Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Lukuvi: Nina Hofu na Uislaam aka "Islamophobia".

Status
Not open for further replies.
Daima mtu muovu hutafuta pa kuanzia kutekeleza uovu wake. Hata wewe mtoa uzi huu ni mdini unania ya kuwaamsha wadini wenzako waingilie mlango wa hotuba ya Lukuvi aliyoitoa kanisani. Shabani Robert katika kitabu chake cha insha na mashaii anasema mtu 'ana uwezo wa kulifanya jambo lolote kubwa au dogo' Kama nia yako ni kuchochea udini basi umepata jukwaa la kusemea lakini kama nia yako sio udini ungeangalia zaidi maudhui kuliko udini.
Hoja ya jeshi kuchukua nchi kama serikali tatu itapitishwa sio ya Lukuvi ni ya Jakaya Mrisho Kikwete. Lukuvi ameitikia korasi ya wimbo aliouanzisha Rais wa nchi- Mwisilam.
Sio mara ya kwanza viongozi wa kisiasa kutoa matamko ya kisiasa kunapokuwa na sherehe za kidini. Hanjaanza Lukuvi. Mifano ni mingi kama unahaja ya kuijua na kuitumia unaweza kufanya hivyo ila kwa sababu unataka kukoleza hoja ya udini kwa madhumuni unayoyajua wewe unaifumbia macho makusudi.
Unataka Lukuvi aondolewe cheo chake ili apewe Mwislam kama alivyoondolewa Dr. Joice Ndalichako pale Baraza la Taifa la Mitihani hata kabla ya kutathmini faida ulizopata kama Mwislam baada ya kuondoka kwake. Una roho ya nyoka wa ndimu anayefukuza watu wanaokuja kuchuma ndimu hali yeye hali ndimu. Unataka Lukuvi aondolewe kwenye cheo chake hali wewe hatukuja kukipata nyoka wa ndimu.
Kudai maadam Lukuvi kasema basi na waislam watasema yaleyale, kwani waislam ni Kasuku kuigiliza kila linalosemwa. Mbona mengi yamesemwa na kutendwa na wakristo lakini waislam hawajaiga? Wakristo wamejenga mashule na mahospitali waislamu hawajaiga hata mara moja. Una maana waislamu hawana uwezowa kuiga mambo ya maendeleoila wanaiga migogoro. Shule za wakristo zinashika namba za kwanza za kumi bora kitaifa na waislam hushika namba kumi za mwisho. Kwa nini mtoa uzi huu usiwachochee waislamu wenzako waige pili hili kwa faida yao, dini yao na familia zao? Kwa nini unachochea migogoro? Una manufaa gani watanzania wakianza kuzozana kwa sababu za kidini. Angalia nchi za kiislam zinavyokabiliwa na migogoro isiyoisha. Unataka watanzania watumbukie huku. Wewe ni mbaya mara mia zaidi ya Lukuvi kwa sababu ubaa jambo lolote ni mtazamo (atitude). Hakuna ubaya mtu kuoa dada yake lakini kimtizamo kutegemea kabila ni vibaya kuna makabila yanaoa na hakuna athari.
Mheshimiwa Rais Kikwete,

Kwa heshima na taadhima na mapenzi ya hali ya juu niliyonayo katika uongozi wako, siyo siri, ni dhahiri shahiri na kila mwana JF anaweza kuwa shahidi yangu kwa hilo.

Kikwete, nnaamini wewe ni mchapa kazi, nnaamini wewe una muono mpana na mrefu, nnaamini wewe unatimiza wajibu wako kwa kadri ya uwezo wako aliokujaalia Mwenyeezi Mungu.

Nakuomba yasikilize maneno ya William Lukuvi kwa umakini na ujifikirie, huyu William Lukuvi anaitakia mema Tanzania hii?

William Lukuvi amma kwa ujinga wake amma kwa werevu wake, ameutia dosari kubwa utawala wako. Ameenda Kanisani kuwaeleza Wakristo wenzake, tena kwa kujigamba na kejeli na kuonesha kibri ya hali ya juu, kuwa hana imani na Waislaam. Kumbuka iwe Muislaam wa Zanzibar au wa Tanganyika au kokote duniani, Waislaam ni kama kiwiliwili kimoja, unapokiumiza kidole kimoja basi mwili wote unasikia uchungu na unapatwa na maumivu.

William Lukuvi, yuko kwenye Serikali ambayo haina dini! lakini yeye mwenyewe ana dini na alienda kuongea kwenye nyumba ya dini na huko ndipo alipowaudhi Waislaam.

Hiyo ni dosari kubwa sana katika utawala wako. Tunakuomba muachishe kazi haraka sana William Lukuvi kabla hajazua balaa lingine, maana hata alipowahi kwenda kujitetea bungeni alionesha kibri zaidi ya kile alichoonesha Kanisani na akatamba na kuwachiwa muda na Mwenyekiti (mkristo pia) zaidi ya mbunge mwingi yeyote aliyechangia mijadala kwenye bunge maalum, ili ajitetee. Nilifikiri kuwa William Lukuvi ataomba radhi lakini cha kustaajabisha hajaomba radhi na karudia tena na tena na tena kuwa ana hofu na alichokieleza kanisani ni hofu yake na hakuna anaeweza kuhoji hilo.

Sisi tumemuelewa na hatumuhoji yeye, tunakuhoji wewe Rais wetu, jee, kiongozi wako ametugawa au ametuunganisha Watanzania kwa kauli zake hizo?

Jibu lako, mimi silijuwi, lakini jibu letu, ni wazi kabisa kuwa William Lukuvi katugawa Watanzania badala ya kutuunganisha, na si kuwa katugawa Watanganyika na Wazanzibari, la hasha, katugawa Waislaam na Wakristo. Na hilo ni hatari kubwa sana kwa Taifa letu.

Tunakuomba chukuwa hatua za haraka sana, umstaafishe huyu Waziri wako kabla hii athari na mpasuko alotuwekea kuzidi zaidi ya hapa alipotufikisha.

Msikilize:

[video=youtube_share;5gvZyIJkTFY]http://youtu.be/5gvZyIJkTFY[/video]

Nnamalizia kwa kutoa shukrani zangu ikiwa utapata wasaa wa kuyaona haya niliyokueleza.
 
Faizafoxy: Self qualification is no qualifiction. Wacha watu wakusifu. Ukiona baba mwenye nyumba anajitapa mbele ya wanawe kuwa yeye ndiye baba wa nyumba ujue pana walakini. Baba mwenye nyumba hujulikana hata bila ya kujipigia upatu, tena kwa watoto wake.
Hujazisoma vizuri, umekurupuka.
 
FaizaFoxy,

Kwa mara ya kwanza nakuunga mkono kwa hoja yako hii.
Najua wewe ni Mwanachama damu wa CCM na muumini wa Serikali 2! Sasa pamoja na kwamba nakuunga mkono kwa hili lakini pia nakushangaa ni vipi unapingana na mawazo ya Waziri Mkuu Pinda ambaye amewakilishwa na huyu Kibuyu mwenzake mwenye elimu ya kuungaunga Bwana LUKUVI.

Maneno haya haya yalitamkwa na Rais wako Kiwete siku ya kuzindua BMK kwamba Jeshi litachukua nchi iwapo Katiba mpya itakuwa na Serikali 3. Sasa kwanini umsakame Lukuvi wakti yeye alifanya kumwakilisha Waziri Mkuu tu?Lakini pia Waziri Mkuu naye ni mwakilishi wa Rais wako Kiwete. Sasa kwanini hujamwambia Rais wako Kiwete kuwa alikosea from day 1 na hiki ndicho kinachoendelea kusumbua sasa kwa Mawaziri na Wabunge wa CCM? Tumesikia maneno haya yakitamkwa na watu wa hovyo kabisa wasio na upeo wowote kisiasa, kiuchumi naa kijamii. Mtu kama Captain Komba, mtu ambaye amefikia hapo alipo kwa kukata viuno kwenye kikundi cha kwaya ya TOT-CCM!

Kepteni Komba akichangia kwenye BMK amenukuliwa akiropoka kama mlevi wa gongo(in this case mlevi wa madaraka)kwamba kama Katiba itakayoundwa itakuwa ni Serkali 3 basi yeye ataingia MSITUNI KUDAI SERIKALI 2!!!!This is absurdity and nonsense.

Hivi huyu Komba ni nani hasa hata adai kwenda msituni kudai serikali 2???Hivi anajua maana ya kuingia msituni kwa lugha ya kimombo tunaita ''armed struggle''. Nina hakika hapo alipo Komba hajapita mgambo wala JKT wala huo u-Kapteni hajaupata kwa kupigwa kwata na Jeshi. Hapo alipo Komba hajui hata gobore linafanyeje kazi! hlafu mtu anadai ataingia msituni, anataka apigane na nani hasa huyu mwendawazimu????Je, Komba anataka kupigana na Wananchi ambao ndiyo wameamua kuwa na Serikali 3???Hii ni hatari kubwa kwa matamshi ya kifedhuli kama haya.

Kwa maana hiyo basi Serikali ya CCM imebariki na imekubaliana matamshi haya ya kijinga kuanzia kwa Rais Kikwete, William Lukuvi na Komba. Kama sakata hili linatakiwa kusuluhishwa basi ni Rais Kiwete mwenyewe kurudi ndani ya Bunge Maalumu la Katiba(BMK) na kufuta kauli hiyo ya kipuuzi kuwa Jeshi litachukuwa nchi na kuwaomba radhi Wabunge wote na Watanzania kwa ujumla; na baada ya hapo awakaripie na kuwapa onyo kali Lukuvi na Komba kwamba wasizoee ku-copy na ku-paste kila kitu toka kwa Rais. Rais wao Kiwete kila siku anawaambia kwamba.''AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZA KWAKO''
 
Faizafoxy: Self qualification is no qualifiction. Wacha watu wakusifu. Ukiona baba mwenye nyumba anajitapa mbele ya wanawe kuwa yeye ndiye baba wa nyumba ujue pana walakini. Baba mwenye nyumba hujulikana hata bila ya kujipigia upatu, tena kwa watoto wake.

Umelewa?
 
Binafsi siwezi kumalaumu Lukuvi, bali alaumiwe aliyempa nafasi hiyo kwani hailingani na uwezo wake! Elimu ndogo, upeo mdogo. Matokeo yake ndiyo hayo.
 
Kwa kikwete sio rahisi kuwaajibisha mawaziri wake na haijawahi tokea zaidi ya shindikizo kutoka sehemu moja au nyengine,hadi tume ziseme au wabunge waseme lkn eti kwa kunuondoa tu sio rahisi maana anaogopa lawana baada ya kustaafu mwakani,anaona kubakiza miezi michache kisha kumuwajibisha mtu ni kuja kulaumiwa na kuwekeana bifu baada ya kustaafu,lukuvi ni mtu mmoja wa ajabu sana miaka yote,sio kiongozi wa kumtegemea,chuki ni kawaida yake sio za kidini tu bali ni nature yake,tunamuelewa vizuri sana lkn kwa hili best lukuvi umebugi step tena umekanyaga ganda la ndizi mbivu kwa taiz zilizo na maji,mh Rais mfukuze kazu huyu atatupiganisha na kutuwekea chuki kati ya waislam na wakiristo
 
Faizafoxy: Self qualification is no qualifiction. Wacha watu wakusifu. Ukiona baba mwenye nyumba anajitapa mbele ya wanawe kuwa yeye ndiye baba wa nyumba ujue pana walakini. Baba mwenye nyumba hujulikana hata bila ya kujipigia upatu, tena kwa watoto wake.

Sijaandika hapa JF kwa kutafuta sifa hata siku moja, lakini nakuhakikishia haya maandiko yangu hayahitaji kupewa sifa, yameshadonyolewa sana humu na kupelekwa majukwaa mengine, na kila apendae yuko huru kufanya hivyo mradi tu kuna maslahi kwa Taifa.

Jisomee: KUTOKA JAMII FORUMS: Kikwete, William Lukuvi Ameutia Dosari Utawala Wako... - Mohamed Said
 
Kikwete hawezi kumuajibisha Lukuvi,Lukuvi kaonge aliyongea kwa niaba ya CCM,ikumbukwe hapo Kanisani alikuwenda kumuwakilisha Waziri mkuu
 
Mbona hapa hakuna hoja kwa kweli; watawala hawajaona kosa lolote la Lukuvi.

Hoja utaiona wapi? maco unayo lakini hayaoi, masikio unayo lakini hayasikii.

Sitegemei mtu kama wewe kuiona hoja katika hili.

Lakini kumbuka, nyuzi hii imesambazwa kwenye mablogu mtandaoni kwa walioiona hoja.
 
Hoja utaiona wapi? maco unayo lakini hayaoi, masikio unayo lakini hayasikii.

Sitegemei mtu kama wewe kuiona hoja katika hili.

Lakini kumbuka, nyuzi hii imesambazwa kwenye mablogu mtandaoni kwa walioiona hoja.

Upo sensitive na topic za udini utadhani crawler za NSA zimeona keywords za magaidi wenzio:heh::heh:. I can't waste my time analyzing kitu kimeandikwa na Faiza Foxy. Na mtu yeyote anayetaka kuanza sober discussion na Faiza Foxy anapoteza tu muda. Faiza Foxy hayuko sober amelewa udini
 
Mbona hapa hakuna hoja kwa kweli; watawala hawajaona kosa lolote la Lukuvi.

Unatakiwa kuelewa kuwa muanzisha uzi ni Islamist, ukisoma bandiko lake kwa mtazamo huo unaweza kuona hoja yake, hoja kubwa sana. Ntashangaa sana kama hajakurushia matusi.

Naungana nae kuwa Lukuvi hafai, lakini sio kwa hicho anachosema yeye.

By the way, naomba kujua kama kuna kitu kinaitwa "Christianist", nimekuwa najiuliza kama kuna watu kama hawa.
 
Upo sensitive na topic za udini utadhani crawler za NSA zimeona keywords za magaidi wenzio:heh::heh:. I can't waste my time analyzing kitu kimeandikwa na Faiza Foxy. Na mtu yeyote anayetaka kuanza sober discussion na Faiza Foxy anapoteza tu muda. Faiza Foxy hayuko sober amelewa udini

Wewe haupo sensitive na si mdini kama Lukuvi ndiyo maana ukaingia kujibu utumbo au siyo?
 
Tanzania ina wajinga wengi ambao wana sauti kubwa kwa hiyo sauti ya wajinga hao ndiyo inakuwa kama inaiwakilisha Tanzania.
 
Faiza Foxy hujamwelewa MMM,hoja zake zimejaa fasihi inayohitaji tafakuri kumwelewa. Hapo anamkumbusha mkulu kujibu hoja yako, nikwamba anafufua hoja hiyo ilikutathmini response ya mkulu.
Ametumia nafsi yake tu kumwakilisha rais.
So kwamba MMM hajaona hoja ila Huyo mkulu hajaona!
 
Hili la lukuvi sio jepesi .linatumika ipasavyo Zanzibar dhidi ya Ccm
Linatumika dhidi ya muungano
Na litakuwa ajenda kuu ya uchaguzi Znz
Hio ilikua ni suicide ya kisiasa .
Ccm kushinda znz hata kwa wizi itakuwa tabu.
Cuf hawana haja ya kampeni kubwa ni kurekodi hixi hii video na kuweka screen kubwa kila kwenye mikutano yao
Kuisambaza znz yote.
Hata yule ccm mwenye matongo tongo ya kijani ata amka kuona dini yake
Nchi yake na mila zake chini ya ccm zipo rehani
 
Upo sensitive na topic za udini utadhani crawler za NSA zimeona keywords za magaidi wenzio:heh::heh:. I can't waste my time analyzing kitu kimeandikwa na Faiza Foxy. Na mtu yeyote anayetaka kuanza sober discussion na Faiza Foxy anapoteza tu muda. Faiza Foxy hayuko sober amelewa udini

Wewe ndo udini umekutawala suala LA lukuvi liko wazi na ile hakuongea kwa kupenda Ila hisia za udini zimemsukuma mpaka kashindwa kujizuia
 
Mheshimiwa Rais Kikwete,

Kwa heshima na taadhima na mapenzi ya hali ya juu niliyonayo katika uongozi wako, siyo siri, ni dhahiri shahiri na kila mwana JF anaweza kuwa shahidi yangu kwa hilo.

Kikwete, nnaamini wewe ni mchapa kazi, nnaamini wewe una muono mpana na mrefu, nnaamini wewe unatimiza wajibu wako kwa kadri ya uwezo wako aliokujaalia Mwenyeezi Mungu.
Una dhihaka mbaya sana wewe na Mh. rais!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom