Low IQ Tanzania, wanafurahia Polisi kuondolewa barabarani!

Kirikuu kukatiza salama mbele ya askari ni kama tajiri kuingia mbinguni😂😂😂 sahizi kirikuu hakitembeagi
 
Hii mada ni Sisi Raia tunabishana na Trafic Police ambao wamo humu ndani,wanatetea maslahi yao.Tuwaambieni nyie mapolisi,ukweli ni kwamba nyinyi mmekuwa kero kutuchelewesha maendeleo.Nyie wenyewe magari yenu ya kipolisi na binafsi ni mabovu nani anawakamata?
 
Bila trafiki police, ile barabara itaua sana. Tuache siasa kwenye mambo ys kitaalam.
Ukweli lazima.usemwe, mfano kutoka Mbalizi Hadi Songwe pale kiwanda cha simenti, Kuna vituo vya trafic police visivyopungua vinne, yaani ndani ya dk 10, mnasimama, kero kabisa
 
Wewe hapo ndiyo unaonekana low IQ dunia hivi sasa inazungumzia ufanisi kwa kutumia teknolojia ya kisasa, wewe unang'ang'ania askari kujazana barabarani kila baada ya mita 1000 wakati hao wangesambaa kuwalinda raia na mali zao, na camera zikafanya kazi unayosema
 
Huko serikalini watu wenye mawazo chanya sijui kwa nini huwa hawasikilizwi ama wanatolewa na wale wenye manufaa na hali ilivyosasa.
 
Pole afande
 
Vipi kamera huwa inakusanya rushwa?
 
yaani tunashukuru pendekezo katoa kinana,hawa wanasiasa hawa.
angekuwa ni kiongozi wa Uma kama PM au VP leo wakazi wa DSM wangeonjeshwa utamu hata kwa masaa 12 tu wajue.

traffic wangeachwa sehemu hizo muhimu halafu shughuli yake kila mtu angeiona.
 
Kinana kashauri tu na siyo kwamba katoa maelekezo, hata hivyi Trafiki hazuii ajali bali ajali huzuiliwa na muongoza chombo, Kwa nyongeza ni kwamba Trafiki kwa kiasi kikubwa wapo kwa ajili ya rushwa tu ndo maana hujazana barabarani pasi na sababu. Mbona kwa kipindi hiki ajali zinatokea na Trafiki wapo kibaaao barabarani?
 
Mkuu umenikumbusha Allegory of the Cave.
 
Wewe ndio low IQ Kinana ameshauri wapunguzwe sio waondolewe,kama suala la ulevi Traffic wamchek dereva kabla hajatoka stand. Pamoja na huo wingi wa traffic Kila Siku wapo mbona ajali Bado zipo
Madereva wote wanaoendesha magari wanatokea Stendi? Hivi ni ajali ngapi za mabasi zimesababishwa na malori ambayo ni marufuku kuingia stendi? Kwa mikoani mtaweza kukaa kimya lakini acha wapungue Dar wiki moja tu mtasema.
 
Kwa Akili zako hujui hawa Polisi ndio wanawaelimisha Madereva juu ya kuzuia AJALI?
huna akili wewe
barabarani kuna madereva kivyeo wapo juu kuliko hao mapolisi
hili ni darasa kubwa kwako kijana
uliza watu wakwambie
 
Madereva wote wanaoendesha magari wanatokea Stendi? Hivi ni ajali ngapi za mabasi zimesababishwa na malori ambayo ni marufuku kuingia stendi? Kwa mikoani mtaweza kukaa kimya lakini acha wapungue Dar wiki moja tu mtasema.
Hata malor yana stand Yao Mkuu Iko pale Kurasin. Mengine pia yanakuwa na stand zao tatizo umekariri tu bus stand
 
Low IQ inaanzia kwako kwa kushindwa kumwelewa mzee Kinana.Narudia kumsikiliza,sisikii akisema traffic police waondolewe,.hebu rudia kumsikiliza tena halafu andika ulichojifunza.
 
Naamini Imemkolea hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…