Pre GE2025 Lissu: UDSM na vyuo vikuu vingine vya Tanzania vimekuwa magereza ambako mijadala ya kisiasa imefungiwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni mara mia uwe maskini wa vitu lakini usiwe maskini wa mawazo! Watu wanahitaji kukombolewa fikra kwanza ndiyo hayo mengine yafuate! Kama wanakosa maji,umeme,nk nani wa kulaumiwa? Siyo serikali hii ambayo imefunga fikra watu kwa kuwadanganya kuwa mtu mmoja analeta maendeleo?
 
Amka ndugu yangu.......Kuna mahusiano makubwa sana kati ya kudai Katiba/uchaguzi Huru na Hako na hayo uliyoyasema.......Tazama Mh. Rais anawaweka Machawa/network yake katika vitengo mbalmbali vya huduma za kijamii bila kufuata utaratibu
 
Nchi yetu Mungu ameibariki vyanzo vingi sana vya maji na umeme lakini shida ya maji na umeme ndo ajenda ya CCM kwa miaka 63 ya uhuru.
Nchi yetu ilipaswa iwe mbali kuliko nchi zote Africa. Hatuna vita wala machafuko na maliasili tunazo za kutosha!!
Haya mambo ya maji, umeme, shule, barabara za vijijini, matundu ya vyoo na mambo pety pety mijadala yake ilitakiwa iishie kwenye baraza la madiwani. Tukienda bungeni tujadili mambo makubwa makubwa. Huwa nashindwa kutazama bunge coz mijadala ni maji, umeme, zahanati vitu ambavyo vinapaswa viwepo na sio kuvisiasisha. Nchi zilizoendelea wana clinic za mifugo yao kama mbwa, paka na kuku inapoumwa wanapeleka kuitibu!! Eti huku kwetu Zahanati na Vituo vya Afya vya kuitibu watu wetu ni changamoto!!!
 
You have spoken the truth. We need stable systems in every sector and thus through those systems it could be very easy for the citizens to access basic needs!!
 
...Ninaamini aumfahamu Lisu au hutaki Kumfahamu sababu ya UCHAWA WAKO......Hapa TZ kila kitu Maigizo tu...Bunge Maigizo, Mahakama Maigizo, Uchaguzi Maigizo, Sherehe za Uhuru Maigizo ..... Watu wanatumia fedha nyingi kusheherekea Sherehe za UHURU wakati watu hatupo huru Kuongea......Ukiongea unapotezwa...Hazoli, KIbao, SOKA,,,,na wengine wengi wapo wapi.....Tazama kinachowatokea WANA-CCM wenzako kama kina Malisa na mh. Luaga Mpina....unatoa maoni unafukuzwa Chama......Lisu Hawezi kuitwa katika RUBBISHI event kama hizo
 
Umesahau alivyowaamsha Wamachinga juu ya wizi walivyokuwa wanaibiwa hela na Magufuli kupitia vitambulisho vya Wamachinga?
 
Kichwa chako kina funza
 
Hayo Maji na Elimu na mazao wameshindwa CCM miaka mingi Tangu huru. usimwangushie Jumba bovu lissu
 
Amka ndugu yangu, kumekucha. Nchi hii kiasilia imekosa nini? Umasikini wetu umeletwa na nini? Fikra kama zako hizi zimeletwa na nini? Ukijikwaa, simama ujiulize kulikoni? Kwa nini umejikwaa?

Mh. Tundu Antihas Lissu anaeleza kwa nini tupo hapa tulipo. Kwa mfano anauliza kwa nini tusiwe na maji na huku maji yametuzunguka? Kwa ufupi kuna kitu tunakikosa na ndio maana tuko hapa tulipo!

Je unakubali tuna watu na tuna ardhi? Tunawatumianje watu na tunaitumiaje ardhi tuliojaaliwa ma Muumba wetu kujiletea maendeleo? Jibu ni kwamba tunahitaji uongozi bora na si bora uongozi!

We cannot solve our problems with the same thinking we used when we created them...Albert Einstein
Hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa mawazo yale yale tuliyotumia wakati tulipoyaumba.

Miaka 64
Chama kilekile, watu wale wale, akili zile zile, fikra zile zile...halafu tufanye mabadiliko, hup ni uendawazimu. CCM must go na ili hilo liwezekane sheria zote zinazoilinda hili genge la wezi lazima zifutwe kwanza. Hicho kisiki kilichosababisha tujikwae lazima tukingóe!
 
Hivyo vyote huwezi kuvipata kwa haki kama kariba yako ni chakavu
 
Wananchi wapi unaongelea we dada?! Hawahawa wanaokunywa maji kwenye bwawa na mifugo na bado kura wanatoa?
 
Wananchi wapi unaongelea we dada?! Hawahawa wanaokunywa maji kwenye bwawa na mifugo na bado kura wanatoa?
Hata Kenya wenye hiyo katiba mnayotaka bado kuna maskini wa kutisha!! Kina Odinga wananeemeka tuuu kisha wanatuma vijana barabarani wakauawe!!

Lissu anataka tengeneza nafasi kama ya Odinga ambayo kamwe hatoweza ipata!!
 
CCM wamekuwa wakizungumzia hizo issues kila msimu wa uchaguzi kama kete zao as if wao CCM ni chama cha upinzani, nini kimebadilika!!?

Lazima uzungumzie tatizo la msingi ambalo ni katiba.
 
CCM wamekuwa wakizungumzia hizo issues kila msimu wa uchaguzi kama kete zao as if wao CCM ni chama cha upinzani, nini kimebadilika!!?

Lazima uzungumzie tatizo la msingi ambalo ni katiba.

Katiba ndo inazungumzia sera na mipango na utekelezaji wake?

Au wewe una illusion kuwa election inafix everything?
 
Unajua maana ya sheria?
Unajua maana ya siasa za masuala/ issues
Hayo unayoyaita wewe matatizo ya wananchi kuna watu ( viongozi wa ccm) waliopewa mamlaka na wqnanchi kupitia ilani yao ya uchaguzi ili wayazungumzie. Kama serikali yako ya ccm pamoja na kukusanya kodi wameshindwa kutatua changamoto ulizotaja hata lisu akizizungumzia ni bure tu mana hana kodi wala bajeti ya kuzitatua.
Mambo yote hujadiliwa ila kwa njia tofauti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…