Lissu ukirudi Tanzania zingatia hili, kumkashifu Baba wa Taifa ni off limits

Lissu ukirudi Tanzania zingatia hili, kumkashifu Baba wa Taifa ni off limits

Pamoja na mazuri yake mengi, kuua mfumo wa vyama vingi kwa takribani miaka 30 ulikuwa ni uamuzi mbaya sana. Mpaka sasa taifa hili bado linakabiliwa na kivuli kizito cha utawala wa chama kimoja kutokana na legacy hiyo.
Ulikua uamuzi mbaya kwa maoni yako wewe, demokrasia ya vyama vingi sio maji kwamba kila mtu lazima atakunywa. China hakuna vyama vingi, Saud arabia pia nk. Huko kote kuna maisha na maendeleo makubwa kuliko nchi za vyama vingi
 
1. Ni vyema kuwa sasa tuanaweza kuwa tunaenda sambamba na tunaelewana. Vivyo hivyo kutofautiana kimitazamo na kihoja isiwe shida kiasi cha upande mmoja kudhani unatukanwa au kukashfiwa.

2. Kuhusu Tundu Lissu kukosoa waliowahi kuwa viongozi wa nchi hii na hawa waliopo, honestly hapo bado sijakuelewa na sina hakika kama naweza kukuelewa

3. Si Tundu Lissu pekee anayepambana na kivuli cha mwalimu bali ni kila mtanzania ukiwemo wewe iwe unajua na hata bila wewe kujua.

Yeye (Nyerere) ndiye aliyeweka misingi (footprints) ya taifa hili. Kuna footprints zingine ni mibaya na kikwazo cha maendeleo ya nchi hii hadi kesho, zinastahili kufutwa kabisa. Kwa hili atakosaje kutupiwa mawe? Haiwezekani bali watu watasema tu kuwa, hili lilisababishwa na Nyerere..!!

4. Na by the way, huwezi kufikiri kurekebisha makosa hayo bila kumtaja Mwl J. K. Nyerere kama mwasisi wa taifa hii. Na kama ambavyo nimekwisha kusema, lengo na dhamira si kumkashfu au kumdharau mwasisi huyu wa taifa hili la Tanzania bali ni kuthibitisha tu ubinadamu wake, kuwa, hakuwa Mungu. Alikuwa binadamu anayekosea pia.

Dhamira ni watu na watoto wetu waijue historia ya nchi yetu, viongozi wao waliyoyatenda, tulikotoka, tulipo na tunakoelekea kwa uzuri au ubaya..

Bado nakuuliza swali lile lile: Kuna ubaya gani TL ku - side upande huo?

Ni wazi kuwa huyu ndiye yuko kwenye njia sahihi kuelekea kwenye suluhu ya changamoto zinazoikabili nchi Kwa kufahamu kwanza chanzo cha matatizo haya.b

Mimi nadhani ukosoaji wa dizaini ya TL unakua mgumu kumezwa na wana - CCM kwa sababu unawaharibia sifa yao kisiasa na kuwapa wakati mgumu kujitetea majukwaani. Tutakwepa sana kusema, lakini shida iko hapa..!!

Kwa kuwa umesema hutarudi Tena. basi huko huko uliko take it as a challenge siku nyingine ukirudi, utie neno.

Good night
Wewe mkuu kweli ni thinker na unaweza ku critise bila kutukan.
Tundu Lissu angekuwa hivyo hakuna mtu angemsumbua.
Hata siku anamaliza muda wake Mwalimu alisema tena hadharani kuwa kama binadamu kuna mabo watanzania wamsamehe, kwani alifanya kwa nia njema.
Sra za viji vya ujamaa na kuwakusanya atu kwa nguvu, lile halikuwa zuri.
Na Mwalimu hadi alitoa machozi wakati akimwomba msamaha Rashidi Kawawa kuwa alilaumiwa sana kwa niaba yake, lakini Kawawa hakuacha kumuamini Mwalimu.

Sisi ni binadamu tunakosea, tuombe radhi pale tunapokosea.

Lakini kumtukana Mwalimu, kumkebehi na kumdhalilisha Lissu styel, madara yake ni makubwa.
 
Lakini kumtukana Mwalimu, kumkebehi na kumdhalilisha Lissu styel, madara yake ni makubwa.
Kwa sifa zingine zote ulizonipa sawa, nashukuru..

Ninachokikataa ni hiki ambacho na wewe unakisema hapa..

Tangu lini kutofautina na kupinga mtazamo na mawazo juu ya mtu fulani kiongozi anachotenda na aliyowahi kutenda ikawa ni matusi na kumdhalilisha?

Tundu Lissu hajawahi kumtukana wala kumdhalilisha Hayati Mwl Nyerere unless uoneshe mifano ya matusi hayo!!
 
Unamzungumzia Tundu huyu aliyesema Serikali itafungwa jela sababu ya makinikia...Tundu huyu anayetetea ushoga..au Kuna mwingine
Unadhani ustahili kujibiwa kweli wewe?

Sentensi hii pekee inakutosha
 
Unasema sera na msingi iko pale pale wakati NYAKATI zinabadilika ! eg. Huwezi ukaleta sera na misingi ya ujamaa nyakati hizi tukakuelewa maana ata waasisi wa ujamaa China na Urusi wameachana nao.

Pia ni ujinga kufikiri kwamba kukosoa ni kukashifu,au hauelewi maana ya kashfa na kukosoa?

Tuache ujinga na umbumbumbu,tutamkosoa yoyote maana hakuna Mungu mtu Tanzania.

By the way nchi imeundwa na wakoloni,pia kuna wengi tu walisaidia kuleta uhuru wa kisiasa na sio Nyerere pekee
umesema ukweli ambao mungu anaoutaka! huwezi kuijenga tanzania imara bila kwanza kukosoa utendaji mbovu wa waliotangulia kuufanya. Hivi leo watanzania wengi hatujui kuongea kiingereza kwa sababu ya mtu mmoja tuu kuamua kingereza kifutwe mashuleni. hivi hiyo ni sawa kweli? leo hata michezo ya jumuia ya madola tunashindwa kuchati na wenzenzetu ambao ni wanachama.
 
Wewe mkuu kweli ni thinker na unaweza ku critise bila kutukan.
Tundu Lissu angekuwa hivyo hakuna mtu angemsumbua.
Hata siku anamaliza muda wake Mwalimu alisema tena hadharani kuwa kama binadamu kuna mabo watanzania wamsamehe, kwani alifanya kwa nia njema.
Sra za viji vya ujamaa na kuwakusanya atu kwa nguvu, lile halikuwa zuri.
Na Mwalimu hadi alitoa machozi wakati akimwomba msamaha Rashidi Kawawa kuwa alilaumiwa sana kwa niaba yake, lakini Kawawa hakuacha kumuamini Mwalimu.

Sisi ni binadamu tunakosea, tuombe radhi pale tunapokosea.

Lakini kumtukana Mwalimu, kumkebehi na kumdhalilisha Lissu styel, madara yake ni makubwa.
Acha kuzingua, acha watu waongee, unafiki kitu cha ovyo sana
 
Back
Top Bottom