Luhaga Mpina: Kuundwe Tume ya kuchunguza 'Utata' wa kifo cha Hayati Magufuli

Luhaga Mpina: Kuundwe Tume ya kuchunguza 'Utata' wa kifo cha Hayati Magufuli

Kwa nini wasiitwe "magufuliGang", maana hiyo "Sukuma" ni wazi kabisa ni misnomer', na tena ni udhalilishaji wa kabila zima bila ya sababu zozote.
Sawa uko sahihi,ila wao nahisi waliamua kuchukua hilo jina ili kuvutia wajinga ambao ni wengi,lakini mkuu sukuma gang siyo kabila la wasukuma ndiyo maana kuna mtu kama Slow Slow na Bushiri. Angalia jinsi mlivyoitwa wanyonge na kuridhika mkawa mnatembea kifua mbele eti nyie ni wanyonge. Amka na utumie akili zako mkuu
 
Angalia jinsi mlivyoitwa wanyonge na kuridhika mkawa mnatembea kifua mbele eti nyie ni wanyonge. Amka na utumie akili zako mkuu
Sijawahi kuwa "mnyonge".

Naona bado hunielewi ninachokueleza tokea huko mwanzo, na kwenye bandiko la mwisho uliloni'quote' hapa. Sasa sijui unataka nikujibu vipi ili unielewe vyema. Huna sababu hata moja ya kuniweka kwenye hayo makundi uliyonayo wewe kichwani mwako. Nina akili huru na timamu kabisa kuwa na msimamo thabiti juu ya jambo lolote ninaloliona na kulipima mwenyewe bila ya kuyumbishwa na yeyote.

Baada ya hapa kama bado utang'ang'ania kuniwekea lebo zisizonihusu, nitajua unafanya maksudi, na nitakuja kivingine kabisa katika kujibu hoja zako.
 
Sijawahi kuwa "mnyonge".

Naona bado hunielewi ninachokueleza tokea huko mwanzo, na kwenye bandiko la mwisho uliloni'quote' hapa. Sasa sijui unataka nikujibu vipi ili unielewe vyema. Huna sababu hata moja ya kuniweka kwenye hayo makundi uliyonayo wewe kichwani mwako. Nina akili huru na timamu kabisa kuwa na msimamo thabiti juu ya jambo lolote ninaloliona na kulipima mwenyewe bila ya kuyumbishwa na yeyote.

Baada ya hapa kama bado utang'ang'ania kuniwekea lebo zisizonihusu, nitajua unafanya maksudi, na nitakuja kivingine kabisa katika kujibu hoja zako.
Pole mkuu kama umekwazika. Siko hapa kumkosea yeyote samahani sana
 
Yaani iko hivi, ukali wa kukemea ufisadi wa Dkt Magufuli waliutumia mabeberu kupitia mbowe na kundi lake kutekeleza mauaji ili kusema Dkt Magufuli ni Dikiteta na muuaji, hivyo inasemekana Mbowe alimuua azory, kamuua ben, alimkosa kosa tundu lisu etc. Hata Mo alitekwa na kundi la akina mbowe na msoga ili kuleta taharuki kuwa serikali inateka watu. Kwa ufupi Dkt Magufuli was very humble and kind sana, ila baadhi ya watanzania walimzidi kete kwa kufanya matukio na kuwahi haraka haraka kuripoti kwenye vyombo vya habari. Kwa ufupi wakisema wachunguze kwa kutumia tume wengi watafungwa
Kama haya yaliyosemwa ni kweli. Then The guy was incompitence, Kwa utitiri ule wa TISS alio ajiri bado alishindwa kua na ushahidi wa haya mambo na kuwa tia akina mbowe hatiani
 
Hee!
Kwani kuwa mpinzani ni lazima kuwa na chama. Hili sikulijuwa? Mimi sitafuti mamlaka ya kuendesha nchi, ila napingana na yanayofanywa na CCM kwa miaka ya hivi karibuni, na hata hii iliyopo sasa.
Na hivyo vyama vya upinzani vinavyotafuta madaraka ya kutimiza sera zao wakiwa kwenye madaraka sioni hata kimoja kinachokidhi matakwa hayo kwa sasa.
Lakini nasema hivi, nipo tayari kuunga mkono chama chochote kinachoonyesha nia ya dhati ya kuiondoa madarakani CCM, bila ya kujali sera zao nyingine. Sera kuu ni uwezo wa kuiondoa CCM madarakani, basi; mengine yanafuata baadae.
Sawa mkuu binafsi nimekuelewa.
 
Unanikosea heshima sana mkuu 'Allency', juu ya hili; kwani nakufahamu siku zote kuwa tofauti na ulivyonielewa kwenye mada hii.
Utaanzia wapi kunifananisha na Bashite, kwa mfano! Kwa vile tu namwona Luhaga Mpina kuwa tofauti ndani ya CCM sasa hivi?
Rudi nyuma uangalie ni mara ngapi umekubaliana nami humu humu JF kwa kukubali nilichochangia kwenye mada mbalimbali, halafu leo kwa sababu ya Luhaga niwe kama Bashite?
Nasema hivi, mkuu wangu 'Allency', inapohusu ilipotufikisha CCM hii, nipo tayari kukubali lebo yoyote ili mradi nisiwe sehemu ya chama hiki kinachotudidimiza sote.
Samahani sana mkuu,jalo kuna comment nilikuwa nimeshakuomba msamaha kabla ya kuona hii
 
Back
Top Bottom