Elections 2015 Lowassa: Tusipopata mabadiliko CCM Wananchi watatafuta nje ya CCM

Elections 2015 Lowassa: Tusipopata mabadiliko CCM Wananchi watatafuta nje ya CCM

Lowasa hawezi kutoka CCM. Ule ni kama ushirika wa mafia waliokula kiapo cha omertà au genge la wauza madawa ya kulevya. NA EL si mwanachama wa kawaida mule; ni mmoja wa vinara walioshikilia mustakabali wa chama wanaojua siri zote na mikakati yote ya ndani.

Kama ilivyo kwenye jumuia za aina hiyo kama yeye ndiye mkuu mwenyewe (the don) basi akivunje chama kabisa. Asipoweza, ana chaguzi mbili tu: ama kuendelea kuwa mwanachama mtiifu (mpole) au kutoweka katika uso wa dunia hii (a la Balali).
 
Mtu mgonjwa sio lazima upate cheti, inaonesha kijana lowasa unamjulia kwrnye picha. umeshawahi kumuona live kwenye hiyo mikutano yake akamuona anavyotetemeka mikono?


Muongo ni agent wa shetani...!!!

Ww mbona hiv + hatusemi na una tumbo kumbe victim mkubwa...!!! Afya ni neema toka kwa Mungu... Mtasema sana mtakosa la kusema...!!! CCM is in another level thru ENL...!!
 
kama unaona anafanya kampeni mwambie Nape amropokee ndio tutaamini anafanya kampeni..
 
Mara . Waziri Mkuu wa
zamani, Edward Lowassa jana
alisema kuwa muda wa
mabadiliko aliyotabiri Baba
wa Taifa, Mwalimu Nyerere ni
sasa na kwamba yeye ndiye
anayeweza kuyaongoza.
Wakati Lowassa akisema
hayo mjini Iringa, kada
mwingine anayewania urais
kwa kupitia chama hicho,
William Ngeleja alikuwa
mkoani Mwanza ambako
alisema kuwa ana dhamira ya
dhati na nia ya kuleta
mabadiliko kwa maisha ya
Watanzania.

Mjini Iringa, Lowassa alisema
kuwa kwa sasa CCM inahitaji
mabadiliko makubwa na
akanukuu kauli ya Mwalimu
Nyerere aliyoitoa mwaka
1995 alipozungumzia haja ya
chama hicho kujisahihisha.
“Baba wa Taifa alisema kuwa
Watanzania wanahitaji
mabadiliko na wasipoyapata
ndani ya CCM watayatafuta
nje ya CCM,” alisema mbunge
huyo wa Monduli kwenye
hafla hiyo iliyofanyika Uwanja
wa Samora mjini Iringa.

“Huu ni wakati wa
mabadiliko. CCM ikijipanga
inaweza kuleta mabadiliko na
mtu wa kuleta mabadiliko
hayo ni mimi,” alisema.
Lowassa alisema aliamua
kuingia kwenye mbio za urais
kwa sababu tatu, ambazo ni
kufanya mabadiliko ndani ya
CCM, kufanyia kazi tatizo la
umaskini na kushughulikia
tatizo la ajira kwa vijana.
Kwa mujibu wa katibu wa
CCM wa Wilaya ya Iringa Mjini,
Zongo Lobe Zongo, jumla ya
wanachama 58,562 kutoka
wilaya zote walijitokeza
kumdhamini.

Mjini Mwanza, Ngeleja alipata
wadhamini 1,253 na
kusisitiza hajatumwa na mtu
kugombea urais na wala
hana kundi.
“Naomba ifahamike kwamba
mimi kugombea kwangu
urais sijatumwa na mtu, wala
sipo kwenye kundi la mtu
yoyote. Naona natosha na
uwezo huo ninao kama
Mungu atanijalia kupata
nafasi hiyo nitadhihirisha kwa
vitendo,” alisema Ngeleja.
“Mambo niliyoyafanya nikiwa
msaidizi wa Rais Kikwete
yanatosha kuonyesha wazi
kwamba nina uwezo wa
kuboresha mambo
mbalimbali na kukuza
uchumi wetu,” alisema
ambaye alikuwa Waziri wa
Nishati na Madini.

Ngeleja alirudia kutaja
vipaumbele vyake kuwa ni
kudumisha amani na
utengamano wa kitaifa,
kupiga vita ufisadi, rushwa na
mmomonyoko wa maadili,
kuboresha sekta za kilimo,
uvuvi, ufugaji, viwanda,
miundombinu na elimu.

Mkoani Mara, Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa, Bernard
Membe amesema ni
wanaume wachache wa
kuigwa kama Makongoro
Nyerere wenye uthubutu wa
kusema ukweli kwa uwazi na
kwa kujiamini kuhusu
mambo yanayoendelea ndani ya CCM.

source: mwananchi
 
Iringa 58,000? basi kama ni yake yake tu!...maana asiyesikia la....huvunjika.... if you can't fight, join him
 
Mwalimu Nyerere alisema haya haya... alitabiri vema kabisa..!!

Lowassa aliwakumbushia tu, kauli ya Mwl. Nyerere, Baba wa Taifa...!!!

Asante Mungu kumleta Lowassa...sifa na ukuu ni wako eehh Mungu...!!!
 
Mkoani Mara, Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa, Bernard
Membe amesema ni
wanaume wachache wa
kuigwa kama Makongoro
Nyerere wenye uthubutu wa
kusema ukweli kwa uwazi na
kwa kujiamini kuhusu
mambo yanayoendelea ndani
ya CCM.
Nisaidieni kumwelewa bernard
 
Hakika, Lowassa ni Messi wa siasa Tz...

Anapiga chenga na magoli, hata wengine hawajui anafanya nn...!!! Siasa inabidi upende watu na watu wakupende in return..!!!

Imagine, mtu yuko alone, anarushiwa kila aina ya propaganda, ila Mungu kamshikilia kama Obama 2008, na akashinda kwa KISHINDO KIKUU...!!! ndio nachoona kwa Lowassa, Mungu akikuinua, hata waje nani, ni bure...!!!

Hakika, Lowassa is the President in waiting...!!! 2015..!!

Vipi umeahidiwa kupewa nafasi ya U-Balozi wa kudumu UN nini mkuu!. Manake kila kukicha wewe ni Lowasa tu!.
 
Iringa 58,000? basi kama ni yake yake tu!...maana asiyesikia la....huvunjika.... if you can't fight, join him

Mnadanganyika kirahisi hivyo,ingekuwa Iringa kapata 58000 basi hata humu Jf asilimia 90 wangekuwa wanamsapoti Lowasa
 
Mtu mgonjwa sio lazima upate cheti, inaonesha kijana lowasa unamjulia kwrnye picha. umeshawahi kumuona live kwenye hiyo mikutano yake akamuona anavyotetemeka mikono?

Huwezi kumwangalia mtu kwa macho ukagundua ni mgonjwa otherwise km wewe ni mganga wa kienyeji
 
Nisaidieni kumwelewa bernard

Benard Jakaya Membe anatapatapa hajui afanyalo. Mara atumie jina la JK, mara atumie kaburi la Baba wa Taifa, mara atamwunga mkono Mwandosya, mara ajipendekeze kwa Makongoro!
 
Mtu mgonjwa sio lazima upate cheti, inaonesha kijana lowasa unamjulia kwrnye picha. umeshawahi kumuona live kwenye hiyo mikutano yake akamuona anavyotetemeka mikono?
mtaongea mengi sana lkn lowasa ndo rais wetu mtarajiwa,
 
Yale yale ya 2005 ya tumaini lililopotea yaani ccm mnatufanya kama changu ahadi kibao kabla hatujavua za ndani afu mkishatugonga basi mnapotea
 
Hawa wagombea wanaongea kwa sababu ni rahisi kuongea ila hawamaanishi wakisemacho...
CCM imekuwa madarakani kwa miaka zaidi ya 50 haijaleta hayo maendeleo wanayopigia chapuo sasa, sasa iweje leo wageuke malaika wa kutoa ahadi ambazo wameshindwa?
 
Vipi umeahidiwa kupewa nafasi ya U-Balozi wa kudumu UN nini mkuu!. Manake kila kukicha wewe ni Lowasa Ty!.




Wala hanijui, sina association nae... but thru CCM, deep within my heart, my soul and looking the mass following him, huku maisha yalivyo kwa wengi, na hayuko serikalini na bado KAWA LULU YA WATANZANIA, inaonyesha waziwazi, HUYU NI MESSIAH...!!" Ni Lowassa pekee ndie anamvuto wa kisiasa, kiuchumi, kijamiii kwa sasa kuliko wote watia nia, tena kawaacha mbali sana...!!!

Lowassa ni mpango wa Mungu...!!!
 
Back
Top Bottom