. Wapo waliolipia gharama ya juu kabisa ya kujitolea ikiwemo uhai wao, mfano watu kama Ben Saanane, Mzee Kibao, Alphonce Mawazo n.k

UNAWEZA KUSIKIA SAUTI YA LISSU AKIELEZEA MAMBO HAYO HAPA"

View attachment 3183725
Lissu mpaka siku kampeni zinaanza atakuwa asharopoka kila kitu na sijui kampeni zikianza ataongea nini. Mwamba wa Siasa za Chadema Ayatollah Mbowe yeye anamzoom tu. Anasubiri dakika ya mwisho, anamaliza!!!
 
Ukiwaangalia hawa Viongozi wawili utaona kuna tofauti kubwa sana kati yao, ndio maana utagundua ni kwanini mmoja alitakiwa kuhongwa na mwingine kuuwawa na Magufuli.

Magufuli alijuwa nani ni threat kwake.
 
Lissu mpaka siku kampeni zinaanza atakuwa asharopoka kila kitu na sijui kampeni zikianza ataongea nini. Mwamba wa Siasa za Chadema Ayatollah Mbowe yeye anamzoom tu. Anasubiri dakika ya mwisho, anamaliza!!!

Kuropoka namna ulivyokataa hela za CCM ni bora kuliko kununuliwa na CCM halafu ukakaa kimya.
 
Unapokubali kuzungumza na adui yako maana yake lazima compromise iwepo vinginevyo hakuna haja ya kuzungumza.

Lissu anawadanganya wajinga wasiojua maana ya neno maridhiano. Mbowe amenukuu watu mashuhuri kabisa duniani wakieleza maridhiano ni nini.

Hizo haki za kikatiba mbona kabla ya maridhiano hazikutolewa na yeye alikimbia nchi? Kama maridhiano hayakuwa na faida angerudi nchini na kulipwa haki zake za ubunge? Mbona huko nyuma hakulipwa na hakufanya kitu si haki za kikatiba?

Maamuzi ya chama sio mtu mmoja bali ni vikao, mtu mmoja nguvu yake ni ushawishi tu; hata wewe ukishinda hutaweza kuimpose mawazo yako katika chama bila maamuzi hayo kuungwa mkono na kupitishwa na vikao.

Lissu mradi wako wa kumchafua Mbowe hautafanikiwa na elewa kabisa baada ya uchaguzi ndio mwisho wako CHADEMA.
Mbowe kajichafua mwenyewe kulazimisha maridhiano ili apige pesa, Mbowe maridhiano yake ni biashara, huwezi kudai haki zako halali na ukipewa useme ni maridhiano, Mbowe pesa za chama zipo kwenye A/c zake mwenyewe katibu mkuu hana mamlaka pesa anatumia atakavyo hakuna ukaguzi wa hesabu juu yake, kwa kifupi Mbowe ni mchoyo amejaa ubinafsi mwingi, sasa anatumia pesa nyingi asalie madarakani kwani akiingia mwenyekiti mpya atakuwa matatani kwa ufisadi wa pesa za chama
 
Mbowe kafanya madudu mengi ikiwemo kula pesa za wale wabunge haramu 19 anaogopa kutoka ofisini kwani huenda yakafichuka mengi ambayo yatamuumbua sana, yupo radhi kuuza hata mali zake zote anunue uenyekiti asalie afiche madudu yake
 
Mbowe kajichafua mwenyewe kulazimisha maridhiano ili apige pesa, Mbowe maridhiano yake ni biashara, huwezi kudai haki zako halali na ukipewa useme ni maridhiano, Mbowe pesa za chama zipo kwenye A/c zake mwenyewe katibu mkuu hana mamlaka pesa anatumia atakavyo hakuna ukaguzi wa hesabu juu yake, kwa kifupi Mbowe ni mchoyo amejaa ubinafsi mwingi, sasa anatumia pesa nyingi asalie madarakani kwani akiingia mwenyekiti mpya atakuwa matatani kwa ufisadi wa pesa za chama
Chochote unachopewa baada ya maridhiano ni matunda ya naridhiano.

Lissu ni mnufaika wa kwanza wa naridhiano.

Maamuzi ya maridhiano siyo ya Mbowe binafsi ni maamuzi ya kikao ambacho hata Lissu alihudhuria.

Akaunti za pesa za vyama vya siasa zinakaguliwa na CAG na kama ingekuwa pesa zipo katika akaunti binafsi za Mbowe CAG katika ripoti zake angesema.

CHADEMA iliwahi kufanyiwa special auditing na CAG wakati wa Magufuli baada ya Mwambe kutoa tuhuma kama za Lissu lakini CAG hakuona kosa.

Tuhuma zote ulizoandika hapa kama ungeweza kureason logically na critically ungeona zote ni porojo.
 
Hata mimi naweza kusema Lissu ametaka kunipa hela nimpambe mitandaoni. Ishu ni kuthibitisha Sasa!!!
Mzee wenje kaja nyumbani kwako kufuata nini ? Kitendo cha kuja tu ni ushahidi pink
Nanona yanayohitajika zaidi ni Maridhiano kati ya Mbowe na Lissu kabla ya Maridhiano ya Samia na Mbowe🐼
Mbowe hana nidhamu kwa viongozi wenzake makamu katibu mkuu hawana maamuzi kwenye fedha za chama huwaburuza sana, hawajui hata kuna tshs ngapi kwenye A/C ya chama, hufuja pesa atavyo na wakihoji huwa mkali sana
 
Chochote unachopewa baada ya maridhiano ni matunda ya naridhiano.

Lissu ni mnufaika wa kwanza wa naridhiano.

Maamuzi ya maridhiano siyo ya Mbowe binafsi ni maamuzi ya kikao ambacho hata Lissu alihudhuria.

Akaunti za pesa za vyama vya siasa zinakaguliwa na CAG na kama ingekuwa pesa zipo katika akaunti binafsi za Mbowe CAG katika ripoti zake angesema.

CHADEMA iliwahi kufanyiwa special auditing na CAG wakati wa Magufuli baada ya Mwambe kutoa tuhuma kama za Lissu lakini CAG hakuona kosa.

Tuhuma zote ulizoandika hapa kama ungeweza kureason logically na critically ungeona zote ni porojo.
Wakaguzi ni binadamu na mbowe anajua kucheza nao ndiyo maana miaka yote huwa kimya hata wakikuta dosari huzifunika, kwanza kitendo cha karibu mkuu kukosa mamlaka ya fedha ndani ya chama ni Dharau kwake, kupewa haki yao ni sawa na kushinda kesi kusha unashukuru uliyemshinda kesi ya madai yako halali
 
Mbowe huendesha chadema kama Duka lake binafsi viongozi wengine wapo kama vibarua upande wa pesa amejipa mamlaka binafsi hataki mtu kuhoji chochote
 
Mbowe alipitisha Sana kuhusu maridhiano, hakukuwa na maridhiano, Bali kulikuwa na mchakato wa maridhiano na yakavunjika.Lissu ni big brain.Mungu amlinde
Unamdai mtu haki zako akikupa unaita maridhiano inashaza sana
 
Lissu mpaka siku kampeni zinaanza atakuwa asharopoka kila kitu na sijui kampeni zikianza ataongea nini. Mwamba wa Siasa za Chadema Ayatollah Mbowe yeye anamzoom tu. Anasubiri dakika ya mwisho, anamaliza!!!
Mbowe ana madudu mengi sana na lisu kataweka akiba ikiwemo alichofanyiwa Heche vyote ataongea siku ya mwisho wa kampeni ndipo wewe utamgeuka mbowe na kumkataa hata kama sasa unakula pesa zake kwa wingi
 
Mbowe alipitisha Sana kuhusu maridhiano, hakukuwa na maridhiano, Bali kulikuwa na mchakato wa maridhiano na yakavunjika.Lissu ni big brain.Mungu amlinde
hakuna mtu wa aina ya Lissu anayeweza kufanikiwa kwenye ulimwengu wa siasa: atafanikiwa tu kwa muda mfupi but in the long run hatatoboa. period.....
 
Mbowe ana madudu mengi sana na lisu kataweka akiba ikiwemo alichofanyiwa Heche vyote ataongea siku ya mwisho wa kampeni ndipo wewe utamgeuka mbowe na kumkataa hata kama sasa unakula pesa zake kwa wingi
Mimi ni CCM na sijali mtamchagua nani kwasababu kwangu wote hawafai. Mbowe ame overstay. Lissu HANA karama ya uongozi.
 
Mbowe hajasababisha watanzania waumizwe. Hata Lissu wako kasababisha, ujinga kama huu ttunaouona kwa wanaoitwa wanaharakati ndio huchangia watu wateseke.
Anayekubali upumbavu kati ya Lissu na Mbowe nani???Wale COVID 19 wako mle Bungeni kwa hisani ya nani kama siyo Mbowe.Acha ujinga wewe tunajadili mambo ya Demokrasia kumbe miongoni mwetu tunao mafisadi na madikteta.
 
Siasa ngumu,yeye alikuwa Ulaya mwenzake alikuwa gerezani tena gereza la Tanzania tena kwa kesi mbaya.Pamoja na yote na makosa Lisu awe na huruma.Kama yeye anaamini maandamano na sheria na uanaharakati mbona alikimbia.Haya mambo tutafakari,uongozi hauendi hivyo
 
Back
Top Bottom