Pre GE2025 Lissu: UDSM na vyuo vikuu vingine vya Tanzania vimekuwa magereza ambako mijadala ya kisiasa imefungiwa

Pre GE2025 Lissu: UDSM na vyuo vikuu vingine vya Tanzania vimekuwa magereza ambako mijadala ya kisiasa imefungiwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Duu!! Hivi ni hayo matatizo uliyoyataja ndio huleta shida kwa watu au hayo unayosema yupo busy ndio huleta hayo matatizo ya watu? Kweli akili ni nywele ila cc black people nywele zetu ni fupi! Sijui unausadifu msemo huu!!

Hata huko kwenye nchi zenye katiba bora na sheria nzuri za uchaguzi, siasa bado wanafanyia kwenye masuala yanayogusa maisha ya kila siku. Au hujawahi kusikia mijadala ya "Tax cuts for the rich", "universal medicare", "unemployment rate", "gas price" Huko marekani?.

Hii ikufundishe kuwa mwanasiasa makini "anapiga miguu yote", siyo kukomaa na mambo ya sheria tu na kuacha kushawishi uungwaji mkono wa umma kwa kutumia hoja za uchumi
 
Ni nadra sana kumsikia Lissu akizungumzia issue zinazohusu.maisha ya kila siku ya wanachi.kama shida ya maji safi ya uhakika, shida ya umeme, elimu.bora, matatizo ya wamachinga kufanya biashara, kodi.zinazoumiza biashara, bei za.mazao ya mkulima, Usafiri wa shida mijini na vijijini n.k.

Yeye yuko busy na mambo ya sheria, uchaguzi etc. Ni.kweli sheria ni muhimu lakini kuna immediate things vinavyowafanya wananchi wapay attention zaidi, na vitu hivyo.vinahusu ugali wao.
if you want to end it, you Nip it in the bud!
 
Tundu Lissu anaongelea chanzo cha matatizo, watu wanaongelea Ugali ni akina Mh Wassira

Wassira amekuwa mkuu wa mkoa wa Mara miaka ya 1970+ , akawa Waziri wa Kilimo wakati wa Nyerere.
Mwezi uliopita alikuwa Tarime kama Makamu Mwenyekiti wa CCM akiwaasa Vijana wasitumiwe na CHADEMA, watulie Tarime Serikali itawawezesha katika kilimo na Mifugo.

Huyu mtu ujana wake alikuwa RC Mkoa wa Mara na Tarime ikiwemo, akawa Waziri wa Kilimo hakuweza kubadilisha maisha ya Vijana wa Tarime, leo anaongelea '' ugali, huduma n.k.'' kama anavyoshauri Missile of the Nation . Yaani aliyeshindwa kutatua tatizo ndiye anayeongelea tatizo lile lile aliloshindwa

Missile of the Nation anataka tuongelee bei za vibaba vya unga, tusiongelee sheria za manununzi zinazokiukwa kwa kununua Magari V8 500 ya kutembelea. Tuna tatizo kubwa katika jamii hasa tunavyofikiri
tatizo wenye madaraka wanataka muone wanachofanya ni sahihi kwa njia yeyote ile
 
"Mjadala juu ya urithi wa Baba wa Taifa kwenye katiba na siasa za Afrika Mashariki kwenye chuo kikuu chake cha kwanza.

Wakati UDSM na vyuo vikuu vingine vya Tanzania vimekuwa magereza ambako mijadala ya kisiasa imefungiwa, Makerere, Chuo Kikuu cha , kimenialika kutoa mhadhara wa umma juu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na ushawishi wake katika siasa na katiba za Afrika Mashariki.

Kupigania demokrasia nchini ni kupigania pia uhuru wa taaluma na uhuru wa fikra na mawazo katika vyuo vikuu vyetu!" - Tundu Lissu, Mwenyekiti Chadema Taifa

View attachment 3259484

Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Naona mwaka umekosewa, badala ya kuandika tarehe 6 March, 2025 imeandikwa tarehe 6 March, 2024!
 
Ni nadra sana kumsikia Lissu akizungumzia issue zinazohusu.maisha ya kila siku ya wanachi.kama shida ya maji safi ya uhakika, shida ya umeme, elimu.bora, matatizo ya wamachinga kufanya biashara, kodi.zinazoumiza biashara, bei za.mazao ya mkulima, Usafiri wa shida mijini na vijijini n.k.

Yeye yuko busy na mambo ya sheria, uchaguzi etc. Ni.kweli sheria ni muhimu lakini kuna immediate things vinavyowafanya wananchi wapay attention zaidi, na vitu hivyo.vinahusu ugali wao.
Bila Haki Uhuru ndiko wanatoa fursa za utekaji wizinwa kura na mengineyo hivyo vingine vinakuja kwa aina ya haki! Hao wanaozungunzia maji mbona huku Dar tuna wiki 2 hamna maji ? Tunanunua ndoo sh500 na sio safi!
Wqambie wenye kutunyanyapaa wawe wakweli tu!! Haki huinua Taifa!. Msikilize Askofu Bagonza ujumbe wa Kwaresima kama unaelewa utaelewana..
 
Back
Top Bottom