M-wekeza kutoka Vodacom Riba 13%

M-wekeza kutoka Vodacom Riba 13%

Kampuni ya vodacom imeanzisha mfuko wa uwekezaji ambapo mwekezaji atapata faida 13% kwa mwaka .

M-wekeza ni huduma inayomuwezesha mteja wa M-Pesa kuwekeza kima cha chini kabisa kuanzia TZS 1000 na zaidi kutoka M-Pesa na kupata faida nzuri bila gharama ya ziada.

Wateja wote wa M-Pesa wanaweza kujiunga na kusajili Akaunti za M-wekeza na kuanza kuwekeza Unachotakiwa kufanya ni kupiga *150*00#>Huduma za Kifedha>M-wekeza.

M-wekeza ni huduma ya kidigitali inayorahisha uwekezaji kiganjani mwako bila gharama za ziada.

Pia kupitia M-Wekeza mteja anaweza kuwekeza Kiwango chochote na kupata faida mpaka 13% endapo atawekeza fedha zake kwa mwaka mzima na unaweza pata taarifa ya kifedha ya uwekezaji wako muda wowote kiganjani mwako.^EK
Kwanini sio kila mwezi uwe mwaka?
 
Wajaribu kwenda kwenye mfumo wa UTT, ili iwe possible ku - withdraw kiasi cha faida monthly, hata ikibidi hawa wa monthly faida iwe 10.5%,ya capital installed. UTT itakuwa niagie, but this is business!
 
Hii sekta passive income inakuja kwa kasi. Voda 13%, nimeona bank ya Azania na wao wameleta 12.5%, nasubiria atakayeleta 25% hata 100%🤣
Hamna atakayezidi ile 15%+ ya BOT kwa sababu wote hao ni madalali wa BOT.

Mnawapa hela wao wanapeleka BOT wakipewa ile 15%+ yao wao wanawapa 13% wanabakiwa na 2% faida yao.
 
Back
Top Bottom